Friday, 11 October 2019

UKIUMIZWA MOYO,USIJIUMIZE NA WEWE

🖤🖤 *UKIUMIZWA MOYO KATIKA MAHUSIANO, EPUKA KUJIUMIZA NA WEWE*🖤🖤
............................................
*_Na Ev Elisha Kazimoto(Psychologist & Counselor)_*
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
.................
.................
_Hello Hello vijana kwa mabinti ambao mpo katika safari ya Mahusiano yakuelekea ndoa, na wengine mpo katika Mahusiano yakuelekea katika ndoa, leo nataka niseme nawe kwa ufupi, Lugha hii Tata ya Kisaikolojia ili Nikusaidie Kutoendeleza Historia ya Maumivu katika moyo wako unapoendelea kuishi,lugha hii Niirudie tena, *"Ukiumizwa Moyo katika Mahusiano, Epuka Kujiumiza na Wewe* Huu umekuwa Ugonjwa kwa watu wengi, Je wewe wewe weza kupona Leo?_ Sentensi yangu kwako ni Alama ya (  Rudi nyuma Fikiri kabla ya maamuzi - 🔙)
🔙Kila anayeanzisha mahusiano(anayeingia) Ana matarajio ya kukidhi Hisia zake za Furaha zilizo msukuma kuingia kwenye Mahusiano,japo Anaweza Kushida Kuziongoza Hisia zake zifikie matamanio yake.( *Kosa la kwanza*)
🔙Kila anayeingia kwenye Mahusiano,anaingia na mtu ambaye Anahisi ana vitu au kitu ambacho kwa nafsi yake na hisia zake zilimwonyesha Anaweza Kupata Furaha,na kutimiza ndoto zake za Kimaisha, Japo Anaweza kushindwa  Kuusoma Ukweli wa Maneno,matendo ya mwenzake hata kupelekea Mahusiano kuvunjika mapema,au baada ya muda mrefu.( *Kosa la Pili*)
🔙Kila mtu aliyeingia katika Mahusiano na mtu,aliamini huyo ndiye mtu pekee wa Kuzigusa hisia zake na kuleta matarajio yake katika Uhalisia alioutamani tangu zamani, ndiyo maana ukamfuata,au ukamkubali, Japo Waweza Kushindwa Kuchochea Uzuri huo uliouona ili uendelee kutimiza hisia zako,ukapelekea kuachana kwa shari au kwa wema( *Kosa la Tatu*)
🔙Kila mmoja anayeingia katika Mahusiano huwa anaangalia Dhamira yake ilivyo njema,na alivyo sahihi katika Mahusiano na alivyo dhamilia kufikia hatima ya ndoa, Ambapo wengi Usahau na Ushindwa Kutambua Madhaifu yao na Makosa yao yanaweza changia wasifike mwisho wa safari. Kushindwa kujua udhaifu wako katika Mahusiano ni kosa kubwa la kisaikolojia ( *Kosa la nne*)
🔙Kila anayeingia katika Mahusiano Uamini aliyeingia naye katika Mahusiano anauwezo mkubwa wa kumfurahisha na si Kumkosea,Japo watu Usahau huyo naye ni mwanadamu kama wewe anachumba cha hisia chanya na hisia hasi,kwa hiyo jipange ukiingia chumba chake hasi wewe ingia ukiwa chanya, ukiingia chumba chake chanya,wewe ingia ukiwa chanya japo yeye anaweza kuonamo hasi kadhaa. Ukishindwa kanuni hiyo Mahusiano yatavunjika( *Kosa la tano*)
🔙Kila anayeingia katika Mahusiano,Uingia akijiona yeye ndo Mkweli na si rahisi kukosea ila mwenzake ndo si Mkweli na ndo mkosaji, ndiyo maana Wengi wa walioingia katika Mahusiano na kutoka katika Mahusiano (Break up mbali mbali) *Uwalaumu jinsia nyingine,au umlaumu mwenzake* Si Rahisi kusikia Anaanisha Makosa yake yaliyochangia Kuvunjika kwa Mahusiano,ndo maana kumekuwa na mwendelezo wa kuumizwa na huyu, na yule, na yule mpaka unachukia Mahusiano ( *Kosa la sita*) kwasababu Hujijui ubovu wako, udhaifu wako.
⚖ *Laiti ungerudi nyuma Ukajipima kwenye Uzani wa Mahusiano Kisaikolojia,Ungeweza kuendesha Mahusiano yako vizuri na Kutibu Majeraha yako ya Moyo*⚖
🎀Kama Ukijua kuwa Unapoingia kwenye Mahusiano una Hisia za Matarajio yako,lakini na mwenzako ana Hisia za Matarajio yake ambazo hizi zote za wewe kutofautiana,au kulandana,ungeweza kulinda Mahusiano yako kwa furaha, ila kwasababu unatafuta kutimiza hisia zako tu huangaiki na za mwenzako, Break up,kuumizwa kutaendelea mpaka pale moyo wako utakapo Uruhusu kukubali hali zote za Mahusiano.( *Utakuwa umeshinda kujiumiza mwenyewe*)
🎀Siku utapo jua,kitu kizuri ulichokiona kwa uliyempenda huyo,kinahitaji kuchochowa,kuboreshwa,Kulindwa na ukatia bidii kufanya hivyo utakuwa Umezuia Kuumizwa.
👉Lakini pia Ukipenda usiwe kipofu nakiziwi ruhusu macho yako yaone mazuri na mabaya,mazikio yako yasikie ukweli na uongo wake, na Ipe akili kazi ya Kutafsiri kufaa kwakwe na kutofaa kwake na ushugulikie mapema taarifa hiyo kabla ujaumia zaidi. ( kuendelea kujikaza wakati unajua ukweli hamuendi popote ni Kuendelea Kujiumiza wakati umeisha umizwa. ( *Hiyo ndo tiba ya kutojiumiza mwenyewe*)
🎀Wengi wetu katika Mahusiano,tunapenda kufayiwa mema zaidi,ila siyo sisi kuwafanyia mema watu wetu,Ndiyo maana Tukiumizwa nasi tunatafuta mwanya wa Kuumiza, hapo ndo Unazidi kujiumiza mwenyewe. Ikitokea Uliyoyatarajia kwa mwenzako Kuyapata,hukuyapata 🔙Rudi nyuma tazama wapi Wewe Ulikosea,ulichangia katika kuumizwa kwako,Ulishindwa Kuchochea Uzuri wake,uli relax? Ili kama mkiyatengeneza au ukipata mwingine Usiumizwe tena, Usipo Rekebisha kwanza, Utajiumiza mwenyewe tena na tena( *Hiyo ndo tiba ya kutojiumiza mwenyewe*)
🎀Ukitaka Mahusiano yako yaishi, uwe Mwepesi wa Kujua madhaifu yako na makosa yako unayo yafanya katika Mahusiano kwa mwenzako,na uwe mwepesi Kuyakwepa yasiwe yakujirudia rudia,hapo utakuwa Umeshinda Kujiumiza mwenyewe, Usipo jua hilo,utakuwa wakuumizwa kila mtu na utawachukia wanaume wote au wanawake wote kumbe ni wewe unaye jiumiza kila mara baada ya kuumizwa mara moja. ( *Hiyo ndo tiba ya Kukiumiza mwenyewe*)
🎀Usisahau kuwa tuna *Date na wanadamu wenye mapungufu yao, Si malaika* Kwa hiyo uwe Mwepesi kujua kuwa naweza kukosewa,nami naweza Kumkosea,ila kama nimeona uzuri wake unao nifaa,nifanye nini ili nisimpoteze? Punguza kujihesabia haki kila wakati,msaidie ajue udhaifubwake na Kuushinda ( *Tiba ya kutojiumiza*) mbali na hapo Utakuwa unajiumiza mwenyewe kila mara kwa kuona wanaume au wanawake ni Matapeli.
🆒 *Labda nikusaidie Acha Kupandisha Joto lako la Kihisia kwa Kutafsiri vibaya Changamoto yako yakimahusiano*🆒
🆒Kama Uliumizwa, Tulia Usiendelee Kuumiza nafsi yako kwa kuona Wanaume au wanawake wote ni Wasaliti, Hiyo haikusaidii bali Inaua na kutafuna Hisia zako za upendo na furaha,maana kutafsiri kwako huko Hakubadirishi Mapungufu yako,wala hakuondoi Uzuri wanaouona watu walio na Wanawake au Wanaume kwenye Mahusiano yao. Utaumia wewe ila wao wanazidi kufurahi,na ukisema wanawake wabaya au wanaume wabaya *Wanakuona Waajabu*
🆒Ukiumizwa,jua uwenda Huyo hakuwa size yako au Kilikuwa kipimo chako cha ukomavu wa akili ya Mahusiano,usiendelee kulalamikia Kosa lile ulilotendewa, halitakusaidia Kuhurumiwa na watu ili Wajitolee kukuoa au kuolewa nawe ili usiendelee kuumia. Tulia jua huo ulikuwa niukurasa wenye maandishi yake,subiri kurasa ijayo isome kwa utulivu,au iandike kwa utulivu.
🆒Ukiumizwa,Unapo jipanga kuingia kwenye Mahusiano mapya, Usibebe Hisitoria za maumivu yako na kuhamishia kwenye kurasa mpya, Utaumizwa tena, jifunze kuandia mambo mapya kwenye kurasa mpya.
🆒Ukiumizwa usijipandishe joto kwa kwa kujumuisha watu wa jinsia hiyo na kuwaona ni wabovu, wewe ndo *Utakuwa mbovu wa Kupindukia* kwakuwa ujui kila chapter ina sentensi zake,lakini kila mmoja ana Asili yake na uzuri wake na udhaifu wake.
🆒Ukiumizwa Usiape kutoyarudia Mahusiano, Haumkomoi  aliyekuumiza, Unajiumiza mwenyewe.... Apa wewe mmwenyewe kutorudia Makosa uliyochangia,na kuboresha uzuri wako.
*_Niishie kwa kusema kwamba, Usipo kuwa mkomavu Kisaikolojia katika Mahusiano,Utakuwamtu wa kujuta katika Mahusiano,ongeza Maarifa juu ya Mahusiano,ongeza ubora wa upekee wako,Hitirafu za Kimahusiano zione darasa la kukomaa Kimahusiano,uta Enjoy Maisha, Hakuna Mtu mbaya katika Mahusiano,ila watu Wanakosa Mbinu sahihi za Kuendesha na Kulinda Mahusiano_*
_Ulikuwa nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, *Ev Elisha Kazimoto*( Psychologist & Counselor)_
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto

No comments:

Post a Comment