*NI UTATA MTUPU*
(*_Ninaye Mpenda Hana Mpango na mimi, na Aliye na mpango na mimi Simpendi_*)
*_Ev. Elisha Kazimoto_*
*0755444078*
❤Miongoni mwa changamoto ya Kisaikolojia vijana wanayokutana nayo katika mchakato wao wa kutafuta wenzi wa maisha ni huu *Utata Mtupu*_Unaye Mpenda ndo kwanza Hana Mpango na Wewe, lakini Usiye Mpenda Ndo anampango mkubwa na wewe_,Nitachambua Utata huu kwa Mitazamo miwili, Mtazamo wa Kibiblia na Mtazamo wa Kisaikolojia.
❤Siku zote ndoa, Mapenzi, huambatana na Tabia zifuatazo;,
💍 *_Hisia kali ya Kupenda Sura, Umbo_* 💍 *_Makadirio ya uzuri wa kitu usicho kiona kwa kutumia taswira ya sura unayoiona_*
💍 *_Matarajio ya hali ya baadaye ya mtu huyo_*
💍 *_Shahuku ya kuwa katika Imaya ya mfumo wa maisha ya mtu huyo unavyo mwona_*
❤Sasa, Utata wa Kisaikolojia unakuja wapi kwa matazamio ya vijana juu ya wenzi wanao wahitaji?
❤ _Saikolojia ina falsafa hii, (Philosophy)isemayo_ *_Beauty is not up on the object, but on ones Eyes_* (_Uzuri haupo katika kitu, ila katika macho ya mtu) ndiyo maana unayesema mzuri wenzako wanaona kawaida sana au Hana Uzuri.
❤Utata huu wa Kisaikolojia umewafanya watu kuchelewa kuoa/kuolewa, au kuoana na mtu ambaye hakutarajia na hakutaka.
❤_Hapa vijana wa kike na kiume muwe makini sana, kwa kuwa unaweza kujiumiza sana, halafu mwisho wa maumivu huwa ni maamuzi yasiyo kidhi mahitaji ya kisaikolojia.
❤ *_Vijana wengi wakianza mchakato wa kutafuta wenzi, huorodhesha vigezo vingi bya mtu anaye muhitaji, na wengi huenda mbali sana kwa kuwa na msimamo usio badirika, wakihitaji vigezo vyote vitimie_* Lakini wanacho sahau katika vigezo alivyo weka inaweza isiwe rahisi kumpata mtu mwenye vyote, au Vigezo alivyo viweka kuna upande mwingine tofauti na yeye na yeye hawahitaji kuwa na mtu mwenye vigezo hivyo, hivyo kwa kishikiria vigezo vyote hivyo ana kinzana na mtu wake sahihi anaye mtafuta.
❤ Kuweka vigezo si mbaya, nikuweka dira ya kufikia malengo yako, lakini unahakika gani kuwa na wewe unafiti katika vigezo flani vya anaye kutafuta ambaye humjui?
❤👉�Baadhi ya vigezo vinavyo sumbua vijana;
💍 *_Awe beautiful /handsome wa ukweli_*
💍👉� *_Awe vizuri kiuchumi_*
💍👉� *_Awe mrefu, mrefu kiasi, mfupi, mfupi kiasi_*
💍👉� *_Awe ananizidi au namzidi Elimu_*
💍👉� *_Asiwe mfanyakazi kada ya Ualimu, Nesi, Askari, nk_*
💍👉� *_Asiwe anatoka familia maskini au yenye watu wengi_*
💍👉� *_Awe na nyumba au usafiri_*
💍👉� *_Awe Mkristo, mchungaji, mwimbaji, TAG, EAGT, EFATA, FPTC nk_*
❤Haya yote ni mazuri, ila wewe umejiuliza unavigezo gani? Vyote ulivyo ainisha unavyo? *_Sasa kama wewe huna vyote, hivyo umemwekea nani?_*
❤ _Ushauri wa Kisaikolojia hapa kwa vjina wa kiume na wakike, usikurupuke kusema *HUYU NO*, Kama hujafanya cross checking ya vigezo vyako watu wakiviainisha kama unauwezo wa kukubalika_
❤ Laini pia angalia katika vigezo ulivyo ainisha, aliye kuja, au unaye mwendea kama hana vyote, inaweza athiriaisha yako ya ndoa, au unaweza kufanya vizuri ila itahitaji kuongeza umakini kuiweka ndoa katika malengo yako? Fanya maamuzi.
*MTAZAMO WA KIBIBLIA*
❤ _Biblia inaweza kutupa majibu ya Utata huu_ ila majibu ya Biblia yanahitaji kutumiwa na mtu aliye na sifa hizi, ndo Biblia inaweza kukupa majibu, ya _Mtu usiye mpenda ndo anakuhitaji, na unaye mpenda hakuhitaji, ikageuza, Yule unaye mpenda hakupendi Akakupenda_
*Ayubu 42 : 2 - Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.*
👉�👆Makusudi ya Mungu hayazuiliwi kwa hisia za mtu za kisaikolojia. Ila kuyatimiza mapenzi ya Mungu katika kuoa na kuolewa uwe upo katika kona hizi:
1⃣ _Uwe upo vizuri na Mungu_
2⃣ _Uwe ni mtu wa kujituma kwenye mambo ya Mungu kwa bidii_
3⃣ _Uwe na tabia ya kumtegemea kumwamini Mungu katika mambo yako yote_
4⃣ _Mtazamo wako kwa ndoa uwe ni kwa faida ya ufalme wa Mungu na kwako_
5⃣ _Uwe unamjua Mungu kweli na unaweza kuyakubali mapenzi ya Mungu_
*Warumi 9 : 11 - *_(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye),_*
❤ _Katika kuhitimisha Utata huu, Sibkwamba huwezi kupata mtu wa vigezo vyako vyote, unaweza pata ila ni neema, lakini pia unapo kutana na Utata huu usiutolee Maamuzi ya haraka, inaweza kuwa unaye mpenda hakupendi si Wako, ndo maana Mungu haja mwekea Connection ya kuambatana na hisia zako, lakini huwenda unaye mpenda hakupendi, hawezi beba future yako ya ndoa unavyo tarajia, ndo maana Mungu hajaweka hali ya yeye akupende, lakini unaye mpenda hakupendo, ukilazimisha akupende kwa mbinu zako, ndani anaweza rudi katika hali yake ya mwanzo ya kutokupenda, utaumia zaidi ya ujana_
👉� *_Anaye kupenda humpendi, tafakari, ameona nini kwangu na yeye ana nini cha ziada, lakini nimi Mapenzi ya Mungu kwa huyu mtu_*
❤❤ Mwisho Lenga sana Kwanza kupata mtu aliye na Hofu ya Mungu❤❤
*_Ev. Elisha Kazimoto_*
*0755444078*
Thursday, 31 August 2017
NAMPENDA-HANIPENDI
Friday, 25 August 2017
KALAMU YA MWANDISHI
✍✍ *NGUVU YA KALAMU YA MWANDISHI*✍✍
Na Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp 0755444078
_Shalom mwana maombi,mtu ukiyejiweka tayari katika nafasi ya kushinda, leo katika mkesha wetu wa maombi,nakuletea ujumbe mfupi lakini wenye nguvu ya kubadiri mwelekeo wa maisha yako hadi uzeeni,na ndiyo operation yetu usiku wa leo, *Operation ya Kufuta maandishi dhaifu na kuandika upya Maandishi ya nguvu*_ utanielewa ninacho kwambia.
*_Zaburi 45 : 1 - Moyo wangu umefurika kwa neno jema, Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi._*
✍Umewahi kusikia,na kujiukiza kwa nini watawala hulia,au upigia kelele waandishi wa habari?
✍Umewahi kujiuliza hivi kwa nini watawala (Rais)wanapo teua mtu au kutengua watu,wanaita waandishi wa habari, au inatolewa barua yenye kichwa, *"Kwa Vyombo vya Habari* wanajua nguvu ya kalamu ya mwandishi.
✍Ndiyo maana kwa mtawala au mwanasiasa ukimnyima nguvu na nafasi katija Vyombo vya habari ni adhabu kubwa kwake,kuliko kumpuguzia mshahara.
✍Namaanisha wewe mtu wa Mungu ni mtawala( *Mwanzo 1:26-27, Ufunuo 5:9-10*) ila unahitaji nguvu ya Kalamu(Mamlaka ya Kristo katika ulimi)
✍Usiku wa leo,unapaswa kujua wako waandishi uchwara,kalamu za mtaani(wachawi,mapepo,watu wenye hila)waliandija na wanazidi kuandika mabaya katika maisha yako.
✍Na katika maisha yako,waloandika wameweka kichwa cha habari kikuubwa cha kuuzia gazeti la maisha yako,kwa mapepo,wanadamu nk,kichwa kisemacho, *Hawezi Kuolewa, Hata fanikiwa, Ni wa magonjwa, Ni wa migogoro katika ndoa au kazini, nk* vichwa vya habari vya maisha yako vimewavutia wachawi,watu,mapepo hata wewe kuendelea kuandika madhaifu katika maisha yalo.
✍Usiku wa leo katika operation yetu,tuna tumia mfuto wa Damu ya Yesu,tunafuta kauli zote,vichwa vya habari vyote viovu,vya kushindwa,kutofanikiwa,kutapata kazi,mme,mke nk na tunatumia Kalamu zetu,na kwa ustadi mkubwa tukiopewa na Bwana wa kuumba,yakaumbika.( *Mithali 18:21*),Futa maandishi ya wachawi,mapepo na watu wenye hila na andija Upya, na Upige Title kubwa, kama hii *WACHAWI HAMNIWEZI TENA, UMASKINI KWISHA, USHINDI LAZIMA,SIRUDI NYUMA NG'O* na zingine na zingine kwa kadri ya upako na ufunuo unao kushukia.
✍Halafu anza kuandika mema yote unayoishi,inabidi yasomeke katika maisha yako,kama mke,mmw,nyumba,usafiri,huduma kuu,kufauru masomo,andika,hayo uyaandikayo ndo yatakufanya uwe na level nyingine.
✍Kwenye maombi kawambie maadui,mliandika shida hizi kwangu,mkahisi hakuna wa kuzifuta?sasa Damu ya Yesu imefuta leo na sasa naanza kuandika upya kwa ustadi mafanikio yangu.
*_Kutoka 17 : 14 - Bwana akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu._*
✍Mara baada ya ujumbe huu wewe unaandika nini? Musa aliambiwa andika andika habari hii iwe ukumbusho jinsi maadui walivyokomeshwa mbele ya wana wa Mungu,ili maadui wafadhaike na wana wa Mungu watiwe nguvu.
_Mimi naanza kuandika sura mpya ya huduma,uchumi,ndoa ,kazi,maisha mengine, naamini nawewe unanafasi ya kuandika ili kila asomaye ajue kuna nguvu imewekezwa na haiporwi kirahisi._
WhatsApp 0755444078
*Ev Elisha Kazimoto*
Friday, 18 August 2017
TAA YAKO ISIZIMWE
🌳 *MAISHA YAKO YA KIROHO NA KIMWILI YANAHITAJI ULINZI MKUU NDO UFANIKIWE*🌳
*_By Ev Elisha Kazimoto_*
WhatsApp 0755444078
_Shalom watu wapendwao na Bwana,leo Bwana amenipa kitu cha kukuongezea katika maisha yako ya kivita katika ulimwengu wa roho. Watu wengi mambo yao yameshindikana,ndoa zimevurugika,wachumba wamekuacha kizembe,elimu imegoma,biashara imeingia hasara,kazini na mtaani unahisi upweke,kuchukiwa na kutengwa,kumbe kuna mchezo mchafu wachawi,maadui zako wanaufanya katika ulimwengu wa roho wa *Kuzima Taa zako* na katika ujumbe huu nakupakulia aina ya taa 4 inabidi uwe nazo makini zisizimwe ndo malengo yako yatatimia_
*_Kulinda Taa Yako Isizimwe na Wahuni_*
*Mathayo 6:22-23*
22 Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.
23 Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo!
✍Taa ni chanzo cha mwanga,unao saidia kuona pa kwenda au kukaa.
✍Maisha uliyo nayo,ni sawa na idadi ya taa zinazo waka au zilizo zimwa.
*2Samweli 21:15-17*
15 Basi kulikuwa na vita tena kati ya Wafilisti na Israeli; Daudi akashuka mpaka Gobu, na watumishi wake pamoja naye, akapigana na Wafilisti; naye Daudi akaishiwa na nguvu.
16 Naye Ishi-benobu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai, ambaye uzito wa mkuki wake ulikuwa shekeli mia tatu za shaba kwa uzani ,naye amejifungia upanga mpya,alijaribu kumwua Daudi.
17 Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti, akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli.
✍Adui anajua taa ikizimwa na uharibifu unaingia.
✍Adui anajua taa yako ikizimwa,uwezo wako wa kukwepa mishale yake ni mdogo na atakuweza.
✍Adui anajua taa yako ikizimwa,Malengo yako hayatimia na ndo kusudi la mchawi.
*Baadhi ya Taa za Mwanadamu*
*1.Kibali(Mithali 3:4-5)*
👉Kibali ni nguvu ya kukubalika(Mvuto kwa watu)/kwa Mungu
👉Mtu akikosa kibali mbele za Mungu na mbele za watu,hupelekea ukomo wa furaha yake na uwezo wa kufanikisha malengo yake.
*2.Heshima(Mithali 8:17-18,Yohana 12:26),*
👉Heshima ni Kustahilishwa, kuwa na nafasi ya upendeleo katikati ya wengine wanao mzunguka.
👉Mtu akiondolewa heshima na maadui,anadharauliwa na kuwekwa katika nafasi ya kupokea,kusikia na kuona mabaya.
*3.Utisho(Kutoka 23:27)*
👉Utisho ni nguvu ya kumdhohofisha aliye mbele yako,aidha akupishe,aachilie mbele yako alo navyo,au atende kwa hofu na unyenyekevu mbele yako.
👉Utisho unaambatana na Mamlaka ya kutoa amri na jambo likafanyika bila kupingwa.
👉Taa ya Utisho ikizimwa mtu anapoteza nguvu ya kutoa amri na ikatekelezwa, lakini hutopishwa na adui yiyote mbele yako,au kuachia vitu vyako
*4.Utofauti/Upekee (Waamuzi 16:17)*
👉Upekee(kuwa wa pekee), ni hali ya kukutofautisha kati yako na wengine.
👉Upekee ni nguvu inayodhihirisha uwezo wako ulivyo tofauti na wengine.
👉Taa ya upekee ikizimwa,hutaonekana umuhimu wako popote,maana huna tofauti na yeyote.
✍Hizo ndizo taa ambazo zinamfanya mwanadamu kuishi maisha ya amani kiroho na kimwili.,zikizimwa furaha kwisha,wokovu mzigo
*2Nyakati 29:5-7*
5 akawaambia, Nisikieni, enyi Walawi; jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu, mkautoe uchafu katika patakatifu.
6 Kwa maana baba zetu wameasi, na kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, Mungu wetu, wamemwacha, na kugeuzia mbali nyuso zao na makao ya Bwana, na kumpa maungo.
7 Tena wameifunga milango ya ukumbi, na kuzizima taa, wala hawakufukiza uvumba, wala hawakumtolea Mungu wa Israeli sadaka za kuteketezwa katika patakatifu.
✍Kuwa makini na wazima taa za ukumbini(moyo wako)
✍Hakikisha unatoa uchafu katika nyumba ya Bwana na uwashe taa.
✍Usikubali mtu mwingine(mchawi) akuambukize roho yake,tabia yake
✍Usiwe mtu wa kuiga matendo ya wahuni(wachawi/ya kichawi)taa yako isizimwe.
✍Ukigundua kuna baadhi ya taa zako hazina mwanga, tafuta watu walio sahihi kiroho wakusaidie kuwasha taa upya.
✍Wakimbie watu wote walio na taa hafifu,au zilizo zimwa, jiambatanishe na walio na taa zinazo waka.
✍Katika maombi yako omba sana,taa zako zisizimwe.
*_Imeandaliwa na Mtumishi wa Mungu Ev Elisha Kazimoto_*
WhatsApp 0755444078
Tuesday, 15 August 2017
KUSUA SUA KWA MAWASILIANO
*Swali la Mahusiano mtu ameuliza( Mdada)*
*_Hivi unaweza kukaa kwa muda gani bila kuchat na mpenzi wako(Mchumba wako)?_*
*_Mimi wa kwangu now yupo busy hakuna cha kuchat labda kameseji kamoja tu asubui na kengine usiku. Najisikia vibaya kwakweli, hii imekaaje naomba ushauri_* 😭😭
MAJIBU: NA MWANASAIKOLOJIA YA MAHUSIANO NA NDOA *_EV ELISHA KAZIMOTO_*
WhatsApp 0755444078
_Kuna mambo ambayo wana mahusiano mnahitaji kuyajua hasa mambo makuu mawili,nayo ntaya chambua hapa katika uchambuzi wangu, karibu tuanze sasa uchambuzi wetu_
1⃣ Siku zote wadada jueni ya kuwa love is two way traffic (ni njia mpeano)siyo kupokea tu. Na hiyo ni mpaka kwenye ndoa, ukishaona tayari tumependana au tumeoana anza kutoa na kupokea matendo ya upendo,kuwa mwanamke siyo kigezo cha kukaa na kusubiri utafutwe kwenye simu,utumiwe vocha,upewe zawadi,usifiwe.. Hapo unalazamisha kukaa stage 1 ya awali ya kutafutwa(hapa mmeisha ingia stage ya kupendana siyo kupendwa)na hili ndo kosa la kisaikolojia na kimantiki wadada na wanawake hukosea. Hata kwenye ndoa wanawake wengi wanasubiri waombwe sex, uliombwa honeymoon ukiwa mgeni,ukikaribishwa,basi saizi umeonja na wewe anza kuitaka upewe na yeye atake apewe ndo love hiyo ya watu wenye akili ya saikolojia ya mapenzi.
Sasa katika mahusiano,kijana alikuwa anajinyima,anawinda mpaka akakunasa,(yeye alikupenda)ila wewe hukumjua,hukumpenda ndo maana kila dakika,alikuwa akikuweka busy kimawasiliano,kizawadi, ili kujuleta karibu,ushibe matendo ya upendo na wewe umpende ili mpendane. Sasa mmeisha pendana wajibu wa kuwasiliana niwakila mmoja kumtafuta mwenzake muda wowote. Hata kijana anahitaji kuona hutu niliye mleta karibu kweli yupo karibu au bado yupo mbali? Usisubiri kutafutwa,mtafute,mpe maneno mazuri hata vocha na wewe mtumiepo mara moja moja(Love is Two Way Traffic )Mpeano. Ukisubiriwa mimi mdada nitafutwe tu,niambiwe maneno mazuri tu,asipi fanya unajiuliza eti mbona amebadilika? Jua amegundua pamoja na harakati za kukuleta karibu iki mfanane(mpendane hazijazaa matunda)bado anakupenda wewe imegoma kumpenda,kitakacho tokea ni KUKUACHA,atafute mwingine atakaye elewa Falsafa ya Mapenzi Kupeana siyo Kupokea tu.
_katika point ya kwanza nadhani wadada na wanawake mloolewa mmenielewa,usisubirie tu ufanyiwe(kama anaye tafutwa bado)kumbe ulisha kubaliana kuwa katika love naye au ndoa,peaneni matendo ya upendo,kama ni mawasiliano nawe mtafute kila ukimfikilia,akikuwahi sawa,ukimuwahi sawa_
*Ukipoteza wewe kwa ujinga na uzembe wanaokota wengine wenye njaa na akiki ya ziada ya kupet pet na hutompata tena,akiangukia mikononi mwa wajanja*
2⃣ Katika Point ya kuwa na mawasiliano hafifu katika mahusiano kwa kigezo cha UBIZE *_Nitoe Angalizo hapo_*
*_Ukiingia kwenye biashara ya Mahusiano(MAPENZI)Kumbuka simaanishi Ngono(Mapenzi ni Msamiati wa Kisaikolojia ulioshiba Hisia kali juu ya mwenza wako) ukiingia katika biashara ya mahusiano(Mapenzi)uwe una uhakika wa kulipa gharama ya ya vitu vifuatavyo._*
1.Gharama ya Muda, uwe unajua ya kuwa mwenzi wako anahitaji presence yako katika mawazo yake(hili ni janga la wana mahusiano) ( *_Mwenzako anahitaji Presence /Uwepo katika Akili yake muda mwingi_*) na hiyo ndo tafsiri ya upendo au mapenzi( ndo maana biblia inasema mpende Mungu wako kwa Akili yako yote, that means ndani ya akili yako iwepo presence ya Mungu. Huko ndo kumpenda Mungu.hivyo hivo hata katika mahusiano kama huna presence y mwenza wako akilini hakuna love hapo mnasindikizana muda wowote break up itatokea akipatikana wa kuweka presence yake sawasawa...
Na ni njia ya kuwasiliana mara kwa mara ndo inajenga presence yako kwenye akili yake. Kwa hiyo kwa vyovyote vile uwapo busy pata dakika chache iwe kwa sms,call,face to face za kuweka ku cement sura yako kwenye akili yake.
2.Gharama ya pesa, 3.gharama kuumizwa hizo sizielezei kwakuwa siyo topic yangu ya kujibu swali.
*NOTE* _Kama mtu anasema yuko busy hawezi hata kuku sms,call hata mara 3,4,5 kwa siku lakini mwanzo alikuwa ana call,sms hata mara 10,20 anza kumfatilia kwa umakini anaweza kuwa anajenga saikolojia yako ya kukuzoeza kuwa mbali naye iki siku atakapo kwambia Bye bye usiumie sana_ maana hakuna ubize saidi ya mwenzako. Love inatunzwa kwa mawasiliano ndo image yako inakaa kichwani mwake na kujenga nguvu ya uaminifu,furaha moyoni mwake juu yako.
*_So usidharau mabadiliko madogo madogo ya kisaikolojia katika mahusiano kama mawasiliano,zawadi,maneno mazuri yakianza kupungua_*
Mwisho, wana mahusiano lazima mfahamiane mazingira yenu ili kuepusha kuhisi tofauti( Psychological Confusion ) peaneni uhalisia wa ubize wenu ili muwe na muda maalumu wa kuongea,kuchati ambao ubize umeisha mpange mfano. Siku nzima mlo busy wote au mmoja yuko busy,basi saa 4-6 usiku,(mfano tu) tutaongea,chati tupeane ya kutwa nzima. Hiyo ndo akili ya mahusian. Siyo kusema upo busy tu, busy muda gani? 24hrs au? Labda hujapenda na kupendwa.
*T A K E C A R E*
*_Ulikuwa nami mchambuzi wa masuala ya mahusiano na ndoa Ev Elisha Kazimoto_*
WhatsApp 0755444078
Fb Elisha Kazimoto
IMANI KATIKA MAHUSIANO
*Swali*: _Kuna mkanganyiko wa dini,dhehebu na Imani, nani nioe au niolewe naye, je madhebubu ya Kikristo yote ni sawa?au kunatofauti?_
*Mchambuzi Ev Elisha Kazimoto*
_Labda niseme kwa mtazamo wa jumla tu kuhusu mambo ya ya imani,kwa kujibu swali ila uchambuzi wa kina kuhusu dini na madhebu na historia yake ni mada kubwa mno yenye nasomo marefu mno,ila kwa Summarization naweza kusema kwa ufupi kama ifuatavyo,hata bila ya maandiko,somo maalumu lina maandiko yakutosha_
Kuna vitu hivi vya kutofautisha,na vinatofautiana
1.Dini
2.Dhehebu
3.Imani.
4.Taratibu
👉Dini ni njia inayobeba mlengo wa mtu/kiongozi mwanzilishi(mfano. Ukristo -Yesu Kristo, Uislamu-Muhamad)hivo hivo,budha,hindu nk
👉Dhehebu matabaka ndani ya dini, yanayoanzisha kwa mlengo wa imani katika maandiko kadhaa kama msingi wa imani yao. Pia madhebubu yanaanzishwa kulingana na ongezeko la watumishi wenye maono mbali, na malengo ya kupanua huduma.( kwa makadirio duniani,Ukristo unamadhebu karibu 14000,na uislamu una madhebubu 7000)
👉Imani,ni msinamo wa dhehebu husika(na hiki ndo kiiini cha wokovu,mapokeo,upagani, na Ushetani)ndani ya dini,dhehebu....
Sasa,mfano. Kuna madhebubu ya Kikristo, yenye imani ya Kipentekoste yanayo amini katika misingi 17 ya Imani ya Kipentekoste ya wokovu(baadhi ya misingi ni, 1.Anguko la mwanadamu(kutenda dhambi na kufukuzwa edeni, 2.Ukombozi wa mwanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, 3.Kufa na kufufuka kwa Yesu,4.Ubatizo wa maji mengi,5.ujazo wa roho mtakatifu,6.Kuishi maisha matakatifu hapa duniani,7.unyakuo wa kanisa,na ujio wa Yesu kristo mara ya pili,8.Uwepo wa mbingu mpya na nchi mpya(maisha ya milele baada ya kufa),10.uwepo wa Jehanamu ya milele, 11.Uwepo wa Mungu mmoja aliye hai, 12. Utatu mtakatifu(Mungu baba,Mungu mwana na Mungu Roho mtakatifu )
Jamani hiyo ni kati ya misingi ya madhebubu ya Kipentekoste yote, kama TAG,EAGT,FPTC,CAG,FGBF(KAKOBE),.... Na baadhi Ministry
(Baadhi ya Ministry za Mitume na Manabii au Wachungaji zina imani ya kipentekoste ila wameingiza vitu vyao vyenye utata, kama mafuta,maji,vitambaa,kukanya watu,kuromance watu,deliverance kwa njia ya ngono, nk)
Baadhi ya madhebubu ya Kikristo, mfano Roman,Anglican,Lutheran Morovian,Sabato,Jesus only, Siloamu nk...misingi ya Imani yao imechanganyika, ya kimapokeo na ya kibiblia(mfano, ubatizo wa watoto, ibada ya sanamu, ibada ya wafu, kuimbea marehemu ahamishwe kutoka motoni kwenda mbinguni,kuokoka ni baada ya kufa,siyo duniani,tutaishi milele duniani hakuna kufa, Yesu alishindwa kazi Adamu Mnuo ndo kakamilisha kazi, hakuna utatu mtakatifu kuna Yesu tu),hakuna ujazo wa Roho mtakatifu,ubatizo hauna maana, kubatiza kuondoa dhambi ya asili,nk hizo ni imani zikizo nje ya Biblia, ni mapokeo ya ukengeufu na Upagani.
Sasa kila mmoja kwa dhehebu lake,imani yake ajipime je, Misingi ya Imani yake ipo katika Biblia au au ni mapokeo ya ubunifu wa wanadamu?
*_Kwa maelezo mafupi waweza tafakari mambo haya ya imani_*
Ev Elisha Kazimoto
Friday, 11 August 2017
UCHAWI UNAMEZWA
*Ev Elisha Kazimoto anakuletea Sehemu ya Somo la Uchawi Haujawahi Kushinda Nguvu ya Mungu*
WhatsApp 0755444078
*Uchawi* ni Nguvu za giza, zinazotumiwa na watu walioamua kumtumikia shetani katika sekta hiyo ya uchawi ili *_Kuua, Kudhohofisha,Kuharibu,na kupoteza mwelekeo wa maisha ya watu wasio na hatia na walio na hatia katika ufalme wa giza_*
Fuatana nami:
*Mtu mwenye Akili ndiye Mwenyekushinda Uchawi*
*Zaburi 14:2,Mithali 15:24,Mika 6:9,Mathayo 7:24*
_Nizungumzie mtu mwenye akili ndipo utajua kuwa kushinda na kushindwa kwako na wachawi ni matokeo ya uwezo wa Akili ya Kimungu aliyo nayo mtu. Na baada ya somo hili umuombe Mungu akuongezee Akili ya Kimungu upate kushinda_
👉(Mithali 15:24.... Inaongelea mtu mwenye akili njia ya uhai uenda juu,sikiliza, mchawi hawezi pambana na wewe ukiwa juu,yeye ni mtu wa ufalme wa chini,ili akushinde lazima apige akili yako urudi chini,ndo akabiliane na wewe) ukiwa na uwezo wa kukaa kiroho juu utawashinda maadui wote.
👉Mtu mwenye Akili ni mwenye uwezo mbele ya adui yake, hata adui anajua hakuwezi kirahisi.
👉Mtu mwenye Akili anauwezo wa kupambanua mitego na njia za adui(wachawi) na njia sahihi ya Mungu.
👉Mtu mwenye Akili maamuzi yake,matendo yake ni kwa faida ya ufalme wa Mungu na nafsi yake.
*_Tukiwa na Akili yaani Uwezo ya Kimungu uchawi utamezwa mbele yetu_*( KUTOKA 7:12)
_Hivi umewahi kutafakari pale Haruni alipotupa fimbo chini ikawa nyoka ,na wachawi wa Farao wakatupa fimbo zao chini zikawa nyoka,ila fimbo ya Haruni ikazimeza,ulisha waza Haruni alipo ichukua fimbo yake ilo kuwa nyoka,ikageuka kuwa fimbo Wachawi Walibaki na nini?_ Jibu jepesi; *Fimbo zao zilishamezwa,walibaki mikono mitupu,ila Haruni tu na fimbo yake*
👉Hapo ndo ujue uchawi mbele ya mwenye Akili(uwezo wa Kimungu )unamezwa halafu adui anabaki bila bila,mpaka anakuogopa.
*_Uwezo wa Kutambua,kupambanua unakufanya kuwa mtu hatari kwa Wachawi na adui yako anaye tumia mitego ya siri_*
( *1Samweli 18:20-28, Luka 12:54-57, 19:41-44*)
👉Ukiwa na uwezo wa kutambua mambo wewe si rahisi kutekwa na wachawi na kukuharibia mwelekeo wa maisha yako.
👉Njia anayoitumia adui kukunasa kwa hila,ukiwa mtu mwenye akili na mwepesi wa kutambua,hiyo hiyo njia ndo itatumika kukuletea ushindi na adui yako (mchawi kuaibika).
👉 _Lakini fahamu hili, Maamuzi yako na matendo yako,huwafanya watu,(Maadui na wenye haki)Kutambua kuwa ni Nguvu ipi,ya ufalme upi inatumiliki(1Smweli 18:28, Marko 8:31-33)_
*ANINA ZA WACHAWI NA UCHAWI WAO*
1⃣ Wachawi walogao kwa kutumia madawa *Mambo ya Walawi 19:26*
2⃣ Wachawi walogao kwa maneno(watu watumiao maneno kwa lengo la kuua,kudhohofisha,kuharibu na kupoteza mwelekeo wa maisha ya mtu) *Isaya 32:7-8*
3⃣ Wachawi(watu wenye roho ya kichawi,matendo ya kichawi)wakiwa na dawa au bila dawa. *1Samweli 18:10-11, Yoshua 9:4-17, Zaburi 10:7, 31:13, 36:3, Mithali 12:20*
4⃣ Wachawi walio tafuta uchawi kwa sababu zao za kulipa kisasi,au maangaiko kwa waganga wa kienyeji kutafuta majibu ya matatizo yao. *Kutoka 7:22, 2Mambo ya Nyakati 16:12,Isaya 19:3*
5⃣ Wachawi walio rithishwa na wazazi wao. Kila mzazi humrithisha mwanae vitu vyema au vibaya ili kuendeleza sifa ya mzazi, kwa faida ya mzazi au mtoto mwenyewe. *Kumbukumbu la Torati 21:15-17, Ayubu 13:26*
6⃣ Wachawi wanao tumikishwa na nguvu ya kichawi bila kujua(matokeo ya kutokaa katika nafasi ya kiroho sawa sawa, au kwakuwa rafiki na wachawi) *Isaya 14:3,1Wafalme 12:4,Wagalatia 4:3,Isaya 19:3*
_Hizo zote ni aina za wachawi wanao tumika kuharibu,kuua na kupoteza mweleo wa watu,kanisa,ndoa,kazi na elimu nk,ila ukiwa mtu mwenye akili na awezaye kutambua hao wote watamezwa mbele yako_
*SOMO KAMILI LINA KUJA*
Friday, 4 August 2017
UBIZE KATIKA MAHUSIANO
*Swali la Mahusiano mtu ameuliza( Mdada)*
*_Hivi unaweza kukaa kwa muda gani bila kuchat na mpenzi wako(Mchumba wako)?_*
*_Mimi wa kwangu now yupo busy hakuna cha kuchat labda kameseji kamoja tu asubui na kengine usiku. Najisikia vibaya kwakweli, hii imekaaje naomba ushauri_* 😭😭
MAJIBU: NA MWANASAIKOLOJIA YA MAHUSIANO NA NDOA *_EV ELISHA KAZIMOTO_*
WhatsApp 0755444078
_Kuna mambo ambayo wana mahusiano mnahitaji kuyajua hasa mambo makuu mawili,nayo ntaya chambua hapa katika uchambuzi wangu, karibu tuanze sasa uchambuzi wetu_
1⃣ Siku zote wadada jueni ya kuwa love is two way traffic (ni njia mpeano)siyo kupokea tu. Na hiyo ni mpaka kwenye ndoa, ukishaona tayari tumependana au tumeoana anza kutoa na kupokea matendo ya upendo,kuwa mwanamke siyo kigezo cha kukaa na kusubiri utafutwe kwenye simu,utumiwe vocha,upewe zawadi,usifiwe.. Hapo unalazamisha kukaa stage 1 ya awali ya kutafutwa(hapa mmeisha ingia stage ya kupendana siyo kupendwa)na hili ndo kosa la kisaikolojia na kimantiki wadada na wanawake hukosea. Hata kwenye ndoa wanawake wengi wanasubiri waombwe sex, uliombwa honeymoon ukiwa mgeni,ukikaribishwa,basi saizi umeonja na wewe anza kuitaka upewe na yeye atake apewe ndo love hiyo ya watu wenye akili ya saikolojia ya mapenzi.
Sasa katika mahusiano,kijana alikuwa anajinyima,anawinda mpaka akakunasa,(yeye alikupenda)ila wewe hukumjua,hukumpenda ndo maana kila dakika,alikuwa akikuweka busy kimawasiliano,kizawadi, ili kujuleta karibu,ushibe matendo ya upendo na wewe umpende ili mpendane. Sasa mmeisha pendana wajibu wa kuwasiliana niwakila mmoja kumtafuta mwenzake muda wowote. Hata kijana anahitaji kuona hutu niliye mleta karibu kweli yupo karibu au bado yupo mbali? Usisubiri kutafutwa,mtafute,mpe maneno mazuri hata vocha na wewe mtumiepo mara moja moja(Love is Two Way Traffic )Mpeano. Ukisubiriwa mimi mdada nitafutwe tu,niambiwe maneno mazuri tu,asipi fanya unajiuliza eti mbona amebadilika? Jua amegundua pamoja na harakati za kukuleta karibu iki mfanane(mpendane hazijazaa matunda)bado anakupenda wewe imegoma kumpenda,kitakacho tokea ni KUKUACHA,atafute mwingine atakaye elewa Falsafa ya Mapenzi Kupeana siyo Kupokea tu.
_katika point ya kwanza nadhani wadada na wanawake mloolewa mmenielewa,usisubirie tu ufanyiwe(kama anaye tafutwa bado)kumbe ulisha kubaliana kuwa katika love naye au ndoa,peaneni matendo ya upendo,kama ni mawasiliano nawe mtafute kila ukimfikilia,akikuwahi sawa,ukimuwahi sawa_
*Ukipoteza wewe kwa ujinga na uzembe wanaokota wengine wenye njaa na akiki ya ziada ya kupet pet na hutompata tena,akiangukia mikononi mwa wajanja*
2⃣ Katika Point ya kuwa na mawasiliano hafifu katika mahusiano kwa kigezo cha UBIZE *_Nitoe Angalizo hapo_*
*_Ukiingia kwenye biashara ya Mahusiano(MAPENZI)Kumbuka simaanishi Ngono(Mapenzi ni Msamiati wa Kisaikolojia ulioshiba Hisia kali juu ya mwenza wako) ukiingia katika biashara ya mahusiano(Mapenzi)uwe una uhakika wa kulipa gharama ya ya vitu vifuatavyo._*
1.Gharama ya Muda, uwe unajua ya kuwa mwenzi wako anahitaji presence yako katika mawazo yake(hili ni janga la wana mahusiano) ( *_Mwenzako anahitaji Presence /Uwepo katika Akili yake muda mwingi_*) na hiyo ndo tafsiri ya upendo au mapenzi( ndo maana biblia inasema mpende Mungu wako kwa Akili yako yote, that means ndani ya akili yako iwepo presence ya Mungu. Huko ndo kumpenda Mungu.hivyo hivo hata katika mahusiano kama huna presence y mwenza wako akilini hakuna love hapo mnasindikizana muda wowote break up itatokea akipatikana wa kuweka presence yake sawasawa...
Na ni njia ya kuwasiliana mara kwa mara ndo inajenga presence yako kwenye akili yake. Kwa hiyo kwa vyovyote vile uwapo busy pata dakika chache iwe kwa sms,call,face to face za kuweka ku cement sura yako kwenye akili yake.
2.Gharama ya pesa, 3.gharama kuumizwa hizo sizielezei kwakuwa siyo topic yangu ya kujibu swali.
*NOTE* _Kama mtu anasema yuko busy hawezi hata kuku sms,call hata mara 3,4,5 kwa siku lakini mwanzo alikuwa ana call,sms hata mara 10,20 anza kumfatilia kwa umakini anaweza kuwa anajenga saikolojia yako ya kukuzoeza kuwa mbali naye iki siku atakapo kwambia Bye bye usiumie sana_ maana hakuna ubize saidi ya mwenzako. Love inatunzwa kwa mawasiliano ndo image yako inakaa kichwani mwake na kujenga nguvu ya uaminifu,furaha moyoni mwake juu yako.
*_So usidharau mabadiliko madogo madogo ya kisaikolojia katika mahusiano kama mawasiliano,zawadi,maneno mazuri yakianza kupungua_*
Mwisho, wana mahusiano lazima mfahamiane mazingira yenu ili kuepusha kuhisi tofauti( Psychological Confusion ) peaneni uhalisia wa ubize wenu ili muwe na muda maalumu wa kuongea,kuchati ambao ubize umeisha mpange mfano. Siku nzima mlo busy wote au mmoja yuko busy,basi saa 4-6 usiku,(mfano tu) tutaongea,chati tupeane ya kutwa nzima. Hiyo ndo akili ya mahusian. Siyo kusema upo busy tu, busy muda gani? 24hrs au? Labda hujapenda na kupendwa.
*T A K E C A R E*
*_Ulikuwa nami mchambuzi wa masuala ya mahusiano na ndoa Ev Elisha Kazimoto_*
WhatsApp 0755444078
Fb Elisha Kazimoto