Tuesday, 31 October 2023

NJIA PANDA YA NDOA

💢💢 *NJIA PANDA YA NDOA ZA KIROHO* 💢💢
*_Imeandaliwa na Mtaalamu wa Saikolojia ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto(Mkurugenzi wa Shirika la Gospel Foundation Tanzania(GFI)_*
Mawasiliano: 0755444078
Email: babaeve755@gmail.com
........................................
_Shalom kwa wana ndoa wote(Maana yake Amani kwa wote waliofunga agano la kuishi pamoja kama mke na mme_
💢Leo nakuletea uchambuzi wa *Kisaikolojia na Kiroho juu ya Ndoa zote zinazo Pumulia Mashine(ziko njia panda) huu ni uchambuzi wa Uponyaji* kama utakuwa UJAFA NAFSI YAKO, kuna watu wamekufa nafsi tayari hao kila kitu uwa wanakiona UONGO ua Hakiwezekani tena.
💢Ila wale wanaoumwa wakikubali kupata dawa wanapona nawale wanao hisi harufu au homa ya shida katika ndoa wakipata dozi hii wanapona.
💢Ndoa nikitu pekee sana duniani(Siyo mbinguni) mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa, nasema duniani, Ndoa ndo *Chombo pekee cha Kutuliza Msongo walo wa mawazo, Ndo chombo pekee Kinaweza kukuua Kabla ya wakati wako wa kufa, ndo chombo pekee kinaweza kukupa maendeleo ya Kimaisha na ndo chombo pekee kinaweza kukufanya Maskini wa kutupwa, ndo chombo pekee kinaweza kukupa Heshima katika jamii na ndo chombo pekee kinaweza kukuvua nguo na kukupa aibu kuu katika jamii ndo Chombo pekee kinaweza Kukulinda ukawa Salama na ukaishi maisha ya Amani na ndo chombo pekee kinaweza kukufanya uishi kama mkimbizi katika nchi ya ugeni,mwisho ndo Chombo pekee kinaweza Kukuandalia njia Ya kwenda mbinguni kwa amani na ndo chombo pekee kinaweza kukuandalia Barabara ya Kwenda Jehanamu aidha unataka au hutaki kwenda jehanamu(mmmmh Hiyo ndo Ndoa) Weka pembeni masuala ya Upako,Imani,nk hayo yanamchango wake mimi nazungumzia Hapa Duniani katika maisha ya kila siku kama Taasisi,nisikilize katika uchambuzi huu wa Kisaikolojia na Kiroho*
💢Kuna kitu walebwa ndoa zinaitwa za Kimungu aunza kiroho KINAKOSEWA sana baada ya Kuoana si *Wanaume wala Wanawake*(wawe wako kiroho sana au hawako kiroho sana wengi siyo wote Wanakikosea) na ndicho kimeziweka ndoa nyingi Njia panda.
💢Kuna maumivu makubwa sana ambayo mama uwezi jua au ambiwa na mmeo Unayo mpatia(akikwambia utajilaumu kamwe) vilevile kuna maumivu baba unampa mkeo akikwambia utajiona ufai kwake kabisa ila *Ameamua kunyamaza tu* Moyo unatiririka Damu akijua yeye mwenyewe( *Hizo ndo uwa sumu za mwili na sumu za wokovu kiroho*) _utaona magonjwa mara presha,vidonda vya tumbo,kuumwa kichwa, kupoteza hamu ya mambo ya Mungu kidogo kidogo_ kumbe ni Maumivu aliyo nayo ambayo Anashindwa kukwambia, au anakosa njiambadala ya kuyatatua maana,kila njia amejaribu UMESHINDWA kubadirika, sasa njia zoote zinazo baki ni Hatarishi kwake kuzichukua LIVE, inabidi AVILIE NDANI KWA NDANI hii ndo hatari sana.
💢Kuna kitu Biblia ilisema sijui kama umewahi kukijua nguvu yake.... *_Aliyeoa au kuolewabAnajishugulisha namna ambavyo atakavyo mpendeza mmewe au mkewe_*
💢Hii sentensi ya Kibiblia niya kisaikolojia Typically siku mwana ndoa yeyote akielewa Mtume Paul alilenga na alimaanisha nini NDOA ZOTE zitapona na amani na furaha na Uaminifu utarejea ndani ya ndoa.
*33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.1 Wakorintho 7:33*

*34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.1 Wakorintho 7:34*
💢Unapaswa kujua kwamba Ndoa niya duniani, unapaswa kujua namna ya kufanya umfanye mwenzako ATULIE NA AKUONE WEWE TU ili kama yupo rohoni atulie mbele ya Mungu kutengeneza mahusiano mazuri na Mungu.
💢Kujishugulisha na mambo ya dunia hii ili kumpendeza mwenza wake *Kisaikolojia ni kusoma Saokolojia ya mwenzako,kujua nini Kinamchukulia nafasi katika maisha yake kwakona kukifanya ili Saikolojia yake itulie*
💢Tuna wanandoa wengi wapo kwenye ndoa, waimbaji,wahubiri, wana huduma mbalimbali ila SAIKOLOJIA ZAO HAZIJATULIA kwa maana hiyo hata HUDUMA au Kiroho chao KIPO KWA NEEMA TU ya Mungu ila tuna sema *They are Vulnerable to Fall Down* yaani wako kwenye hatari ya Maanguko ila wanashikiliwa na Neema ya Mungu na LEGACY ya Kazi  aidha waliyo ifanya katika ujana wao ndo maana wana survive.
💢Alieyo oa au kuolewa kujishugulisha na mambo ya dunia hii ili wampendeze mwenzake, ni *Kufanya mambo ya Kudhibiti Hisia za mwenzako ziwe juu yako na aifurahie ndoa yaani afurahie Kuishi nawe*
💢Hapa kuna maswali inabidi ujiulize,..
1️⃣Nini mwenzangu kinamchukulia time baada ya kuoa au kuolewa UJITAHIDI kumfanyalia..... Mwingine anahitaji ;
1)Heshima sana, yaani ukimpa heshima na kumfanyia mambo ya kumuheshimu aaah anasikia raha.
2)Mwingine ni Lugha nzuri, yaani anahitaji maneno laini na matamu ya mahaba aah anaenjoy.
3)Mwingine ni sex( yaani ndo kama chakula au maji yake) yaani akihitaji sex muda wowote pasiwepo vikwazo na visababu vya ajabu ajabu au masharti aaah anasikia ni kama ameoa au ameolewa na bonge la mtu pekee duniani.
4)Mwingine anahitaji kujaliwa, kuhudumiwa, akipata vitu hivyo yaani yeye anasikia dunia yote yake.
_Yako na mambo mengine na mengine hapo nimekupa mifano tu michache sasa wewe *FIKIRIA WAZA NI KIPI UWA KINA KUCHUKULIA AKILI YAKO KWENYE NDOA KWA MWENZAKO* hicho ndo ambacho anasema Hujishugulisha na dunia hii Ili ampendeze mwenzake_
💢Ndoa nyingi zinaingia NJIA PANDA kwakuwa Watu *Awajishuguli na Dunia Hii namna ya Kumpendeza mwenzake* Maadamu alishaoa au kuolewa anaona imeisha kwani utaenda wapi,kwani kunaaja gani ya kujiangaisha.
💢Wanasahau kwamba kuna Gharama ya Kumpata mtu(kuna maangaiko ya dunia hii kumpata mke au mme,ila pia kuna Gharama ya kumlinda mwenzako)baada ya kumuoa au kuolewa naye.
💢Ndoa nyingi wanaishi pamoja ndani kwenye nyumba moja ila Kila mmoja yupo Nje ya nyumba kisaikolojia.
💢Ndo maana kunawanandoa wengi ambao *Wanaweza Kufurahishwa haraka sana, Kufarijiwa sana, kupendwa sana na watu wa nje kuliko wa ndani* Una dhani nini shida, Saikolojia ya mwenzake Kujishugulisha na dunia hii ampendeze mwenzake HANA, ila kuna watu wa nje wanaweza Kujua namna ya kumpendeza mtu mwimgine ambaye ndo MMEO AU MKEO.
💢Kuna janga moja la SILENCE RELETIONSHIP ambalo kwa sasa linazikumba ndoa nyingi(WAO HAWAJUI) anayejua wewe umebahatika na ukibahatika USIPANIC angalia UNAKOSEA WAPI  *Rekebisha Utaona mwenzako Anaua Mahusiano ya Kimya kimya,Kimya kimya unabaki wewe* usije angaika Kupambana kuzuia mahusiano ya kimya kimya kwa kelele zako bila Kuangalia wapo umekosea.
💢Kisaikolojia tunasema, *Ukiona mtu aliye kwenye mahusiano flani ya uchumba au ndoa* anaanzisha mahusiano mengine ya kimya wakati hatangazi kuyaacha ya kwanza waziwazi jua...
1.Kuna GAP(ufa) moyoni, au akilini ambalo limetafutiwa wakuliziba kimya kimya ili asogee mbele.
2.Kuna Tabia ya kutoridhika ambayo niya asili hii inatokana kurithi au makundi.
3.Kuna kuchoka na kuzoea mahusiano yasiyo na ubunifu wa jambo jipya(yanatafutwa mapya maana kila mahusiano mapya yana ubunifu wa jambo jipya kila siku)ndo maana Biblia ikasema *Unatakiwa Ujishugulishe na Dunia hii ili ujue namna ya kumpendeza mwenzako kila siku* kujishugulisha ni kubuni kila siku unatafuta jambo jipya.
2️⃣Nini nikifanya namuondoa mwenzangu kwenye Mood kabisa na anaweza chukia siku nzima hata wiki.
💢Unajua kuna watu ambao uwa *Awajali Hisia za Mwenzake* hata kidogo, anaweza fanya lolote,akaamua lolote liwalo na liwe hii inaua Hisia za mwenzako sana kiasi kwamba unampelekea *Akuone ni Mtu baki tu kwenye maisha yake, basi tu anaishi nawe ndo shida* ila hana hamu nawe kwa lolote.
💢Ndo maana wana sailolojia wanasema *Fanya kitu kinachoitwa Mistake Analysis kwa mwenzako kwa makusudi na baadaye usizirudie* yaani unamkosea mwenzako mambo mbalimbali unamnyima haki zake flabi flani kwa vipindi kadhawakadha kutafuta kujua *Nini Kina mwondoa kwenye furaha na changamko lake kwako* ukisha jua weka nyota USITHUBUTU kufanya kosa hilo,labds itokee kama ajali na ikitokea wahi kumwomba msamaha kabla moyo wake aujararuliwa na kukufuta. *Huko ndo kunaitwa Kujishugulisha na mambo ya dunia hii Ili Kumpendeza mwenzako*
💢Kwani wewe unahisi kujishugulisha na dunia hii ni nini? ( _Kupika? Kufua? Kuosha vyombo? Kununua nguo? Kuacha pesa za matumizi nyumbani?_) hayo yako ndani ila nikuchanganua kila siku kujua *Dunia hii tuliyomo,inamwitaji mmeo kiasi gani, inamwitaji mkeo kiasi gani, inamuwinda mmeo au mkeo kiasi gani halafu sasa wewe ujipange Kuidhibiti isimpore mikononi mwako*
💢Ukumbuki Yesu alisema kwamba baba wote ulionipa _Hakuna atakaye mpokonya mkononi mwangu hata mmoja, au hakuna niliye mpoteza isipokuwa mwana wa uptevu (Yuda)_
💢Inabidi mwanandoa wewe upambane kwenye nafasi yako kujishugulisha na dunia Kutimiza Wajibu wako kwa mwenzako hata kama kuna Upotevu wowote unazaliwa au unatokea kwa mwenzako YEYE AJIHUKUMU MWENYEWE kwa Nafsi yake,lakini asiseme sentensi ya Adamu ya Mke Uliye nipa ndo Amenisababisha( Wewe Usiwe Sababu).
💢Namalizia kwa kusema kwamba, *_Kwa nyakati za sasa dunia inaenda kasi sana kuziharibu ndoa nyingi, ndo maana watu kujiua ni kwingi, watu wanakufa katika umri mdogo tofauti za zamani watu ambao walikufa katika uzee na wakizikana mke na mme wakiwa wote, kwa sasa Divorce nyingi, Single Parent family ndo nyingi, wengine wanaishi kiugumugumu kwa aibu ya kuachana wataonekanaje kwa watu au kanisani._* Nini kifanyike sasa ili kwamba Tutoke Njia panda?
1️⃣Kwasasa Wanahitajika Wana Saikolojia wengi sana watusaidie kutibu majeraha ya kisaikolojia ya Wana ndoa na mahusiano(Wafundishe na kufundisha)
2️⃣Wafanyaji wa Utafiti waongeze Uwanja wa kufanya utafiti juu ya Vyanzo ya Migogoro ya ndoa na waje na Masuruhisho yake yafundishwe siku kwa siku.
3️⃣Watumishi wa Mungu wajikite katika Kufundisha watu neno la Mungu na kuwasihi watu Warudi kwenye Msingi wa Mwongozo wa Neno la Mungu kuhusu Nafasi, Wajibu na Haki za Mwana ndoa(Ke kwa Me)
4️⃣Mwanandoa Usimkatie Tamaa mwenzako, anaweza kuwa hivyo kwasababu ya Ujinga wa Kutojifunza na Malezi hafifu aliyo yapata kwenye familia, endelea kumwelekeza kwa upendo na wewe kujifunza zaidi ili umbadirishe.
*_Hii Imeandaliwa na Mwanasailojia Ev Elisha Kazimoto(Mkurugenzi wa Shirika la Vijana la Injili Duniani(GFI)_*
Phon: 0755444078
Email :babaeve755@gmail.com
Facebook :Ev Elisha Kazimoto.
YouTube channel.. Ev Elisha Kazimoto

Friday, 14 July 2023

USHINDI UNAHITAJI AKILI

🥅🥅 *USHINDI WOWOTE UNAHITAJI AKILI* 🥅🥅

ANDIKO KUU NI ZABURI 53:2
*_2 Toka mbinguni MUNGU aliwachungulia wanadamu, Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu.Zaburi 53:2_*

_Imeandaliwa na Mtumishi wa Mungu Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)_
Whatsapp *0755444078*
_Haleluya mwana wa Mungu uliye okoka na unayempenda Bwana na kukumtumikia kwa moyo wako wote, leo nina ujumbe wako maalumu kutoka kwa Bwana karibu ubarikiwe na uinuliwe_
✍️Ushindi wowote katika maisha ya kiroho au ya kimwili unahitaji *Akili* tena Ikiwa ni maisha ya Kiroho tunasema unahitaji *Akili ya Kimungu kubwa*
✍️Lakini mtu mwenye akili Biblia imesema ni yule mtu *Amtafutaye Bwana* huyo ndo Kabisa Amefuzu katika Elimu ya Mungu anastahili kukabidhiwa Gamba la Kiroho kwamba huyu ana *Akili*
Hivi kwanza tujue AKILI NI NINI?
1️⃣Akili ni Nuru, ni nguvu ya kutoa mwangaza wakati wa giza.
✍️Ndiyo maana wakasema Elimu ni mwanga wa maisha.
✍️Sasa kiroho tunasema mtu amtafutaye Bwana ana akili na kama ana akili maana yake *Ana Nuru katika Giza* linalo shindana naye.
2️⃣Akili ni Mlango wa Ushindi.
✍️Wakati watu wanajiuliza nafanyaje kutoka hapa mbona kama niko gerezani, Amtu amtafutaye Bwana mwenye *Akili ana mlango wa kutokea*
✍️Ujasoma andiko linalosema *Njia za Kutoka Mautini zina yeye Bwana?* Akili ni Mlango wa kutokea katika mapigano yako.
3️⃣Akili ni Stamina ya kuhimili Mapito.
✍️Vita,Mapito tunayokutana nayo yanalenga *Kututoa Relini, uhame njia* lakini mtu amtafutaye Bwana, mwenye *Akili ana Stamina* hatoki mchezoni kisa vita au majaribu.
4️⃣Akili ni nguvu ya kudharau kelele za Maadui nyuma yako.
✍️Siku zote adui upiga kelele ili akutishe, akytengenezee hofu uache kumtegemea na kumwangalia Bwana umwangalie yeye ili akumalize.
✍️Sasa, mtu mwenye *Akili amtafutaye Bwana akipigiwa kelele yeye anainua macho yake kwa Bwana* hana haja na kuangalia adui au kusikiliza adui anasema nini, sikia Mungu anasema nini nawe wakati huo wa Vita.
5️⃣Akili ni Nguvu ya Maamuzi inayo jua wakati wa kusema na wakati wa kunyamaza.
✍️Si kila wakati unalazimishwa Kusema Useme, na si kila wakati unalazimishwa kunyamaza untamaze.
✍️Kuweza hayo unahitaji *Akili inayo mtafuta Bwana* itakupa wakati sahihi wa kuyafanya hayo yote mawili Kusema na Kunyamaza na hapo *Umewaweza Adui Zako*
✍️Una jua nini, Wakati Adui anategemea useme na hausemi, *Inamuuma* na wakati anategemea *Unyamaze ila we ndo Unasema inamuuma pia*

_Kwanini Mungu anatafuta mtu mwenye Akili Duniani kwa mujibu wa Zaburi 53:2?_
✍️Kwanza inabidi ujue Mungu anafanya kazi na wanadamu( Warumi 8:28).
✍️Kwa maana hiyo ili kutimiza kusudi lake anawataka awapate watu wenye Akili ndo wanauwezo wa Kutimiza kusudi la Mungu duniani.
1️⃣Mtu mwenye Akili anauwezo wa kutimiza kusudi la Mungu bila kuzuiwa na mazingira magumu.
2️⃣Mtu mwemye Akili anaisikiliza Nia ya Mungu(Kristo)ndani yake na si Nia ya watu juu yake.
✍️Katika pointi hizo 2 juu soma *1Samweli 17:26-30* utaona Nia za watu juu yako nikukuzuia usiende au kutimiza kusudi la Mungu.
3️⃣Mtu mwenye Akili aumizwi na vita juu yake, bali anaumizwa na maamuzi ya kupoteza alichokibeba ndani yake kwasababu ya vita juu yake.
✍️Unajua nini, Vita yoyote inayokuja juu yako hailengi maisha yako au wewe kama wewe, vita yoyote inalenga *Kuua au Kupoteza Ulichokibeba* (Kusudi la Mungu ndani yako) MATHAYO 2:13
✍️Herodi alikuwa ataki kuua Yesu, alikuwa anataka kuua Mfalme wa Wayahudi(Yesu alitambulishwa ni mfalme wa Wayahudi) maana yake Herode hana ufalme tena(hii mdo ilikuwa hofu ya Herode) kumbe Yesu ufalme wake si wa ulimwengu huu.
4️⃣Mtu mwenye Akili Aishi kwa kauli za *Watu wananisemaje tu* bali Mungu na Nafsi yake inasemaje kwa habari yake? *Mathayo 16:13-17*
✍️Watu wana muono wao juu yako, kuna wanaokuoa *_vibaya, kuna wanaokuona mtu mwema, kuna wanaokuona mtu jeuri, una kiburi, unajiinua, unajisifu, maskini, mjinga, local sana, mshamba sana, unamuda mchache utapotea_* Kila mtu anamuono wake juu yako.
✍️Kwa maana hiyo usilazimishe wote wakuone unavyo jiona.
✍️Wanafunzi wa Yesu walimpa majibu Yesu ya watu wanavyo muona Yesu, kila mtu alikuwa na jibu lake hata wale ulio *Hisi wangekuona Unavyojiona wewe utashangaa nawao wanaungana na watu wengine wanaokuona tofauti na ulivyo*  ndicho kilitokea kwa Yesu.
✍️Yesu akawauliza na ninyi mnasemaje? WOTE WALIBAKI KIMYA IKIWA NAMAANA NA WAO WALIMUONA YESU KWA NJIA ILE ILE YA WATU WALIVYOKUWA WAKIMSEMA YESU TOFAUTI.
✍️Ila Mungu ni mwema sana katika weengi wanaokuzema tofauti KUNA PETRO WAKO mmoja tu *Atautambulisha Uhalisia wako* huyo ndo atawajulisha wengine wewe ni nani.
✍️Kuna watu uwa wanaumizwa na *Kusemwa Vibaya* mmmmh hicho nikiwango kidogo cha Akili ya Kimungu, ujasikia Biblia inasema *Amebarikiwa(Heri) Astahimiliye Majaribu?* Maana yake nini?
👉Unabaraka kama ukiwa na uwezo wa kuendelea na wokovu ikiwa wewe unapigwa vita usiokoke.
👉Umebarikiwa wewe unayeweza kuendelea Kumtumikia Mungu kwa moyo wote wakati Unazushiwa Mabaya.
👉Umebarikiwa wewe unayeweza kuendela na huduma bila kukata tamaa wakati huduma yako inapigwa Vita kila kona. *YAKOBO 1:12*
*_Hizi ndo baraka Biblia inazitoa kwa watu wenye Akili yaani uwezo wa Kukaa kwenye Reli ya Kiroho wakati wanakutana na Tufani ya kuwavunja Moyo_*
✍️Mungu akupe Akili, Akupe Neema ya Kumtafuta Yeye, Akupe Neema ya Kuendelea mbele katika nyakati zote.
*Hili ndo Neno la Bwana kwako,kutoka katika kinywa cha mtumishi wa Mungu*

Ev Elisha Kazimoto(C.E.O-G.F.I)
Whatsapp: 0755444078
Email: babaeve755@gmail.com
Facebook: Ev Elisha Kazimoto
YouTube channel :Ev Elisha Kazimoto