🗝🗝 *UFUNGUO WA 9: KAMA MOYO WAKE UTAUMIA NA MIMI NITAUMIA*🗝🗝
_Hello wana Ndoa Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, Msaikolojia *Ev Elisha Kazimoto* Anakuletea ufunguo wa 9 kati ya 12 wa ndoa yanye Furaha, fuatana nami katika ufunguo huu,ili ufungue chumba chako cha Stress uingize furaha_
🗝Kuna vitu ambavyo ukishaingia kwenye ndoa inabidi kila mmoja Ujiulize ndipo utaruhusu chemi chemi za furaha katika ndoa yako.
🗝Kumekuwa na kawaida ya wana ndoa kutojali Maumivu ya mwenzake,kwa hiyo anaweza fanya lolote kwake akidhani *Anamkomoa mwenzake* anashindwa kujua kwamba kwenye Ndoa Mungu alisha sema ninyi ni MWILI MMOJA, Kauli hii Kisayansi tunaipata kwa bwana mmoja mwana FIZIKIA(PHYSICS) anaitwa Archimedes,kwenye *Third Law of Motion, anasema "To Every Action,there's equal and opposite Reaction"* mwisho wa kumnukuu.... Akimaanisha kwamba _Kwa kila tendo kuna usawa na kinyume cha tendo hilo_ mfano mwenye baiskeli akigongana uso kwa uso na gari, Wote wanaumia sawa japo sisi tutaona wa baiskeli kakanyagwa kanyagwa na kufa...ila kikanuni ya mwendo na gari limeumia sawa na baiskeli.
🗝Sasa katika Ndoa,watu wanasahau kwamba Mwenzako Akiumia moyo wake kwa majeraha uliyo yatengeneza mwenyewe,jua na wewe *Utavuna au utakula sehemu ya maumivu hayo* yeye hawezi umia wewe ukacheka. Kuna vitu utavikosa vya Kihisia kutokana na Kuumia kwake.
🗝Ndiyo maana tunasema katika ndoa,kila mmoja kimbizana na kutafuta namna gani *Uuburudishe moyo wa mwenzako* ili nawe Uburudike.
🗝Ni vigumu kucheka na mtu aliye jeruhika moyo, ni vigumu kutoka out ma mtu aliyejeruhika moyo,ni vigumu kumsifia mtu aliyejeruhika moyo,ni vigumu kufanya mipango na mtu aluyejeruhika moyo,ni vigumu Kushiriki tendo la ndoa na mtu mwenye majeraha ya moyo.( hivyo ni baadhi tu)
🗝Kwa mazingira hayo,Epuka Kumezea,kutemgeneza mazingira ya maumivu kwa mwenzako,na umigundua umemuumiza, Ebu tafuta namna ya kuuganga moyo wake airudie hali yake ya furaha. *_Mwenzako akifurahi,nawe utafurahi,na mtaishi maisha ya Ushindi katika ndoa_*
_Mimi kwa leo niishie hapo niseme kwamba Ndoa ni Tamu kama utaamua wewe uitengenezea mazingira ya utamu,na ndoa ni chungu kama wewe utaamua kuiandalia mazingira ya uchungu_.
*Ulikuwa nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa _Ev Elisha Kazimoto(Psychologist &Counselor_)*
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
Saturday, 12 October 2019
UFUNGUO WA 9
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment