Thursday, 17 October 2019

ZINAA NA MCHUMBA WAKO NDOA MOTO

💣💣 *UKIONA UMEANGUKA KWENYE ZINAA NA MCHUMBA WAKO JIPANGE KWA YAFUATAYO KATIKA NDOA*💣💣
_Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto*(Psychologist & Counselor)_
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto.
......................................................
_Hello kijana wa kiume, Hello kijana wa kike, Hello mwana Ndoa, nina Alama muhimu za Nyakati chache zikusaidie kwa Taadhari,au Kugundua Maangaiko yako,ujiponye au Upambane_
💣Mara nyingi tumekuwa tukichukulia kawaida  suala la Mahusiano ya kirafiki na kiuchumba na kuona nikama kipindi cha Kujiachia,au cha Kujaribu jaribu kama kuna bahati yako au la, kumbe nikipindi Muhimu ambacho ni msingi wa ndoa ya mtu.
💣Ndoa nyingi zina machafuko yasiyokoma,ambayo masuluhisho mengi ya kwa wazazi,wasimamizi,wachungaji,mpaka na mahakama yamegonga mwamba hakuna kutulia,yametoka katika vyanzo vikuu 3, mimi nitazungumza 1, viwili vipo kwenye lecture zangu kama nimfatiliaji wa masomo yangu katika magroup mengi ya WhatsApp na Facebook. Machimbuko hayo 3 ni:
1⃣Ukosefu wa Maarifa ya Kisaikolojia ya kuendesha mahusiano ya uchumba au Ndoa (watu wanajikwaa katika mlima wa ujinga. HOSEA 4:6).
2⃣Kuto apata mtu sahihi(Uchaguzi usio makini) Unafoji ubavu.... (Jua hautakuja kutulia na mtu wa mwingine)
3⃣Msingi Mbovu wa Mahusiano yenye Harufu ya Zinaa.
💣Miongoni mwa vitu ambavyo wengi wa wanaofunga ndoa upuuzia nakuona ni kitu kidogo,ni *Ni wao kuanguka katika zinaa(Kushiriki ngono)kabla ya ndoa halafu wakaoana* wakiamini wanaendeleza Upendo,kumbe ndo wamefuta upendo.
💣Labda nikupe siri hii ya Kisaikolojia na kiroho *SEX INAPANDE MBILI ZA SHILINGI* Ni TAMU na Inaunganisha Nafsi za watu na kuwafanya wawe na Sura moja( *_Kama imefanyika katika muda muafaka kwa watu sahihi bila hatia_*)

19 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakasali mbele za Bwana, kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye Bwana akamkumbuka.
1 Samweli 1:19
👉👆Sex ikifanyika kwa watu waliosahihi yaani mke na mme ina MKONO WA BWANA WA BARAKA.
👉Pili  SEX inakawida ya *Kuwaachanisha watu nafsi,kufuta upendo,Amani,furaha kati ya watu Walioifanya Kinyume,nje ya muda na si watu sahihi*
10 Amnoni akamwambia Tamari, Kilete chakula chumbani, nipate kula mkononi mwako. Basi Tamari akaitwaa mikate aliyoifanyiza, akamletea Amnoni nduguye mle chumbani.
2 Samweli 13:10

11 Naye alipokwisha kuileta karibu naye, ili ale, Amnoni akamkamata, akamwambia, Njoo ulale nami, ndugu yangu.
2 Samweli 13:11

12 Naye akamjibu, La, sivyo, ndugu yangu, usinitenze nguvu; kwani haifai kutendeka hivi katika Israeli; usitende upumbavu huu.
2 Samweli 13:12

13 Nami nichukue wapi aibu yangu? Wewe nawe utakuwa kama mmoja wa wapumbavu wa Israeli. Basi, sasa, nakusihi, useme na mfalme; kwa maana hatakukataza kunioa.
2 Samweli 13:13

14 Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.
2 Samweli 13:14

15 Kisha Amnoni akamchukia machukio makuu sana; kwa kuwa machukio aliyomchukia yakawa makuu kuliko yale mapenzi aliyokuwa amempenda kwanza. Amnoni akamwambia, Ondoka, nenda zako.
2 Samweli 13:15

16 Naye akamwambia, Sivyo, kwa kuwa mabaya haya ya kunitoa ni makuu kuliko yale uliyonitendea. Lakini alikataa kumsikiliza.
2 Samweli 13:16

17 Ndipo akamwita mtumishi wake aliyemtumikia, akasema, Mtoe sasa mwanamke huyu kwangu, ukafunge mlango nyuma yake.
2 Samweli 13:17

👉👆Wakati sex isiyo halali inakuwa ina vutia na inapofusha macho nikama unajituliza ila matomeo yake baadye INAFUTA KILA AINA YA FURAHA NA AMANI KATIKA NAFSI ZA WAWILI hawa,sasa ikisha futa na mkaoana *Hiki ndo kinatokea kwenye ndoa yenu* Kiroho na Kisaikolojia:
1⃣Uaminifu kati yenu ndo basi tena( Hakuna atakaye kuja kumwamini mwenzake daima)
👉Hapa hata mwenzako aone unatoa pepo,viwete wanatembea,unaimba mpaka unabubujika, Nafsi mwake *Hana Imani na wewe* ana ❓❓❓nyingi.( _Kwa nini,kwasababu ulikuwa na Ujasiri wa kuvunja uaminifu wako mbele zake katika ujana,kwa sasa ndo anaona huwezi shindwa vunja tena_) Mtaishi maisha ya kuwindana,kulaumiana sana.
👉Kawaulize wote walioangukia Kona hii hata kama ni watumishi wa Madhabahuni,wamalazimisha kuaminiana mdomoni ila Moyoni na Akilini *wanashutukana*
2⃣Thamani yako kwa mwenzako inashuka chini ya 50%. Ukiona umevua au umevuliwa nguo kabla ya ndoa na huyo huyo mkaoana, *Respect kati yenu inashuka chini ya nusu* kwa nini, Usiri wamiili yenu unabeba *Heshima ya mioyo na utu wenu* Mkisha vuana nguo Usitegemee, *Baba mwenye nyumba kupata full respect,au mama kupendwa full love* utakuwa na Partial.... Maana respect na love vilivuliwa moyoni mwako nje ya ndoa,hukuja navyo ndani ya ndoa
3⃣Kuna uwezekano wa KUACHANA kimwili (divorce) kwa nini vitu muhimu vinavyo shikilia Ndoa,hamkuingia navyo ndani mliviacha pale mlipovuana nguo( *Vitu kama, Usiri,Aibu,heshima,shahuku kwa mwenzako,*) kwa hiyo mgogoro ukianza ndani Hauzimwi unatafuta Kuachana.
4⃣Fujo,magomvi,kunyimana tendo la ndoa haviwezi kukoma kati yenu....(Maana moyo wa Upendo uliisha chukuliwa na adui)mtasuluhisha ila muafaka haupo,wanacho laumiana ni kidogo sana ila kinakuzwa na mbegu ya zinaa iliyofanyika. Mwaweza ishi ila si kwa Amani na upendo,mtakuwa na vipindi vifupi vya furaha na kipindi kirefu cha dhoruba.
_Nini nataadharisha vijana ambao bado hamjaingia katika ndoa, Komaa mpaka mwisho,rafiki au mchumba akikushawishi kwa sex kimbia na PIGA ❌ kuanzia kichwani pake mpaka muguuni pake,usipo fanya hivyo uta enjoy kwa mwezi,wiki na siku ila Utajuta maisha ya ndoa Yote._
👉Mlioko kwenye Ndoa,Nahisi ukisoma haya utajua kuwa kama Ulipitia huko Haya ndo Maisha yako, *Huna heshima kwa mwenzako,Sex hupati inavyotakikana,upendo haba sana,Amani hakuna,Uaminifu hakuna,unahisi kumchoka mwenzako* nini Kifanyike Lazima mtibiwe wote Kiroho na Kisaikolojia ili mpunguze makali ya Maisha mnayoishi ila mbali na hapo  mpaka kaburini au Mtaachana tu.
*_Ulikuwa na mimi Mchambuzi wa Masuala ya Ndoa na Mahusiano Ev Elisha Kazimoto (Psychologist & counselor)_*
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto

No comments:

Post a Comment