💢💢 *SAIKOLOJIA YA KINYWA(KUONGEA) KATIKA MAHUSIANO*💢💢
_Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, *Ev Elisha Kazimoto*(Psychologist & Counselor)_
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
.......................................................
_Hello kijana wa kiume na kijana wa kike(binti),leo nikuongezee kitu kimoja muhimu sana katika mahusiano na Ndoa, ( *Mawasiliano/Kuongea*) tendo ambalo linatumika kila muda kila siku wakati wote wa maisha yako._
💢Kuongea ni njia moja wapo ya *Kufunua Uhalisia wako(Uzuri wako au Ubaya wako)* katikati ya watu wanao kuzunguka.
💢Nature ya mtu, Tabia ya mtu,nguvu ya mtu na udhaifu wa mtu, *Ufafanuliwa na Lugha yake(Maongezi yake)*
💢Kuna maeneo mawili makuu ambayo watu *Upima Uzuri na Ubaya wa mtu* Eneo la Kwanza *MAONGEZI YAKE(lugha) na Eneo la Pili ( MWONEKANO WAKE(Presentation)yake kwa watu(Personality)* hayo ndo maeneo makuu watu wanaweza ku Judge mtu kama anafaa au hafai kuwa mke au mme, au kuongoza au kusimamia eneo flani,ila hapa mimi naongelea mahusiano na Ndoa.
💢Ikumbukwe kuwa Lugha yako,(maongezi yako) *Yanaweza wasilishwa kwa Maneno ya sauti au kwa njia ya Maandishi* kupitia njia hizo kuu 2 watu wakajua wewe ni nani.
💢Unapo anza safari ya kutafuta mwenzi wa maisha( *Mke au Mme*), Anza na Safari ya Kurekebisha Maongezi yako na Mwonekano wako.
💢Unapo fanya maombi ya Kuombea mwenzi wako usiye mjua, ( *Anza pia kuombea Uwasilishaji wa Hisia zako kwa maneno na maandishi*) viwe vinavyo faa kwa watu.
💢Kisaikolojia na wanasaikolojia *Hauangaiki sana kujua Tabia ya mtu,kufaa kwa mtu, udhaifu wa mtu, endapo una Nafasi ya Kusikia maongezi yake na Kusoma Maandishi yake* hapo ndo unaweza Kujua huyu ni nani na Akili yake ikoje na moyo wake ukoje.
💢Lakini Uzuri wa Somo hili, Si Saikolojia pekee ilo bainisha haya, hata Biblia Takatifu imeweka wazi *Mtu ni nani,mtu ni Maneno yake* Yaliyo jaa moyoni ndiyo yatakayo semwa na ndiyo yatakayo tendwa.
*Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.Luka 6:45*
💢👆Hapa ndipo wana saikolojia wakafafanua zaidi, Kwamba Tabia ya mtu utaifahamu kwa kadri ya uwasilishaji wake wa hisia zake kwa watu kwa njia ya maneno au maandishi.
💢 Tuna mjua mtu huyu ana Dharau, kwa maneno yake, mtu huyu Hajali, kwa maneno yake, mtu huyu ni Mkorofi kwa maneno yake, mtu huyu ana Hasira kwa maneno yake, mtu huyu ji Rough kwa maneno yake,mtu huyu ni mpole,muungwana,ana hekima kwa maneno yake, mtu huyu uwezo wake wa Kufikili,Kuamua mambo,ni mkubwa au mdogo kwa maneno yake( Anavyo yawasilisha kwa sauti au kwa maandishi)
💢 *KWA MSINGI HUU KIJANA WA KIKE NA WA KIUME HASA KATIKA ZAMA HIZI ZA TEKNOLOJIA YA MITANDAO YA KIJAMII*
1⃣Watu wengi wameshusha na watashusha Hadhi zao, watakataliwa sana,watachelewa kuoa au kuolewa kwasababu ya namna wanavyo wasiliana katika Magroup ya mitandao ya kijamii.
