Saturday, 12 October 2019

UFUNGUO WA 11

🗝🗝 *UFUNGUO WA 11:FURAHA YETU KATIKA NDOA NDO MWANGA WA MAKUZI MEMA YA WATOTO WETU*🗝🗝
_Hello Hello mwana Ndoa,kwa mara nyingine Mtaalamu wetu na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto* anakuletea ufunguo wa 11 wa ndoa yenye Furaha karibu_
🗝Kuna mambo ambayo wana ndoa wanaweza kuwa wanayafanya wao kama wao lakini hawatafakari kwa habari ya Uzao wao nini wana vuna kutoka katika Mahusiano ya ndoa yao.
🗝Mahusiano ya wazazi kama wana Ndoa ( *Yana nguvu kubwa katika Kuathiri Makuzi ya watoto na tabia za watoto wao*) hilo ndo jambo kubwa ambalo wanandoa wengi hawajui,na hawajali.
🗝Migogoro na magomvi kati yenu yanaathiri Saikolojia na tabia ya watoto wenu, kwa muda huo mwaweza kuona kama wako kawaida ila kuna mbegu mbaya imepandwa itakayo waendesha pale watakapo fikia umri wa kufanya Maamuzi binafsi,ndipo tabia zao, maisha yao yataonyesha Uhalisia wa Mahusiano ya wazazi wao jinsi yalivyo kuwa mabaya.
🗝Kama wana Ndoa watajutahidi kulinda Furaha katika ndoa yenu,na watoto wenu wakayaona Mahusiano yenu yalivyo mazuri tangu wakiwa watoto, kwanza *Mnawapa afya ya kiakili darasani, wanajengewa uwezo wa kutafakari na kufanya maamuzi sahihii,tabia njema inaumbika* lakini mnaetengeneza uwezo wa malezi safi ya uzao wenu.
🗝Wana Ndoa watoto wakiwa wadogo,mnaweza kila mtu kutojali,kila mtu anafanya kumkomoa mwenzake,hamuoni matokeo,ila kumbuka mnapanda mbegu ya *Mbuyu* watakapo kua watu wazima ambao wanaanza kufanya maamuzi yao binafsi na sikuamliwa 100% hapo ndipo mtakapo anza kuvuna matunda ya Magomvi yenu,visilani vyenu na ndipo mtaona Umuhimu wa Kusameana,kupendana na kuheshimiana kama wana Ndoa,lakini muda utakuwa umechelewa,mpaka kwa Neema ya Mungu aangilie kati ya uzao wenu ila mtakuwa na *Uzao mbaya usio na historia ya maisha ya kuigwa* Epuka Kulaaniwa na Watoto wako na kuburi lako kupigwa mawe, Lipa gharama ya kuhakikisha unalinda Mahusiano ya Furaha katika Ndoa.
_Niishie hapo kwa leo,ulikuwa nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, *Ev Elisha Kazimoto (Psychologist & Counselor)*
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto

No comments:

Post a Comment