Friday, 23 November 2018

MWANA DINI NI NAREHEMU?

🖤🖤 *SINTOFAHAMU YA KUOANA NA MPAGANI, NA UKAKASI WA DINI/IMANI ZINAZO ZALISHA WATU NILIOWAITA KWENYE POST YANGU "MAREHEMU WANAOTEMBEA" UFAFANUZI WAKE KWA WALIOPATA UKAKASI*🖤🖤
............
............
_Ev Elisha Kazimoto(Mjumbe Mkali *Mithali 17:11*)WhatsApp 0755444078_
..................

👆👉 Sasa niweke sawa Kuhusu Imani,na wokovu na Maana halisi ya post ya Marehemu.

*MTU YEYOTE AMBAYE HAJAOKOKA(NI MTENDA DHAMBI NI MAREHEMU ANAYE TEMBEA) NA HUU NDO MSIMAMO WA NENO LA MUNGU,SIPINDISHI WALA KUPUNGUZA MAKALI MTU YEYOTE AMBAYE NAFSI YAKE INA HATIA JUU YA DHAMBI,UOVU,MATENDO ANAYO YA TENDA SI YA KUMPEMDEZA MUNGU,HAIJALISHI UPO DINI GANI WALA DHEHEBU GANI WEWE NI MAREHEMU UNAYE TEMBEA.*

1 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
Waefeso 2:1

2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;
Waefeso 2:2

3 ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine.
Waefeso 2:3
👆 *Wokovu Ni Badiriko la Moyo na Matendo* kinachofuata baada ya Badiriko la moyo na matendo ni Kupata watumishi sahihi/Mahala sahihi panapo Fundisha NENO LA MUNGU HALISI SIYO MAPOKEO na maneno ya wanadamu. Na hapa Haijalishi dini gani,dhehebu gani, Uzuri kweli,huwa inajitenga na uongo na Yesu alisha sema mtawatambua kwa matunda yao, SI LAZIMA NIKUBAINISHIE kuwa dhahebu hili ni sahihi ili si sahihi.....TUNAJUA TU KWA KUTUMIA NENO LA MUNGU,kuwa huu ni utapeli,haya ni mapokeo ya wanadamu siyo MAAGIZO ya Mungu, ili NI NENO LA MUNGU.

1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
1 Yohana 4:1

2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.
1 Yohana 4:2

3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
1 Yohana 4:3

👆Kwa hiyo imani yoyote tunaipima kama imekidhi matakwa ya Neno la Mungu, kama haikidhi matakwa ya Neno la Mungu, dhehebu hilo,imani hiyo, kanisa hilo, mchungaji huyo ANAZALIZA MAREHEMU WENGI WANAO TEMBEA.
Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.

Ufunuo wa Yohana 3:1
👆Hilo ndo neno la Bwana.
Uzuri neno la Bwana limejikamilisha,halina mapungufu lina COVER maeneo yote kwa kipimo sawa.

5 Kila neno la Mungu limehakikishwa; Yeye ni ngao yao wamwaminio.
Mithali 30:5

👆Neno la Mungu limehakikishwa tena ni safi, linafaa kwa mafundisho na kutengeneza watu Hai walio uhishwa na Kristo kwa kumwamini kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao.
6 Maneno ya Bwana ni maneno safi, Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; Iliyosafishwa mara saba.
Zaburi 12:6

👉👆 *DINI NI NJIA TU,* ila njia yaweza kukupeleka shimoni,au eneo unalotamani kwenda.(NENO DINI NI LA KIARABU MAANA YAKE NJIA)  umakini ni JE, NJIA HIYO INAKUPELEKA WAPI?

12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
Mithali 14:12

👆Suala hapa si kuangalia *Dini/Dhehebu langu limefananishwa na nini...... Suala ni NJIA YANGU NINAYOTEMBELEA INA VIGEZO VYA KUNIFIKISHA MBINGUNI*? Mimi liwe kanisa langu,dhehebu langu lifananishwe na nini, Hainihusu swala ni YESU WANGU AMEFANANISHWA NA NINI maana Yesu ndo Sura ya Uhai,dini hakuna uhai..... *DHEHEBU/DINI NISAWA NA MWILI WA MTU PASIPO ROHO* Huu mwili wangu ikiondoka Roho nitaitwa Marehemu, Roho ndo inanifanya niitwe EV ELISHA, vivyo hivyo DINI/DHEHEBU kama HAKUNA ROHO WA BWANA (ROHO MTAKATIFU-NA NENO LA MUNGU LILILO HAI)dini au dhehebu linabaki kuitwa KUSANYIKO MFU.

27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Yakobo 1:27

👆Kama njia(mtu)hajilindi na dunia PASIPO MAWAA(dhambi na uovu) hiyo dini(mtu)ni Marehemu.
*UKWELI NI HUU*
_Wale watu wa zamani kidogo kuanzia utawala wa mkapa mpaka nyerere,mmtajua jambo hili na ntaleta lecture kama 2 juu ya Imani,dini,wokovu...... MADHEHEBU KADHAA unayoyajua mengi yalikuwa HAYAAMINI KWA HABARI YA WOKOVU,NA MTU KUWA MTAKATIFU AKIWA DUNIANI LABDA AKISHA KUFA,ndo atatangazwa kuwa mtakatifu._ Sasa *Huu ni Utapeli wa shetani na Kwenda kintume na NENO LA MUNGU NA NDO UMAREHEMU UNAANZIA HAPO KUZALISHWA, kwakuwa wanakiuka andiko hili la Mungu anapendezwa na watakatifu WALIOPO DUNIANI siyo waliokufa*

3 Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Zaburi 16:3

👆Miaka ya hivi karibuni kuanzia miaka ya 2000 ndo kumeanza kushika kasi ya KILA MTU KUSEMA AMEOKOKA,KILA DINI,DHEHEBU KUSEMA NA SISI TUMEOKOKA, vikumdi vya UHAMSHO, vya kiinjili kuanzishwa na kuwa kanisa B ndani ya kanisa A..... Kumbe WOKOVU UPO, ningekuwa group la Be strong ningeeenda ndani zaidi na kutoa historia ya vikundi vyote na aababu ya kuanzishwa, dhehebu moja badala ya lingine,ila hapa na jibu hoja kwa jumla kuhusu KUOANA NA MAREHEMU(MPAGANI)....
*HOJA SIYO DHEHEBU WALA DINI, HOJA HAPA NI  2 TU*
1⃣Wewe mtu binafsi UMEOKOKA? Unaishi maisha MATAKATIFU? Nafsi yako haikupigii kelele kuwa wewe HAPANA NI TAPELI(unafanya hivi,hivi,hivi Mungu hapendi?)

3 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu.
1 Yohana 3:3

4 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.
1 Yohana 3:4

5 Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake.
1 Yohana 3:5

6 Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua.
1 Yohana 3:6

8 atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.
1 Yohana 3:8

9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
1 Yohana 3:9

10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
1 Yohana 3:10

20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.
1 Yohana 3:20

21 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu;
1 Yohana 3:21

👆👉Mistari muhimu ya mtu binafsi kujipima wala hapa uhitaji kuambiwa wewe ni MAREHEMU AU HAI,binafsi unajihukumu kwa NAFSI YAKO. Japo ukitaka kujitetea ili ujulikane umwema utazuga kwa watu lakini nafsi inasema wewe HAPANA HUJAOKOKA.
Ndo maana siku ya hukumu Mungu hatahitaji Shahidi kama mahakamani No unaye shahidi wako NAFSI YAKO inaongea kila te do,kila wazo,na kila njia yako.(sasa hapa haijalishi upo dhehebu gani wala dini gani) MAANA WENGI UKIKBILIA KUSEMA NA KWA WALOKOLE WAPO WATENDA DHAMBI WAKUBWA KULIKO WAPAGANI......Jibu jepesi sana nikweli kwani *Hata Yesu likuwa na wanafunzi 12 ila moja alikuwa Yuda msaliti na Yesu hakuwahi kusema si mwanafumzi wangu ila hakwenda mbali panga la haki lilimpitia,ila alionywa kila mara....Yesu alisema kati yenu mmoja atanisaliti* na ndicho kinahubiliwa huko kwa walokole ACHA DHAMBI wakusikia anasikia asiye sikia njia yake ni fupi.
2⃣Hoja ya pili ni *ALIYE MBELE YAKO,AU ENEO LAKO LA IBADA LINAIFUNDISHA KWELI? Lina kemea dhambi?lina imiza maisha matakatifu? Kama hayo hakuna linapita kwa mwaka mara 1 tayari unajua watu gani wanazalishwa. Maana kuna madhehebu mengine na imani nyingine.... Dhambi kwao siyo agenda,ndo maana mtu anaweza kwenda nyumba ya ibada akiwa na promise ya Ngono baada ya ibada,au anatoka ibada anapitia Bia na sigala,hawala nk, anaenda ibadani KUPUNGUZA DHAMBI, SIYO KUKUTANA NA MUNGU. 
👉Imani zingine zinaenda ibadani kupata nafasi ya kuzikwa atakapo kufa aombewe aende mbinguni siyo kuyaandaa maisha yake ya baadaye akiwa hai.....

27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;
Waebrania 9:27

👆Hilo andiko hawalisomi na hawalioni.
*SHIDA NI MOJA NA ITABIDI NIISHIE HAPA MAANA HUMU NI MAHUSIANO NA NDOA ILA KISAIKOLOJIA NAKIROHO*

_Watu wengi sana wakisha Penda wanahitaji na Mungu apende kama wanavyopenda,wanataka Mungu awafuate matakwa yao siyo wao wafuate mapenzi ya Mungu,ndo maana mtu anaweza sema SI NIKIOANA NA MPAGANI MIMI NAWEZA MBADIRISHA AKAOKOKA AKAMJUA MUNGU?_
*NOTE*. Msingi wa wokovu SIYO MAPENZI NI msimgi wa wokovu NI MOYO WA TOBA ULOTAMBUA HATIA YA DHABI NA UOVU, kumleta mtu wa Yesu kwa msingi wa mapenzi nisawa na KUMTUNUKU PhD kondakita wa gari akiyeishia darasa la 2 halafu ukaaza kujisifu kwamba huyu ni msomi hatari ana PhD ni mtaalamu wa uchumi huku ukijua wewe ndo umempa hiyo phd hewa.
Kwa Mungu hakunaga kufoji.

Shida ya pili watu wanahitaji wasikie maneno laini na ya uongo yakuwafurahisha siyo kweli inayo choma ili kubadirika.

9 Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya Bwana;
Isaya 30:9

10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo;
Isaya 30:10

👆👉Hii ndo shisa na kizazi cha sasa na kilichokuwepo tangu zamani.
...........
...........
*_Ev Elisha Kazimoto(Mjumbe Mkali -Mithali 17:11) WhatsApp 0755444078_*

WACHUMBA KUITANA MAJINA YA MAHABA

💝💝 *Swali: Jaman hivi ni sahihi kwa marafiki tu wa kawaida au wadada kuitana Honey,love,sweetheart, n.k mf unakuta mdada anamuita mkaka sweetheart sio mpenx wake wala nn, au anapewa au kafanyiwa kitu na mkaka anasema asante my love. Namm huwa napenda kweli kuita watu hvo*💝💝
............
............
_Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto(WhatsApp 0755444078)_
*MADA HII IPO KISAIKOLOJIA NA KIROHO*

_Kwanza tujue kitu kimoja jina lolote ni ANWANI ya mtu aitwaye,na niufafanuzi wa Hisia alizo nazo mtu juu ya mtu,mazingira au mapito_
👉Mtoto akizaliwa anapewa jina,watoa jina HAWAITI ILI MRADI JINA, wanakuwa *Wanamsukumo* aidha wa Shukrani kwa Mungu,Mapito magumu, muujiza,mahusiano mabaya ndo utasikia majina kama SIKUJUA,TABU, SHIDA, EBENEZA,SHANGWE nk..... Kwa maana hiyo USIDHARAU NGUVU YA JINA.
👉Biblia inasema heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi, kwa nini.... Kwa sababu *_Jina linabeba nguvu ya matendo utakayo tenda_*
👉Kwa nini mtu aitwe jina zuri afurahi, naaitwe jina baya achukie? Ni kwa sababu jina lina *Tibua Hisia*
👉👆Kwamaana hiyo kama jina linatibu hisia zinazotakiwa zitoe *Matendo sawasawa na jina likiloitwa* je,vijana kuitana majina ya *Kimahaba*(Mpenzi,mke wangu,Laazizi,)nk lina athari zozote.
👆👉Kumbuka Nguvu ya neno kwa maisha yako ni *Kuishi sawasawa na Maneno yako* Biblia imesema mwanadamu ATASHIBA mema ya matunda ya midomo yake.... Jina lolote unalimwita mwenzako naye kukuita linaunda BOND kwenye akili,inayoanza taratibu kufuta mipaka muhimu kati yenu, hisia za ukaribu zinatibuliwa,na mzizi wa urafiki ukomaa,namzizi huo unaweza pelekea kuwa huru nje ya mpaka wamahusiano yenu na mwisho LOLOTE LAWEZA TOKEA(Aidha kuanzisha mahusiano ambayo hayakutarajiwa,au sex ambayo haikutarajiwa.
*NB:* UTUMIAJI WA MAJINA katika mahusiano ufuata Levels of Intimacy ndomaana tuna jina kama jina la mtu,tuna jina la rafiki,tuna jina la mchumba mtarajiwa natuna jina la mke au mme.
Swali kwako, je ukimuita rafiki mpenzi,honey,sweetheart nk mmeo,mkeo utamwitaje.....?unaweza usione shida ila KISAIKOLOJIA umejipunguzia nguvu ya Hisia za kutofautisha mwenzi wako na rafiki yako wa karibu.

*UHURU WAKO wakutumiajina hilo ndo kipimo chako cha usalama wa kihisia*
NOTE: Kwa kawaida mtu anamwita jina mtu zuri,la mahaba kulinganana degrees za huyo mtu katika moyo wake na jina likikolea uendelea kupandisha degree kwenye moyo na hisia, sasa kama rafiki atachukua jina la *Mpenzi wa Moyo* na Mchumba wako au mmeo,mkeo atachukua degrees ngapi maana hatunaga *WAPENZI WA MOYO* tuna mpenzi wa moyo....Kisaijolojia...Ndo maana inashauliwa mwite mtu jina lenye mpaka wa kuhifadhi nafasi maalumuya mtu maalumu kwako.
*_Ni sawa na mtu hata akikuiendezaje,na akakuhudumia sana huwezi muita/kumpa jina la MUNGU WANGU, nafasi hii unaiacha kwa kuwa unajua huyu nikimpasifa na jina la Mungu na Mungu ntapa lipi_*
Weka mpaka ulinde nafasi ya hisia za mtu maalumu kwako.
   *Ev Elisha Kazimoto(WhatsApp 0755444078)*

VIPI KUMKISS MCHUMBA WAKO

😘😘 *Swali: Hivi ni sahihi kumkiss rafiki yako au mchumba?*😘😘
........
........
_Anajibu msaikolojia Ev Elisha Kazimoto(WhatsApp 0755444078)_

*MADA YA KIHISIA*
_kila tendo au neno linakuwa na msukumo wa Nia nyuma yake,suala hapa la kujiuliza ni KWA NINI UMKISS? hilo tu ukilijibu utajua ubaya na uzuri wa kiss_
👉Suala la msingi hapa ni Aina za Kiss na Lengo lake.
1⃣Kiss ya kumwansha hisia mwenzako tayari kwa kuitikia sex( Romance,kiss ya muda mrefu zero distance)
2⃣Kiss ya Chap chap ya salamu( cheek kiss)
3⃣Kiss ya deep love and Intimacy (confusing kiss) kwa paji la uso.
4⃣Kiss of special care(ya mkononi)
5⃣Sex Kiss( Romance + Zero distance Hug)
_Katika hali ya kawaida,wengi upenda kiss simple ila hujikuta wanaingia sex kiss_ ndio maana  wachumba au waba mahusiano wasiopebda kuanguka dhambini, wanashauliwa kuwa open kwenye nazingira,jana ni kiss usijifiche piga openly jwa ujasiri,usisubiri mkiwa wa 2 tu, mtaanguka.
*Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*

KUACHANA NA UMPENDAYE

🎁🎁 *Swali Muhimu la Kimahusiano:* _Hivi ufanye nini au utafanyaje kama mmependana na mtu(dada/kaka)mkiwa mnajiandaa kuanza michakato ya uchumba na ndoa, MUNGU akwambia HUYU SIYE MTU SAHII KWAKO muachane. *Unafanyaje*_🎁🎁
.......
.......
_Anajibu Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto(Whatsapp  0755444078)_

*Nihitimishe Mada hii kwa kusema mambo kama 3 hapa la kiroho na kisaikolojia na kimwili*
👉Kuanzisha mahusiano inaweza kuwa rahisi sana  maana unakuwa juu ya Hisia na nguvu ya furaha, ila kuvunja mahusiano ni kazi kubwa na gharama kubwa kwa maana *_Unakuwa chini ya Hisia na maumivu ya moyo_*
👉Kuanzisha mahusiano ni kujiongezea *Stability of mind* ila kuvunja mahusiano ni kujiongezea *Stress and Depression of heart*
👉Kwa msingi huo ni muhimu sana kutulia unapoenda kuanzisha mahusiano na mtu. Maana kuna kuhitimisha mahusiano kwa furaha( *Kuungana*) au kumaliza kwa Stress( *Kuacha au kuachwa*)
👉Katika mahusiano ni *Heri kuachwa kuliko Kuacha* anayeachwa anaulinzi wa kihisia, anayeacha anaongeza wingi wa wasiwasi kihisia.( _Anayeacha lazima aunde sababu za kutosheleza maamuzi yake ambazo baadaye kama si sahihi zaweza mgharimu katika mahusiano mengine au ndoa,ila anaye achwa anabaki na sababu moja tu nimesalitiwa nina haki_)
👉 *Nijibu swali sasa* Kumuacha mtu unaye mpenda ni kazi Kisaikolojia,ila kiroho ni kazi ndogo.
🥦Kama wote mliopendana mnamjua Mungu vizuri,haina sababu ya kuogopa ni kuitana mkakaa mkaambiana sisi tunapendana,ili tungie katika ndoa takatifu,na ndoa ni kusudi la Mungu,sasa kama *Hakuna amani kwa mmoja wetu,basi tujipe muda wa kuomba kuuliza amani hii inayopotea inamaanisha nini* wote mshugulikie hilo mpaka mpate jibu,ndo muagane kwa upendo na kuombeana kila mmoja Mungu ampe mtu wake.
🥦Suala la mtu mmoja kufanya maamuzi ya kuvunja mahusiano eti Kisa *SIJISIKII AMANI MOYONI JUU YA MAHUSIANO HAYA NI UTAPELI NA UHUNI MKUBWA* kwa nini? *_Wakati unaanza mahusiano hukulazimishwa, na pengine ulienda mbali na kusema Hakika nasikia Amani sana juu yako,nakupenda,nahisi hakuna mwingine kama wewe,namshukuru Mungu kunipa mtu kama wewe_* hayo yote uliyatoa kwenye Amani gani, ya nafsi yako,ya macho yako, au ya Kristo? Sasa kwakuwa ukimwaminisha mwenzako kuwa wa mpenda kwakuwa unaamani kuu Basi mkae tena muombe mdhibitishe hiyo hali ya amani kupotea
👉Maana kuna watu amani inapotea kwasababu zifuatazo:
🥦Walikurupuka kusema huyu ndiye kabla ya kujua Mungu karidhia au la( *Kwa tamaa zake*)
🥦Baada ya kuona Maslahi anayo tegemea huwenda hayatatimia akiwa na huyo( *Hofu ya maisha hasa kiuchumi*)
🥦Ushawishi wa marafiki,au wazazi kuhusu huyo mtu kuwa hakufai.
🥦Matarajio makubwa,lakini unaona madogo katika mahusiano
✍Kuanzisha mahusiano mapya kwa siri huku ukiwa na mtu mwingine( Huleta utata wa kujua nani ni chaguo sahihi...na lazima mmoja atavuta sana kuliko mwingine moyoni mwako)mmoja ataanza kupoteza sifa na amani juu yake itapotea.
*_Hayo mambo ndo watu uanza kusema sina Amani na mahusiano yetu,nakuanza kutafuta gia za kupiga chenga_* hapo si busara,busara kabla hamjaenda mbali,humtaki mtu mwambie mapema mkubaliane muachane kwa amani na si kiuadui.
👉Kuna wengine ambao Nature yao ni *_Ni ku hold wakaka au wadada tu,kula hela zao,muda wao,vitu vyao au kuwatumia kimwili,wakiwa hawana malengo nao, wakiona wenzao wamekazana,wanania ya Kuingia kwenye ndoa, ndipo huanza lugha za SINA AMANI MOYONI, wakiogopa hatua inayofuata ni Aidha kulipa mahari,kupelekwa kwa mchungaji au wazazi kutambulishwa,sasa anajiwahi kuvunja mahusiano kwa kisingizio cha sina Amani_* huu utapeli si mzuri.
🥦Rai yangu ya mwisho Kuvunja mahusiano si Ugomvi wala uadui,kama mlivyo toka out kuanzisha mahusiano,basi tokeni out mzungumze kuvunja mahusiano. Isipokuwa kwa mahusino ambayo huonyesha hati hati ya Revenge za ngono,huwa hayo tunashauri yavunjwe kimya kimya.
Mchambuzi na mshauri wa masuala ya mahusiano na ndoa
        *Mwanasaikolojia*
*Ev Elisha Kazimoto(Whatsapp  0755444078)*

Monday, 12 November 2018

WADADA WALIO ADIMU

🍇 *MWANA DADA ALIYESOKONI NA NI BIDHAA ADIMU*🍇🍇
_Huu ni Ujumbe wangu Mtumishi wa Mungu Ev Elisha Kazimoto na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa_
🍇Mdada aliyesokoni ni yule anaye *Jitambua kuwa ni Mdada wa Kutafutwa* hii Siri weeengi inawashinda Kabisa kabisa, wadada wanaingia kwenye nafasi ya *Kutafuta badala ya Kutafutwa* hapa unaweza maliza miongo hata 4, 4.5 huja fanikiwa kupata mme.
👉Mdada anayejua yeye ni Bidhaa Adimu inayotafutwa, *Anajipanga kutafutwa* anaishi maisha ya kutafutwa, na huyo akipatikana na watafutaji *Aachiwi,achezewi wana wahi kushugulikia hatua zote awe Queen of the house* aachwi muda wa uchumba, wala kuchezewa.
*_Sifa za Mdada Adimu aliyejipanga Kutafutwa_*
🎁Maisha yake Ameyawekeza Kwa Mungu. ( _Huyu ni mdada amchaye Bwana,anajikita na mambo ya Mungu, amejiapiza kuishi maisha matakatifu na kujitenga na dhambi, Ratiba zake nyingi ni za Kiroho, kusoma Biblia,Maombi,Ibada,Huduma na utumishi mwingine wa nyumba ya Mungu_) Binti huyo anatafutwa sana maana watafutaji wanajua moyo wa huyo unamilikiwa na Mungu,majanga hayatakuwepo kwenye ndoa.
🎁Hajirahisishi kwa wanaume,ila anawapima wanaume, ( _Hana pressure ya kuolewa kiasi kwamba kila kijana anayekuja anahisi ni mwokozi wake amekuja kumwondolea aibu...Ila yeye anapima huyu aliyekuja amekuja kwa Mkono wa Bwana au wa Tamaa zake au shetani ili kuniangusha?_)kama ni kwa mkono wa Bwana anaitafuta amani ya (Kristo na Kusudi la Mungu juu ya aliye kuja huku akiyasoma maisha ya kijana ni mtakatifu au ni
mwigizaji)
🎁Anaye jishugulisha kuyamudu maisha yake ili moyo wake usinaswe na watoa zawadi ili waharibu maisha ya wadada.( _Mdada wa aina hii hakai nyumbani na kusubiri wa kumbariki au kumpa vizawadi ndo atokelezee, hapa utakuwa na mahusiano hata 10 na utaanza utapeli. Mdada Adimu anasoma mazingira yake anaanza kujishugulisha na vitu vya kuingiza kipato hata kama ni kidogo lakini anauwezo wa kumudu mahitaji madogo madogo ya kila siku huyu dada anatafutwa sana maana atakuwa msaada wa familia akiolewa si Mzigo_)
🎁Kauli zake ni Kauli za Staha( _Mdada mwenye uwezo wa kukubali kwa adabu na kumkataa mtu kwa adabu ndo bidhaa adimu, wengi wanaponzwa na mdomo wanajifanya kuwa rohoni sana, kwa wale wasiowapenda wakiwa approach wanawajibu majibu ya mkato,ya dharau,ya matusi kiasi kwamba kijana anamshukuru Mungu kwa wewe kukataa maana kama una majibu mabovu hayo hujaolewa,ukiolewa mkakwazana ndo utatukana mpaka basi_) Kinywa chako kifanye kiwe na Nidhamu ya kupendeka.
🎁Mdada asiye tumia Mahusiano kama *Chanzo cha Mapato yake*( _Kuna wadada wanageuza mahusiano kama kitega uchumi au Saccos yao ya maendeleo, huwa wavulana wao hawawaambii ila wanaumia na wanawasema kwa wenzao kuwa mchumba wake *Ni Chuma Ulete* kila kitu,kila siku ni pesa,pesa....Jiulize kama usingekuwa kwenye mahusiano ungekuwa unatunzwa na nani? Lakini kuhudumiwa ni upendo wa kutoa kama zawadi siyo Madai, mdada ambaye anaweza kukaa kwenye mahusiano hadai kutunzwa,kuhudumiwa,mpaka mkaka mwenyewe ndo anaamua kukuhudumia,huwa wana sifa kubwa na si rahisi kuachwa,ila hata yeye mdada anaweza mtafutia zawadi mkaka wake hawa ni Adimu_) Wadada wengi ni Mchwa,wanakulaa wee ili wakiachwa waseme bora nilikula vitu vyake.
🎁Mdada anayechukia NGONO kabla ya ndoa( _Wadada wenye msimamo kwenye mahusiano ya kutovuliwa nguo,kunyonywa ndimi(Romance),kuchezewa mwili wao(sexual plays,kushikwa maziwa,sehemu za siri nk)mpaka unakuwa wet unatamani umalizie kabisa sex ila basi tu, mdada ambaye hata akitishiwa kuachwa kama hatakubali sex yuko tayari kuachwa, huyo mdada Ni bidhaa Adimu_) Wengi wa wadada wamejirahisisha sana mahusiano hayaishi,hawaingii kwa ndoa wakiwa na siri kwa wachumba zao,wanakuwa wamezoeleka miili yao si mara 1,4,10.
*_Hiyo ni Hekima zangu kwako dada, ukizingatia utatafutwa na ukipatikana uachwi njiani mpaka ndoa_*
       By Ev Elisha(whatsapp 0755444078)