2⃣Watu wengi watafunua udhaifu wao na wanafunua udhaifu wao ambao ingekuwa vigumu kuujua, na kukulindia heshima yako,ila kwasababu ya kukosa Saikolojia ya Mawasiliano watu wanawasilisha Hisia zao kwa maandishi au kwa sauti bila kujiwekea Taadhari.
3⃣Watu wengi wanaweza na wataweza kuwahi Kuoa au Kuolewa, kugombaniwa na watu kwasababu ya Uwezo wao wa Kuwasilisha Hisia zao kwa maaandishi ana sauti, vinawa Promote zaidi kwa watu na kuonekana ni watu wa pekee.
💢 *ANGALIZO KATIKA SAIKOLOJIA YA MAWASILIANO*
👉Kukaa kimya siyo tafsiri ya uwezo wako mzuri na mkubwa wa kuwasiliana, ila *Umepunguza kujulikana haraka kwa watu*
👉Kuongea sana katika kila kitu, Hakutafsiri uwezo wako wa kujua au uwezo wako mkubwa wa kuwasiliana, *Ila umewarahisishia watu kujua wewe ni nani*
💢Hayo mambo yaangalie sana yatakusaidia kwakuwa kila siku unaongea unaandika, unaonekana(Mwonekano wa nje - Personality)
🎀 *SAIKOLOJIA YA MAWASILIANO INAKUTAKA KUZINGATIA ALAMA ZIFUATAZO*🎀
1⃣Ongea kitu ulicho na uelewa nacho vizuri( Utaonyesha uwezo wako wa Akili)
2⃣Kabla ya Kujibu Hoja ya mtu, Angalia yeye Ameiwasiliaha katika hali gani(ya hasira, furaha,uzuni,upole,dharau nk) ukijua ameiwasilisha kwa Aina gani, Itakusaidia Kumjibu katika Nafasi iliyo nzuri itakayo funua Hekima yako na uwezo wako wa Kutafakari.
3⃣Kabla ya kujibu hoja ya mtu, Sikiliza ndani yako ile hoja uliyoisikia au isoma *Imeibua nini ndani yako*(Hasira,Furaha,Uzuni,Chuki nk) Ukijua aina ya msisimko uloibuliwa ndani yako, itakusaidia Kujibu kwa Umakini Maana utakuwa na Taadhari ya Kulinda Hisia zako.
4⃣Kabla ya kujibu hoja iliyokufikia kwa maandishi,au sauti.... *Angalia kwanza Nafasi yako kwa watu wanaokuzunguka(Status)* (Je, wewe ni kiongozi, Mkubwa Kiumri,mdogo,Una ndoa au huna) waza athari zinazoweza tokea pale watu watakapo tafsiri ujumbe wako kama ndivyo ulivyo.... Hii itausaidia Kuongea au kujibu Umakini zaidi nanKutunza Heshima yako na kuonyesha *Kiwango cha Ukomavu wako*
_Ninapo maliza kwa leo yako mambo mengi ila leo niishie hapo, Lakini cha kujifujza hapa ni kwamba wewe mwenyewe unaweza jitengenezea *Kibali machoni pa watu au Kuharibu Kibali chako machoni pa watu* kutokana na uwasilishaji wako wa maneno kwa watu wanaokuzunguka_
💢💢 *_Uchambuzi huu umeletwa kwako na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, Mwanasaikolojia EV ELISHA KAZIMOTO, Ambaye ni Mkufunzi wa Masuala ya Kiroho(Neno la Mungu) na Masuala ya Kimahusiano na Ndoa na Saikolojia ya Maisha_*
Mawasiliano: WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto.
*NB: Ana Magroup ya WhatsApp 8 tofauti anayo yasimamia yanayotoa Elimu mbali mbali za Kiroho na Kisaikolojia*
ULIYE TAYARI KARIBU.
©2019
Wednesday, 30 October 2019
SAIKOLOJIA YA MAWASILIANO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment