Thursday, 26 November 2020

NJIA YA KUVUNJA MAHUSIANO

Mwl. Naomba Ukija uje na Majibu  ya Ipi njia nzuri ambayo haiumizi  moyo wakt mnataka ku-break up mahusiano yenu...  kwa  njia ya SIMU  / SMS,   Au   Mnakutana sehemu  Mna-break kwa kuOnana.

Ipi? njia nzuri hapo😁

maana wengine utashaanga tu! mmeachana😂😂
*Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*
*NJIA YA KUVUNJA MAHUSIANO SIYO COMMON NI CONDITIONAL*
👉Unapo amua kuvunja mahusiano inategemea una mtu wa character.
👆Kuna watu una kaa naye mvunje mahusiano Reaction yake italeta hasara(Kubakwa,Kukupiga,Kukuaibisha au palepale kufanya tukio baya) huyo usikae naye tumia njia zingine.
👉Sababu ya kuvunja mahusiano ni kwasababu ya tabia, mmeshindwa kuelewana,au mnapendana ila mapenzi ya Mungu yamegoma
👆Angalia ipi njia ipi haitaleta athari kati yenu mbaya.
👉👆Mahusiano katika nyanja hizo wapo ambao mtakaa eneo la wazi site huru mtaambiana kwakweli hatuna budi kuend up mahusiano mta break na kuachana(kama wote saikolojia zenu ziko vizuri)
👉👆Wengine tumia simu mpe taarifa ya kusitisha mahusiano na sababu zako kwa upendo kabisa na sitisha.
👉👆Mwingine mpe ishara kimya kimya unamkatia mizizi chini kwa chini mti ukisha kauka ndoa unamalizia na taarifa ya nilisha futa mahusiano nawe kwa sababu hii na hii.
*Kuwa makini unapovunja mahusiano isiwe ni kwa sababu za tamaa zako, na kukurupuka usije ukaumia wewe mwenyewe ikakugarimu*
By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)0755444078

KULIPA MAHARI

Nina swal......

*Je ni sahihi kwa kijana kusaidiwa kutoa mahari, mfano kusaidiwa na ndugu zake au hata mwanamke anayetarajia kumuoa........na je akisaidiwa huyo mke hawi wa wote waliochangia mahari?*
*KULIPA MAHARI KIMANTIKI NI KAZI YA KIJANA MUOAJI*
*Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*
👉Kijana unapoanza kuhisi kichwani mwako unahitaji *Kuchumbia* jambo la kwanza anza kujipanga kutafuta mahari.
👉Ukianza kuchumbia uwe na uhakika wa kulipa mahari mwenyewe.
👉Usichumbie kwa imani na kuwatwisha mzigo ndugu, wazazi na kanisa wakulipie Mahari.
👉Mahari kwa tafsiri ya haraka ya kimantiki Ni Gharama inayoonyesha kiwango cha Utayari wako na Upendo wako kwa huyo unaye mtaka, Upo tayari kugharimika kiasi gani hata umpate? Sasa usipo Lipa mahari au ukisaidiwa mahari nani mwenye upendo wa umuoaye wewe Au ndugu zako au kanisa? Heshima ya mwanamke iende kwa nani?wewe mmeo au ndugu au kanisa lililolipa mahari?
👉Kabla ya kuanza kuchumbia jua wewe kijana(mwanaume) Biblia imekufananisha na Yesu Kristo(wewe ni kichwa cha mkeo) Yesu alilipa Gharama hata mauti ili atupate sisi,je wewe umelipa gharama ili umpate mkeo?
👉Wazazi,ndugu,kanisa wacha wapambane na maandalizi ya harusi,wewe *LIPA MAHARI* kwa namna vyovyote.
👉NB: Suala la wazazi kukusaidia,kukulipia mahari isiwe ni kwasababu Umeshindwa iwe ni kwasababu Mzazi anapendelea,ametaka kuhusika na hapo pia,ila kijana mwenye akili zaidi,lipa wewe mahari pesa ya wazazi na ndugu ielekeze kwa mambo mengine.
👉Kama uneshindwa kulipa mahari,wakakusaidia siyo dhambi ila haitakupa heshima na nguvu.
👉Mdada kukusaidia kulipa mahari siyo dhambi ila umevua kofia yako umempa yeye awe kichwa, yeye anachoweza kukusaidia *Nikuongea na familia wasikutoze mahari zaidi ya uwezo wako,mwambie mimi ninauwezo wa kulipa laki 5 tu😎😎 ikizidi hapo tutasogeza mbele harusi au sioi 😍😍 sasa kama anakupenda yeye aende apambane na hali ya familia yake mpaka washushe to laki 5.
👉Na si vizuri kukopa mke,eti muoane utamalizia mahari huko ni kujidharirisha na kujipa mzigo mkubwa baada ya kuoana,si wote uwa wanamaliza kwa wakati wengine mpaka wanazaa watoto miaka 5,10 ndo wanakuja kumalizia deni.
*ANGALIZO LANGU KWA VIJANA*
1.Kama unahisia za kuoa pia uwe na hisia za kutafuta pesa mapema.
2.Kama bado huna uhakika wa kupata pesa Usitongoze mdada yeyote, *Jifanye Uwaoni, au wote ni dada zako wa kuzaliwa* ila ukishaanza kupata kipesa fungulia speed za kutafuta.
3.Mahusiano ni gharama ukiamua kusema I LOVE YOU JUA KUNA NA I GIVE YOU.....
4.Vijana msikwepe kazi, au kupenda kazi za kukaa kwenye kiti, chimba hata mitaro,chota maji,buruta toroli tafuta pesa kila kona mahusiano na ndoa ni MATUMIZI.
5.Na ninyi wadada ukianza kuchumbiwa Soma na Angalia uwezo wa mchumba wako ulo mkubali, *Kipato chake cha 50elfu kwa mwezi,wewe unamtaka 50elfu kila wiki ya kusuka,unataka IPhone simu wakati yeye ana tekno ya batani, huu nikuwa CHUMA ULETE* umemkubali huyo taka vichache kwake,mkioanana pambaneni wawili kuinua kipato chenu.
6.Dada japo pesa ni muhimu katika mahisiano ila,kabla ujaingia kwenye mahusiano uliishije? Balance mazingira,usimpende au kutompenda mtu kwa sababu ya uwezo mdogo,maisha ni safari ya mabadiriko ujui kesho anaweza kuwa milionea.
*By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)0755444078*

NDUGU KUCHUMBIA BINTI MMOJA

*Swali:* Kuna wa kaka 2 mtu na mdgo wake yn wamekutana ba mkubwa na mdogo,,,yule kaka mkubwa alikua na mahusiano na bint lengo amuoe 🤗lkn ikafikia kipind yule bint gafla t akamwambia huyo kaka kuanzia leo ckutaki hata kukuona😫bac kaka wa watu akakubali matokee maisha yakaendelea,,,,,baada y muda flani mdg mtu akamwambia kaka ake kua nimepata bint wa kuoa lkn kaka naonba unisamehe mm ndo nmemshawish mchumba ako akukatae ili nimuo mm je kama n ww unafanyaje🤗na je ndugu yko akishaoa utaweza kwenda kwake maana hapo awali bint alikwambia htk hata kukuona inakuaje hapo🤔
*Anajibu Msaikolojia...Ev Elisha Kazimoto*
*UNAWEZA KULIPOKEA KIRIHO ILA KISAIKOLOJIA LITAKUTESA*
👉Suala la mahusiano ni gumu sana kisaikolojia tofauti na watu wanavyo dhani, likibebwa kirahisi linaweza kukufanya *Kichaa aliye timamu*(Mtu aliyepoteza uwezo wa mchakato wa akili katika utulivu japo haokoti makopo na kula uchafu)
👉Mahusiano yanahitaji ukiyaanza ujipange sawa, *Uingie kwa sababu za Msingi zitakazo shibisha akili na moyo wako amani, na Ukitoka ujue unatoka kwa sababu za Faida ya Usalama wako wa uzuri wa baadaye,siyo sababu ambazo zitakuuma ukikumbuka ukagundua ni uzembe au hila flani za watu*
👉Sasa hawa ndugu na mke wao mmoja wote wako kwenye Mtihani mkubwa kisaikolojia ambao unaweza kugharimu (Mahusiano ya kiundugu, kiroho,na kindoa) hapa kila mmoja ana mtego na maumivu yake.
1⃣Mdada mwolewaji(Yuko kwenye mioyo wa watu wawili ambao ni ndugu wa karibu) anaweza kutumika kama silaha ya kuua hao ndugu,familia zao au ndoa zao.
👉Mdada anakuja kwenye familia ila haji kukiwa amani anakuja kama CHANZO CHA MACHAFUKO kwa ndugu wawili na familia yote.
👉Namna ya kupunguza shari *Akubali kwa siri Awe mchepuko wa Kaka mtu(kaka wa mme wake) ampe penzi la kutosha naye kisiri siri ili kaka mtu atengeneze amani kati yake na mdogo wake na wazazi.
👉Ila itakuwa ni hatari kama mmewe atagundua moto na vita vitatokea.
*Huo ndo mtihani alio nao*
2⃣Kumbuka kaka mtu anampenda bado mke wa mdogo wake maana yeye aliachwa si kwamba aliacha.
👆👉Upendo huo unao fukuta ndani, vipi ukiibuka wote wakiwa wameoa lakini huyu akaendelea kumfatilia mke wa mdogo wake( Ndoa zao wote ziko hatarini) 
👉👆Kaka mtu akiamua ku REVANGE(kulipa kisasi )kwa ajili ya kutibu majeraha ya moyo kwasababu ya kumeshwa sega la asali mdomoni kwa hila?(hapo kuna hatari zaidi)
3⃣Mdogo mtu ameua undugu kwa tamaa,Alifanya kwa upumbavu, itakuwa ni vigumu kueleweka kwa kaka yake na familia, mpaka wawe na kiwango kikubwa cha Kiroho.
👉Jambo la msingi hapa *Refarii ni Mdada, AWAACHE WOTE wawili akaolewe kwingine, maana yeye na mdogo mtu wote Hawana Akili* wanapooana hawaendi kukaa mawinguni, wanakaa kwa jamii na ndugu zao ni hao,unakuja umeisha wagawanya mioyo,unadhani baba na mama na baadhi ya ndugu mawifi na mashemeji *watakufurahia kuona wewe ndo umewafanya mtu na kaka yake wasiingiliane,wasipendane,wasisaidiane nk, Utapendwa na wawili ila kumi watakuona mchawi wa Familia na wazazi Watakulaani milele* acha, acha kabisa mzazi yeyote anapenda kuona wanae wanapendana wanasaidiana sasa wewe umewagawanya,hata kama una pesa watakuona wee mchawi wa uzao wa tumbo lao.
👉👆Ushauri wa dada awaache wote. Ajue huyo mdogo mtu ni mbovu kuliko kaka yake.
By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)0755444078

ZAWADI ZA NGUO ZA NDANI

*MADA YA LEO 27  MAY 2020*

Katika Mahusiano yeyote zawadi kwa  ndugu zangu wa-maasai huita sawadi, ina nafasi gani katika kukuza penzi au mahusiano yenu? Je  Pia?  kuna  baadhi ya zawadi inapaswa isitolewe kwa watu walioko katika mahusiano     mfano: Wapo wapenzi   wana nunuliana hadi CHUPI  na BOXER, 

Hii  imekaaje? JE ZAWADI ZETU kwa watu tuwapendao ziwe na mipaka au full kujiachia.

*N:B:* Siku Mkiachana  roho yako  isikuume wala  kuzidaii kwa Ex  wako huyo.


‼️‼️ KARIBUNI
*Nianze na hii ya zawadi*
_ZAWADI NI MIONGONI MWA VICHOCHEO VYA MAPENZI KATI YA WANA MAHUSIANO_
👉Zawadi ina kazi kubwa kwa anaye toa na anaye pokea kwa hiyo wote mnahitaji kuwa makini sana Kiroho na Kisaikolojia.
1⃣Kwake atoaye zawadi anawekeza( *Anatafuta nafasi chumba cha kukaa katika moyo wa anayepokea zawadi*)Hii ni kibiblia👇👇👇👇
21 kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako. 
Mathayo 6:21

👉Kazi ya zawadi ni kuhifadhi moyo wa atoaye zawadi ndani ya moyo wa aliyepokea zawadi.
👉Kwa hiyo hapo jua pindi utumiapo au uishipo na zawadi ya mtu jua *Unaishi na moyo wake* 
👉Sasa kama ni zawadi njema jua upendo utakuwa mkubwa kati yenu na mioyo yenu itaambatana sana.
👉Kwa sababu hiyo, Zawadi ni mpeano kila mtu tafuta nafasi ya kukaa moyo wako ndani ya mwenzako.
👉Kama unataka upokee tu zawadi jua mwenzako *Yupo moyoni mwako,ila wewe haupo moyoni mwake* ndo maana mkiachama wewe utaumia sana ila yeye hataumia sana,atapona haraka wewe utachekewa kupona machungu.
2⃣Kazi ya zawadi kwa apokeaye, inakufanya wewe kuwa *Mtumwa wa Nafsi, Hisia,Maamuzi kwa aliyekupa zawadi* ndiyo maana unapaswa kuwa makini na zawadi na aina ya zawadi....Hii ni kibiblia pia👇👇👇👇
Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe; Bali achukiaye zawadi ataishi.

Mithali 15:27
👉Zawadi inakuondolea Ujasiri binafsi mbele ya aliyekupa zawadi.
👉Zawadi inakawaida ya kununua Hisia zako,na maamuzi yako.... _Ndiyo maana wengi wanaopoteza Usichana wao au uvulana wao,wokovu wao nk Zawadi zilitangulia kununua maamuzi yao,akija kuambia Sex,au hitaji lolote anaona ni gumu lakini akifikilia zawadi alizopewa,alizokula anaona mwenyewe *Atakuwa si muungwana kumkatalia* atakuwa mkatili kumgomea, anaona aibu kukataa lolote._
👉Ni watu wachache ambao Zawadi hata ziwe za gharama *Haziwezi nunua Maamuzi na Nafsi yake* hao ni WACHACHE NA WAWE WAMEIVA KIROHO NA KISAIKOLOJIA ila wenye wokovu wakawaida wa wengi wetu HUCHOMOKI( a.k.a HUTOBOI).
👉Kiwango cha zawadi ndo kiwango cha nguvu ya Kulainisha moyo wa mpokeaji na kununua nafsi yake na maamuzi yake.
👉 *NB: _Zawadi ni muhimu kuzichunguza na kuwa nazo makini, Zawadi ni Sadaka katika Madhabahu ya moyo,ikinenewa maneno ya kiroho au ya kipepo inauwezo wa kutekeleza matakwa,ndo maana unapaswa kujua zawadi hii inatoka kwa nani,viwango vyake vya wokovu,au utu wake na inahusiana na nini_* Kuna zawadi ukiipokea kwa mtu,ukiitumia
1.Hutokuja kuzaa
2.Hutaolewa au kuoa
3.Magonjwa yanaanza hapo
4.Laaana na mimosi juu ya mafanikio yako.
NIMALIZIE KWA KUSEMA KATIKA POINTI YA SWALI:
👉Zawadi ya nguo ya ndani katika Uchumba *Usipokee* Narudia Usipokee labda wale bao wefikia kiwango ambacho zile nguo zinapelekwa kwenye sendoff kwaajili ya bibi harusi kwaajili ya harusi kesho yake.
👉Umekosa zawadi zote mpaka ununue nguo za ndani kwa mwenzako.
👉Sehemu za Siri ni maeneo maalumu ya AGANO,so na kinachofunika pale lazima kiwe safi kina enda na nguvu ya kuhifadhi agano.
👉Umewahi kujiuliza kwa nini wachawi uwa wanaiba *Nguo za ndani za wamama na wadada wengi,wanakuta imeibiwa haionekani tena au anakuja kuipata baadaye ila matokeo baada ya kuipata au kupotea waulize wanajua shida zake,ni somo maalumu hilo si la humu VERY DANGER* NDO MAANA HATA WADADA NA WAMAMA MSIZOEE KUFUA NGUO ZA NDANI NA KUANIKA NJE ZIKALALA,ITAKUGHARIMU SIKU ADUI YAKO AKIFANIKIWA KUISHIKA.
By *Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)*
0755444078

MAHUSIANO NI GHARAMA

NAULIZA HIVI,
          Baadhi ya watu  wanasema wanaogopa kuanzisha penz kwa sababu wanaogopa gharama ya penzi lakn pia wengina wanasema,
  Penzi la kweli halina gharama je ni kweli au wapendwa hiyo imekaaje hapo? Majb na maon tafadhali🙏🙏🙏
*Anajibu Msaikolojia Ev  Elisha Kazimoto*
*KILA KITU KINACHOLETA MATOKEO CHANYA,RAHA,FURAHA MCHAKATO WAKE LAZIMA UHUSISHE GHARAMA*
👉Ni muhimu kujua kuwa gharama ni mchakato ambao unakulazimisha kufanya jambo husika ili utoe matokeo chanya, kwa lugha nyepezi *Inakulazimu kufanya jambo hata kama unahisi ugumu au uwezo ni mchache,inakulazimu ufanye* ili kutimiza Azma ya furaha yako.
👉Sasa mahusiano ni sekta ambayo mwenye akili timamu unapoingia mchakato wa kuanzisha na kulinda mahusiano LAZIMA UINGIE GHARAMA KUBWA ili utoe matokeo unayoyahitaji na usipo ingia gharama basi utapokea matokeo au majibu tofauti na shauku yako.
*Baadhi ya Gharama ambazo unaziingia kwenye mahusiano*
1⃣MUDA: Ukianzisha mahusiano,uwe tayari kutoa muda wako kwaajili ya mwenzako,muda wowote ili kulinda furaha na upendo.
👉Wengi walioanzisha mahusiano na KUJIFANYA BUSY,mahusiano yao Yalivunjika,au walienda bila furaha.
👉Kuna wakati umebanwa,lakini inakulazimu uwe na muda wa kuwasiliana na kumsikiliza,kumwambia kitu mpenzi wako.
2⃣GHARAMA YA PESA. Ukianzisha mahusiano uwe mkaka au mdada USIWE MBAHIRI AU KUHURUMIA PESA, jua tu utaingia gharama ya kuhudumia mwenzako kwa PESA.
👉Usipo taka pesa ikitoke ukakwepa gharama mahusiano yata yumba au kuvunjika.
NB:Uwe makini hapa kuna watu wanaingia kwenye mahusiano wanalengo la kutengeneza KITEGA UCHUMI,wengine kwa sababu ya malezi au hali zao wana uhitaji mkubwa wa kutunzwa kipesa. Sasa usipo jipanga kwa gharama ya pesa UTAYAKIMBIA MAHUSIANO.( Ila ushauri usiwe mchwa kwenye mahusiano unatafuna tu, kuwa ng'ombe unalishwa nawe unanywesha maziwa)(yaani hudumiwa nawe hudumia kwa pesa)
3⃣Gharama ya KUUMIZA NA KUUMIZWA, kwenye safari ya mahusiano kuna wakati UTAMUHUMIZA MTU AU ATAKUUMIZA kwa makusudi au kwa bahati mbaya,ujipange kwa gharama hiyo kubeba maumivu ya muda na kuyatua kwa amani na mahusiano yanendelee.
4⃣Gharama ya WEWE KUTUMIA AKILI KUISHI MJINGA/KICHAA MZURI.
👉Wengi hawajui kwenye ndoa au mahusiano *Mmoja wapo ni Mjinga au Kichaa mrembo/handsome* ambaye ukiamua ujibizana naye au ku ACT kwa matendo yake juu yako NDOA AU MAHUSIANO yatavunjika au itakuwa kelele kila mara.
👉Dawa ya kukwepa kero na migogoro wewe ongeza uwezo wa akili timamu,ila mwenzako umuhesabu kama *Kichaa mrembo au handsome* kama haleti madhara makubwa hasa katika uchumba ila kwneye ndoa WEKA MUHURI kwamba ninaishi na mgonjwa,mimi ni mzima hapo mtazeeka pamoja.
👉Msiwe vichaa wote ndani,mmoja awe mwenye akili,APUUZIE Shari hizi,hapo mnaenda, sasa KUPUUZA KILICHOKUUMA NDO GHARAMA HIYO KUBWA EVER HAPPENED.
Niishie hapo zipo nyingi.
*By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)*

MAHUSIANO AYLIYO KUFA

*Hapa Kuna sababu kadhaa Hatari*
1⃣Mlianzisha mahusiano BILA MALENGO HALISI, inafikia hatua uhalisia ukikosa watu wanapoteza hamu kati yao.(maana kinacho BOND watu ni Malengo)
2⃣Umeanzisha mahusiano ukiwa na Mbadala moyoni au njiani katika safari ya mahusiano kuna Abiria mwingine umempa lift ameshusha upendo wa mtu wa kwanza.(uwezi kubeba watu 2 kwa upendo sawa ndani yako, mmoja atapotea)
3⃣Mmekosa Maarifa ya Kisaikolojia ya kuendesha mahusiano ili mtie bidii kuyalinda na kuchochea upendo.
4⃣Mkisha juana kimwili(sex) kunazaliwa mazoea na dharau unzuri(kuna dharau mbaya) ambayo mtu anakudharau kwa kukuchukia, ila dharau mzuri ni mtu *Anakuona kawaida,huna jipya kwake,mvuto wa kumuangaisha akae akikiutafuta tafuta* ila kwa uhalisia HAKUCHUKII.
*By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)*

USALITI WA WAZI KWA NINI?

Kuna Dada mmja ameolewa sasa wana mtoto mmoja na mwingine tumbon ,,,,lkn mume cku y Jana amefanya kituko yn amerudi nyumban akiwa na mwanamke mwingine na nyumbani mke wake yupo,,,,,iv wanaume mnakwama wp kitu kama hiko unategemea kitokee nn labda 🤔
*Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*
*Hapa inabidi turudi nyuma sana,katika INTIMACY YAO, tusianze kuangalia kituko alichokifanya mume, kila kitu kina Catalyst*
👉Kuna mambo yanapelekea maamuzi mabaya au ya adhabu ya kisaikolojia kufanyika.
1⃣Kama watu wana mahusiano mazuri ya kindoa,mwanaume awezi fanya kitu kama hicho,na kama anatabia ya unzinzi atafanya kwa siri huko ila si kiivi alivyo fanya.
2⃣Kama wana mgogoro ambao umepelekea mwanaume kukosa baadhi ya haki zake kama SEX,HESHIMA nk, ataamua kukuonyesha anaweza kupata mahitaji hayo nje na wewe.
👉Sasa hapo hatuhukumu mtu mmoja lazima tuwangalie wote,chanzo cha shida kiko wapi,nani anapaswa kubadirika ili mwenzake abadirike.
Ila kisaikolojia hapa *Mwanamke kuna mahali amejisahau*
👉Wanaume wengine si wepesi wa kupiga,kutukana,au kukufukuza ila ATAKUJIBU KWA KUKUUMIZA KISAIKOLOJIA, inaitwa *Psychological Punishment*

MUDA SAHIHI WA KUINGIA KWENYE NDOA

*🌷🌷MADA*🌷🌷🌷 *Je! Niwakati gani sahihi unafikiri kijana aoe au Kuolewa ??*
Karibu Sanaa🥰
*Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*
*MUDA SAHIHI WA KUOA NA KUOLEWA*
👉Kikawaida jambo lolote ili lifanyike kwa ubora na uzuri na mtu alifurahie au limnufaishe lazima lizingatie mambo yafuatayo...
1⃣Uhitaji wako ni mkubwa kuliko kutolihitaji.
👉Kuna muda ambapo kuna jambo unalihitaji ila halina umuhimu sana kwa wakati huo,kuna wakati lina umuhimu,na kuna wakati lina ulazima.
*Muda wa umuhimu na ulazima* ndo muda sahihi wa kuoa au kuolewa.
_Viashiria vya Umuhimu na Ulazima_
1.Kusudi ulilo nalo moyoni mwako la Kimungu linahitaji mtu wa pili akusaidie?
2.Majukumu yako kuongezeka na kuanza kushindwa kuyamudu.
3.Vishawishi vya zinaa kuongezeka kila mara na kuelekea kukushinda.
2⃣Ukiwa Tayari kimaandalizi kumtumza mme au mke bila kuhisi umeongezewa mzigo mzito katika maisha.
3⃣Kumpata mtu sahihi wa kuanza naye safari ya maisha ya ndoa.
4⃣Kigezo cha umri miaka 20
_Hivi ni vitu vinavyo mwongoza mtu kuingia katika ndoa na akaishi maisha ya amani na raha na mwenzake._
By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)

MAWASILIANO NA EX -WAKO

Swali:
*_Je, ni sahihi kuendeleza mawasiliano na Ex boyfriend/Ex girlfriend? Je, inawezekana watu walokuwa wapenzi wakaachana kuwa marafiki?_*
*Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*
*KUACHANA SI UADUI,ILA LENGO LA KUACHANA LISIPO ZINGATIWA INAWEZA KUWA TANZI KWAKO(UNAHITAJI KUJIULIZA KWA NINI MLIACHANA,SABABU HIYO ITOSHE KUKUWEKEA MIPAKA YA MAWASILIANO NA HUYO EX WAKO*)
👉Usipojua Dhana ya kuachana,utavuruga mahusiano yako mapya au ndoa yako.
👉Sababu iliyofanya muachane ndo inapaswa kukuongoza kukata mawasiliano ya karibu na ex wako,usipo kata mawasiliano naye ATAVURUGA MAISHA YAKO MAPYA ya ndoa au mahusiano wakati yeye anamtu wake au ana maisha yake au atakauwa na maisha yake bila wewe.
👉Unashauriwa ex wako muwekee mipaka ya mawasiliano,kusaidiana,kukutana nk....
👉Walio wahi kuwa kwenye mahusiano,pamoja na kuachana,kuna namna mioyo yao iliwahi kuungana,kuaminiana na kupendana, *kwa hiyo mawasiliano ya mara kwa mara,yanaweza TIBUA hisia za mwanzo na kuwafanya wa RUDIANE kihisia na kujikuta wanaanza mapenzi ya siri nje na ndoa zao au mahusiano yao*

By Ev Elisha Kazimoto(Psychologist)

SUALA LA NDOA NI SUALA LA WAKATI

🪁🪁 *SUALA LA NDOA NI SUALA LA WAKATI*🪁🪁
_Kila jambo muhimu katika maisha ya mwanadamu,uwa tamu na zuri kama likitokea kwa wakati wake unaofaa_
🪁Wakati wa ndoa siyo umri, wala wkati wa ndoa siyo uwe umepata kazi, wala siyo uwe uko well off,suala la Ndoa *_Nila wakati ambao Mungu anamleta mtu sahihi, awezaye kusimama nawe kwa wakati ulio nao_*
🪁Siyo kila mtu anaweza kusimama nawe kwa wakati flani(hata kama amaeokoka au anauwezo kiuchumi)
🪁Kuna Majira ukimpata mtu kwa wakati wa Mungu, anafuta *Historia za Maumivu ulizo pitia,anaondoa Distance ya muda mrefu ukiokaa bila kuoa au kuolewa*
🪁Kwa upande mwingine waweza pata mtu katika muda wa haraka sana,mwenye uwezo sana,ila *Akauumiza Moyo wako na Ukachukia Mahusiano* Shida siyo yeye,shida ni Muda mliokutana haukuwa Muda sahihi kwako kukutana naye.
*_Jifunze Kuutafuta na Kuungoja na kuuombea Wakati wa Bwana kwako ambao utakuletea Furaha ya maisha katika ndoa na si majuto. Unapaswa kujua Mungu aliumba watu PAIRE, kila mtu anawake,usiwe na hofu ya kutokuolewa au kuoa_*
              ©2020 
*Ev Elisha Kazimoto*(Psychologist)
Whatsapp 0755444078

MAUMIVU YA MAHUSIANO

💊💊 *KATIKA MAUMIVU YA MAHUSIANO KUNA FAIDA YA KUTIBU MOYO WAKO*💊💊
_Mara nyingi watu wanaotuumiza katika mahusiano hawajui kuwa wanatujengea uwezo mkubwa wa kuendesha mahusiano mengine au ndoa yako bora zaidi kuliko jinsi wangetufurahisha. Kwa mwenye uwezo wa kuingia katika mahusiano kwa nia ya kuandaa FUTURE yake, kila maumivu ya kwenye mahusiano ni Darasa la Ushindi kwa Kesho yako,na ukishindwa kujifunza kwa yale yaliyokuumiza uwezi kujifunza kuboresha au kustawisha mahusiano yako au ndoa yako.Kwa hiyo Usimchukie aliyekuumiza kwenye mahusiano,bali amekujengea uwezo wa kutokosea tena ukaumia zaidi._
*Falsafa ya Kisaikolojia na Ev Elisha Kazimoto*(Psychologist )0755444078
         ©2020

MAAMUZI YA KUPENDA NA KUPENDWA

😘😘 *MAAMUZI YA KUPENDA AU KUPENDWA*😘😘
_Maamuzi ni Chaguo analolifikiria mtu ili kulifanikisha. Wengi wetu katika safari ya Kuanzisha maamuzi hatuanzishi mahusiano kwa Matokeo ya *Fikira za Kudumu* juu ya Maamuzi, wengi wetu tunasukumwa na *Mazingira Shawishi* juu ya kuanzisha mahusiano, ndiyo maana mahusiano mengi hayafiki kwenye *Ndoa* Break up zinakuwa nyingi. Shida ni Fikira ya Kupenda au Kupendwa ilitoka kwenye Mazingira au Kwenye Nia ya Dhati iliyolenga kutimiza Shahuku la Ndoa katika Muda Husika_
*Falsa ya Mahusiano na Ev Elisha Kazimoto*(Psychologist ) 0755444078
            ©2020

KIJANA KUMUWEKA NJIA PANDA MDADA

*SWALI KUTOKA KWA MDADA*
Jamaniiiiiiii wanaume munapotoka from one relationship to another be very careful,unapomwabia binti nitakuoa,anakaa na matumaini akikusubiri, lakini unavyo muache dhuuuuuuuuu,amekusubili miaka amejitunza juu yako,all over sudden una break his heart, lazima mutaigia kwenye ndoa na laana tu, wanaume kuweni makini musitamani mwanamke alie sababu yako,
*_Anajibu Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto_*
*Message hii ni nzuri ila inge COVER jinsia zote boys and girls, kwakuwa watu wengi wanatumia mahusiano kama site ya kutimiza short terms plans,(Malengo yao ya muda mfupi) mbali na lengo la muda mrefu la ndoa.*
Wengi wanapoingia kwenye mahusiano....
1.Hawana uhakika kama wako tayari wao kuongia kwenye ndoa.
2.Hawana uhakika kama walioingia nao kwenye mahusiano ya kuelekea ndoa ni watu sahihi wa kuoana
3.Hawajawa na dhamira ya dhati ya kuipenda ndoa.
4.Wanateswa na historia za waliyopitia nyuma
5.Wanateswa na taarifa za mazingira yanayowazunguka
_Mambo hayo ndo yanawafanya watu wote wote vijana kwa mabinti kuwa wasaliti au kuvunja mahusiano bila sababu za msingi._

MAVAZI KATIKA MAHUSIANO

*Miongoni mwa majukumu na wajibu wa kila mmoja kwa mwenzake ni kuangalia mwonekano wa mwenzako ukoje*
👉Ukiwa bachela unavaa kwa kadri uonavyo vema wewe ila ukiingia kwenye mahusiano Imara au ndoa utavaa kwa kadri ya mwenzako aonavyo vema kwake(unafanya kitu kinacho shika hisia zake siyo za wengine)
👉Sasa hapa mahusiano mengine yamevunjika mengine yamekuwa hatarini kwakutojua saimolojia ya mahusiano na mavazi au urembo.
👉Narudia pamoja na kwamba unavaa ili upendeze,kimbuka unapendeza kwaajili ya nani, kwaajili yako ili utafutwe au upendwe na wengine au kuufurahisha moyo wa mpenzi wako ajisikie Alichagua Cute au Hb na ajisifie kwa wengine?
👉Wao wanao sema mme wangu au mke wangu hawezi nipangia nivaeje nitokeje,aniache....Kweli atakuacha atawafuata wanaomwambia hivi ulivyo vaa umebamba au wanao vaa kama anavyotaka yeye, USIJE KULALAMIKA.( *Umekataa mwenyewe kuingia kwenye Hisia zake*)
By Ev Elisha Kazimoto(psychologist )0755444078

MSHAWISHI MKUU WA KUFANYA MAPEMZI

*KWA MSAADA WAKO NA WENGINE HAPA TUWEKE KUKBUKUMBU VIZURI ZA KIROHO NA KISAOLOJIA*
👉Kwanza kabisa,hali yoyote unayoweza kuiona huifurahii au ni changamoto kwako juu ya mchumba,mkeo,mpenzi wako huyo..... *Inamahusiano ya moja kwa moja ya kiroho na Kisaikolojia Umeisababisha wewe Mwenyewe Kijana na SI BINTI* ( Hivyo katika lawama unazoweza kutoa,zitoe kwa NAFSI YAKO halafu utafute msaada wa kutoka katika mzigo huu)nasi na darasa hili lipo kwaajili ya kukusaidia.
NB: *_Tunakila sababu ya kusema ukweli,kuchanganua kwa kina ili TUKUSAIDIE,tukikupa polee na ushauri mwepesi,Tutakupoteza na kuwaua wengine wajao ila hatutakupa ufumbuzi_*  (Sasa Fuatana nami)
1⃣Alama ya kwanza kwa mwanaume au mwanamke mwenye mapenzi ya Dhati kwako na anayeweza kukupenda daima hata kwenye ndoa,ila ambaye HAWEZI KUKUSALITI na kuwa na mahusiano ya siri mengine ni yule *Anayeweza Kuwa mwaminifu Kutokutaka MFANYE NGONO kabla ya Ndoa*
👉Sasa kwa maelezo yako, binti alijitahidi kwa mara ya kwanza kutimiza kanuni hii ya kukukwepa Msishiriki Ngono(SIYO TENDO LA NDOA KAMA ULIVYOLIITA MAANA NINYI SI WANA NDOA) ALIKATAA KUSHIRIKI NGONO NA WEWE,lakini ukatafuta ushauri pengine,ukaja na mbinu nyingine UKAMSHINDA mkashiriki NGONO kinyume na kanuni za kiroho,kinyume na kanuni za Kisaikolojia( *Hapo ndo uliharibu kila kitu*)
👆👉Upendo wa dhati na furaha yake juu yako,na uaminifu wake kwako ulikuwa umefungwa kwenye Siri ya kutojuana kimwili,baadaya ya kujuana....
1.Heshima,Upendo,Uaminifu Vikapotea(Maana mlivifungua kabla ya Kiapo ch Uaminifu)
👉Sasa unataka Akupede kama nani? Akuheshimu kama nani?Akuamini na kukulindia uaminifu kama nani? *_Wakati anakuona wewe ni muhuni,mlaghai,mtu asiye mvumilivu,na mwaminifu?_* Kwasababu tendo la mpakanafanya ngono Lugha ya udanganyifu ilitumika,lakini mlifanya wote mkijua hii SI HALALI.
👉Kwa maneno mengine kiroho mmeuondoa mkono wa Mungu juu yenu uletao amani,furaha na upendo kwenu,mkabaki WAKIWA.(Laana hiyo ya Zinaa kibiblia)
👉Lakini kisaikolojia mkavuruga system ya Siri ya uminifu na hamu ya kujua siri(mkabaki WAKAWAIDA)
2️⃣Ulifanya jambo la kuumiza moyo wa binti kwa wakati ambao alikuwa hajawa tayari kuumizwa ndo maana AKAKUCHUKIA.
1.Umemlazimisha kufanya ngono,Ukambebesha Mzigo wa Majukumu ya malezi....Nje na wakati.
A)Mfano kama alikuwa bikira wewe umemdhalilisha na kuondoa heshima yake kabla ya kiapo...Unataka akupendeje,akuheshimu na kukuamini kwa Lipi?
B)Kama alikuwa si bikira, alijilinda asipate mimba muda mrefu ila wewe UMEMLAZIMISHA APATE MIMBA BILA KUTAKA(Unataka akupende kwa lipi hapo,au akuheshimu,ajivunie uwepo wako kwake kwa lipi?)wakati umemuanzishia safari ya miaka yakutokuwa huru?
3⃣Umemvuruga kisaikojia wakati alikuwa hajajipanga kiwa mama mwenye mtoto,changanya na maudhi ya mimba(mlio olewa na kuoa mnajua kipindi cha mimba kilivyo)sasa huyu mdada anateseka wakati jamaa aliye mtesa HANA MUDA WA KUMUHUDUMIA 24HRS/7DAYS? Asikuchukie wee nani?.
👉Kwanza kama alikuwa na wapenzi wengine means alikuwa bado hajadhibitisha nani wakumuoa,we ukamuwahi ukampamzigo wa mimba,kwa hiyo anaingia katika hofu na wasiwasi wa nani atamuoa na kukpa furaha..Je niwewe uliyempa mzigo?,ni yule aliyempenda kwanza je ataendelea kumpenda na mzigo wa mwingine?
NB:Vijana kwa mabinti fahamuni hili, *_Upendo wa uchumba au mahusianobya urafiki,Haulindwi au kuimarishwa na NGONO kabla ya ndoa,Inalindwa na Uaminifu wa wewe KUKATAA NGONO kabla ya ndoa,Kijana au binti atakaye kuacha kwa kigezo cha humpendi kwakuwa imemnyima ngono, Jua huyo ALIKUWA TAPELI,KIBAKA NA MUHUNI na Hafai kuwa mke au Mme_*
👉Sasa kijana nikushauri sasa. _Jambo la kufanya hapa baada ya kuharibu, Kwanza nenda katubu,uokoke upya,uongozwe sala ya toba upya,halafu ongea na mzazi mwenzio kuhusu hatima yenu,muulize atakuwa tayari muoane au muachane Utunze damu yako tu? Jibu atakalokupa yeye NDO ULIFUATE,Ukishakosea huna namna,tumikia kosa lako kwa amani ili usizalishe Matatizo makubwa bya baadaye_
*Imechambuliwa na Mchambuzi wa masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto(psychologist)*
   WHATSAPP 0755444078
        ©2020

MUDA WA KUTOA JIBU UKITONGOZWA

*MUDA WA KUTOA JIBU LA NDIYO AU HAPANA HAUKO FIXED,BALI UTATEGEMEA MTAZAMO,HISIA, ZA MWAMBIWA JUU YA ANAYE AMBIWA,PIA KAMA MTU NI MCHA MUNGU ITATEGEMEA CONNECTION ALIYO NAYO NA MUNGU ILI KUPATA JIBU LA NDIYO AU HAPANA*
NB: _Wengi katika kutoa majibu, wanazingatia mambo yafuatayo....._
1⃣Kukariri kwa mazoea ya watu kwamba mwanaume usimpe jibu haraka ataona kama ulikuwa umeisha sota kutafuta mme(Kwa hiyo hata kama anakupenda au siku nyingi anasubiri umwambie neno atajifanya hana muda na wewe mpaka umsumbuepo tena.( Angalizo: Unaweza kusubiri usumbuliwe tena jamaa akatafuta mwingine ukabaki na maumivu)
2️⃣Kuna watu wanachelewa kutoa jibu kwa kuanza kufanya utafiti wa *Uhalali wako wa Kumuoa,asije chukuliwa na Jambazi la kiroho au la kimaisha*(Hii imekaa sawa)
3⃣Kuna watu wanachelewa kutoa jibu la ndiyo au hapana kwa kusema Amauulize Mungu ila wengi wao *Wanauliza Mungu hali ya Hewa(ya mfukoni mwako)ikoje...Akigundua ATM inasoma maisha yako poa,hata Mungu hajasema chochote utasikia NIMEPATA AMANI KUBWAAAA SANA JUU YAKO baada ya kumuuliza Mungu, wengine kama *Wewe ni Kijana wa Kuishi kwa Imani(Wale wa Mbele ninaendelea...)Utaambiwa SIJAPATA KIBALI KWA MUNGU JUU YAKO,ila ukweli ni kwamba Ameona Mambo yako hayasomi.
*_Ushauri:Dada Toa jibu kulingana na Nia ya moyo wako,na kama ni Mungu basi muulize Mungu,kama unacheki hali ya hewa cheki vzr,na usimkawilishe mtu itakugharimu,Ukimpenda mpe jibu hata kama ni papo kwa papo,kama humpendi mwambie kwa ustaarabu Sijaona kama itawezekana_*
By Ev Elisha Kazimoto(Pychologist)0755444078

SAIKOLOJIA YA KULINDA MAHUSIANO

❤️❤️ *SAIKOLOJIA YA MAHUSIANO NI NGUMU SANA*❤️❤️
_Watu wengi ushangaa hivi imekuwaje na huyu tume break!!tume divorce!! Hivi huyu mtu amekuwaje tulianza kwa upendoooo wa motooo leo dah kama tunalazimisha vile!!_
👉Iko hivi, ili mahusiano yako yadumu, jambo la kwanza:
*_Unajua udhaifu wako na mapungufu yako, udhibiti mapungufu yako kwanza kabla ya kuyapigia kelele ya mwenzako,utafanya muda wa break up kusogea mbele,muda wa kuchokana usogee mbele( Yaani kama ilibidi (mbreak ndani ya miezi 6 muda utasogea mpaka mwaka 1)_*(Hiyo ni Faida kubwa)
👉Pili, _Akikisha unapomsifia mwenzako na Kumuona anakufaa sana (Katika Muda huo Yachungulie Madhaifu yake uyabaini) usikae unamsifia tu na Kujifanya Huoni madhaifu yake kisa upendo wenu mbichi na upo fire.(Muda wa upendo ukiwa juu ndo muda wa kumshauri na kumkosoa mwenzako na akaendelea kukupenda zaidi,ukisubiri upendo ushuke ukimkosoa ataona hufai na atakuchukia na itakuwa lango la break up au divorce_)
👉Tatu, Usisubiri ufanyiwe jambo ndo umfanyie mwenzako,wewe fanya kwake utalinda upendo na mahusiano( *Usisubiri upigiwe simu,usalimiwe,utafutwe,usifiwe,upewe zawadi, fanya wewe kwanza*) hayo mahusiano yata dumu imara.
*_Kutoka Meza ya Mwanasaikolojia Ev Elisha Kazimoto_*
       ©2020