Sunday, 10 December 2017

MPASUKO WA NDOA

💔💔 *MWANZO WA MPASUKO KATIKA NDOA*💔💔
*_Lecture from Material Adimu University(Group)_*
*Ev Elisha Kazimoto(Psychologist & Counselor)*
WhatsApp 0755444078
_Shalom mwana darasa na mwana ndoa uliye nje ya darasa la chuo hiki cha mtandaoni kinacho kokotoa masuala ya Mahusiano kwa vijana na NDOA, hii ni miongoni mwa Lecture katika chuo hiki chini ya mchambuzi wa masuala ya mahusiano na ndoa Ev Elisha Kazimoto, karibu uongeze maarifa kuhusu *Viashiria vya mwanzo wa mpasuko katika ndoa* uwe makini katika ndoa yako_
❣Kwanza kabisa kabla ya kujua mwanzo wa mpasuko wa ndoa inabidi ujue dhana ya ndoa ndo utajua kwa nini mpasuko utokea. *_"Wakati unafunga ndoa mlifungishwa ndoa watu wawili wewe na mmeo /mkeo,waliowekewa pete 💍💍 ni ninyi wawili,mlokuwa mnashangiliwa ni ninyi wawili,mliopewa zawadi ni ninyi wawili,mlopelekwa Honeymoon/nyumbani baada ya harusi ni ninyi wawili, mlofunguliana nguo na kujuana miili yenu na kushiriki tendo la ndoa ni ninyi wawili, watu wengine wooote, wachungaji,mitume,manabii,wainjilisti,marafiki,wazazi,ndugu na majirani waliishia kuwatazama,nakuwatakieni maisha mema na wengi waliishia ukumbini au sebuleni na kama kuna yeyote alifanikiwa kufika chumbani kwenu ni siku hiyo tu hapamuhusu tena..."_* hiyo ndo dhana ya ndoa uliyoingia inakuonyesha wahusika wa raha na taabu ni ninyi wawili tu na Mungu wenu.
❣Ndoa inakuwa tamu na raha endapo wawili wanaweza kukabiliana na changamoto za maisha kama watu wawili na Mungu wao.
❣Ndoa yako inakuwa na heshima,na mwenzako umamuona wa maana pale kukiwa na USIRI wa maisha yenu ya ndoa,raha na changamoto zenu mzijue ninyi na mzishugulikie ninyi, hapo ( *_hakuna mzazi,ndugu,mchungaji wala shemasi wala mtume na nabii_*)ni ninyi wawili tu,hapo ndoa yenu itaenda miongo mingi kwa utulivu na upendo na furaha.
❣Ndoa ina utamu kama hutatengeneza mazingira ya kuichoka na ukajua namna ya kushughulikia vyanzo vya mpasuko.
*_Sasa baada ya kuiangalia dhana ya ndoa katika kuwepo kwake,nikupeleke katika mazingira yanayoweza kuipasua ndoa yako Kisaikolojia, kiroho mpaka kimwili_* ukiyajua hayo utailinda ndoa yako.
👉Kwanza inabidi ujue mpasuko wa ndoa kisaikolojia tunasema unaanzia Katika Saikolojia(Akili/Hisia) ndo utaona unatokea mpasuko wa kiroho(kuacha wokovu au kuanguka dhambini)na kumalizikia kimwili kutengana kabisa(Divorce)💔kuachana. Lakini mpasuko huu usababishwa na matendo ya kisaikolojia (kihisia kuingia dosari) fuatana nami ujue kona hizi;
💔 *Kona ya kwanza ya Mpasuko Kumuona wa kawaida sana mmeo/mkeo* Wanasaikolojia tukisemaga mambo haya madogo watu huyaona yakawaida sana maana walitegemea yasemwe makuubwa,kumbe ndoa haibomolewi kwa kuwa mwanaume hujajenga nyumba,kununua gari,huna pesa za matumuzi ya familia,hivyo ni vitu vya nje vya hitimisho la vidogo vya kihisia. SIKILIZA....
👆👉Miongoni mwa ngome ya hisia inayo linda mahusiano ya ndoa ni kulinda *Upekee wa huyo uliye mchagua* yaani maamuzi ya kuoana na huyo ukawaacha wadada wote,vijana wote ukaambata na huyo kisaikolojia iliashiria huyo ni *Unique*(sio wa kawaida) sasa kuna mambo ukiyafanya kwake,uliongea kwake mpaka akaona unafaa,yakianza kubadirika,maana yake unafuta upekee na kuweka ukawaida utakao pasua hisia zako kwake,na hisia zikiisha pasuka💔ndoa hiyo inaanza safari ya kuelekea kaburini.
👉 *Utajuaje mwenzako anaanza kufuta upekee wako na kukuweka katika ukawaida utakao pelekea ndoa kupasuka?*
1⃣Kuna lugha hakuwai kukuambia sasaivi anakuambia.( kuna lugha ngumu ambazo kabisa msemaji anajua hii itamchana moyo,itamtoa machozi,itamfikirisha lakini itamfanya ajione duni UKITAMKIWA) Mfano: _Wanaume huwa mko wa ovyo, wanawake hamnaga akili, kwenu ninyi ni watu wa ajabu, huna pa kwenda wewe nikikuacha,sioni faida yako au umuhimu wako humu kwangu,nilikosea kuoa,kuolewa, laiti ningejua nk,nk_ lugha hizo ukianza kuzisikia jua ni mwanzo wa kuondolewa kwenye umaalumu(upekee na kuwa wa kawaida)na zikizoeleka masikioni mwako saikolojia ya mpasuko wa ndoa itachukua nafasi kupelekea mpasuko wa kimwili na kiroho kwa waliookoka(kuachana na kuanguka dhambini) kwa watu wa kawaida Usaliti na visasi vitachukua nafasi mpaka hapo ndoa hakuna tena.
2⃣Ulikuwa unashirikishwa mambo ya mipango mbalimbali ya familia,kwa sasa unashtukia hili limefanyika,unaambulia kupewa taarifa ya yaliyo tekelezwa au unayaona yamefanyika ila huna maelezo yake. ( _Mpaka hapo jua nimeisha kuwa wa kawaida,sina umaalumu tena niliokuwa nao naulizwa kwanza,iki kikoje,nifanyeje hapa,unaonaje hakuna tena)jiandae kisaikolojia muda unavyozidi kwenda mtaachana msipo chukua hatua za dhati.
3⃣Ulikuwa ukimkosea mwenzako au akikukosea,haraka sana unasema samahani,au unaombwa samahani, ila sasa kimya kimya,ukilalamika unapewa majibu makali na magumu. ( _Msamaha ukishaanza kuwa mgumu kuombwa au kutolewa jua umekuwa wa kawaida,wewe na makosa au maumivu ni haki yako kukaa nayo_) ndoa hiyo inajiandaa kupasuka.
💔 *Kona ya Pili ni Kupeleka kesi ya ninyi wawili kwa mtu wa tatu yeyote awasuruhishe* Kisaikolojia hatuamini na ndivyo ilivyo mtu wa tatu kuwaletea amani na maelewano yenu wawili, haitatokea na haipo,kinacho fanyika pale mmejichezea saikolojia zenu kuzivisha hofu ya watu ila mgogoro wa nafsi uko pale pale na unakua taratibu. *_Na ndiyo maana uliza,fanya uchunguzi wana ndoa walioshitakiana kwa kosa moja,ndo ulikuwa mwanzo wa kesi ya pili,ya tatu,nakuendelea hata mkikaa miaka 10 bila kushitakiana,lazima ufa mliouwela utaibua shitaka lingine hata kama mna miaka 50 katika ndoa mtashitakiana tena_*) hakunaga msuluhishi wa hisia,kuna msuluhishi wa maslai(pesa,chalula,mavazi,maendeleo nk)ila hisia msuhishi huwa ni nafsi yako tu,uigeuze iamini kile unachotaka kukiamini. ( *_Narudia tena,ukiktaka kukomaa kisaikolojia katija mahusiano ya ndoa, Mzazi,Mchungaji wako,ndugu na rafiki Hatokupa majibu ya kuponya HISIA ndoa ni hisia siyo vitu,ninyi wawili kwa changamoto yoyote,tatizo la mwenzako kero IMALIZE WEWE NA YEYE bora ikuchukue hata miezi,siku na masaa ila muimalize ninyi_*)Uliyezoea kushitaki shitaki kila mkihitirafiana na mwenzako ndoa ya utulivu na amani hutoipata,ila utakuwa na vipindi vya mapumziko ya migogoro ila siyo suluhisho la migogoro. Ambaye hujawai mshitaki mwenzio omba na hakikisha hauanzishi safari isiyo isha ya migogoro na mashitaka.
👆👉 _Hata ofisi zetu za wanasaikoloji(Counselors hatutatui migogoro yako,ila uzuri na ubora wa wataalamu Nikukupa maarifa,mbinu wewe binafsi uende ufanye marekebisho ya makosa na hitirafu tunazo kuonyesha,hapo unaufuta mgogoro wote._)
💔 ​Kugomea tendo la ndoa au kushiriki kwa masharti​ Hapa kuna hitirafu nyingi,kwakuwa ni tatizo ndani ya tatizo, yaani tendo la ndoa ni la Hisia halafu lipo katika kuharibu hisia,mpaka mfanye tendo la ndoa kunahitaji kutengeneza mazingira ya utulivu wa akili,inayoshawishi kuibua hisia za kuhitajiana kimwili, sasa ikitokea mambo yaumizayo yanaanza kujengwa katika moyo wa mtu uua hisia,kuhitaji tendo la ndoa kunaanza kuwa kugumu,ikifikia hatua mnaona ugumu wa kushiriki tendo la ndoa,mwaweza pitisha wiki,1,3,5,miezi mpasuko wa kisaikolojia tayari upo unafuata wa kimwili. ( _Hakikisha unaepuka maneno,lugha,matendo na mazingira ya kuua hisia zako na za mwenzako,ili muendelee kushiri tendo la ndoa kwa amani na Uhuru kwakuwa tendo la ndoa linawaunganisha kihisia na kuwaunga pamoja kimwili na kisaikolojia na kuchochea upendo kati yenu_)
❣❣ *_Hii ni lecture ya kwanza usikose mfululizo wa lecture hizi katika chuo chetu cha Material Adimu cha mtandaoni,tumalenga kuimalisha Mahusiano ya vijana na mahusiano ya ndoa Kiroho na Kisaikolojia, tumepanua wigo wa kusaidia watu bapo tuna pia Darasa la Tiba ya Kisaikolojia kwa mahusiano na ndoa( Psychological Healing Class, Nitalinda Ndoa yangu, Paradise University)hayo ni baadhi ya magroup yaliyo branch ya chuo hiki. Kutana na Mwanasaikolojia Ev Elisha Kazimoto(Group Admin and founder)katika madarasa yote hayo upate kupona._*
WhatsApp 0755444078
Fb Elisha Kazimoto
Instagram Elisha Kazimoto
Twitter kazimoto_elisha(Elisha kazimoto)
Blog Materialadimuuniversity2017
Google Andika MATERIAL ADIMU utakutana na masomo mengi kwenye blog.
*_Mahusiano na ndoa havina mzoefu na mkongwe vinahitaji kila siku uongeze Maarifa mapya_*
@Ev Elisha Kazimoto(Baba Evan)

Sunday, 26 November 2017

SWALI: STYLE ZA SEX NANI AANZISHE

Swali: *Hivi ni vibaya mwanamke kuanzisha style mpya ya sex kwa mume wake? Au anatakiwa atumie mbinu gan kuianzisha?*

Anajibu: Ev Elisha Kazimoto(Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na ndoa)
WhatsApp 0755444078
_Kwanza Ndoa ni uwanja wa watu wawiliwa amani,furaha na upendo na uhuru, mwana ndoa anahitaji kuwa huru kwa mwenzake,na kila linalofanyika ni la kwenu wawili, sasa maudhui ya umoja wa wana ndoa yakibadirika ndoa inakuwa chungu,na ndoa ikiingiwa tu na mdudu uwezekano wa kwenda mbinguni,unaanza kuwa mdogo_
👉 Kweli ni kwamba ndoa ni mlango, ni chombo kizuri cha usafiri kwenda mbi guni au jehanamu, ambao hamjaoa au kuolewa, kwenye ndoa hupaswi kuishi katika ndoa kwa kujikaza au kiugumu, jua mbingu una asilimia 10 kati ua 100 kuiona. Ndiyo maana tunawashauri vijana usiingie kwa ndoa kutafuta sex, tafuta kusudi la Mungu, usitamfute mtu wa mitoko na kukidhi mahitaji ya kiuchumi, tafuta na omba mtu atakaye kusogeza karibu na Mungu na kukufanya utimize kusudi la Mungu.
👉Unapo kwenda kuoa au kuolewa jua ndoa yaweza kuwa ngumu au nzuri(nyepesi)kutokana na aina ya ndoa utakayo chagua kuishi.
Kuna aina 3 za ndoa, *Moja , Ndoa ya Kirafiki, pili Ndoa ya Kitoto, tatu Ndoa ya kibosi* wengi hasa wasiopenda kujifunza na hasa walokole(siwasemi vibaya maana miongoni mwa walokole mimi ni namba moja najivunia neema hii) ila wengi wao maarifa ya kidunia wameyatupilia mbali kwa kisingizio cha wanajua tu maarifa ya biblia nayo hawako vizuri,kwa hiyo kote hawako vizuri ndo maana ndoa zinakuwa ngumu sana wengi wao wana ndoa za KIBOSI hapo ni amri,uchifu, nk lakini ndoa ya kitoto ni kucheza na kufurahi na kusameana,ndoa ya kirafiki ni kusaidiana ka hivyo ku mshave mwenzako,kumuogesha,kusaidiana vikazi vya haoa na pale kwa upe do si kwa kuagizana.
Kuna kawimbi ka wahuni wa imani, kutafuta namna gani ya kutengeneza vitisho kwa watu,au tofauti ya imani nawe uwe ni mwana imani iliyo tofauti na wengine,bila kuzingatia neno la Mungu na Nature of Creation.(  _Wanasema wana ndo kufanya tendo la ndoa kwa style mbalimbali ni dhambi, ni style moja tu ya chali mama baba juu ndo takatifu_) Huu niuhuni mkubwa wa kiroho.
Mungu alipotuumba alitupa intelligence(Akili) . Sasa imani ya style hii takatifu na hii dhambi ni mavumbuzi ya wanadamu,Ukisema neno dhambi ni Katazo la Kimungu. Sasa sijawahi soma aina ya style kwenye biblia, ila intelligence ya uumbaji inatusaidia  kutafuta pozi zuri la kufurahia sex. Kwani nani alikupa agizo la ukilala ulalie mkono wa kulia au kushoto,au chali...kwa nini huwa unajigeuza ukilala? Ni katika kutafuta pozi la kuenjoy usingizi alotuumbia Mungu hivyo hivyo na styyle za sex.
Zipo zaidi ya style 100 za sex ila nyepesi 15,inategemea na flexibility ya miili yenu wotw wawili.
NB: *_Kilicho marufuku na dhambi kwa raha zenu zoote,kwa mifumo yenu yote, style zenu zote msifanye machukizo ya kuingiliana kinyume na maumbile(msibadiri matumizi ya asili ya mwanamke au mwanamme)neno limesema hivyo._*
👉Kwa suala la nani wa kuanzisha zoezi la kunlbadiri style kati ya mwanamke au mwanamme ni yeyote ila Kisaikolojia, kabla ya tendo la ndoa mwanamke anakuwa na aibu, na akili inashuka, wakati huo mwanaume hana aibu,aikili inachaji asilimia mia, sex ikianza in and out...mwanaume anapoteza akili(akili inashuka) mwanamke ujasiri unaongezeka na akili inaongezeka, na controller wa game ni mwanamke ... Shida maarifa kwa wana ndoa zero,hakuna watu wa kujitoa muhanga ku calculate mambo ya mahusiano kwa kina, tunaishia kufundishana kanisani MSINYIMANE,MTII MMEO NA MPENDE MKEO semina zote. Hii ndo Shida .Uliza wana ndoa wenye umri miaka 15 mpaka 50 kwenye ndoa, usikie haya tunayo fundisha na kufundishwa kizazi hiki kama wao waliyapata. Kwanza  kujadiri mambo haya ya sex enzi hizo ni dhambi kubwa,ukiyasikia unaingia maombi ya kufunga siku 3 kujitakasa. Mmmh shida kweli. Ndoa zilitembelea kwenye neema ya Mungu tu 100% bila maarifa mengine, sasa dunia ya sasa siku za mwisho maarifa yameongezeka,usipo kuwa nayo ndoa utaichukia.
👉Tendo la ndoa lina nogeshwa na vitu vingi tangu kuandaliwa na wakati linafanyika. Vitu kama kiss,romance,sex play nk.
Nijambo la kushangaza kukwepa romance ya mke wako au mmeo, moja ni dalili ya kutokomaa kisaikolojia katika ndoa, lakini kuna mambo ya msingi kwa wana ndoa kuyaweka vizuri, USAFI WA KINYWA, ili usiwe kero kwa mwenzako harufu mbaya. Pili busu haiwi ya fujo, iwe ya kitaratiibu,yakimahaba, iwe na maandalizi ya gentle touching,sex touch & sex play ndo romance inakuja automatically, siyo unavamia kichwa cha ntu na kuromance.
👉 Ndoa nyingi watu wanaishi kwa fujo kukuru kakara, hawana vionjo vipya,hawajui jipya,hilo hilo waliloanza nalo mpaka kuzeeka ndo hilo,mpaka ndoa inachosha, kazi za walimu,wasomi na watumishi wahubiri kunusurisha ndoa za wana wa Mungu kwa kufundisha kwa kina.
👉 *_Sasa tuhitimishe hii topic hivi, Tendo la ndoa kwa wana ndoa kwanza ni Huru, ni la raha,si la kulazimishana, siyo la kuibiana ni suala la makubaliano baina ya watu wawili, linahitaji kugusa feelings,kuongea kuhusu hisia zako kwa mwenzako, unataka akufanyie nini,ashike wapi, akaeje, tendo la ndoa halifanywi kibubu, gizani,ghafla linahitaji maandalizi ya kisaikolojia na kimwili,hakuna mwenye hati miliki ya tendo kuliko mwenzake wote mnapaswa kufurahia na kufikishana kwenye kilele cha raha_*

Kwa wakati wa tendo ongeeni raha unayo ihisi,unatamani uhisi nini zaidi,sema na mwenzako tukae hivi sasa,muulize mkao huo anahisi raha au kuchoka na kuumia,hapa ni mtu yeyote kuongea.
Shida watu tangu siku ya kwanza ya ndoa sex ni kifo cha mende,mpaka first born,2,5,.   Huu ni ushamba na kuchokesha ndoa na miili yenu.
Wana ndoa wengi wanafanya tendo la ndoa kama WAJIBU ,au kutimiza hisia zao ila si kama ENJOYMENT.

Badirika usiwe Regidy,Static, conservative utamchoka mwenzako.
*_By Ev Elisha Kazimoto_*
WhatsApp 0755444078

Friday, 10 November 2017

UZUSHI KATIKA UCHUMBA

MADA SWALI

...hivi upo ktk mahusiano na mtu mmoja tu lakin ikatokea habari zinazoeneaenea kidogo kuwa u mzinzi upo na mahusiano na waschana wanne na huyo mmoja wa ukweli akiwemo!! Ukizingatia wewe ni mtu mwenye wadhifa Fulani wa kiongoz ktk kanisa,na wapo wanaokuamin na kukuheshimu sana!! Na yule Mwenzako wa ukweli yeye anaelewa na anakuamin sana kuwa u mwaminifu!!na ni kweli mwaminifu...

Je, utafanyeje??

Anajibu: Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp 0755444078

Kwa kuhitimisha mada hii, tuyaangalie mahusiano haya katika jicho la wawili kwanza kabka ya watutu

Mara nyingi watu 2 mlo kwenye mahusiano ndo mna hatima ya kuamua mahusiano yenu yawe na harufu gani kwa watu.(kwa kuwa ameuliza nini kifanyike katika hali ambayo imeisha kuwepo,basi nitakazia upande huo.
👉Kwanza binti na kijana wakae pamoja wafanye Psychological Cross-checking ya mazingira ya mahusiano yao(maadamu wamethibitisha WANAAMINIANA) basi wakae waongee humu kanisani,ofisini,au mtaani tulimo watu wagani wamo?(wadada wengi? Vijana wakiume ndo wengi?wanawake?au wanaume?)....eqution .....(i)
(Wanaoongelea mahusiano yetu kwa wingi na kuzusha maneno hayo ni watu gani(wadada? Wakaka?wamama?au wababa?au wote?)........ Equation......(ii)
Wanaoongea wana msakama nani(binti/mkaka)..... Equation .....(iii)
Uongeaji wao watafuta nini kwetu( kutuachanisha, kutuchafua,kutusaidia kiroho,au kupata nafasi ya kupendwa wao?)......Equation......(iv)
Baada ya kusolve Equation hizo by substitution mtagundua maisha gani muishi,na agenda gani muibebe.
Tukianza kufanya Substitution katika Equations zetu
👉Equaton (i)kama wamo wengi wadada au wakaka jua mpo kwenye competition kubwa ya kutafuta nafasi ya kuoa au kuolewa(hapo ninyi kazeni kamba kuziba masikio wasiwagawanye kisaikolojia) maana hapo formula inayowasumbua kwenye mazingira ni Scarcity of Resources (girls/boys)to marry
👉(ii) kama ni wadada au wakaka (kila mmoja wenu achunguze past zake)kama ziko swa jua hao wanatafuta mpenyo.... Na kama ni wamama au wababa(jiulize nani ana binti mkubwa au kijana mkubwa umei wa kuoa au kuolewa)kama yupo tafakari mvuto wako kwa watu upo juu ? Kama huyupo tulieni.
👉Equation (iii)anaye sakamwa kaka ni mkaka(mdada ongeza ulinzi,kama ni mdada mkaka ongeza ulinzi)ulinzi wa kuwa mwaminifu,na kuongeza viwango vya kumpenda huyo,na kumsaidia mwenzio asiporwe
👉Equation ya (iv)lengo laazungumzo mtalijua kama watu wanawafuata kuwambia au unasikia wanaongea huko.(tendea kazi mazunhumzo yao)
By Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp 0755444078

Tuesday, 7 November 2017

MDADA KUSEMA NO INAMAANA GANI

Mada ya kuna athari gani kuoa mke ulombembeleza akakukataa kwanza baadaye akakukubali, vipi athari zake kwenye ndoa

​Anajibu​ ​Ev Elisha Kazimoto​
WhatsApp 0755444078
👉Si kila mkatao wa mwanamke umemaanisha kukukataa usiwe mme wake, mkatao huo unakuwa na maana kama mbili tatu, moja.. Bado saikolojia yake haijakusoma iambatane nawe(kubuka mwanamke,hapendi mpaka apandiwe wazo la kupendwa,yeye alizungushe akilini ili lizae wazo la Yes au No.
👆kwa sababu hiyo No inaweza kuja muda huo au muda wote ambao bado akili yake haijazungusha na kupata jibu la moja la ndiyo au hapana. Na mwanamke mpaka ashawishiwe, kumbuka wewe kijana ndo uliyejiridhisha kwa binti ndo maana ukaamua kumfuata na kutaka kuwa naye, unampandia wazo jipya,ambali hakuwa nalo, kwa hiyo ulinzi wake wa kutafuta jibu sahihi la hisia zake ni (NO, AU NTAKUPA JIBU)
👉Pili mkatao ule unaweza kuwa Unalenga kupima NIA YAKO ni muoaji au ni mwenye tamaa ya kumtumia( Are you a real husband to be or a boy of enjoyment) mara nyingi a real husband akipenda, moja hatakata tamaa kufatilia mpaka amekubaliwa, pili hata tafuta short cut kuomba basi sex kama hutaki tuoane, tatu ni msitaarabu kufatilia kwake si kwa kero,bali kwa upendo. Kwa maana hiyo wadada husema No mpaka aone nia yako ya ndani ni ipi,inaendana na shahuku yake?
👉Mkatao mwingine unalenga kukupa taarifa ya Kajipange kimaisha, wanawake wengi huwa wana ​worry about life style​ kabla ya kumkubali mtu wanataka wajiridhishe uwezekano wa kutunzwa na kuishi maisha ya furaha na amani. Kwa sababu hiyo akisema No mara ya kwanza baadaye akakukubali ni kwamba alikuwa anakupa message ya kajipange kimaisha uwe well off then come, ndo maana wengine usipo onyesha badiriko la kimaisha tangu ume propose ukirudi utaikuta No, ila ukienda ukajipanga ukirudi unakuta Yes.
👉Mkatao mwingine unamaanisha Si Muda Muafaka, wengine wadada wamejiwekea malengo ya nitaanza relationship ya kuingia kwenye ndoa nikiwa na umri kadhaa,au nikiwa level flani ya elimu, au uchumi,nk sasa ukienda kabla ya muda utakuta No mpaka muda wake ukifika ndo utaikuta Yes.
👉Mkatao mwingine niwa Kusibiri Mlinganisho,( inamaana kuwa wapo wadada wasemao No,wakisubiria wafike watu 2,3,4 ili waone kama nani yuko best kuliko wengine ndo aseme Yes kwako, akikosa atasema yes,wakija akaona umewazidi sifa waliokuja atasema yes
👉Kuna mkatao wa ​TOTALLY I DON'T LOVE YOU​ huu ni mkatao wa you dont fit to me, sasa mkatao huu una viashiria vyake, moja hutaheshimiwa kwa namba yoyote,utakatiwa simu zako zote,au hutajibiwa simu zako au ataku block,hatakusema vizuri kwa marafiki zote,utapewa majibu ya mkato tu,utaambiwa live mapungufu yako, hatapokea offers zako, na akizipokea bado hata kuomba kitu
​Sasa mtu wa namba hii kijana ukitumia ushawishi mkubwa wa pesa,zawadi,wazazi wake,ndugu zake,marafiki zake ili akukubali, siku akikukubali mkaingia ndani akikisha unajipanga kwenda naye kwa taadhari, ila athari utapata heshima kidogo,lakini itabidi maea kwa mara uwe mpole kwake,utaporwa position yako ya kichwa​
Jifunze kusoma ishara ya upendo ndo uokomaye naye,asiye na upendo hatakama ni Angel piga kona kwenye ndoa sura yake hutaiona, uraona matendo korofi, utajuta.
Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp 075544078

Tuesday, 31 October 2017

FAIDA YA SEX

*FAIDA ZA SEX YA MARA KWA MARA NI KWAWANANDOA TU,KWAKO KIJANA NI SUMU KUBWA HATA KUDUMBUKIA MARA MOJA*

_Kwanza niondoe dhana ambayo hasa vijana wa kiume na wakike uitumia kuji defend ili wafanye sex au michezo ya sex, kwa kisingizio kwamba ukikaa muda mrefu bila ku sex kuna matatizo makubwa kama kupata shida za kiafya au tatizo la ugonjwa wa chekelea *Hili ni pepo la ngono, Mungu hakuumba watu wajichafue kabla ya muda wake ili kuepuka chekelea na magonjwa ya kubuni.* Suala ni Kijana kukaa na Mungu vizuri na kuwa na muda na mambo ya Mungu na kuwa busy na shughuli zako,mwili wako utakaa sawa, binti hutavamiwa na vimapepo vya kuchekelea na kutamani ngono_.

*KWA WANA NDOA*
👉🏾Kwa waliooana sex ni kitu kimoja muhimu sana kwa watu walio couple kina faida zake muhimu kisaikolojia katuka kuijenga ndoa ikawa imara sana.
1.Sex kisaikolojia inafungua nafsi za wanandoa na kuruhusu furaha
2.Sex inapunguza au kuondoa stress(msongo wa mawazo)
3.Sex inaufanya mwili kuwa mwepesi
4.Sex inatuliza akili na kumfanya mtu kufanya shughuli zake kwa umakini bila kukosea kosea(hasa wale wa ofisini,wana mahesabu,wanaofanya kazi za typing, na wanao hudunia wateja)
5.Sex unamfanya mtu kuwa na uso wa furaha(welcoming face)
6.Sex inawaungamisha wana ndoa kinafsi(kuaminiana na kupendana).
7.Sex ina leta heshima na kujaliana kati ya wana ndoa ikifanywa kwa ubora.

*MADHARA*
👉🏾Kana mtaifanya mara kwa mara ila pasipo ufundi, mtaichoka, mtaumizana,mtatamani kutoifanya kwa muda mrefu.
👉🏾Kwa mwanaume ni kuchoka mwili,maana inahitaji nguvu.
*NB: _Sex ina madhara machache kwa watu washamba wanaoikurupukia madhara ni marefu, ila ushauri huwa ni huu jaina haja ya mara kwa mara kila siku,kila siku wakati mpo wote milele, hata chakula kutamu ukikila kila siku mnakichoka,ila uzuri wake uko palepale, pia wanaume hushauriwa kila mechi,usifunge mabao zaidi ya 3 kiafya, kumbuka bao kutoka ni nguvu kubwa unachomoa, (ndo maana biblia ikasema usimoe nguvu zako kahaba). Kama itakuwa mara kwa mara basi funga bao 1,2.. Kwa kadri mnavyo sex mara kwa mara nguvu ya kupakua maya ili ufunge bao usogea nyuma mupungua, ndo maana mtu aliye kaa mwezi,1,2,3 bila kusex na yule ambaye kwa wiki ni mara 5, mkianza pamoja kusex yule wa maea 5 kwa wiki atachelewa sana kufunga goli la 1, ila wa miez 2,3 hata dk3 haziishi ameisha funga goli la 1_*
Sex inafaida kwa waba ndoa kwa mabachela inakongoroa nafsi,moyo,akili hata sura na kukuzalishia hatia. Tulia ufikiwe kwenye foleni yako.

By Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp 0755444078

Monday, 23 October 2017

KUHUDUMIANA KIUCHUMI WACHUMBA

*Swali. Katika process za uchumba kuelekea ndoa ni sahihi kijana wa kiume kumuomba binti pesa au akopeshwe na binti?*

ANAJIBU: Ev Elisha Kazimoto(Mwanasaikolojia)
*WhatsApp 0755444078*
_Niweke bayana dhana ya uchumba kisaikolojia ndo tupate mwanga wa kujibu swali hiki kwa ufasaha_
✍ Neno *Mchumba/Wachumba*  _Ni mtu au watu wa jinsia ya kike na kiume walio katika mahusiano ya kati,ya maridhiano ya kuoana na kuishi pamoja kama mke na mme, waliozungatia vigezo vifuatavyo_:-
1⃣ Wamependana kwa hiyari upendo wa kuwa mtu mke na mtu mme, upendo *Tosherevu* (Selective & Specific Love) yaani umechagua kati ya wengi,umebaini huyu tu ndo anafaa na h as. una mwingine. ( *_Kama unatafuta,una mtu hujafikia kiwango hiki cha upendo, Kisaikoljia ni marufuku kumwita mchumba_*)
2⃣ Mmefuata taratibu za kiroho(kidini) au kifamilia za kuonyesha ridhaa ya wazazi au walezi wa pande zote mbili kuridhia mchakato wenu wa uchumba kuanza.( *_Ikiwemo barua ya posa,utambulisho kwa familia, kwa mchungaji(kwa wakristo),kulipa maali, kuvishana pete za uchumba nk_*)
3⃣ kupima afya zenu kwa madhehebu yenye taratibu za kupima
✍Mambo hayo yakizingatiwa ndiyo msingi wa uchumba wenye *_Mwelekeo wa ndoa_* kinacho baki ni Akili ya mtu binafsi aliyeko kwenye mahusiano kumsona mwenzake kufahamu ni mtu wa aina gani, ni mkweli ki kiasi gani,ni muwazi kiasi gani, vision yake iko imara kiasi gani, present action yake hiw it define future life, hiyo ni akili binafsi ya mahusiano ya kisaikolojia kubaini kama mtu ni tapeli,mtu sahii,nk(  *_kwa ufupi uchumba una terminology 2 tu, Muda wa Kumsoma mwenzako tabia na Muda wa Maandalizi ya harusi_*)
✍  Kwakuanza kujibu swali letu: _Suala la Kuhudumiana kama wachumba ni jambo jema na muhimu kwa watu walio serious kama vigezo tajwa hapo juu, ila akili,uangalifu na kiasi vizingatiwe iki kuepusha maumivu ya moyo.( Katika mambo yote Akilini mwako inabidi ujue *Uchumba Si Ndoa muda wowote ikiwepo sababu kubwa ya msingi unavunjika*) kwa hiyo mambo yote mnayo yafanya iwe kusaidiana,kufabta maendeleo uwe na taadhari akilini.
✍ *Kuhusu kijana kumkopa binti* Si suala la kukopa tu,hata binti kumuhudumia kijana kimavazi,kipesa,kumfungulia miradi nk, kama mme we mtarajiwa haina ubaya *_Inategemea kiwango cha Akili alocho nacho msichana, na anavoona mwenendo wa mahusiano yao na hali halisi ya kiuchumi ya kijana_* tafsiri zingine za kujishusha,unapoteza heshima, nk inategemea mitazamo yenu na nia yenu ya mahusiano ni dhana potofu kama wasemavyo wengine, *kuoa mke msomi kukuzidi,mwenye cheo kukuzidi,nk utadharauliwa* ni ufinyo wa akili ya mahusiano kisaikolojia maana Upendo wa ndoa *Never deal with Envirimental issues but Internal & unconditional issues* yaani moyo wako umempenda kwa sifa za ndani na si ana nini kwa nje hiyo ndo tunaiita REAL LOVE. Kwa mazingira hayo badala ya kumkopa utamsaidia tu,  maana ni kwa manufaa yenu( Ustawi wake ni ustawi wako)
✍ NB: Kisaikolojia kulingana na ongezeko la usanii, kushuka kwa akili( ongezeko la watu walovurugwa kisiasa,kijamii,kiuchumi,kiroho nk, tunashauri umakini uwepo sana katika kuhudumiana, wengine wamegeuza mahusiano kama mradi wa kuendesha maisha,na kusababisha majeraha mengi kwa wapenzi wao. Ndiyi maana tunanema hudumianeni watu wenye akili,umemsoma mwenzio kiasi kikubwa na watu mlo katika uchumba kama vigezo pale juu siyo uchumba wa WhatsApp ,Instagram na fb na wa uchochoroni, wa kuiyana wachunba na kupeaba promises kibao,hata wazazi hawa mfahamu ,hata barua ya posa haipo, ndo unajitundika kumfungulia duka,isafiri,unaenda bank kukopa unampa mkopo wako,my friend utapata ugonjwa wa kisaikolojia wa kuwachukia watu wa jinsia yake milele pale atakapo kusaliti na ku break relationship. Kumbe wewe ndo ulitumia akili fupi kuendesha mahusiano.
Quote: *_Katika kuanza mahusiano Kijana akili yake huwa juu sana,na ya msichana ushuka sana(anapoteza akili kiasi flani), na mkioana mwana mke anaongezeka akili, mwanaume anapoteza akili kiasi flani_* (Kuwa Makini na Mahusiano is not simple as you think)
*Imeandaliwa na Msaikolojia na Mshauri, mchambuzi wa masuala ya mahusiano na ndoa. Ev Elisha Kazimoto(Baba Evan)*
WhatsApp 0755444078

Saturday, 21 October 2017

ZINAA SIYA BAHATI MBAYA

*Swali : UMEJIENGAGE  KWENYE UHUSIANO NA MTU AMBAYE SURELY UNAJUA NI MTU KUTOKA KWA MUNGU NA NDIVYO ILIVYO THEN KATIKA KUWA KATIKA MAHUSIANO MKAJIKUTA KATIKA DHAMBI YA KUFORNICATE JE NINI KIFANYIKE KUNUSURU MAHUSIANO YENU NA HAMTAKI KUACHANA BADO MNAPENDANA SANA SANA*.

_Majibu mafupi kutoka kwa Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078
*Toba ya zinaa inagharama kubwa kama ilivyo gharama kufanya zinaa* kabla hujafanya zinaa kuna hatua ngumu,na za makusudi watu wanazipitia,na ndo maana kwa Tafsiri yangu ya kiroho,kisaikolojia,na kimwili *Hakunaga suala la Ninejikuta nimezini, yaani bahati mbaya nimeanguka kwenye zinaa* hakuna kitu cha namna hiyo kwa zinaa, isipo kuwa *Mtu aliye vamiwa ghafla na kundi la watu,au mtu mwenye nguvu, akambaka* na hapo uwe umeonyesha jitihasa za kumshinda,amekushimda nguvu,siyo amekukanata kidogo unarusharusha tu mikono na miguu halafu unatulia aendelee, hiyo ni *Umejibaka*
*ONA HATUA ZA ZINAA NDO UTAJUA SIYO YA BAHATI MBAYA AU KUJIKUTA* Ili ukienda kutubu,usifikiri nikitoa sadaka Mungu ananisamehe fasta,aliye kwambia Mungu ni kama TRA kuwa na uchu na sadaka yako nani,kwanza anasema sadaka ya mwenye dhambi ni chukizo kwake *Inanuka* na watu wamejidanganya,anasheratika,anakimbia kutoa sadaka,nakujikopa anajikopa atoe hata laki 1,hiyo ni hewa,hata baraka hakuna, mwingine eti anafunga 3 kavu chumbani anatubu hiyo umefanya ila bado hujaigusa zinaa.
1⃣ Unamshawishi mtu,na kumfanyia kila likilo zuri,ili mradi akuweke akilini mwake(uibue hisia zake za ngono)
2⃣ Unamuomba au kumtengenezea mazingira kumuonyesha unahitaji ngono(unalazimisha asome hisia zako na kukubaliana nazo)
3⃣Mnapanga eneo la kukutana lisiwe la wazi(mnahakikisha hakuna wa kuwaona wala kuwasumbua mpaja mmalize yote)
4⃣Mnakutana na kuanza kupandishana hisia za mwili kwa kufanya vitendo vya kupasha miili joto la zinaa(mpaka hapo umejikuta tu,yaani hujui?)
5⃣Mnaamua kuziba macho ya aibu, unaondoa nguo ya juu(aibu ya kawaida)
6⃣Mnaondoa nguo ya kati ndogo(aibu ya kati)
7⃣ mnaondoa nguo ya ndani 👙aibu kubwa(mpaka hapo unajikuta eeh)
8⃣Mnaamua kujiweka mlalo mzuri ili mpate raha ya kina,miguu na mikono na macho vinashiriki kutafuta pozi zuri la penetration of .....(bado wewe hujui,umejikuta)
9⃣ Unaanza in and out na kujiliza unajiliza,na wewe maneno ya mahaba yote yanakutoka(bado uko kwenye bahati mbaya!) Tapeli mkubwa wewe,unamdanganya nani kuwa umejikuta.
1⃣0⃣ Una ejaculate, bado ni bahati mbaya
1⃣1⃣ Unamaliza round 1,unaenda second selection mpaka 3,au unaishia na moja, (bado ni bahati mbaya) muhuni mkubwa wewe
1⃣2⃣ Mnamaliza,mnajipanguza ma uchafu yenu(bado nibahati mbaya)hujielewi wewe
1⃣3⃣ Mnavaa nguo ya kwanza hadi ya mwisho,mnatoka kwa interval ya muda eneo mlilo kubaliana kukutana(halafu unasema bahati mbaya)jambazi mkubwa wewe
1⃣4⃣ Unafika nyumbani unampigia simu kama amefika salama(bado tu mmejikuta mmeanguka) wee umelaaniwa kabisa.
*_Uongo huo hata shetani mwenyewe hajawahi kuutunga_*
_Usiwadanganye watu,sema matamaa yamenipelekesha nikaona niyape yanachokihitaji, na hili ngazi zote hizi 14 ziporomoke kwa toba,kaianike dhambi hiyo wazi kwa watumishi wa Mungu wakuombee na wakushauri la kufanya,wewe huji la kufanya *Maana wewe ni marehemu tayari* marehemu atafungaje,atatoaje sadaka? Nenda wakufufue kwanza ndo ujue la kufanya.
*Ev Elisha Kazimoto*(Sii entertain dhambi,wala kuipaka mafuta)
WhatsApp 0755444078

UMUHIMU WA HONEYMOON

*Mada mpya*

*Kuna ulazima gani kufanyia honeymoon gest/hotel na si nyumbani imakaaje hii..utamaduni huo ni mzuri...kuna maandiko yasaport hii...vitu gani vinafanyika huko saidi ya sex..ntafurahi kupata majibu.*

ANAJIBU: EV ELISHA KAZIMOTO
*WhatsApp 0755444078*
_Hapa kwanza niweke vizuri mtazamo wa swali kabla ya kushughulikia hoja Potofu ambazo huwa watu wanazijenga kuingiza hisia zao kwenye hoja huru_
👉 *_Kuhusu ulazima wa kwenda Honeymoon kwa mabibi harusi baada ya kufunga ndoa, HAKUNA ULAZIMA( maana yake Ukienda hakuna shida,usipoenda hakuna shida, kitu kikisha kuwa na ulazima maana yake kisipo fanyika hivo kuna athari kubwa)sasa hapa hakuna ulazima ILA KUNA UMUHIMU WW KISAIKOLOJIA NA KIJAMII(Umuhimu maana yake,jambo hilo lapendeza likifanyika hivyo maana kuna vitu vitafanikiwa, ila hata isipo fanyika hakuna athari ila kuna vitu vitakosekana, huo ndo umuhimu)_*
👉Kwa Habari za *Maandiko ya neno la Mungu kuthibitisha ulazima au kutokubalika, HAKUNA ANDIKO/FUNDISHO HILO ila itategemea mtazamo na tafsiri binafsi ya mtu na msimamo wake* ila kuna Falsafa za kisaikolojia
👉Kuhusu kuwa *Utamaduni huu ni mzuri au mbaya, hii inategemea na mwono wa mtu binafsi* kisaikolojia  _Uzuri au ubaya uwa katika macho ya mtu binafsi na si katika kitu chenyewe, tafsiri yako na mwono wako ndo unaotafsiri ubaya na Uzuri wa kitu_
✍ Baada ya kuwela vizuri Dhana 3 za swali, sasa niingie kuuzungumzia honeymoon na maharusi.
*HONEYMOON (Eneo la mapumziko kwa maharusi baada ya kufunga ndoa) Guest au Hotel* ni maeneo ambayo maharusi uchagua kwenda kwa mapumziko kwa siku zozote zile 1,2,5,10 kulingana na uwezo wao,matashi yao, au Budget ya Kamati ya Harusi. Kwa nini watu waende Honeymoon hotel/guest baada ya kufunga ndoa?  *Ziko sababu kadhaa za kisaikolojia na kijamii( hakuna sababu za kiroho kama ilivyo, mkiamua kwenda nyumbani kwa bwana harusi,hakuna sababu za kiroho ila sababu za kijamii)*
1⃣Kutafuta Faragha(Maala tulivu,pasipo na mwingiliano wa sura za wenyeji).
_Sababu hii ni muhimu kwa mazingira ya watu ambao wanaoana ndo mara yao ya kwanza kujutana kimwili(Mabikira) kuna changamoto nyingi za watu mabikira kukutana kimwili siku za mwanzoni, (kwa wana wake,kisaikolojia ni watu wanao jali sana privacy sanaa katika sex kuliko wanaume), mwanamke ili afanye sex kwa uhuru na ajiachie na aifurahie,hupenda kujihakikishia USIRI, ukimya,( sasa kulingana na maisha,kuna watu wanaoa wapo kwenye nyumba za kupanga,au nyumba zao ila hazina uhuru, kisaikolojia ni makosa makubwa kufanya rendo la ndoa kwa kujiiba,kujibana,kujishtukia uwepo wa watu,au kusikiwa. Ndiyo naana Hotelini au guest inakupa uhuru wa kujiachia kihisia._
2⃣ *Sababu ya Mapumziko ya Kisaikolojia* Harakati za harusi na mapambano ya harusi huchosha mwili na akili, ndiyo maana watu hupenda kutafuta sehemu tulivu,mazingira mapya ambayo hayata kudai kuyaweka sawa tena ila tu ,uke,unywe na upumzike, bila mwingiliano na mtu yeyote na maeneo hayo niya hotel au guest, nyumbani hakuna utulivu, mnafunga ndoa tu, wapo watu wanakaa hapo kwako ndugu,jamaa wengine wanakuja kusalimia kesho yake haluna utulivu unaohitajika kwa watu wapya. Guest au Hotel mnakuwa na muda wa kutulia kutathimini na kupongezana mwa safari yote ya mwaka 1,2,3 5... Bila usumbufu wa mtu yeyote.
*NIWEKE BAYANA DHANA CHACHE POTOFU ZINAZOIBULIWA*
👉 *_Dhana ya Kuacha baraka za ndoa Guest/ hotekini badara ya Nyumbani_*  _Hii ni dhana dhaifu kwa watu dhaifu kiroho. Baraka siyo mchanga au jasho,au kimiminika kwamba vikimwagika tunaviacha kule, baraka zinabebwa katika mionyo kwa imani na si katika nguo. Kama unahisi maombi unayoombewa ya harusi yanakaa kwenye suti na shera na ngozini, wewe huna tofauti na mbeba irizi,ila bado mchanga kiroho. Kumbuka hauendi hotelini kuzini,kwamba unarnda kuanguka, unaenda kwa mapumziko na tendo halali na takatifu._
👉 *Dhana ya Kuzoa mapepo* Hii ni dhana ya watu wasiokomaa kiimani, kuna maeneo mengi kila kona,kuanzia njiani,shule,vhuoni,sokoni na hewani,mapepo yanakaa ila wana wa Mungu tunaishi na tunatembea huko na kule bila kuvaliwa na mapepo, kama unahisi hotelini ndo kuna mapepo, bado ufahamu wako wa kujua ulimwengu wa roho wa giza na wa nuru unafanyeje kazi zake uko chini sana. Mapepo yanavaa Nafsi wazi isiyo na Mungu,au dhaifu kwa imani au yenye dhambi,popote pale,shambani,njiani nk.
👉 *Dhana ya Guest/ Hoteli kuna uchafu mwingi unafanyika* hii ni dhana ya mtu mwenye ufahamu mfupi,karibu kila kitu kina uchafu, unajua Daladala(mabasi) kuna unachafu mwingi,kuanzia wa ukahaba mpaka wa kimatambiko? Unajua nguo hiyo ya mtumba unayoivaa alivaa kahaba nani au mtu mwenye mapepo gani? Ofisini unako fanya kazi unajua seat hizo zimekaliwa kwa shuguli gani? Labda niseme huu ni uchanga wa kiroho. *swali la msingi: Ukisafiri uwa unaenda na kitanda chako? Guest au hoteli unaenda kulalia nini? Au wahubiri wanapo kodishiwa hoteli,guest huwa wanaenda na vitanda vyao! Hujui sisi tubapokanyaga tunanguvu ya kumiliki na kupatawala,panatakaswa kwa matumizi yetu? Isingekuwa hivo kuna vitu vingi tungeviacha, ilibidi tumiliki vya kwetu popote duniani.*
_Ndo maana katika maombi ya Yesu akaombea wanafunzi wake,kwamba Baba siombi uwatoe ulimwenguni bali uwalinde na yule mwovu_
👉 *Dhana ya Kuharibu pesa* Hii ni Dhana ya Akili ya kiumaskini na mtu maskini, Pesa haitakuja kutosha au kuingezeka kama haitumiwi,kujibana siyo kutajirika ila mpangilio wa maisha na malengo.
✅ Aina ya harusi yako ndo inatoa picha uende wapi,hivi unajua pesa ya honeymoon inatoka kwenye Kamati ya harusi ambayo ni michango ya watu ya harusi ambayo si pesa yako ya kuanzia maisha
👉Lakini dhana hii ya umaskini imezifanya ndoa za walokole watu wajiitao wa rohoni *Kuchuja* tangu mnaoana hakuna zawadi za surprised wala kutoka out, january mpaka December ni ndani kisa, eti kutumia laki 1 kwa out, au laki 3,si bora ufanye maendeleo🤔🤔, maendeleo gani yanayozidi kuendeleza furaha na shangwe ya ndoa?.
*MY TAKE* _Kama mtazamo wako haupo katika kutumua pesa ili ije nyingine, tulia,ila wenye mawazo ya kuongezeka na kufanikiwa,wabatumia Pesa kujenga saikolojia zao ili wafanye maendeleo kwa utulivu wa kifikira. Tangu umebana pesa umewahi kufanya kitu gani cha kutishia watu wanaotumia pesa kujenga saikolojia zao? Mbona maisha yakawaida, usiishi kwa kujibana ukingojea kutajirika kutoka hewani, mafanikio ni pamoja na kuwa na saikolojia iliyo huru na kufunguka._
*_Imeandaliwa na Ev Elisha Kazimoto(Baba Evan)_*
WhatsApp 0755444078

KISS KWA WACHUMBA

*Habari ndugu zangu*

*_Nina swali nalo ni...Je ni makosa kwa wapenzi kubusiana (kumbusu mwenzake)?_*

Anajibu: Ev Elisha Kazimoto (Baba Evan)
*WhatsApp* 0755444078

*_Katika swali hili, lugha iliyo tumika ni lugha tata (Ambiguity ), MPENZI( Mpenzi kwa maana ya watu walio katika mahusiano ya kimapenzi-wanaoshiriki sex? Au Mpenzi kwa maana ya mtu uliyenaye katika mahusiano anaoupendeza moyo wako(mpenzi-mchumba).?_*
Kwa namna yoyote ile nitoe taswira halisi, *Kama ni suala la Mpenzi, mnaoshiriki sex, busu yoyote haina shida, simple au deep kiss haina shida,maana sex ni more than kiss* (Angalizo kwa watu waliookoka,wana wa Mungu HATUNA MSAMIATI WA MPENZI wa sex, HATUNA MCHUMBA wa sex)
Kwa habari ya mchumba kuna vitu tunaviita *_Maadili ya Uchumba kwa watu waliookoka_* hapa ndipo tunapo tofautiana kati ya wachumba wapagani, wachumba wana dini,nawachumba watakatifu(waliookoka) *MAADILI NI PAMOJA NA:
1⃣ Kulinda Ushuhuda katika kipindi cha uchumba chote, msilete tafsiri itakayo fanya watu wawaone hamjaokoka(epuka kulitukanisha jina la Yesu kwa mwenendo,tabia yenu nk.
2⃣ Kuto fanya mambo yanayoweza chochea kwa kasi hisia za miiki yenu na kuwafanya muanguke kwenye dhambi ya zinaa( mfn, sex touching,sex plays,Kisses, hasa deep kiss, hug hasa Zero distance hug (hug ya dk 1,2,5,10...mnatafuta nini)🤔🤔
3⃣Kuto kutana kwenye mazingira ya uficho yanayoweza kuwaingiza katika vishawishi vya zinaa.
*KISS & HUG*
_Kiss na hug havina ubaya wowote,wala dhambi yoyote, suala nia yenu ya kiss na hug ni nini? Je mko huru kukiss na ku hug publically? Au mpaka muwe wa 2 tu?_
Kuna dhana na mwavuli wa kiss takatifu.... Huu ni uongo ni utumiaji wa maandiko vibaya kutimiza mahitaji ya kiihisia. Kiss takatifu haitofautiani kwa jinsia zote(ndo mtume Paul aliisema) sasa kama kaja yako,dada yako,mama,bibi, mchungaji wako mana mchungaji wako na mshirika wowote waweza mpa kiss hiyo hiyo unayotaka kumpa mchumba  wako basi hiyo ndo busu takatifu kwa watakatifu wote
Kinachoongelewa na vijana wasasa kuhusu kiss siyo kiss wanaongelea ROMANCE ila wanapunguza makali kwa kuiita kiss, hivyo si jambo jema kwa wachumba wakiroho kuromance(deep kiss) mnachokitafuta si ku express love, ila mna express sex feelings zitakazo wagharimu katika safari yenu.
*_By Ev Elisha Kazimoto_*

Wednesday, 11 October 2017

SEX NA KUFUNGA NA HUDUMA

*TENDO LA NDOA NA MFUNGO*
Swali: Je, Ni Sahii kushiriki tendo la ndoa mkiwa kwenye mfungo wa maombi, au unakiandaa kwenda ibadani kuhudumu.?

*Anajibu Ev Elisha Kazimoto*
WhatsApp 0755444078
_Kwanza niweke sawa dhana na tafsiri ya tendo la ndoa kwa wana ndoa. *Tendo la ndoa kwa wana ndoa ni Safi, na Takatifu, na huru kwa wana ndoa muda wowote ili mradi wamekubaliana na kwa utaratibu*_  na hiyo ni kwa mujibu wa neno la Mungu.👇👇👇👇👇
*1Wakorintho 7:1-5*


1 Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke. 

2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe. 

3 Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. 

4 Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe. 

5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu. 
✍ Inabidi tujue jambo moja, hakuna unajisi wowote,ubaya wowote katika tendo la ndoa, hizo ni imani potofu na misimamo binafsi si ya Neno la Mungu. *Uharamu wa tendo la ndoa,na Muda wake ni kwa watu wasiyo wana ndoa, ila kwa wanandoa ni Safi,Ruksa muda wowote* Dhana za Huruhusiwi kushiriki tendo la ndoa siku ya ibada, au kama unaenda kufanya huduma, kusimama madhabahuni, huu ni ushetani, ni upotofu, ni huujumu wa ndoa, ni kuwafunga watu kongwa lisilo la haki. *_Alicho kibariki Mungu,utakihitaje kimelaaniwa? Mwanzo 1:28_* Mungu alilibariki tendo la ndoa na hakuliwekea majira wala nyakati za kuli attend,iwe asubuhi, mchana,usiku, usiku wa manane, free enjoy wana ndoa, unaenda kuimbisha saa 9 mchana, unahitaji kuburudika na kutuliza saikolojia yako hata saa 7 zimua, it's your property, zingatia tu utaratibu,muda wako na Mungu na muda wako na mpendwa wako. Ni muhubiri unaenda kuhubiri mkutano wa nje,una wife wako umemuhitaji mchana, Enjoy your blessings, wee ndo unajua muda uloutenga na Mungu na wako na mke wako. *Tendo la ndoa halina Limitation ya Kibiblia kwa wana ndoa* lavda ushauri na mawazo tu ya mtazamo na mapendekezo kulingana na hali ya mazingira,kitu ambacho siyo kanuni wala sheria.
*Tendo la Ndoa na Kufunga* _Nahisi wana ndoa wanajua nitakacho eleza hapa, kwa vijana wanaweza wasijue, Tendo la ndoa si kama kunywa chai,kuchovya mkate kwenye chai, *Ile ni Kazi Ngumu japo ni Enjoyment* ila inahitaji nguvu za ugali, muscular. *Ogopa kazi inayo toa jasho mtu* hiyo siyo mchezo mchezo.
✍Tendo la ndoa kulifanya linahitaji nguvu,uwe umeshiba,uwe na joto lawili ndo itaisimamisha misuli ya *Fimbo ya ufalme*,au mama ndo utahimili mapigo.
✍Tendo la ndoa linahitaji akili safi iliyo tulia,yenye oxygen ya kutosha ili kuibua hisia za sex, *_Sasa mtu aliye funga, ana njaa,akili inachoka,oxygen imepungua,lakini joto la mwili limeshuka, nguvi hana za kusimamisha fimbo muda mrefu kwa sababu ya chakula mwilini hakuna_* kwa sababu hiyo tendo la ndoa litakiwa gumu. Tena afadhali kidogo kwa Mwanamke anapokea,ila mwanaume anaye toa, one goal uchovu wake ni kama mwendo wa alotembea more than 5 km kwa miguu.
✍ *_Kama umefunga una nguvu za kusukuma mzigo na isikupe shida kuchoka, hakuna unajisi ingia kazini. Hivi ni vitu vilivyo barikiwa,sasa ukiokoka kupita maelezo kila kitu unakiita dhambi, kumbusu mkeo siku 6a j2 dhambi, ku sex siku ya ibada dhambi, acheni kutengeneza dhambi, Tendo la ndoa kwa mwana ndoa halina unajisi kwa siku wala muda._* Alivyo vitakasa Bwana wewe usiviite najisi, vitu vyote ni safi kwa walio safi,ila ni najisi kwa walio najisi.👇👇👇👇
*Tito 1 : 15 - Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia.*
✍Mwisho ushauri wangu na taadhari yangu, tusitumie utashi wetu usio na fact za kibiblia kuonyesha kosa au dhambi, tutumie ujuzi,experience na neno la Mungu kiwaonyesha watu ukweli wa mambo.
NB: Tendo la ndoa lonahitaji utulivu, maandalizi, nguvu na muda mzuri na kuridhishana, lisifanyike kwa kukimbia kimbia au kumridhisha mtu mmoja,mnapo lifanya,muwe mmefunga,mnaenda ibadani,au mmetoka ibadani hakikisheni ni kwa furaha yenu wote na kufurahi wote pamoja.
*_Ulikuwa na mchambuzi wa masuala ya kisaikolojia na kiroho katika mahusiano na ndoa, Ev Elisha Kazimoto(Baba Evan)_*
WhatsApp 0755444078

Tuesday, 10 October 2017

AGANO LA UBIKIRA

*SWALI*: Bwana Yesu asifiwe.
*Ninaomba kujua kuna nguvu gani ya kiagano ktk bikira ya mwanamke.*

Au kuna agano gani alilonalo mwanamke ktk mwili wake km agano la mwanamke au mtoto wa kiume kutahiriwa baada ya siku nane kuzaliwa.

*Anajibu Ev Elisha Kazimoto*
WhatsApp 07554440708.
_Kwanza naona muuliza swali ameuliza maswali mawili lakini yote yana dhana moja ya Agano la damu,kote kwa pnde mbili, kwa jinsia ya kike na kiume_
✍ *Agano ni nini kwanza* _Ni maridhiano,makubaliano baina ya pande mbili kwa sababu maalumu za kiupendo,kisheria,kimalengo._
✍ Agano laweza kuwa la maneno, viapo vya maneno,la uhai wa mtu,mnyama,ndege nk na la damu.
✍ Mara nyingi, *_Agano la Damu lina nguvu kubwa kuliko agano lolote,maana ni agano la uhai, (katika damu ndimo kulimo uhai)_* na Mungu tangu mwanzo alitumia agano ili la damu kwa watu wake, na shetani anapenda kulitumia kwa kuwa kuna nguvu ya uhai ambayo ndo maisha ya mwanadamu.
*Kutoka 24 : 8 - Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote.*
✍ *Nianze na suala la Bikira kwa mwanamke* _ Bikira kwa mwanamke ni Alama ya Uaminifu wake kwa mume wake, ni Agano la mwili kati yake na mume wake(mwanaume).
✍Na Bikira ilikusudiwa iwe agano la mwanamke na mume wake,siyo na mume mwingine.👇👇👇👇👇
*Kumbukumbu la Torati 22 : 17 - angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.*
_Ubikira ulifatiliwa kwa ukaribu mno,na kuweka mavazi(mashuka)kuthibitisha kama mwanadada huyu alikuwa bikira au la,na mavazi yele yalipelekwa kwa wazee wa mji kuwaonyesha huyu alikuwa bikira.
✍Katika ubikira ndimo kulimo damu,damu ndiyo agano la kuungwa na mume huyo( Labda ni semee kwanza kuhusu tendo la ndoa, Lile tendo lina kazi ya kumuunganisha mtu na mwenzie kihisia, & kimwili, na alama ya *_Agano la kuunganishwa ni Bikira na Nguvu ya Agano hilo la kuunganishwa Katika ndoa ni Damu ya Ubikira_*  (Sex inakuunga na mtu huyo mnaye sex)
👇👇👇👇👇👇👇
*1 Wakorintho 6 : 16 - Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.* Ndiyo maana likaitwa Tendo la Ndoa, watu maalumu,ili likuunge na alokuchagua Bwana,siyo ujiunganishe na kila mtu,ilikusudiwa uungwe na mmeo au mkeo.
Na Agano hilo lilikuwa ni kwa faida ya wana ndoa kwani Ubikira kwa mume na mke, _Ni Ishara ya Uaminifu, Uvumilivu, Upendo, Heshima katika ndoa_.👇👇👇👇
*Mambo ya Walawi 21 : 13 - Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake.*
✍Ulitakiwa umwoe mwanamke katika ubikira wake, kulikuwa na maana kubwa na umuhimu mkubwa wa kuunganishwa na mtu mwenye Alama na Nguvu ya Agano la mwili. Japo wengi wa watu wa leo wamelichukulia kiurahisi suala la Ubikira, ndiyo maana na ndoa nyingi zinachangamoto kubwa sana ,fujo na vurugu, kuna vitu vinakosekana vya kiagano, vinavyo imarisha agano.
✍  Kufunga ndoa kuna agano la maneno lina tumika, ila Alama na Agano hilo huwa ni pete, na Nguvu ya Agano lake la mwili kwa mwanaume ni Ubikira. *_Sasa ondoa mtazamo finyo, na wa kujitetea kwa udhaifu wako, kuwa mbona ziko ndoa nyingi za waliooana bikira ila zina changoto nyingi kuliko za waliooana bikira hakuna, huo ni mtazamo finyu, wala hilo Halibadirishi formula ya Kimungu ya kuufanya ubikira uwe agano la ndoa_*
✍ _Kwa sababu hii niwatake wadada wote ambao hawajaolewa na bado wana sifa hii ya ubikira tafadhari tunza na bado nguvu ile ipo kwenye ulimwengu wa roho na kinatenda kazi. *Tunza Bikira* uliye poteza kwa kutojua, enzi za ujinga, au kwa kujua yaani ukiwa katika wokovu, hakikisha unakuwa mwaminifu katika maisha yako yote ya ujana Mungu atakutokea kwa njia nyingine._ Tafuta somo langu linalosema *Uzaliwa wa kwanza, part 1,3 & 3*
✍ *Suala la Kutahiriwa* hili nalo lilikuwa ishara ya agano kati ya watu na Mungu, agani nalo hili liba nguvu ya damu,au alama ya damu.( Hili ni Agano la mwili)👇👇👇👇
*Mwanzo 17 : 13 - Mzaliwa nyumbani mwako, na mnunuliwa kwa fedha yako, lazima atahiriwe; na agano langu litakuwa katika mwili wenu, kuwa agano la milele.*
Lakini hili liliashira Usafi, Agano hili lililenga kuobyesha usafi wa watu wa Mungu kwa hiyo katika agano la kale Israeli walilifatilia sana. Tendo hilo hilo lilifanywa na YESU kwa kumwaga damu na kututahiri mioyo yetu(Tohara ilihusisha kuondoa magovi ya miili ya mwanaume(katika uume) kama ishara ya usafi,damu ilimwagika. Baada ya Kifo cha Msalama cha Yesu kila amwaminiye tayari anatahiriwa roho yake, govi la dhambi la roho linavuliwa na damu ile ile ya msalaba inakuwa imetumika kama utakaso.👇👇👇👇
*Wakolosai 2 : 11 - Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo.*
✍ Sasa baada ya kuokoka, au kwa waliookoka *Tohara/Kutahiriwa* kimwili(govi la uume) halipo kiroho tema kimaagano, limebaki kiwa ni tendo la *Kiafya/ Sayansi* ila halina mahusiano tena ya kiroho.👇👇👇👇
*1 Wakorintho 7 : 19 - Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu.*
_Kwa sababu hii niwashauri watu wote wamama kwa wababa, kutafuta kutahiriwa mioyo yao maana kuna magovi ya dhambi zao,na humo ndo kuna agano takatifu la damu ya YESU lililo imara na la milele. Kwa kuhitimisha, Tuulinde ubikira wetu ambao ni Uzaliwa wa kwanza(Malimbuko ya miili yetu na roho zetu) ili tuyapate yale mema yaliyowekwa katika ubikira(limbuko)_
*_Ulikuwa na Mchambuzi wa masuala ya Kimahusiano na Ndoa Kisaikolojia na Kiroho_*
         EV ELISHA KAZIMOTO
WhatsApp 0755444078

Monday, 2 October 2017

AINA ZA MAWASILIANO YA WACHUMBA

*MAWASILIANO KATIKA UCHUMBA*
_Mahusiano ni nguvu ya kisaikolojia inayo vuta hisia na moyo wa mtu juu ya partner wake. Mahusiano hai,imara huwa kuna nguvu inayo chochea hisia,ambapo mtu huwa radhi kusema chochote na kufanya chochote kwa partner wake ili mradi amridhishe,na kumfurahisha partner wake. Hiyo ndo Saikolojia ya Mahusiano_
✍Nature ya mahusiano ni kwa kila mtu,awe ameokoka,mchungaji,nabii,mtume nk wote nguvu ni moja ya mahusiano, ila tofauti ni kwamba, *Mtu aliye okoka,aliye na Roho mtakatifu,hofu ya Mungu, Neno la Mungu,anajua katika mambo yote ya kimaisha, kunahitajika KIASI na hekima ya kulinda Ushuhuda na Utakatifu wenu* kwa maana hiyo nguvu ya saikolojia uwekwa sawa.
✍Kuna vitu vya kutofautisha, *_Mawasiliano ya sms, call au live ya kimahaba, na ya Kiupendo_* mawasiliano kwa mchumba wako yanayo lenga kufunua uchi,kutimiza hisia za ngono, kumfanya mtu atamani kutimiziwa kiu ya ngono, hayo ndo mabaya na makosa kwa wachumba WALIOOKOKA,ila kwa wapagani ni kawaidaa hawana mipaka,ila watapata shida ya kisaikolijia ya kuonjwa na kuachwa.
✍Ukweli ni kwamba unapokuwa na mchumba( Expected Wife,or Husband )mawasiliano yenu,ni tofauti naunavyowasiliana na mtu mwingine *_Na ndivyo inavyo hitajika, onyesha kupenda, onyesha kumjali,onyesha kuwa wa pekee,_* lugha za upendo, kama kumsifia alivyo mzuri, unavyo mpenda, nk,lugha za upendo, sasa usichanganye lugha za mahaba ya ngono na upendo, mambo ya *Umelala na nguo au uchi?, umevaa under wear gani? Maziwa yako yakoje, umbo la sehemu za siri likoje, njoo tulale wote, nikumbatie hapa nina baridi nk,hizo si lugha za upendo ni za mahaba,nazo uibua hisia za mwili,jambo ambalo upelekea kuingia katika zinaa kabla ya ndoa,au kujichua baada ya mazungumzo,na hiyo ndo athari zake* kujikinga tumia Lugha za upendo siyo za mahaba kwa mchumba wako, mkioana, tumia zote, moto ukipanda mna uhuru wa kuuzima na hakuna dhambi wala kuhukumiwa.
*By Ev Elisha Kazimoto*(0755444078)

Tuesday, 26 September 2017

KUVALISHANA PETE

💍💍 *PETE YA UCHUMBA NA NDOA KATIKA KUVALISHANA*💍💍
    _Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078
Swali limeulizwa: *_Nani anapaswa kupiga goti wakati wa kuvalishana pete_*
MAJIBU:
👉 _Kwanza pete niishara ya agano baina ya watu wawili kwa maridhiano ya kuwa pamoja, ni Ishara,Alama inayoashira Umilikiwa. Tangu mwanzo kwenye biblia pete zilitumika kwa tafsiri hiyo, ila ukitaka kuvaa,au kuto vaa siyo dhambi ila kimapokeo na kitafsiri yafaa kutumika kuashiria badiriko katika ulimwengu wa mwili kwa wale waonao. Kwenye Biblia Pete zipo na zimetumika, hila si Andiko la Biblia kuwa imeagizwa kuvaa pete, ila kama kuna watu walivaa,walitumia na si katika dhambi ila ni katika utaratibu wa kawaida kuvaa tuna vaa_
👉 *Kuvalishana pete ya uchumba* Kwanza tuachane na kuiga,bila kujua asili na tamaduni za watu kwa nini wanafanya hivi, tufanye kulingana na tamaduni zetu,na *Kimantiki*
👉Swali hili si la kiroho,ila lina mantiki ya kiroho,pia siyo sheria,japo linamantiki ya kikanuni.
💍 *_Mantiki katika kupiga goti kati ya mwanaume na mwanamke wakati wa kuvalishana pete hiko hivi_*(Mantiki ya kibiblia ila siyo andiko)
✍ Kati ya kijana na binti nani anatafutwa( jibu ni binti) hii ni sawa na kati ya mwanadamu na Yesu nani anamtafuta mwenzake(jibu ni Yesu), Kati ya kijana na binti,nani anastahili kushuka,kunyenyekea,kupiga goti,kuona kati ya weeengi,amenichagua mimi akiona na mfaa? Kabla ya kukupa jibu,tujiulize(kati ya nwanadamu na Yesu nani anastahili kushuka,kunyenyekea,kuona nimechaguliwa mimi kuwa sehemu ya maisha ya Yesu?) jibu ni jepesi ni mwanadamu,maana  mpo wengi atafutaye ni mmoja,kama amekuchagua wewe unapomoka mpaka nchi,kuonyesha why anichague mimi? Nashuku
👉Kumbuka biblia inasema,Mwanaume ni kichwa cha mwanamke,na ni mfano wa Yesu Kristo alivyo kichwa cha Kanisa. (kwa mantiki hiyo,unataka kusema Yesu akimtafuta mtu dhambini imempasa kunyenyekea,kuona hakustahili,imekuwaje amenikubali,nashukuru kwa kunikubali, hiyo ni roho ya uasi ya kishetani ya kubadili kanuni za Kimungu kwa jutaka kuwepo usawa na mfanano wa haki,na utashi.
👉Biblia inatuita watu wote tubao mkubali Yesu kuwa ni mabibi harusi na Yesu Bwana harusi,kanisa ambalo ndo bibi harusi tunapofanyiwa jamvo na bwana harusi wetu tunapiga goti,tunanyenyekea na kushukuru,why mimi amenichagua,angeenda kwa wengine,wala nisinge mlaumu kwa kutokuja kwangu,( *_Ndo hivyo hivyo,binti hachagui,hapeleki proposal, yeye anaitikia au kukataa,sasa uhuru wa kuitikia na kukataa haukupi kibali cha kuonekana unyenyekewe kama umemsaidia)ndomaana Yohana 1:11-12,anasema Yesu alikuja kwa walio wake,wakamkataa,ila akayageukia mataifa tukaokolewa kuwa watoto wa Mungu,kukataa kwso hakumfanyi Yesu kuonekana naye amepoteza,bado yeye ana choices nyingi na mda wowote,na ndo alivyo kijana
👉Mantiki ya pili,(ya kibinadamu na kimakuzi) *_Kati ya anaye toa kitu na anaye pokea, nani anapaswa kushukuru? Kuonyesha ishara ya heshima? Jibu ni aliyepewa ndo ata shukuru,na kunyenyekea hata kupiga goti(Kijana anampa binti alama ya agano pete 💍 wa kupiga goti ni msichana,kaheshimiwa,kachaguliwa,kapendwa.
_Sasa mitazamo mingine,niyakuiga Western culture ambazo wala hamziwezi, makuzi,malezi,namna ya kuonyesha upendo tofauti na sisi, wazungu kuonyesha anakupenda anakuletea ua🌹mwafrika ili ujue anakupenda akununuli smartphone kali,nguo,gari nk,ujiiga iga vyote,ikikushinda tumia makuzi yako ila yaboreshe yapendeze._
*_Huo ni uchambuzi wangu siyo sheria, ukitaka kija kupiga goti mchumba wako asimame sawa,ujiweza mvaoishe ukiwa umelala kifudifudi au chali sawa,haikupeleki jehenamu wala haikufanti uwe na ndoa nzuuri, hayo ni maigizo,ukimleta ndani unaanza kujionyesha mwanaume mpaka anajuta kwa ubabe,sasa ulipiga goti la nini? Ila nakushauri binti mwente akili timamu, piga goti,shuka pokea heshima ya mmeo mtarajiwa anayo kupa,wewe huwezi mtafura,ila yeye anaweza kukutafuta,lakini utakuwa uneonyesha tafsiri halisi ya kanisa na Yesu Kristo,tofauti na hapo utakuwa umeonyesha tafsiri ya rusifa na Mungu_*
Mcgambuzi wa masuala ya ndoa na mahusiano, mwanasaikolojia *Ev Elisha Kazimoto(Baba Evan)*
WhatsApp 0755444078

Tuesday, 19 September 2017

KIJANA MVIVU KUCHUMBIA

*Swali:Hivi inakuwaje kijana anakuja kukuchumbia,hajishughulishi na chochote,kwa kifupi mvivu,anaanzisha mahusiano na wewe ila anamtegemea binti amtunze mwanzo mwisho, hapa kweli kuna uwezekano wa kuwepo ndoa?*

Majibu na Ev Elisha Kazimoto.
WhatsApp 0755444078.
Katika swali hili,kuna mambo ya msingi yakuyaangalia,:
*_Ndoa haijengwi kwenye vitu,ila kwenye upendo wa dhati ulogundua kitu cha ziada kwa mwenzako,chenye faida kwenye maisha yako, na hicho huwa kinawafanya watu wenye vision kukubali kumuoa huyo mtu,au kuolewa na huyo mtu_* kijana kuwa na pesa na kutokuwa na pesa,hakipimi uwezo wa kuwa na wewe. Anaweza kuwa hana kitu muda huo,ila mbele ya safari atakuwa navyo,au wewe ndo uliye lango la yeye kufikia ndoto zake.
2.Pili Tunapo anzisha mahusiano(au kabla ya kuanzisha mahusiano)au kusema yes tuanze safari lazima ujue *_mahusiano ni gharama, gharama ya pesa,muda,gharama ya kuumizwa,gharama ya kusamehe,na gharama ya kuonyesha mwelekeo wa maisha_* kijama wa kiume kama huna uwezo wa kujua gharama hizi lazima nizibebe,au kama unazikwepa,hupaswi kuoa,na unastahili kuachwa.
NB: *_Kwenye kitafuta na kuelekea ndoa,tunaishi kwa vision na plans, kwenye ndoa tunaishi kwa Imani na Uvumilivu, sasa usilete tabia za ndoa imani na uvumilivu kwenye mahusiano,tafsiri yake ni wewe hujielewi,na huna uwezo wa kuishi na mtu._*
Fanya kazi,pambana kwa namna yoyote uonyeshe vision na plan kwa unaye taka kumuoa,usimfanye kuvumilia na kuwa na imani kabla ya muda.
*MWISHO WA MADA*

Thursday, 14 September 2017

WALOKOLE NA WAPAGANI

*SWALI KUHUSU WALOKOLE NA MAHUSIANO NA WATU WA MATAIFA*
      _______
Ninaswali kiongozi.
Linanitatiza sana napenda nijibiwe kwa fikra zaidi moja.

1) _Hivi kwanini walokole wengi huwa hawana upendo na watu wasio walokole.. Yaani hujitenga sana kiasi cha kuweka mipaka._

2.) _Nimeliona hili nilipokuwa sekondari mpaka chuoni.Hasa wale wa makanisa wanaoita ya kiroho_

3.) _Lakini matendo yao wengi ni Wachoyo Wasengenyaji,Wachochezi,Viburi_

4.) _Na hawana uhusiano mzuri na watu anaolala nao kwa kujiona wao ni watakatifu sana hawatakiwi kuwa karibu na mataifa hata kwa jambo la jumuia kama kusoma na michezo (mpira wa miguu na pete)_

5.) *Naomba unisaidie.*
_Chanzo ni nini..Nini kifanyike kuwasaidia walokole wa namna hii maana kila taasisi wapo tena wengi tu._


*Mchambuzi wa Swali hili ni Ev Elisha  Kazimoto*
WhatsApp 0755444078.
_Ndugu na rafiki yangu uliye uliza swali,swali lako ni moja,ila *nimelitenga katika vipengele 5 ili Nikupe ufafanuzi kwa kuzingatia vipengele hivyo* naamini kufikia mwisho utajua Walokole ni watu gani na kwa nini wanaishi maisha hayo unayoyaona na kuyatafsiri hivyo ulivyo uliza swali lako_
👉Swali lako majibu yake yapo kimaandiko zaidi kuliko kifikira,na kwakuwa umeuliza vizuri kuwa *_.....Hasa walokole wa Makanisa ya Kiroho....._* tayari tunatafuta Itikadi yao,katiba yao inawaelekeza vipi ndipo tujue namna ya kuelezea tabia zao. ( _Kwanza tuanze na Ufunguo wa Kwanza wa Msitari wa biblia unaotuonyesha Chanzo cha watu 2 kutofautiana tabia na matendo_)👇👇👇👇
*Amosi 3 : 3 - Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?*
👉Hapa Biblia inaongelea watu wawili walio eneo moja(Duniani) ila wanasafiri kwenda maeneo 2 tofauti( Mbinguni na Jehanamu) _Safari ya watu hawa,ina mahitaji mawili tofauti,kila njia ina kanuni zake,mizigo yake ya kusafiri nayo,maadili yake, kila mmoja anaenda kulingana na kanuni za aendapo, ndo akasema *hawa watu, hawawezi kwenda pamoja sambamba,kushikamana,mpaka kwanza wapatane, aidha wakubaliane njia moja iwekwe pembeni,watumie njia moja, yaani mmoja wapo,aamue kuachana na njia yake,afuatane na mwenzake,hapo watatembea pamoja,wata panga moja,watashirikiana katika kila jambo maana wamepatana kutembea njia moja*_ 👉Sasa Watu waliookoka,(walokole) huonekana tofauti na wapagani kutokana na kutofautiana *katika kile wanacho kiamini,maadili ya safari yao, tumainilao* aliyeokoka Anaambiwa,na anaamini Kuishi maisha matakatifu hapa duniani,ambaye hajaokoka,au mwana dini anasema huwezi kuishi maisha matakatifu hapa duniani, tunaokoka baada ya kufa. (Kwa hilo tu,watatofautiana mahitaji ya kuishi,kukaa,kufanya mambo yao) anaye amini katika utakatifu *Atajilinda na mambo mengi,* asiye amini katika utakatifu,hana kizuizi,atafanya lolote,na kuishi vyoyote.👇👇👇👇👇
*_Waebrania 12 : 14 - Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;_*
👆👆👆👆Aliyeokoka ameambiwa atafute utakatifu,maana hakuna mtu atakaye mwona Mungu asipokuwa nao. Ambaye hajaokoka hana sharti hilo.
*_1 Petro 1:15 - 16 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; 16. Kwakuwa imeandikwa mtakuwa watakatifu,kama mimi ni mtakatifu_*
👆👆👆hii ndo sababu ya walokole kuwa makini na nazingira yanayoweza kuwaondolea sifa ya utakatifu.
*Sasa nianze namba moja hadi nyingine katika swali lako moja la msingi, kwa nini walokole wanaonekana hawana upendo lwa mataifa*
_Kwanza hapa niweke sawa,tunatofautiana katika kutafsiri neno upendo, kunaanaye tafsiri upendo,mwingine Anaamini upendo ni mtu kuambatana na mimi katika kila jambo nitakalo mwambia,liwe zuri au baya akikubaliana nami huyo anamipenda(huu ni mtazamo wa mtu asiye sahihi)_👇👇👇
*_Waamuzi 16 : 15 - Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi._*
👆👆👆kama wewe ni Mkristo utaijua habari hii ya Samsoni na Delila, Delila aliutafsiri upendo ni Samsoni amwambie siri ya nguvu zale,lakini lengo la Delila lilikuwa kumuuza Samsoni kwa adui zake.
👉Upendo wa kuuana,kupotezeana mwelekeo wa tumaini langu siyo upendo,ila ni Sumu iliyopakwa asali. ( _Upendo wa walokole ni mwingi sana kwa watu ambao hawajaokoka,maana hufunga na kuomba kuwaombea wale wenye shida,wasiomjua Mungu watoke mikononi mwa shetani,hulipa gharama ya kiuchumi,kuandaa mikutano,safari kwenda kuwahubiria neno la Mungu,kuombea watu wenye vifungo vijakali mpaka wafunguliwe wawe huru, huu ni upendo mkubwa,ambao mpagani hawezi kufanya,gharama kuilipa,ya kufunga siku 3,7,10,14 huli chakula,hunywi maji,na unatoa pesa laki 1,5,mil 1,2 ili muite muhubiri awaletee sulihisho hawa wapagani wanao teswa na mapepo na wachawi, huu ndo upendo mkuu_  upendo wa kwenda kilabuni kupiga bia,kufanya zinaa,na vijiwe vya story za kihuni,huo siyo upendo sahihi.
*Kwa nini walokole kujitenga na wamataifa?*
👉Tumeishaanza kuona majibu,wanajitenga kwakuwa hawafanani matarakio yao na matendo yao,kipa mmoja anajiadhari mwenzake asimuondoe katika lengo lake. Mbali na hiyo Neno la Mungu limeonya mahusiano yasiyo zaa jambo jema kati ya walokole na wapagani yasowepo.
*2Wakorintho 6:15-17*
14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 

15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 

16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
*_Msitari wa15,na 17 ina majibuya wazi,ni katika kulinda kitu kinachoitwa Utakatifu_*  Kujitenga huku si kama wanavyokusema wale wasiookoka, kujitenga huku kunalenga kutoambatana katika mambo yawezayo kuchafua vazi lako la wokovu la usafi( ila mtu akianza harakati hizo,uhesabika kuwa anajitenga kwa mambo yoote)
_Aliye okoka hapaswi kuafuatisha kila kitu wanachokifanya wapagani,maana lengo letu siyo moja_👇👇👇👇
*Warumi 12 : 2 - Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.*
👉Pointi ya tatu ya walokole wengi wachoyo,waongo,wenye viburi nk.... Hii inategemea aliyeona haya matabia ni wa mlengo gani,anatasiri wokovu katika sura ipi,aliomba nini mpaka akaona ni wachoyo,alisikia wanasema nini mpaka akasema niwasengenyaji( huwenda walikuwa wakisema tabia zake mbaya,zinawaumiza,waongea ili wamwonbee atoke huko, nk) mfno, vijana wengi wakiume wasiookoka huwasema vibaya wasicgana wakilokole kwamba wana viburi,wanajiona,wachoyo, kisa alimtongoza akakataa,alimshiti,alimpa kauli ya usirudi tena. _lakini biblia inasemaje kwa mtazamo wa watu wa mataifa kwa walokole? Huyu ni Yesu mwenyewe anasema haya maneno_👇👇👇
*_Yohana 15 : 19 - Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia._*
👆👆Sasa siku zote mtu anaye kuchukia hata ungetenda jema analiona baya,hatakusena vizuri kwa lolote. Ila mzizi wachuki umetokana na kutofautiana na njia.
*_Pointi ya nne ya wao kutokuwa na mahusiano na watu wanao lala nao au kaa nao_* Hii inarudi katika tafsiri ya mwanzo ya watu wenye mahusiano mazuri lazima wawe na lengo moja,wanafanya mambo yanayo fanana, mfano chuoni, *_Mpo hostel  wanafunzi wa4, mmoja ameokoja watatu hawajaokoka, au vice versa, huyu anakuja na demu wake,au boyfriend wake kufanya uchafu humo,huyu hana hayo mambo,au hawa wanakuja na bia huyu hanywi,twende disco hutu hawezi kwenda njia yake na katiba yake hairuhusu, automatically watamwona hafai,anajitenga anajifanya mtakatifu,siyo anajifanya ndivyo ilivyo ni mtakatifu,hapaswi kushiriki matendo ya giza_*
👉Kwa lugha fupi ni kwamba wanatimiza kilichoandikwa na kusemwa na Mungu kupitia neno lake.
*_Waefeso 5 : 11 - Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;_*
👆Ukiyakemea matendo yao hayo,ya ulevi,ngono,ukahaba,disco,nk ndo utaonekana wewe unajifanya mtakatifu sana,na ndipo utaanza kuambiwa wewe nawe unadhambi,unakufuru kujiita mtakatifu. Hii kwa walokole si jambo la kushangaza *Hata Yesu mwenyewe walimsema hivyo,aliposema mimi ni mwana wa mungu* kwa hiyo ni mwendelezo wa kile kilichoanzishwa na mwasisi wa imani ya Kikristo.👇👇👇
*Mathayo 26:59-67*
59 Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua; 

60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi. 

61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu. 

62 Kisha Kuhani Mkuu akasimama akamwambia, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini? 

63 Lakini, Yesu akanyamaza. Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu. 

64 Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni. 

65 Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake; 

66 mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa. 

67 Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi, 
Pointi ya 5, Nini kifanyike kuwasaidia watu wa aina hiyo, ni hii.... *_Jambo la ili usione tatizo lao KUOKOKA kuamua kuambatana nao hilo ndo jibu la msingi,utakuja kuona mpo kitu kimoja,mnashirikiana,mnapendana na hautaona utofauti ulokuwa ukiuona kwanza. Ukiokoka unakuja kwe ye familia ya Mungu,kwa hiyo mnakuwa na upendo wa kindugu_* kama watoto wa familia moja ya Kimungu.
*Yohana 1:12*
_Bali wote wakiompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu ndoyo wale waliaminio jina lake_
*NDUGU MPENDWA KARIBU KWA YESU*
_Imeandaliwa na Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078

WALOKOLE NA WAPAGANI

*SWALI KUHUSU WALOKOLE NA MAHUSIANO NA WATU WA MATAIFA*
      _______
Ninaswali kiongozi.
Linanitatiza sana napenda nijibiwe kwa fikra zaidi moja.

1) _Hivi kwanini walokole wengi huwa hawana upendo na watu wasio walokole.. Yaani hujitenga sana kiasi cha kuweka mipaka._

2.) _Nimeliona hili nilipokuwa sekondari mpaka chuoni.Hasa wale wa makanisa wanaoita ya kiroho_

3.) _Lakini matendo yao wengi ni Wachoyo Wasengenyaji,Wachochezi,Viburi_

4.) _Na hawana uhusiano mzuri na watu anaolala nao kwa kujiona wao ni watakatifu sana hawatakiwi kuwa karibu na mataifa hata kwa jambo la jumuia kama kusoma na michezo (mpira wa miguu na pete)_

5.) *Naomba unisaidie.*
_Chanzo ni nini..Nini kifanyike kuwasaidia walokole wa namna hii maana kila taasisi wapo tena wengi tu._


*Mchambuzi wa Swali hili ni Ev Elisha  Kazimoto*
WhatsApp 0755444078.
_Ndugu na rafiki yangu uliye uliza swali,swali lako ni moja,ila *nimelitenga katika vipengele 5 ili Nikupe ufafanuzi kwa kuzingatia vipengele hivyo* naamini kufikia mwisho utajua Walokole ni watu gani na kwa nini wanaishi maisha hayo unayoyaona na kuyatafsiri hivyo ulivyo uliza swali lako_
👉Swali lako majibu yake yapo kimaandiko zaidi kuliko kifikira,na kwakuwa umeuliza vizuri kuwa *_.....Hasa walokole wa Makanisa ya Kiroho....._* tayari tunatafuta Itikadi yao,katiba yao inawaelekeza vipi ndipo tujue namna ya kuelezea tabia zao. ( _Kwanza tuanze na Ufunguo wa Kwanza wa Msitari wa biblia unaotuonyesha Chanzo cha watu 2 kutofautiana tabia na matendo_)👇👇👇👇
*Amosi 3 : 3 - Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?*
👉Hapa Biblia inaongelea watu wawili walio eneo moja(Duniani) ila wanasafiri kwenda maeneo 2 tofauti( Mbinguni na Jehanamu) _Safari ya watu hawa,ina mahitaji mawili tofauti,kila njia ina kanuni zake,mizigo yake ya kusafiri nayo,maadili yake, kila mmoja anaenda kulingana na kanuni za aendapo, ndo akasema *hawa watu, hawawezi kwenda pamoja sambamba,kushikamana,mpaka kwanza wapatane, aidha wakubaliane njia moja iwekwe pembeni,watumie njia moja, yaani mmoja wapo,aamue kuachana na njia yake,afuatane na mwenzake,hapo watatembea pamoja,wata panga moja,watashirikiana katika kila jambo maana wamepatana kutembea njia moja*_ 👉Sasa Watu waliookoka,(walokole) huonekana tofauti na wapagani kutokana na kutofautiana *katika kile wanacho kiamini,maadili ya safari yao, tumainilao* aliyeokoka Anaambiwa,na anaamini Kuishi maisha matakatifu hapa duniani,ambaye hajaokoka,au mwana dini anasema huwezi kuishi maisha matakatifu hapa duniani, tunaokoka baada ya kufa. (Kwa hilo tu,watatofautiana mahitaji ya kuishi,kukaa,kufanya mambo yao) anaye amini katika utakatifu *Atajilinda na mambo mengi,* asiye amini katika utakatifu,hana kizuizi,atafanya lolote,na kuishi vyoyote.👇👇👇👇👇
*_Waebrania 12 : 14 - Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;_*
👆👆👆👆Aliyeokoka ameambiwa atafute utakatifu,maana hakuna mtu atakaye mwona Mungu asipokuwa nao. Ambaye hajaokoka hana sharti hilo.
*_1 Petro 1:15 - 16 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; 16. Kwakuwa imeandikwa mtakuwa watakatifu,kama mimi ni mtakatifu_*
👆👆👆hii ndo sababu ya walokole kuwa makini na nazingira yanayoweza kuwaondolea sifa ya utakatifu.
*Sasa nianze namba moja hadi nyingine katika swali lako moja la msingi, kwa nini walokole wanaonekana hawana upendo lwa mataifa*
_Kwanza hapa niweke sawa,tunatofautiana katika kutafsiri neno upendo, kunaanaye tafsiri upendo,mwingine Anaamini upendo ni mtu kuambatana na mimi katika kila jambo nitakalo mwambia,liwe zuri au baya akikubaliana nami huyo anamipenda(huu ni mtazamo wa mtu asiye sahihi)_👇👇👇
*_Waamuzi 16 : 15 - Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi._*
👆👆👆kama wewe ni Mkristo utaijua habari hii ya Samsoni na Delila, Delila aliutafsiri upendo ni Samsoni amwambie siri ya nguvu zale,lakini lengo la Delila lilikuwa kumuuza Samsoni kwa adui zake.
👉Upendo wa kuuana,kupotezeana mwelekeo wa tumaini langu siyo upendo,ila ni Sumu iliyopakwa asali. ( _Upendo wa walokole ni mwingi sana kwa watu ambao hawajaokoka,maana hufunga na kuomba kuwaombea wale wenye shida,wasiomjua Mungu watoke mikononi mwa shetani,hulipa gharama ya kiuchumi,kuandaa mikutano,safari kwenda kuwahubiria neno la Mungu,kuombea watu wenye vifungo vijakali mpaka wafunguliwe wawe huru, huu ni upendo mkubwa,ambao mpagani hawezi kufanya,gharama kuilipa,ya kufunga siku 3,7,10,14 huli chakula,hunywi maji,na unatoa pesa laki 1,5,mil 1,2 ili muite muhubiri awaletee sulihisho hawa wapagani wanao teswa na mapepo na wachawi, huu ndo upendo mkuu_  upendo wa kwenda kilabuni kupiga bia,kufanya zinaa,na vijiwe vya story za kihuni,huo siyo upendo sahihi.
*Kwa nini walokole kujitenga na wamataifa?*
👉Tumeishaanza kuona majibu,wanajitenga kwakuwa hawafanani matarakio yao na matendo yao,kipa mmoja anajiadhari mwenzake asimuondoe katika lengo lake. Mbali na hiyo Neno la Mungu limeonya mahusiano yasiyo zaa jambo jema kati ya walokole na wapagani yasowepo.
*2Wakorintho 6:15-17*
14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 

15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 

16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
*_Msitari wa15,na 17 ina majibuya wazi,ni katika kulinda kitu kinachoitwa Utakatifu_*  Kujitenga huku si kama wanavyokusema wale wasiookoka, kujitenga huku kunalenga kutoambatana katika mambo yawezayo kuchafua vazi lako la wokovu la usafi( ila mtu akianza harakati hizo,uhesabika kuwa anajitenga kwa mambo yoote)
_Aliye okoka hapaswi kuafuatisha kila kitu wanachokifanya wapagani,maana lengo letu siyo moja_👇👇👇👇
*Warumi 12 : 2 - Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.*
👉Pointi ya tatu ya walokole wengi wachoyo,waongo,wenye viburi nk.... Hii inategemea aliyeona haya matabia ni wa mlengo gani,anatasiri wokovu katika sura ipi,aliomba nini mpaka akaona ni wachoyo,alisikia wanasema nini mpaka akasema niwasengenyaji( huwenda walikuwa wakisema tabia zake mbaya,zinawaumiza,waongea ili wamwonbee atoke huko, nk) mfno, vijana wengi wakiume wasiookoka huwasema vibaya wasicgana wakilokole kwamba wana viburi,wanajiona,wachoyo, kisa alimtongoza akakataa,alimshiti,alimpa kauli ya usirudi tena. _lakini biblia inasemaje kwa mtazamo wa watu wa mataifa kwa walokole? Huyu ni Yesu mwenyewe anasema haya maneno_👇👇👇
*_Yohana 15 : 19 - Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia._*
👆👆Sasa siku zote mtu anaye kuchukia hata ungetenda jema analiona baya,hatakusena vizuri kwa lolote. Ila mzizi wachuki umetokana na kutofautiana na njia.
*_Pointi ya nne ya wao kutokuwa na mahusiano na watu wanao lala nao au kaa nao_* Hii inarudi katika tafsiri ya mwanzo ya watu wenye mahusiano mazuri lazima wawe na lengo moja,wanafanya mambo yanayo fanana, mfano chuoni, *_Mpo hostel  wanafunzi wa4, mmoja ameokoja watatu hawajaokoka, au vice versa, huyu anakuja na demu wake,au boyfriend wake kufanya uchafu humo,huyu hana hayo mambo,au hawa wanakuja na bia huyu hanywi,twende disco hutu hawezi kwenda njia yake na katiba yake hairuhusu, automatically watamwona hafai,anajitenga anajifanya mtakatifu,siyo anajifanya ndivyo ilivyo ni mtakatifu,hapaswi kushiriki matendo ya giza_*
👉Kwa lugha fupi ni kwamba wanatimiza kilichoandikwa na kusemwa na Mungu kupitia neno lake.
*_Waefeso 5 : 11 - Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;_*
👆Ukiyakemea matendo yao hayo,ya ulevi,ngono,ukahaba,disco,nk ndo utaonekana wewe unajifanya mtakatifu sana,na ndipo utaanza kuambiwa wewe nawe unadhambi,unakufuru kujiita mtakatifu. Hii kwa walokole si jambo la kushangaza *Hata Yesu mwenyewe walimsema hivyo,aliposema mimi ni mwana wa mungu* kwa hiyo ni mwendelezo wa kile kilichoanzishwa na mwasisi wa imani ya Kikristo.👇👇👇
*Mathayo 26:59-67*
59 Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua; 

60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi. 

61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu. 

62 Kisha Kuhani Mkuu akasimama akamwambia, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini? 

63 Lakini, Yesu akanyamaza. Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu. 

64 Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni. 

65 Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake; 

66 mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa. 

67 Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi, 
Pointi ya 5, Nini kifanyike kuwasaidia watu wa aina hiyo, ni hii.... *_Jambo la ili usione tatizo lao KUOKOKA kuamua kuambatana nao hilo ndo jibu la msingi,utakuja kuona mpo kitu kimoja,mnashirikiana,mnapendana na hautaona utofauti ulokuwa ukiuona kwanza. Ukiokoka unakuja kwe ye familia ya Mungu,kwa hiyo mnakuwa na upendo wa kindugu_* kama watoto wa familia moja ya Kimungu.
*Yohana 1:12*
_Bali wote wakiompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu ndoyo wale waliaminio jina lake_
*NDUGU MPENDWA KARIBU KWA YESU*
_Imeandaliwa na Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078

Tuesday, 12 September 2017

TATIZO LA KITANDANI

*Swali: Utafanyaje ikitokea umefunga ndoa na kijana unaingia ndani siku ya kwanza,anashindwa kufanya kazi,wiki,mwezi...mnara hausomi.?*
_Anajibu Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078
*_Kwanza kabisa,wapendwa suala la ndoa ni suala tata sana na jepesi sana,na ni la kiroho 50% na la kimwili 50%,kwasababu hiyo umakini u ahitajika sana_*
👉Nianze kwa kuwashauri vijana na kuwaondolea wasiwasi, Ndoa inahitaji uiendee ukiwa vizuri mbele za Mungu,uwe na uwezo wa kiroho wa kuweza kushughulika na changamoto mbakimbali kiroho na kimwili,.
👉Ukiiwndea ndoa ukiwa vizuri na Mungu atakupa mtu wa kufanana na wewe,atakuepushia balaa zingine kama hizo( _Lakini kama zitaruhusiwa na Mungu,ujue Mungu ameona uwezo wako wa kiroho unaliweza kulibeba,na litakuwa na jibu,maana biblia inasema Mungu hakupi jaribu zaidi yaimani yako_) kwa hiyo ukiwa na Mungu vzr utavuka kwa namna atakavyo kupa njia ya kutokea,jaribu halikai daima, adhabu ndo inakaa daima,na jaribu haliumizi na kujuondoa mstarini,ila linakuimarisha na kukupa hatua.
👉 Pia vijana ambao hamja oa,kuweni na maarifa ya kuombea ndo yako ijayo,ombea kila kitu acha kuwa na aibu mbele za Mungu, mfn. *_Ukiwauliza wachumba mlo humu,na wana ndoa,nani alikuwa akiomba Mungu ampe mme au mke wa kumtosheleza katika tendo la ndoa,ampe mtu wa size yake kimaumbile?_* utakuta katika 100 ni 5 tu au 2.tunakosa maarifa wakati mwingine, Ndoa ni taasisi inayo windwa mno,unaweza andaliwa stress kubwa na shetani ili uiache imani. Haya mambo yashugulikie mapema kuwa wazi kwa baba,au *Unatatizo mwambie Mungu ili tatizo mbona litamnyima furaha mwenzangu?* shugulikia
*Usipo kaa na Mungu vizuri na Mungu,ndo utajichanganya kufanya sex kabla ya ndoa ili kujua uzima wa mwenzako, ndugu yangu huja win ila ume fail, vp ukishaoana ukakatika kiuno? Au ukapoteza viungo muhimu vya kukusaidia kufanya sex kwa uhuru?utakaa kwenye ndoa au utatoka?* silaha kubwa kwako kijana si kuogoa changamoto bali kujiweka vzr na Mungu atakupa mtu sahihi na aliye vizuri.
👉Jambo lingine, *_watumishi wa Mungu tumezidi kuongea na vijana,wawe wawazi,kusema kama yuko fit au anamapungufu, lakini pia waaimamizi wa ndia ni watu wakaribu kwa hawa wana ndoa watarajiwa, wa kiume kwa wakiume,wakike kwa wakike,kuulizana ata kutazama kama minara inasoma. Huku wachungaji nikumwapisha kijana,hata kabla ya kufunga ndoa,tuhakikishie uimara wako,hatuitaji kesi baada ya ndoa_* nyakati hizi haya yanafanyika.
👉 Lakini kuna suala la kushambuliwa ki nguvu za giza,unaweza kuwa fit,kijana au binti,ila unaingia ndani tu, kijana unaona laini haisomi,wiki,mwezi nk,au mdada ile kubisha hodi mlangoni wala hata kuweka mguu ndani,binti kilio machozi kama maji,maumivu makali, utafanyaje ?ndo maana yangu ya kuwa na mngu vizuri. *Ntawaletea somo la maandalizi ya kiroho ya kuingia katika ndoa* kuna kina ameo rafiki yangu mwaka jana yuko fiti,ila kwenye harusi walichezewa game na wachawi,mambo ya zawadi mtu alimpa pipi akala wakati wa kutoa zawadi,na sabuni, kufika ndani walionja tu,network zika kata miezi karibu3,walipanda mlimani,network zikarudi, mwezi ulo pita wamepata mtoto. Sasa si kila network kukata ni ugonjwa kwamba kijana hakusema,kuna *Kushambuliwa*
👉Jambo lingine,watu mkiwa katika uchumba,nimambo ya kawaida, kumuuliza kitekiniki mfano, *_Ana ugonjwa gani,tatizo linalo msumbua, nk_,amezaa watoto,kuna ex wake anaye msumbua,* na wakati wa kuwa wazi ili kuepusha migogo ya ndoa baadaye.
*Kama mmepitia hatua zote tangu mwanzo,na mmewashirikisha watumishi wa Mungu (walezi)wenu tangu mnaanza mtaepusha mengi,wanajua mengi, shida ya vijana wanachumbiana kimya kimya wanawashirikisha watumishi yote walisha maliza,sasa ukiambiwa *huyo kijana ni Toashi mnara hausomi,utakubali,?au utaona wanakuonea wivu, au huyu binti ametoa mimba nyingi na kizazi hana,utaamini, au huyu kwao wachawi naye dada ni mpaaji balaa,utamuacha na mmeisha fika mbali?* shirikisha watumishi mpunguze matatizo.
👉Kama limekukuta kama huyo honeymoon *_Usipaniki,tulia,ongea na mwenzako kwa upendo na utaratibu,ujue ni tatizo la kuzaliwa,ukubwani,ndo wa kuathirika na kunichua,au ndo ameshambuliwa, kama lipo nje ya uwezo wenu,waone watumishi wawashauri,wawaombee,kama ni hospital mpate matibabu, maadamu mmependana,mmekubaliana kuoana,na kuapa kuishi wotw milele Mungu atatoa njia_*
NB: kwa watumishi wengine kama kijana ni Toashi,yaani hafanyi kazi,wanaifungua ndoa,maana ndoa inakamilika kwa tendo la ndoa.
*Ev Elisha Kazimoto*
0755444078

Monday, 11 September 2017

MAHUSIANO MTANDAONI

*_Tunafunga mada hii kwa namna hii_*
_Ifike hatua,vijana wa kike na wakiume,mjue jambo moja kuwa, ndoa siyo biashara,kwamba nisipo pata wateja soko hili napeleka pengine na nikipata hasara ntafanya biashara nyingine. Ndoa ni maisha,unapo amua kuoa au kuolewa,unatengeneza mkataba wa maisha ya Amani,au wa majuto mpaka kaburini(kwa ndoa za wana wa Mungu )hivyo usifanye mambo ya RISK(kujihatarisha)ndo maana vijana wengi wanasema siku hizi hakuna waoaji,na wakaka wanasema hakuna wanawake waolewaji,ndoa hazidumu ila migogoro ni mingi, shida vijana MNA RAHISISHA SANA NDOA kama kumtuma mtoto kwa MANGI DUKANI ANUNUE CHUMVI, ndoa inahitaji;_
👉  *Maandalizi ya kisaikolojia ,kimwili na kiroho*
👉 *Ndoa inahitaji Uhakika wa kujiridhisha kuwa chaguo hili litanifaa kiroho,kimwili*
👉 Ndoa ahitaji kudhania(to predict) mbeleya safari atabadirika
👉 *Ndoa inahitaji uingie na mtu unaye mfahamu vizuri,ndo maana inashauriwa,usimtamkie mtu kumuoa/kukubali  akuoe bila kumfahamu kwa kina*
_Sasa jambo la hatari na kushangaza,unaanzishaje mahusiano online mtu humjui(hamjawahi kumeet face to face),huu si niuongo wa Phd,ukiulizwa,umenipendea nini,unajibu( utasema sura?),anavyo type haraka? Voice note zake au,tabia?umeiona wapi........ Kwa namna hii wengi wameoa majini_
*Unaachiaje moyo kwa mtu,moyo wa upendo wa ndoa kwa mtu usiye jua kwao,hujui ndugu zake,wazazi,historia yake na familia, ndo maana wengi wanapigwa mimba na kuachwa,wengine wanaolewa kwa wachawi balaa,watoto wako wote wanaliwa wakiwa wadogo*
Vijana msiseme siku hizi ndoa mbovu,sema ninyi ndo wabovu,mke/mme unempataje?yaani *_Eti unavyoona watu wanachangia humu,fasta unafata mtu inbox,nimekupenda tuanze mahusiano yakuelekea ndoa, wee Jambazi mkubwa,unependa au umetamani na hujui unalofanya,_*
Ndiyo maana wachumba wote mnaowapata mitandaoni wanawapiga kibuti humo humo mitandaoni.
*KAA ULIMPENDA MTU ONLINE SASA AMANI INATOWEKA JUU YAKE,UNATAKA NINI,URUDISHIWE AMANI FEKI YA KISHETANI ILI UFE? HUTAKI MUNGU AKUSAIDIE KUKUEPUSHA MABAYA?*
   Ev Elisha-Counselor

Saturday, 9 September 2017

UCHUMBA,MUDA WAKE KISAIKOLOJIA NA KIROHO

*UCHUMBA NA MUDA WAKE KISAIKOLOJIA NA KIROHO*
      _Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078
_Shalom vijana wote mnao taka kuingia katika mahusiano na mlio kwenye mahusiano, karibu tuchambue Uchumba na makando kando yake kisaikolojia na kiroho_
👉 Kuna mkanganyiko kati ya uchumba na urafiki(mahusiano) kwanza nivitofautishe hivi vitu viwili ili tujue muda unao faa wa uchumba,na muda wa kutambulishana kwa wazazi na marafiki nk.
1⃣ *Mahusiano ya kirafiki* ni mahusiano yaliyojengeka baina ya watu wawili,yenye msingi wa *_Mrandano,kupatana,na kuona umuhimu wa Huyo mtu katika kufikia malengo flani_* mahusiano ya kirafiki ndani yake hayana kauli ya agano la kuoana,na mara nyingi urafiki auna siku maalumu ya kuunda,ila unatokea Autonatic kutokana na kuona vitu flani muhimu juu ya mtu mwingine vinavyo kufaa wewe,ndipo ukaribu uanza kujengeka na kugubdua mnaelewana sana.
👉Urafiki hauna mtu mmoja,unaweza kuwa na marafiki hata zaidi ya 10,20 ila marafiki hutofautiana ukaribu kulingana na vitu kila mmoja alivyo navyo vinavyo kuvutia.
👉Katika urafiki wa kijana na binti hauna habari za ndani za kiba,wala hakuna makubaliano yoyote(wala hakuna zuio la huyo rafiki,kumnyima uhuru wa kuwa na maamuzi mbadala ya kuwa na marafiki wengine wengi)
👉Lakini katika urafiki haishauriki ufunue siri zako zote kwa hao/huyo rafiki maana hauna afano naye, na pamoja na kuwa naurafiki wa kina kuna mipaka mikubwa ya kufanya vitu(sex no,mazawadi ukiyatoa hakuna ujira wake,wala tegemeo maana hakuna agano)
👉 *Uchumba* Ni hatua nyingine kubwa inayo husisha maamuzi ya watu wawili,wanaoona waweza kuishi pamoja kama mke na mme,walio tayari kupeleka taarifa zilizo rasmi kwa watu wanaohusika katika pande zote mbili,ili kurasmisha nia yenu ya kuoana,hatua hizi zifuatazo zikifanyika ndo watu uitwa Wachumba:-
1⃣ Wawili walopendana kukubaliana kuwa twaweza kuoana.
2⃣Walezi wa kiroho wenu kupewa taarifa(hapa ziko aina 2 za taarifa,moja _Kuna taarifa ya kuna mtu nimemuoana anahitaji kunichumbia/kumchumbia vipi maisha yake ya kiroho na ya kimwili kwa ujumla_) sasa mlezi wa kiroho atakacho kwambia ndo kina kupa kuendelea mbele au kusitisha safari. Taarifa ya pili ni, _Baba nina mtu niliyempata tayari,tumeongea,tumekubaliana kuoana,sasa tunalileta mbele yako ili liwe rasmi na taratibu zote zianze za kuelekea ndoa_
3⃣ Kupeleka barua ya posa kwa wazazi wa binti,ukikubaliwa mnaendelea mbele. Ikigoma basi hekima zingne utafutwa.
4⃣Kupima afya zenu kama mna maambukizi au la, kama kuna maambukizi,safari imeishia hapo,au mpaka kwa maridhiano mengine.
5⃣Taratibu za kutambukishana kifamilia hufuata.
_Baada ya hatua hizo muhimu ndipo wengibe hupeleka mahari ya kwanza,ili wazazi waruhusu hatua ya kuvikana pete💍💍 ndipo sasa Hasa watu uitwa wachumba,na kanisani utangaza Rasmi flani na flani ni Wachumba_ *Na hiyi ndo hatua rasmi ya hatua watu kuitwa Wachumba* kabla ya hapo ninyi ni *_Marafiki tu kwa lolote la kutokea,break up,kutapeliwa pesa,mali nk usimlaumu mtu yeyote ukubali kuumia peke yako_*
👉Sasa suala la *Kutambulishana kwa marafiki na ndugu* nimerleza hapo juu hatua hizo zikifuatwa automatic kuna watu watakuwa wamejua kulingana na hatua mnazoingia na ukaribu na umuhimu wa watu kwenu. Ila kwa marafiki wengine mnajitambulisja kulingana na umuhimu wa rafiki yako kwako.
*Ushauri wa kisaikolojia na kiroho,usifanye biashara ya kutambulisha mahusiano yako kwa kila mtu,maana kuna Athari kuu 2,ya kiroho na kisaikolojia :*
1⃣ Kisaikolojia, kwakadiri watu wanavyoongezeka wanaojua mahusiano yako,utapata changamoto ya mahusiano yako kuchambuliwa,kuibuliwa madhaifu ya mwenzako,kuzushiwa mambo mabaya,jambo ambalo linaweza athiri mahusiano yenu,upendo,kuaminiana nk.hata kurumbana kwasababu ya maneno ya watu
2⃣ Kwa kadiri mnavyo ongeza idadi ya watu kufahamu mahusiano yenu,ndivyo *Mnavyoongeza uwanja wa mashambulizi ya kiroho juu ya safari yenu ya ndoa* hivyo mjipange, mishale kutoka kwa watu 5,kuikwepa ni rahisi kuliko itoke kwa watu 100.
👉 *Muda wa kukaa katika uchumba* unategemea na maandalizi na uwezo wenu juu ya harusi. Japo inashauriwa isipungue miezi 6,na isizidi miaka 1.5 hadi 2 kuepusha uchumba kuvunjika,kuchokana na kuanguka katika dhambi ya zina.( na muda maana yake unahesabika tangu mlipoitwa wachumba kwa mujibu wa hatua nilizoeleza juu) wengi  mna hesabu na muda wa urafiki ambao unakuta miaka 3,4...jambo ambalo si kweli.
NB: _Uchumba si ndoa,ni ruksa kuvunja hata siku mnakula kiapo ukakataa,ndoa haifungwi,na hakuna dhambi,maadamu kuna the shocking information,isiyo vumilika. Ndiyo maana pia,kisheria kabla ya siku ya kufunga ndoa,uchunba unatangazwa siku 21,na fomu zibabandikwa makanisani,akitokea mtu anasababu ya kusitisha,anaruhusiwa. Japo,omba sana lisikutokee maishani ni kovu la kisaikolojia la kukugharimu kimawazo._
*Ulikuwa nami mchambuzi wa masuala ya mahusiamo na ndoa Ev Elisha Kazimoto*
WhatsApp 0755444078

Friday, 8 September 2017

NITAZIMA SHANGWE ZAO GHAFLA

✅ *NITAZIMA SHANGWE ZA ADUI ZANGU GHAFLA*✅
   *_Ev Elisha Kazimoto_*
    WhatsApp 0755444078
_Shalom watu wa vita. Usiku huu wa mkesha ni usiku wa Operation ya Kuzima shangwe ya adui zangu ghafla_
*WAAMUZI 16:23-30*
23 Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu. 

24 Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu. 

25 Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, Mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili. 

26 Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, Niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea. 

27 Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza. 

28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili. 

29 Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto. 

30 Samsoni akasema; Na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. Basi wale watu aliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati wa uhai wake. 
👉👆Kupitia mistari hiyo,Roho wa Bwana akufundishe kitu tunapoenda kuanza maombi ya kuzima Shangwe ya hao maadui wanao shangilia shida yako.
👉Samsoni alilibeba kusudi la Mungu,na alitumika kwa nguvu zake zote kuhakikisha Mungu anainuliwa daima( _Hii ndiyo kazi tunayo fanyasiku zote,na kama unahitaji ushindi siku ya jaribu lako tumika kwa Mungu kwa nguvu zako zote_)
👉👆Utumishi wa Samsoni ulileta hasara kubwa kwa maadui wa taifa la Mungu (wafilisti),walimsagia meno,walimuwinda kumuua( _Ndicho kinacho endelea kwako na kwangu,tunapo omba,fanya kazi ya Mungu kwa nguvu,ni hasara kwa shetani,wachawi nk, wanaanza kutuwinda watuue_)
👉👆Samsoni alipita katika  *kipindi cha kutoona, kutokuwa na tumaini,nywele hana,macho hana,na yupo katika kambi la adui zake* ( _Hiki ni kipindi cha wengi wanakipitia,adui amekushambulia,huoni njia,jaribu kali wala hujui na huoni pa kupenyea,lakini watu wanakudhihaki kwa jaribu lako,tatizo lako_)
👉👆Wafilisti walishangilia,walisifu miungu yao na mungu wao Dagoni wakisema mungu wao amemtia Samsoni adui yao mikoni mwao( _Unapo pita katika jaribu na wakati mambo yako magumu,ndoa ina shida,uchumi umeyumba,umri unaenda hujaoa au kuolewa,bado Uzao huna katika ndoa miaka inasonga,wapo wanao dhihaki,wanashangilia,wanadhani dawa zao,kafara zao,mganga wao amekushugulikia, *Hilo lisikuvunje moyo* hicho ni kipindi tu cha Nywele za Samsoni hazijaota_)
👉👆Nywele zako zokiwa bado fupi hazijaota,utatukanwa matusi yote,kila mmoja atakudharau,isikupe shida *Nywele zako zina rudi,utumishi wako mbele za Mungu hazijasahaulika,utazizima shangwe zao Ghafla*
👉👆Shangwe zilipo zidi za maadui wa Samsoni (wafilisti) waliitisha sherehe ili wamlete samsoni hadharani awachezee wafurahi(yaani wafurahie tatizo lake la kutokuwa na macho) ( _Siku zote adui zako huwa hawajui kipindi chao kupigwa na kuziba vinywa vyao,ili wewe utoke katika jaribu_) hawa wafilisti walimuita Samsoni wakasahau nywele zake zimeota tena( wakati wako unakuja,furaha yako inarudi tena)
👉👆Samsoni aliletwa haoni,ila kuna kijana alimshika mkono kumsaidia kwenda mwisho wa jaribu lake( _Nawe Mungu akuinulie mtu wa kukushika mkono akusaidie katika jaribu lako unapoelekea mwisho wake_)
👉👆Samsoni alipofika ukumbini maadui zake walishangilia kweli,shangwe ya dhiaka,ilimuuma sana(kama unavyoumia wewe unavyosimangwa), ila Samsoni akamwambia kijana yule aliye mleta *_Niache niziegemee nguzo hizi mbili ambazo jengo hili lote linazikalia_* (uuuuuuuh saa ya kichapo imefikaaa, shangwe yao inakwenda kuzima ghafla wao bila habari)
👉👆  *_Usiku wa leo tafuta nguzo mbili za jaribu lako,tatizo lako,maadui zako,twende kuzima shangwe ya wahuni waliotudhihaki muda mrefu_*
👉👆 Katika nguzo Samsoni aliomba maombi makali akiwa amezishikilia nguzo( *_Nawe sasa ukiwa umeshikilia nguzo za tatizo lako,za maadui omba maombi makali, mwambie Bwana nikumbuke leo nipate kuzizima shangwe za maadui zangu_*
👉👆 Kwa nguvu zote samsoni akazivuta nguzo,nyunva ikaanguka,na kuua watu wengi mno kuliko aliowaua kipindi cha uhai wake( _Maombi yetu leo tunavuta nguzo hizo za utasa,umaskini,magonjwa,kukataliwa na yote yanayo kusibu_) sikiliza, mwisho wa jaribu lako ni mkuu sana utukufu wake kuliko ulivyokuwa wakati unaanza tatizo.
_Sasa anza maombi ya kuita kwa nguvu, Ee Mungu unikumbuke sasa jengo hili la maadui liangushwe na shangwe zao zizimike_ Anza maombi.
     *By Ev Elisha Kazimoto*

NITAZIMA SHANGWE ZAO GHAFLA

✅ *NITAZIMA SHANGWE ZA ADUI ZANGU GHAFLA*✅
   *_Ev Elisha Kazimoto_*
    WhatsApp 0755444078
_Shalom watu wa vita. Usiku huu wa mkesha ni usiku wa Operation ya Kuzima shangwe ya adui zangu ghafla_
*WAAMUZI 16:23-30*
23 Kisha wakuu wa Wafilisti wakakusanyika ili kumtolea sadaka Dagoni mungu wao, na kufurahi; maana walisema, Mungu wetu amemtia Samsoni adui wetu mikononi mwetu. 

24 Na hao watu walipomwona wakamhimidi mungu wao, maana walisema, Mungu wetu amemtia mikononi mwetu huyu adui wetu, aliyeiharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu. 

25 Ikawa mioyo yao iliposhangilia, wakasema, Mwiteni Samsoni, ili atufanyie michezo. Basi wakamwita Samsoni atoke gerezani, akacheze mbele yao wakamweka katikati ya nguzo mbili. 

26 Samsoni akamwambia yule kijana aliyemshika mkono, Niache nizipapase nguzo ambazo nyumba hii inazikalia, nipate kuzitegemea. 

27 Basi nyumba ile ilikuwa imejaa watu waume kwa wake; na wakuu wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na juu ya dari palikuwa na watu elfu tatu waume kwa wake waliokuwa wakitazama, wakati Samsoni alipocheza. 

28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili. 

29 Kisha Samsoni akazishika nguzo mbili za katikati ambazo nyumba ile ilikaa juu yake, akazitegemea, moja kwa mkono wake wa kuume na moja kwa mkono wake wa kushoto. 

30 Samsoni akasema; Na nife pamoja na hawa Wafilisti. Akainama kwa nguvu zake zote; ile nyumba ikawaangukia hao wakuu, na watu wote waliokuwa ndani yake. Basi wale watu aliowaua wakati wa kufa kwake walikuwa wengi kuliko wale aliowaua wakati wa uhai wake. 
👉👆Kupitia mistari hiyo,Roho wa Bwana akufundishe kitu tunapoenda kuanza maombi ya kuzima Shangwe ya hao maadui wanao shangilia shida yako.
👉Samsoni alilibeba kusudi la Mungu,na alitumika kwa nguvu zake zote kuhakikisha Mungu anainuliwa daima( _Hii ndiyo kazi tunayo fanyasiku zote,na kama unahitaji ushindi siku ya jaribu lako tumika kwa Mungu kwa nguvu zako zote_)
👉👆Utumishi wa Samsoni ulileta hasara kubwa kwa maadui wa taifa la Mungu (wafilisti),walimsagia meno,walimuwinda kumuua( _Ndicho kinacho endelea kwako na kwangu,tunapo omba,fanya kazi ya Mungu kwa nguvu,ni hasara kwa shetani,wachawi nk, wanaanza kutuwinda watuue_)
👉👆Samsoni alipita katika  *kipindi cha kutoona, kutokuwa na tumaini,nywele hana,macho hana,na yupo katika kambi la adui zake* ( _Hiki ni kipindi cha wengi wanakipitia,adui amekushambulia,huoni njia,jaribu kali wala hujui na huoni pa kupenyea,lakini watu wanakudhihaki kwa jaribu lako,tatizo lako_)
👉👆Wafilisti walishangilia,walisifu miungu yao na mungu wao Dagoni wakisema mungu wao amemtia Samsoni adui yao mikoni mwao( _Unapo pita katika jaribu na wakati mambo yako magumu,ndoa ina shida,uchumi umeyumba,umri unaenda hujaoa au kuolewa,bado Uzao huna katika ndoa miaka inasonga,wapo wanao dhihaki,wanashangilia,wanadhani dawa zao,kafara zao,mganga wao amekushugulikia, *Hilo lisikuvunje moyo* hicho ni kipindi tu cha Nywele za Samsoni hazijaota_)
👉👆Nywele zako zokiwa bado fupi hazijaota,utatukanwa matusi yote,kila mmoja atakudharau,isikupe shida *Nywele zako zina rudi,utumishi wako mbele za Mungu hazijasahaulika,utazizima shangwe zao Ghafla*
👉👆Shangwe zilipo zidi za maadui wa Samsoni (wafilisti) waliitisha sherehe ili wamlete samsoni hadharani awachezee wafurahi(yaani wafurahie tatizo lake la kutokuwa na macho) ( _Siku zote adui zako huwa hawajui kipindi chao kupigwa na kuziba vinywa vyao,ili wewe utoke katika jaribu_) hawa wafilisti walimuita Samsoni wakasahau nywele zake zimeota tena( wakati wako unakuja,furaha yako inarudi tena)
👉👆Samsoni aliletwa haoni,ila kuna kijana alimshika mkono kumsaidia kwenda mwisho wa jaribu lake( _Nawe Mungu akuinulie mtu wa kukushika mkono akusaidie katika jaribu lako unapoelekea mwisho wake_)
👉👆Samsoni alipofika ukumbini maadui zake walishangilia kweli,shangwe ya dhiaka,ilimuuma sana(kama unavyoumia wewe unavyosimangwa), ila Samsoni akamwambia kijana yule aliye mleta *_Niache niziegemee nguzo hizi mbili ambazo jengo hili lote linazikalia_* (uuuuuuuh saa ya kichapo imefikaaa, shangwe yao inakwenda kuzima ghafla wao bila habari)
👉👆  *_Usiku wa leo tafuta nguzo mbili za jaribu lako,tatizo lako,maadui zako,twende kuzima shangwe ya wahuni waliotudhihaki muda mrefu_*
👉👆 Katika nguzo Samsoni aliomba maombi makali akiwa amezishikilia nguzo( *_Nawe sasa ukiwa umeshikilia nguzo za tatizo lako,za maadui omba maombi makali, mwambie Bwana nikumbuke leo nipate kuzizima shangwe za maadui zangu_*
👉👆 Kwa nguvu zote samsoni akazivuta nguzo,nyunva ikaanguka,na kuua watu wengi mno kuliko aliowaua kipindi cha uhai wake( _Maombi yetu leo tunavuta nguzo hizo za utasa,umaskini,magonjwa,kukataliwa na yote yanayo kusibu_) sikiliza, mwisho wa jaribu lako ni mkuu sana utukufu wake kuliko ulivyokuwa wakati unaanza tatizo.
_Sasa anza maombi ya kuita kwa nguvu, Ee Mungu unikumbuke sasa jengo hili la maadui liangushwe na shangwe zao zizimike_ Anza maombi.
     *By Ev Elisha Kazimoto*