🎀🎀 *NDOA NI TAASISI NYETI SANA INAYO HITAJI WATU WALIO NA AKILI TIMAMU NA KOMAVU*🎀🎀
_Imeandaliwa na Mwanasaikolojia na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Mtumishi wa Mungu Ev Elisha Kazimoto_
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto.
............................................
_Hello Hello wana ndoa na wana ndoa watarajiwa,nasema nanyi leo kuponya watu wachache wenye Akili Timamu ya Ki Mungu na ya Kisailojia,na wale waliogonjweka hii ni Saa ya Kupona ( *Kama ukitaka*) ila ukiona Huwezi Badirika, Amini unacho amini ila Historia Itajirudia HAUTAKUJA KUWA NA FURAHA MAISHANI kama wanayoipata wegine walioko kwenye NDOA_
🎀Kwanza, nimesema ndoa inahitaji watu wenye *Akili timamu* Kwa nini nasema akili timamu, _Kabla ya kufanya Maamuzi ya Kuoa au Kuolewa,inabidi uwe na uwezo wa kutambua mazingira yafuatayo ndo yanayoonyesha wewe una akili timamu ya Kindoa_
1⃣Naenda kuolewa au kuoa nimetaka mwenyewe, imenipasa kukabiliana na yoyote yatakayotokea huko kwa Busara.
2⃣Naenda kuoana na Binadamu na si Malaika, anamadhaifu kama mimi,atanikosea,nitamkosea ila inabidi niangalie namna ya kuishi naye kwa Amani.
3⃣Ndoa yetu(Makazi yetu) yatakuwa hapa hapa duniani na si Mbinguni,kwa hiyo kama dunia isivyo tambarale na maisha ya ndoa yetu hayawezi kuwa tambarale, lakini kuna watu waipenda ndoa yetu na wengine watatafuta namna ya kutugawa ila nijue namna ya kumlinda mwenzangu na kujilinda.
4⃣Kuoa na kuolewa ni Heshima kijamii(kwa Mungu ni kupata Kibali mbele za na baraka) *_Ila Kuachika,Kufukuza mke,Kutoka kwenye ndoa,kudai Talaka na Kutoa Talaka Ni Fedheha,na Aibu ya milele kwenye jamii na mbele za Mungu ni Laana_* Maana Mungu anasema ANACHUKIA KUACHANA.( yaani hapo hajaweka sababu yoyote Amesema ANACHUKIA, HIVI MUNGU AKICHUKIA UTASALIMIKA WEWE.
*Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana.Malaki 2:16*
🎀Lakini pia Unapoingia katika ndoa au kama wewe upo kwenye Ndoa Tunaona *Akili yako Imekomaa Kiasi gani,na Ulifaa kuoa au kuolewa kwasababu una akili komavu ya Kindoa pindi Utakapo kuwa na uwezo wa kufanya mambo Yafuatayo*
1⃣Kama utakuwa na uwezo wa kukaa na mtu ambaye si ndugu yako, mmekutana ukubwani, ukaweza Kuishi naye kwa hali yake yoyote, mkakaa kwa Amani na Furaha( *Yaani uwezo wa kutengeneza mazingira Rafiki ya amani*)
2⃣Kama utakuwa na uwezo wa Kukosewa na ukasamehe kabisa bila kulipa kisasi,au Ukakosea ukajua na kuomba samahani ili kulinda amani ya ndoa yako.
3⃣Kama utakuwa na uwezo wa Kuboresha madhaifu ya mwenzako mpaka akayaacha na kuwa vizuri,bila kumchoka na kumkatia tamaa.
4⃣Kama utakuwa na uwezo wa Kutimiza wajibu wako wa kijinsia na wa kindoa kwa mwenzako kwanza bila kusubiri UFANYIWE NDO UFANYE.
5⃣Kama utakuwa na Uwezo wa Kuhurumia Uzao wako,na kuwaonyeshea mfano mwema wa kuigwa ili nao wakue wakiwafurahia baba na mama na wawabariki hata muwapo wazee.
6⃣Kama utakuwa na uwezo wa kumpenda mwenzako hivyo alivyo, Mmejaliwa uzao au La, mnamali au mmefilisika, mzima au mgonjwa.
7⃣Kama una uwezo wa kuficha madhaifu yake watu wasiyajue bila sababu,na unauwezo wa kumwombea Mungu amsaidie awe vema.
8⃣Kama unauwezo wa Kuchukia KUACHANA na kupambana kwa namna yoyote ukae na mwenzako.
*_Hizo ndizo baadhi ya Kanuni za Kisaikolojia hasa katika Falsafa ya ndoa na Kibiblia(sija taja maandiko yako mengi) kama wewe Unajiita ni mtu wa Mungu, au kama unapenda kuishi nje ya Stress_*
NB: _Maamuzi yoyote ya wanandoa,jua mnapanda mbegu kwa uazo wenu wataishi maisha kama hayo hayo kwa vizazi 4(miaka 400baada yako) Usikurupuke kufanya maamuzi mabaya,utatesa uzao wako watakulaani hata kaburi lako_
(Fatilia wazazi walioachana,roho inawafuata hata watoto,Magomvi na kupigana,fatilia utaona kwa watoto, mama hamweshimu mmewe,fatilia watoto wake wa kike wakiolewa ni shida nk)
*TUPENDANE,TUJIFUNZE,TUREKEBISHANE HIZO NDO CHANGAMOTO ZA DUNIANI*
_Ulikuwa na Mwanasaikolojia na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa,Ev Elisha Kazimoto(WhatsApp 0755444078, Facebook Elisha Kazimoto)_.
Wednesday, 16 October 2019
NDOA INAHITAJI AKILI TIMAMU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment