💚💚 *NIMEUMBWA KWA KUSUDI JEMA LA MUNGU,WACHA NIJIVUNIE HILO*💚💚
*_Ujumbe huu umeandaliwa na kuletwa kwako na Mtumishi wa Mungu Ev Elisha Kazimoto_*
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
_Shalom mtu wa Mungu,unaye pendwa na Bwana,leo nataka nizungumze na wewe Dada(Malkia Esta wa zama hizi)_
*Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana, Zaburi 139:14*
💚Nataka nikusemeshe uzuri wako,waweza kuwa umekata tamaa pengine unapoona umechelewa kuingia katika ndoa,au mahusiano yako yanaishia njiani waweza kuwa na maswali nafsini mwako, *_Hivi mimi ni mbaya?, Siwavutii wanaume,au mimi nimeumbwaje?_* Neno la Mungu limetupa jibu wewe Umeumbwa kwa *Jinsi ya Ajabu mno* ambayo Unafaa mbele za Mungu na mbele za Mme wako atakaye kuoa.
💚Unacho paswa kujua ni kuwa Uzuri wako si kwaajili ya wanaume wote, na si wote wa kuuona uzuri wako, na wakiuona wengine *Wasio wako, hawatakupenda bali watakutamani* na wakikutamani watakuchezea na kuumiza moyo wako maana safari yako itaishia kwenye mahusiano si ndoa.
💚Leo na kufundisha Uzuri wako uliowekwa kwenye kwenye chemba ya Moyo wa Mme wako Usiye mjua bado kwa sasa,huyo ndo aliyebeba sura yako,tabasamu lako,chozi lako,furaha yako,huyo akifunuliwa kwako tu *Lazima moyo wako Ulipuke kwa furaha* Na yeye huyo Atakupenda,atalinda moyo wako,hisia zako na huyo ndo atafuta machozi ya mapito yako, na huyo ndo *Atasimulia na kuelezea Uzuri wako* Ulivyo na ndiye ataujua Uzuri wako, hatakama wengine watasema No kwako, yeye atasema Yes, wengine wakikuambia Haufai, yeye Atasema wewe ndo wa Pekee katika wana wake wote.
*Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote,Mithali 31:29*
💚Mwanaume wa aina hii mwenye lugha hii, Atapatikana tu pale utakapo *_Jituliza kwa Bwana,na kuzama magotini kwa maombi na Utumishi mbele za Mungu_* Na hapa ulipo ni mahali sahii pa Kupata waume wema,kwakuwa Tunasema MUNGU NIPE UBAVU WANGU,siyo mazingira,elimu,kabila,baba au mama,tumesema MUNGU,kwa lugha nyingine *Group hili tumejipanga kumtafuta Mungu kwa Bidii mpaka ajibu watu wake* Na tumeona,tunaushuhuda kwa maombi yetu watu wamejibiwa maombi wamepata wachumba sahii na wengine Wamefunga ndoa tiyari... Mungu wetu Anajibu.
*USITISHWE NA UPEPO WA KUKOSA WACHUMBA, AU WENGINE KUKUACHA*
👉Mungu wetu huyu uwa ni Mungu anaye fanya mambo kwa kusudi lake,na kwa wakati wake, wakati unalalamika unasema *WHY ME?* Upande wa pili kuna *Wema wa Mungu ulio kuzunguka na kukuepusha na Majuto makuu* ila hukuona,umeona tu tukio la kuachwa,au kuchelewa kuolewa,kumbe upande wa pili Mungu amekuepusha na *Kuwa mjane ukiwa bado mdogo,Amekuepusha na Divorce katika umri mdogo wa ndoa,Amekuepusha na kuishi wa Migogoro isiyo isha,Amekuandalia mtu wakutimiza ndoto zako za kihuduma,kiuchumi na kimaisha kwa ujumla*
💚Binti yangu, Kila mahusiano Unayopitia ni darasa tosha kwaajili ya maisha yako ya baadaye.
💚Wengine mebeba nafsi za watu wengi maishani mwenu ambao wanahitaji kufundishwa,kushauriwa,kuepushwa katika majanga ya kindoa na kiahusiano, nani awezaye kufanya kazi hiyo kwa ufanisi mkuu wakati hana *History ya Mapito ya ushindi?*
Utawasaidia watu kwa ubora zaidi ikiwa Ulipita na ukashinda..... _You have a living testimony_
*Daudi akasema, Bwana aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na Bwana atakuwa pamoja nawe. 1 Samweli 17:37*
💚Wajuaje wewe ni mtu mkubwa utakaye ponya kizazi cha mabinti wengi wajao nyuma yako, walio nyumbani mwa Bwana? Watoto wako?washirika wako? Wajuaje utakuwa Great Figure in the world utakaye kuwa ukisema na ulimwengu mzima,taifa zima,mkoa mzima, wajuaje utaolewa na mme ambaye ni mtumishi mkuu wa Mungu asimamaye mbele za maelfu wengi?.
💚Mara nyingi tunatishwa na muda wetu ambao kwa mtazamo wetu twa hisi ndiyo sahihi,lakini pamoja na kuona muda wetu ndiyo sahihi, *Sisi kama wanadamu twaona karibu mno* wala hatuyajui ya baada ya dakika moja, lakini Mungu wetu anaona mbali,anajua yote na yote anayotuwazia ni Mema,kwa hiyo *_Anaweza kwenda kinyume na Muda wetu,siyo ili atuumize,bali aulete Utukufu mkuu wa muujiza katika maisha yetu_* ili tuwe na furaha timilifu ndani yake.
1 Basi mtu mmoja alikuwa hawezi, Lazaro wa Bethania, mwenyeji wa mji wa Mariamu na Martha, dada yake.
Yohana 11:1
3 Basi wale maumbu wakatuma ujumbe kwake wakisema, Bwana, yeye umpendaye hawezi.
Yohana 11:3
6 Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.
Yohana 11:6
💚Kuchelewa kwa Mungu kukupa hitaji lako, kwa Tafsiri ya Kiroho, *_Ni Mungu kukuthamini mno nakutaka kukupa kitu bora zaidi_* In fact Mungu achelewi,(hiyo nikatika mtazamo wa Muda wetu)ila katika Muda wa Mungu huo ndo wakati na majira yako yanayo faa kupokea Zawadi hiyo ya Mungu.
💚Wakati mwingine watu wanao tuzunguka wanaweza *Kuwa changamoto,kwa kukukatisha tamaa,au kukupandisha hamasa ya kutaka kuingia katika ndoa kwa namna yoyote* unaona wengine walio chini ya umri wako wanaolewa wanakuacha.... *USI PANIC* Subiri muda wako,huo ni muda wao.... Usifanye maamuzi ya Kubebwa na yeyote, subiri ubebwe na *Mtu maalumu*.
*Kwa nini ni Hofu wakati najulikana na Mungu tangu zamani?*
💚Ni muhimu kulisoma Neno la Mungu na kulitumaini maishani mwako kwakuwa limebeba majibu ya maisha yetu.
💚Huna sababu yakuwa na hofu na kuhisi Umepoteza mwelekeo, _Mungu aliyekuumba,mwenye maamuzi ya mwisho juu ya maisha yako anasema anakujua wewe hata kabla hujazaliwa_ kwa maneno mengine hakuna jipya linalotokea maishani mwako hajui.....
*4 Neno la Bwana lilinijia, kusema, Yeremia 1:4*
*5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.Yeremia 1:5*
💚Kukujua kwake,si kwa bure,anasema Anataarifa zako za kwa nini uchelewe,na atafanya nini katika kuchelewa kwako.
💚Mungu Hawi na Taarifa zetu mapema ili Atuchekiiii na kutuacha, Anakuwa na taarifa zetu kwa misingi yakuweka mazingira sawa ya mapito yetu ili Tupate vitu vinavyo tufaa.
💚Uzuri wa pekee wa Mungu wetu ametufanya tuishi maisha ya Historia kwa Mungu,kwetu ni mapya ila kwake ni History, angalia anavyosema.....
9 kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi;
Isaya 46:9
10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.
Isaya 46:10
💚Kama Mungu anatangaza *_Mwisho wako tangu mwanzo(tangu unazaliwa,tangu unaanza mchakato wa kuomba mchumba)Mungu anatangaza mwisho wako(ndoa ya heshima) kwa hiyo wewe kabla huja kata tamaa Mungu alishatangaza mwisho wako wa utukufu, kazi yako ni Kuvumilia na kumtumaini yeye_* mpaka uufikie Muda wako wa furaha.
_Nimalize kwa Kusema,wewe unathamani kubwa sana machoni pa Bwana,na Hayuko tiyari aone Ukiabika kama mtoto wake,atafanya na mlango wa kutokea ili Uvikwe taji ya utukufu,
*_Unachotakiwa kama Dada wa KiKristo, katika mchakato wa kuielekea ndoa Takatifu uwe na sifa hizi,au fanya haya_*
1⃣Tengeneza Profile ya maisha yanayo someka kwa ubora na sifa njema( Attractive life)
2⃣Ibua vitu pekee ukivyo navyo ndani yako vifaye kwa bidii uwe tofauti na wengine( Be Unique and Potential)
3⃣Hata siku moja Usijidharau ulivyo,thamini nature yako jikubali ulivyo.
4⃣Jijue mapungufu yako uyarekebishe yasiendelee kuwa ukuta,au kuchafua Profile yako ya maisha.
5⃣Mwombe Mungu,mwamini Mungu,Mungoje Mungu wa kwako yupo atakuja kwa wakati.
*NB: _Katika kuomba hakikisha unamwambia Bwana fungua sura yangu katika ulimwengu wa Roho ionekane katika uhalisia wa ulivyoniumba ili mme wangu auone Uzuri wangu ulioniumbia_*
Nikutakie Maombi mema,na matengenezo mema ya maandalizi yakuingia katika ndoa njema ya Baraka.
_Ulikuwa nami mnenaji wa siri hizi Mtumishi wa Mungu, *Ev Elisha Kazimoto(Psychologist & Counselor)*
Facebook Elisha Kazimoto
WhatsApp 0755444078
No comments:
Post a Comment