Saturday, 12 October 2019

UFUNGUO 12

🗝🗝 *UFUNGUO WA 12: AMANI YA NDOA YETU INATOKA KWA MUNGU,TUKAE NA MUNGU VIZURI*🗝🗝
_Hello Hello wana Ndoa,kwa mara nyingine tunasogea katika meza ya Maarifa ya Kisaikolojia kwa wana Ndoa,upo nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, *Ev Elisha Kazimoto (Psychologist & Counselor)* karibu tuhitimishe kwa Ufunguo wa 12 wa ndoa yenye Furaha katika maisha._
🗝Mara nyingi watu wengi wanakuwa na mzigo mkubwa wa kuomba,kumtafuta Mungu wakati wanatafuta wenzi wa maisha,ila wakishawapata wanastarehe biashara ya kuomba,kuombeana,kuhimizana katika mambo ya Mungu inabaki ni kwa mtu binafsi na wakati Mwingine kila mmoja anaweka Silaha chini.
🗝Siri kubwa ya kuimarisha Ndoa yako na kuifanya kuwa ya Furaha,ni pale wana Ndoa mtaamua kukaa na kupanga namna yayay kuishi na Mungu katika ndoa yenu,namna ya kumtumikia Mungu katika maisha yenu ya ndoa,kubebana koroho na kuhimizana katika mambo ya Mungu.
🗝Ndoa inatoka kwa Mungu,hivyo inahitaji kurudishwa kwa Mungu kwa njia ya Maombi ili iwe salama.
🗝Miongoni mwa Taasisi yenye vita,inayowindwa na adui na inapigwa vita ni Ndoa, adui akifanikiwa kuwagawa katika Ndoa, *Amefanikiwa kushika uchumi wenu,kushika uzao wenu,kushika maendeleo yenu* na lolote laweza tokea lililo baya
🗝Mkifanikiwa kuwa watu wa vita,watu wa maombi, watu wa kumtumikia Mungu,watu wa kushirikishana mambo ya Ki Mungu,mtafanikiwa *Kulinda furaha,amani,na upendo* kati ya ndoa yenu.
🗝Wekeza nguvu kubwa ya kumwambia Mungu kila siku kwa maombi yako,kwamba Mungu linda mwenzangu,nilinde na mimi,upendo,uzuri na furaha niliyo iona kwake tangu siku ya kwanza nilipomuona,iendelee kudumu kati yetu,utupe uzee mwema,kataa vifo vya ujanani kwa watoto wenu na kwenu,kataa roho za migogoro,magomvi,mafarakano kati yenu, mwambie Bwana ifanye ndoa yetu iwe mfano wa kuigwa kwa watu wote.
_Mtu wa Mungu niishie hapa kwa leo,nikutakie baraka tele katika ndoa yenu na mkono wa Bwana uwaongoze katika kuishi maisha ya Furaha. Ndoa ni Njema kama wewe mwana ndoa ni mwema,na ndoa ni mbaya kama wewe mwana ndoa ni mbaya_
*Vitu vyote ni safi kwa hao walio safi; lakini hakuna kilicho safi kwao walio wanajisi, wasioamini; bali akili zao zimekuwa najisi, na nia zao pia.Tito 1:15*
_Ulikuwa nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto* (Psychologist & )_
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto

No comments:

Post a Comment