🚍 *MWANAUME KAMA KICHWA* 🚍
*_Ev. Elisha Kazimoto_*
*0755444078*
🚗Tafsiri hii imechukuliwa kwa upeo wa chini sana na pande zote wanaume kwa wanawake, hali ambayo imepelekea ndoa nyingi kuyumba
🚗Tafsiri ya Mwanaume ni kichwa, wengine wameitafsiri kuwa Mwanaume ni mbabe katika familia, aliye Alfa na Omega, Dictator, asiyestahili kuheshimiwa, kushaurika nk
🚗Wengine wameitafsiri kuwa Mwanaume ni kichwa cha Kuhudumia Familia, kutafuta pesa, kulisha familia nk
🚗🚗Lakini kwa mtazamo wa Biblia na tafsiri halisi ya Mungu, mpaka Mwanaume kuitwa mfano wa Kristo Yesu, SI jambo dogo Kuna maana kubwa
🚗🚗Na kama wana ndoa watatumia, wataiangalia tafsiri ya biblia ndoa yao itakuwa Paradiso ndogo
🚗🚗Kiuhalisia na mtazamo wa Biblia, Mwanaume ameitwa ni kichwa cha mkewe na familia kwa ujumla, kama Yesu alivyo kichwa cha kanisa, kwa kutazama umuhimu na kazi za sehemu 7 za kichwa
🏢 *SEHEMU 7 ZA KICHWA NA KAZI ZAKE* 🏢
👦🏼Kichwa hiki unachokiona (Mwanamke kwa Mwanaume) ni kiungo kikubwa na kina kazi kubwa sana 7,
👦🏼Mwanaume ukitambua ulivyo wa pekee, na ukitumia kwa umakini sehemu hizo 7 ndoa yako utaifurahia milele
👦🏼Mwanamke ukitambua nafasi na umuhimu wa Mume wako kama kichwa na unatengeneza mazingira mazuri ya Heshima, Adabu, Utii na Unyenyekevu kwa mmeo, ndipo hizi sehemu 7 zitakuletea furaha, upendo na amani katika ndoa yako
👦🏼👦🏼Popote ukiona kichwa jua kina sehemu zifuatazo;Akili, Macho, Masikio, Pua, Ulimi, Mdomo (lips),na Meno haya ni maeneo muhimu sana
👦🏼👦🏼Utakuja kujua kwa nini Mungu alimpa Mwanaume nafasi au sifa ya kichwa na kumfananisha na Yesu Kristo
🏫 *SIFA NA KAZI ZA KICHWA* 🏫
🏡🏡UBONGO (AKILI):Kichwa kina ubongo ambayo ni injini ya maamuzi, fikra, tafakari ya mwanadamu
🏡Kazi kuu ubongo ni kuchanganua mambo kabla ya kufanya maamuzi, ni kuzalisha hekima na njia mbadala katika mambo magumu
🏡Mwanaume kama kichwa, unahitaji kutumia akili sana kufanya maamuzi ya faida kwa familia yako kwa amani, Biblia inasema hata Kuishi na mkeo kama mwili (uliobeba Moyo) unahitaji Kutumia AKILI SANA(1Petro 3:7)
🏡🏡MACHO:Macho ni kiungo muhimu sana, yana kazi kuu mbili, Kutazama na Kuona
🏡Kutazama, ni kutambua jambo likivyo ktk sura yake na Kuona ni Kuchanganua sura ya kitu na kukitendea kazi, kubaini ubora na mapungufu yake
🏡Mwanaume kama kichwa chenye macho unahitaji Kutazama na kuona mambo kwa mkeo na familia kwa ujumla, kuyachanganua, kujua yapi ni bora uyaboreshe na yasiyo bora utumie Akili kuyadhibiti
🏡Mwanaume macho yako (ya tafsiri ya kichwa) yakiwa mbovu ndoa itayumba (Mathayo 6:22-23)
🏡Macho yako kama Mwanaume (ya tafsiri ya kichwa) yakiwa vizuri, mkeo ataenjoy na ndoa yenu itakuwa salama. 🌏🌏MASIKIO:Masikio yana kazi ya kusikia na kusikiliza, hizo ni kazi kubwa na ngumu, kwa kuwa ndizo zinazo tengeneza mawazo na maamuzi
🌏Kusikia ni kupata sauti yoyote masikioni, iwe inamaana au haina,
🌏Kusikiliza ni kuweka umakini na utulivu, juu ya sauti unayoisikia na kujua ina maanisha nini na kwa nini isikike katika hali hiyo
🌏Mwanaume kama kichwa chenye masikio, ili ndoa yake iwe makini anahitaji Kuwa na uwezo mkubwa wa kutambua sauti ya mke wake na watoto wake, kujua hii sauti ya mke wangu inamaana gani na aifanyie maamuzi ya busara
🌏Mwanamke, anahitaji kujua mme wake anapata sauti nyingi huko na huko akiwa nje ya nyumba, akirudi ndani inabidi ni mpe sauti itakayo mfanya atulie, atabasamu na kunipenda zaidi.
🌏🌏PUA:Pua ni kiungo muhimu katika kichwa, ina mawasiliano na ushirikiano mkubwa na moyo na mapafu
🌏Lakini kazi ya pua ni kunusa(to detect) harufu nzuri na harufu mbaya na kufanya maamuzi ya kupokea harufu nzuri tu
🌏Mwanaume kama kichwa, unahitaji kunusa na kubaini harufu ya mambo yatakayo hatarisha ndoa na familia yako na kuyadhibiti, kunusa harufu za mambo mazuri mkeo abakufanyia uyaboreshe na kumtia moyo ili kulinda ndoa yenu.
🌏🌏Hayo yakizingatiwa mtaona kila siku mnacheka na kufurahiana daima..
🌏🌏Lakin Mwanamke ajue hasiruhu kuwa njia ya kupitisha harufu mbaya(kero) utaondoa amani kwa utaondo 🎒🎒MENO:Miongoni mwa viungo muhimu ktk kichwa, na msaada kwa tumbo ni meno, kazi kuu yake ni kuhakikisha usalama wa tumbo kwa vitu vyote vipitavyo kinywani
🎒Meno kazi yake ni kuvunja vunja vitu vigumu nakuviweka katika ulaini ili tumbo lipokee vitu salama
🎒🎒Mwanaume kama kichwa chenye meno, unahitaji kushughulika na mambo magumu, hatar kabla ya kumpasia mkeo, Hakikisha yakifika kwa mkeo hayata leta madhara
🎒Kuna mambo mengine ktk maisha, vifua vya kukabiliana nayo, tunatifautiana kati ya Mwanaume na Mwanamke, usipo Anglia utamfanya mkeo kukata tamaa
🎒Mwanamke mweshimu sana mmeo isimuone hivyo unavyo muona ukahisi ndo alivyo, Kuna vitu anamalizana navyo, anapambana, anaumia Makusudi wewe uwe na amani, ufurahi, maisha yaende
🎒Lakini wanawake wengine wanaweza kumdharau mme wake na kumbana muona wa kawaida sana, unakosea sana, yeye kana kichwa chenye meno anaumia kutafuna mambo magumu, ili wewe uenjoy maisha. 🚆🚆ULIMI:ulimi ni kiungo kikali sana, kinafanya kazi na akili, umasikio na macho ili kuhakikisha maelekezo yanayo tolewa na ulimi yako kamili
🚆Mwanaume kama kichwa chenye ulimi, unahitaji, kuonya mambo yasiyo na faida ktk familia yako yasiendelee, kufundisha mambo mapya ili kuisaidia ndoa yako,
🚆Kwa kutumia ulimi jua, ulimi una nguvu ya kujeruhi, na kuganga, hivyo unapoongea na mkeo onyesha kumjali, kumpenda na kumhurumia ili amani idumu
🚆Mwanamke unahitaji kujiadhari na tabia, vitendo vinavyo hudhi, ibua hasira,vitendo vya dharau, usimwonyeshee mmeo, ukivifanya atatumia ulimi vibaya kama kichwa na ATAKUJERUHI, na huo ndo utakuwa mwanzo wa migogoro mizito katika ndoa yenu.
*_By Ev Elisha Kazimoto_*
*0755444078*
Tuesday, 18 April 2017
SEHEMU 7 ZA KICHWA
Thursday, 13 April 2017
CHAGUO BAYA LA KUOA/KUOLEWA
💍💍 *UKICHAGUA VIBAYA,UTAISHI VIBAYA,UKICHAGUA VIZURI UTA ENJOY MAISHA*💍💍
_Ev Elisha Kazimoto_
*0755444078*
_Shalom vijana mnaojiandaa kuoa na kuolewa,na wale mlo katika mahusiano ya uchumba,leo nasema nanyi kwa ufupi sana kuhusu Hatima yako itokanayo na uchaguzi katika ndoa_
*_Mithali 22 : 1 - Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu._*
✍Kuna changamoto kubwa kwa vijana katika kuchagua wenzi wao wa maisha,utata huu unakuja pale kijana anapotaka kupata mtu kulingana na Plans/Interests zake(hapa ndipo palipo na kichefuchefu)
✍Kila chaguo nyuma yake kunamsukumo wa *Matamanio,Lengo na matarajio na muono wa macho ya muhusika* hiki ndo kichefuchefu kilicho wafanya wengi walipoingia kwenye ndoa Waanze Kutapika na Kuishiwa nguvu za kuishi katika ndoa.
✍Sasa watu wanakosea kuchagua kwa sababu ya kuwa na *Msingi Mbovu wa Kiroho, Msingi mbovu wa Malezi,Mazoea Mabaya ya maisha,Makundi ya watu wasio na malengo, Mtazamo/muono usio na nguzo shawishi* Vijana kuwa na umakini katika maandiko hayo juu katika (Bold style)kilio na vicheko katika ndoa vimetokana na maneno hayo,hata wewe uliye katika ndoa, _Umepotelea humo au umepata faida kutoka humo_
✍Unahisi kwa nini Biblia inasema *_Heri kuchagua jina jema kuliko Mali nyingi_* Jina ni Mtaji na Mali nyingi ni Faida,sasa upofu mwingi kwa vijana ni kukimbilia kuchagua faida na kuacha mtaji, sasa siku zote hakuna faida bila mtaji,na sibkila faida ni halali au njema(mfano kuna wenye mali nyingi lakini wamezipata kwa kafara,dhoruma,wizi na urithi na Akili ya Kimaendeleo)hawa wote wanaonekana wamefanikiwa ila ndani ya maisha yao kuna maumivu na wengine kicheko.
✍Msingi mbovu wa Kiroho(yaani kutokuwa na wokovu halisi,au wokovu wa njia panda,michanganyo) kumewafanya vijana kuchagua wenzi kwa hisia zao na mitazamo yao na si katika mapenzi ya Mungu. _Mtu asiye na msingi mzuri wa kiroho hana mahusiano mazuri na roho mtakatifu hivyo hata wakati wa uchaguzi wa wenzi Roho wa Bwana huwa kimyaa,na kusababisha mtu kutumia akili yake na kuingia katika ndoa mbovu_
( *_Nikuulize kijana, hivi umeokoka kweli? Maisha yako ya kiroho yanaushawishi mbele za Mungu hata ukastahili kupewa mme/mke na Mungu?, hivi kona unazopiga na mabinti na vijana halafu unasema mimi namtumikia Mungu ni sahihii kupewa mtu mwema? Wangapi umewaonja na wamekuonja kwa ridhaa yako,halafu unategemea kuwa na ndoa sahii ya baraka?_* huo ndo msingi mbovu wa wokovu nauongelea urakao kufanya uchague bomu la ndoa.
✍Msingi mbovu wa malezi umezigharimu ndoa nyingi na umekuwa kitanzi cha uchaguzi wa mwenzi. Kuna watoto wamelelewa malezi yaskujiachia,wanafanya wanavyo taka,wanaonywa kwa kubembelezwa( Imewafanya vijana wawe na kiburi,kujiona na dharau)wakati wa kuchagua mwenzi lazima uumie. ( *_Kuna walio lelewa kwa kupewa maneno ya wewe utaoa/kuolewa kwenye familia tajiri, mtu mwenye pesa,dactor,lawyer,nk na kuwafanya wawe na jeuri,wawe na nyodo,kujikadiria,kupotezea vijana wanaokuja kuchumbia_*) Na hii ndo imewafanya wengi kuingia kwenye ndoa feki za tamaa zao na siyo mpango wa Mungu.
✍Kuna watu wamezoea vibaya kiasi kwamba wanahitaji mazoea hayo wapate wenzi walio na mazoea hayo( _Kuna waliozoea maisha ya kuhurumiwa,kudekezwa,kuheshimiwa hata ka ni kadogo,anakuwa anahitaji achukuliwe hivyo hivyo_)ifike hatua ujue mazoea ya kwalo siyo ya mwenzi utakaye mpata,jua kubadirika na muda na mazingira.
_Kwa ujumla, ndoa siyo taasisi ya ili mradi nimepata mtu wa kunioa,au wa kumuoa,ndoa ni zaidi ya kutimiza tamaa za mwili,kuzaa watoto na ku make life,ndoa ni chombo maalumu kinacho kuunfanisha wewe na Mungu au kukutenganisha na Mungu, chombo cha kutuliza maisha yako au kukupa Stress(msongo wa mawazo),kukupatanisha na watu au kukutenganisha na watu, Si kila ndoa mnapo oona kina pesa,mmeoana mnacheka nje ya utaratibu wa Kimungu ukahisi ita Last katika vicheko,bado safari ya ndoa ina mwitaji Mungu mwanzoni mwake,safarini mwakebhadi mwishoni mwake, kosa kubwa kwa vijana ni kuanza na Mungu ila wakati wa kuchagua na kuoana wana mtupa Mungu,ili waje wamuokote ndani ya ndoa hiyo ni bonge la Mistake_Mimi nakuhasa Anza na Mungu kila hatua na Mungu utasafiri vizuri na mpenzi wako hadi kifo.
*_By Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve )_*
*0755444078*