Friday, 15 May 2020

UVULI WA MKONO WA BWANA

🏹🏹 *USIKU WA MAOMBI NA KUOMBA UVULI WA  MKONO WA BWANA UWE JUU YETU*🏹🏹
_Na Mnenaji :Ev Elisha Kazimoto_
Whatsapp 0755444078
.............................................
_Shalom mwana wa Mungu leo nitanena nawe siri ya Bwana kwa watu wake,walio lishika Agano lake_
👉Mungu ni Mungu wa kulishika Agano lake kwa uaminifu.
👉Bwana ana wivu siku zote kwa watu wake, hataki na hapendi kuona wanaonewa.
👉Uweza wa Bwana wa kuokoa ni mkuu sana pale Ghadhabu yake inaposhuka katika nchi, *_Anao uweza wa kupiga adui,wabaya katika eneo moja na Kuwahifadhi watu wake salama walio katika Eneo moja na waovu_*
SOMA MISTARI HII KWA UTULIVU.
43 Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani. 
Zaburi 78:43

44 Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa. 
Zaburi 78:44

45 Aliwapelekea mainzi wakawala, Na vyura wakawaharibu. 
Zaburi 78:45

46 Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige kazi yao. 
Zaburi 78:46

47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu. 
Zaburi 78:47

48 Akaacha ng'ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, Na makundi yao kwa umeme. 
Zaburi 78:48

49 Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya. 
Zaburi 78:49

50 Akiifanyizia njia hasira yake; Wala hakuziepusha roho zao na mauti, Bali aliiachia tauni uhai wao; 
Zaburi 78:50

51 Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu. 
Zaburi 78:51

52 Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani. 
Zaburi 78:52

53 Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunikiza adui zao. 
Zaburi 78:53

54 Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume. 
Zaburi 78:54

55 Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao. 
Zaburi 78:55
👉Majanga,Tufani,Magonjwa hatari,Dhoruba katika dunia(nchi )havijaanza leo tangu zama za kale zilikuwepo.
👉Ila Mungu ana kanuni yake *Hapatilizi wabaya na wema* kwa pamoja.
👉Wabaya upatilizwa kwa ubaya wao na *Wema uhifadhiwa kwa Uvuli wa mkono wake*
🏹Unaweza jiuliza inakuwaje, soma mistari hapo juu, uliwahi kufikilia *Wakati Mito inageuzwa damu Misri Waisraeli Walipata wapi maji?* Kuna Mito Haikugeuzwa damu kwaajili tu ya Taifa la Bwana.
👉Mazao ya wa Misri yalipoliwa na nzige na tunutu, Mashamba ya waisraeli hayakuguswa hata kama yalikuwa yamepakana.
👆👉 *Kilichokuwa kikifanya kazi pale ni Uvuli wa mkono wa Bwana kwa Waisraeli*
👉Mkono wa Mauti,upepo wa mauti,maangamizi yalipo pita katika nchi, wana wa Mungu,waliokusudiwa na Mungu kwaajili ya Uaminifu wao,walipewa *Angalizo,Jambo la kufanya ili wawe salama kati ya mauti inayopita* Enzi za Yoshua,Ahabu kahaba kwa kuwaficha wapelelezi aliambiwa ili awe salama wakati upanga wa mauti unapita katika mji, *Afunge kamba Nyekundu katika Dirisha la Nyumba yake* Alama ya *Uvuli wa Kuhifadhiwa* mbali na mauti wakati wa maangamizi, akaongezewa mkazo Akae ndani asitoke nje ya nyumba, na watu wake wote wanaotaka usalama wakae ndani wasitoke nje ya nyumba hiyo, na atakaye toka damu yake ikimwagika hatia itakuwa juu yake mwenyewe.
18 Angalia, tutakapoingia katika nchi hii, funga kamba hii nyekundu katika dirisha hili ulilotutelemshia; nawe uwakusanye kwako nyumbani mwako, baba yako, na mama yako, na ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako. 
Yoshua 2:18

19 Itakuwa mtu awaye yote atakayetoka katika mlango wa nyumba yako kwenda njiani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, na sisi tutakuwa hatuna hatia; na mtu atakayekuwa ndani ya nyumba yako damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu, mkono wa mtu ukimpata. 
Yoshua 2:19
👉Unajua nini, hata sasa ziko *Kamba Nyekundu kwenye ulimwengu wa Roho* zinafungwa katika mioyo yetu, hizo ni ALAMA YA UVULI wa kutuepusha na Mabaya.
🔹Utakatifu ni kamba nyekundu
🔹Utumishi mwaminifu kwa Bwana ni kamba nyekundu
🔹Jina la Yesu ni kamba nyekundu
🔹Damu ya Yesu ni kamba nyekundu
🔹Maombi yatokayo katika moyo safi ni kamba nyekundu
🔹Imani katika Bwana na Neno lake halisi ni kamba nyekundu kwenye moyo wako.
👉Shida kubwa ya watu wa Mungu baadhi,ni *Kuruhusu Upepo wa Hofu na Vitisho kuzunguka mioyoni mwao na kuyeyusha Imani zao* Wanalia kama waio mjua Mungu waliavyo, wanasema kama wasiomjua Mungu wasemavyo..... *Kumbe nyakati za Dhaoruba wana wa Mungu wana Lugha yao tofauti na wana wa giza*
👉Sasa kazi ya wana wa Mungu ambao tumeambiwa tufunge Kamba nyekundu kwenye madirisha ya mioyo yetu,maombi yetu kwa Bwana ni kumwambia Bwana *_Tunaomba Uvuli wa mkono wako utufunike na utuhifadhi katika nyakati mbaya_* Mungu ni mwaminifu atatuhifadhi,atatuficha,nyakati za Tauni,dhoruba,vitana njaaTutapita katikati yake na Kuvuka salama, *Unachotakiwa ni Kulisikia na Kuliamini Neno la Bwana* Ukiliamini kuna uponyaji na ushindi.
39 Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne. 
Yohana 11:39

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu? 
Yohana 11:40
👉👆Amini, Amini Ushindi Upo....Ingia kwenye maombi sasa sema na Mungu,haijalishi Kuna historia gani juu ya tatizo lako, wewe Amini tu.
*_Mungu akubariki,ulikuwa nami mnenaji wako Ev Elisha Kazimoto(0755444078)_*

Wednesday, 13 May 2020

MAVAZI NA MAPAMBO

👖🥻 *MAVAZI KWA WALOOKOKA LIMEKAAJE?*🥻👖
*_Mtu ameuliza swali katika group la whatsapp hili hapa,.....Wapendwa mie Nina swali kidogo kuhusu mavazi kwa mtu aliyeokoka, Avaeje,Mavazi yapi yanaruhusiwa kuvaliwa kwa mlokole?_*
..................................................
Anajibu Mtumishi wa Mungu *_Ev Elisha Kazimoto_* 
Whatsapp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
_Shalom wapendwa wote mnaoamini katika Neno la Mungu na katika Wokovu,huu mjadala wa Mavazi na Mapambo si waleo,unasumbua wengi sana vichwa,ila leo Sitatumia Andiko la Biblia ila nitakupa HEKIMA ZA ROHO MTAKATIFU kama msimamizi wa Mioyo yetu wanadamu hasa Tuliookoka_ Karibu tujifunze:
*MAVAZI,MAVAZI,MAVAZI*
👉Suala hili linawapa shida Wakristo wengi,ila ni walio wachanga kiroho,au ambao hawajaonja Utamu wa juu wa Mungu baba,lakini hili ni jambo Jepesi sana kwa mtu aliyeokoka ila kwa ambaye hajaokoka ni chamgamoto kubwa au kwa mchanga kiroho au kwa mtu ambaye amekoka sawa ila bado anakiwango cha kawaida sana.
*Nitawapa Siri moja na Wala usije ingia katika mijadala ya Mavazi ikakuumiza kichwa, wasaidie watu Wamjue Mungu kwa Viwango vya juu*
Utakuwa umemaliza ubishi na mijadala ya Mavazi na Mapambo.
👉Kwanza hakuna Vazi Maalumu lililoanishwa kwenye Biblia kuwa la Mtu aliyeokoka(kama ilivyo Kanzu kwa Waislamu au buibui)
👉Pili Tunatofautiana tamaduni kutoka jamii moja na nyingine kwa hiyo ni vigumu kuhukumu vazi husika.
*HIVYO BASI, UKWELI NI HUU*
👉Mungu anafanya kazi na watu NADHIFU(hiyo utaikuta kwenye Biblia)ndoa maana kufua mavazi,lugha za mavazi safi ziko nyingi kwenye Biblia.
👉Lakini pili, Mungu (Bwana Yesu)amejitambulisha ni Bwana wa Mabwana, Mfale wa Wafalme, Mtakatifu, Mungu wetu, Baba yetu kwa sifa hizo tu *Zinakupa Akili ya kujua mimi kama mtoto wake,mtumishi wake, NITOKE vipi kimwonekano ili KUMWAKILISHA katika sifa zake* 
👉Mfano mdogo tu, *_Tutashangaa na kubaki kujiuliza,na kulaani endapo tutamkuta mtoto wa Rais yuko rafu,amevaa ovyo ovyo,kwa nini itazua gumzo NI MTOTO WA NANI,ila akivaa mtoto wa mkulima au wa mtaani tutaona kawaida,ni mazingira yake_* Kwa hiyo sisi tukiookoka Tunaongozwa kimavazi na STATUS YA MUNGU WETU katika kuvaa.
👉Sasa itashangaza mtu Anahoji NIVAE VIPI WAKATI ANAJUA ANATOKEA FAMILIA IPI,NA WATU WANAITAZAMA NA KUITAFSIRI VIPI HIYO FAMILIA,tutakacho jua kwa mtu huyo ni HAJUI STATUS YA FAMILIA YAKE KWAKE NA MBELE ZA WATU. Kosa hajui status ya baba yake na cheo chake kwa watu na huyo ni MTOTO(Because hata mtoto wa rais wa mwaka 1,2 kukaa na Tope na mkojo ikulu au kwa watu aliko baba yake hataona shida maana hajui,mpaka walezi wamkamate na kumbadirisha mavazi ili afananie ufalme) na ndicho kinacho fanyika makanisani *Kukemea mavazi ya aina flani ni Kumshika mtoto mchanga mwenye mikojo atoke sebuleni arudi chumbani avae kulingana na hadhi ya baba yake ndo aje sebuleni(kanisani)*
👉Sasa Iko hivi,Ukisha okoka unapewa Roho mtakatifu,huyo *Atakufundisha kuvaa,kuongea,kufanya maamuzi yote* kuna mambo atakwambia hili HAPANA ulilifanya sawa ila kwa sasa NO haliendani na Hadhi ya Ufalme uliomo.
👉Mengine siyo dhambi ila atakwambia USIFANYE, Shida ya waliookoka UNA KIWANGO HICHO CHA KUMSIKILIZA ROHO MTAKATIFU NA KUMFUATA ANAVYO KUELEKEZA? Hapo ndo kuna shida.
👉 *Shida siyo kuambiwa Suruali kwa mwanamke ni ruksa au siyo ruksa,kusuka,kuvaa wigi au kuto vaa ni dhambi au siyo dhambi na mambo mengine yanayowachanganya watu makanisani na kuzua mijadala, Shida ni Hivi Umemjua Mungu wako aliyekuokoa kwa Kiasi gani* na Kiongozi uliyepewa Roho Mtakatifu unamtunza na kumsikiliza anavyokushauri?
👉Si kila jambo utakikuta kwenye Biblia unaambiwa Fanya au Usifanye, ndio maana tuliookaka tunasema Kumcha Bwana ni ZAIDI YA KUSHIKA AMRI 10,wokovu ni zaidi ya amri 10.Ukitembea na Amri 10 tu utakuwa mchanga kiroho mpaka unaingia kaburini na mbingu utaikosa ila shetani atakushinda.
NB: *_Ni hitimishe kwa kusema suala la mavazi na mapambo ukitaka kuliweka sawa iwe kanisani au maishani mwako,Fundisha watu au wewe jifunze, Ongeza Viwango vya Kumjua Mungu na Kumweshimu Mungu na Kumsikiliza Roho mtakatifu, Utavaa,utajipamba sawa sawa na Heshima ya ufalme wa Mungu na Hutahukumiwa na Mwanadamu wala Mungu na kwenye foleni ya kuhesabu namba kuingia mbinguni utakuwa front line_*
NI USHAURI WA KIUTUNISHI NA EV ELISHA KAZIMOTO
Whatsapp 0755444078