🔥 *MADA INAYOWAPA KIZUNGUZUNGU WATU WALI HAI NUSU NA MAREHEMU NUSU*🔥
..............................................
Yupo kwenye mahusiano ya muda mrefu na mwenzake ila wametofautiana kwenye dhehebu. Yeye ni mlutheri(na ameokoka), mwanaume ni mkatoliki (na hajaokoka). Binti hayupo teyar kumfuata mwanaume na mwanaume vivyo hivyo. Kadir siku zinavyoenda na mwanaume anaona kuwa binti kasimamia misimamo wake, akamwambia binti hivi, akubali wafunge ndoa ya kikatoliki, then wakiwa ndani ya ndoa yeye atabadilika na kuwa mlutheri. Sasa hapo, ndio pamemuacha binti, njia panda. Haelewi afanye nini, haelew akubaliane nae au akatae...
Uhusiano wao una miaka 6 sasa, na tatizo liko hapo tu. Wanapendana na wanaelewana vizuri
..............................................
*_Anajibu Ev Elisha Kazimoto(Whatsapp 0755444078)_*
Hii mada inahitaji,utulivu katika kuichambua,ni mada ngumu isiyo hitaji ushauri au majibu mepesi. Vitu vya kisaikolojia au kiroho ni vitu vigumu kweli inapokuja kuvifanyia maamuzi.. *.kwanza mada hii Muhusika ni mtu mmpja tu,ndo anastahili kujadiliwa naye ni Binti*
👉Kwa maneno yake haya, *"Nipo kwenye mahusiano na kijana mimi ni Mlutheri(na nimeokoka),kijana Romani(Hajaokoka) mpka hapo tu,* _Inaonyesha mambo kama 3/4 kwa binti._
1.Binti hajui maana ya wokovu na hajawai kuokoka,ila amejipa jina la kuokoka kama FASHION.
2.Binti hajui maana ya ndoa na ndoa ya baraka na amani i atoka kwa nani.
3.Hakuzingatia kigezo chochote cha kiroho kumpata mme ila amempata kwa tamaa za mwili ikiwemo ngono,pesa,elimu,au uzuri.
4.Kiroho yuko 0% hawezi kutofautisha mapenzi ya Mungu na ya shetani, haki na dhambi,uchafu na utakatifu.
👉Pili kwa sentensi ya*Binti hayuko tayari kumfuata mme na mme hayuko tayari kumfuata binti* ni ishara kwamba binti Ni miongoni mwa waumini matapeli wa kiroho wanao shawishi watu wawafuate kwaajili ya kutimiza matakwa yao.
"Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,"
(1 Wakorintho 2: 4)
Msingi wa wokovu haufungamani na kuwaleta watu kwa Yesu kwa njia ya ushawishi,yaani kutumia pesa,vitu au mifump kama ya ndoa au ajira. Binti anadhihirisha wazi,kama kijana atasema *NAHAMIA* huko binti atakuwa tayari kuolewa. Swali la msingi,ni kijana amevutwa na injili ya Kristo au na mapenzi, kijana hataki kuukosa uzima wa milele au hataki kumkosa mdada mwenye shape hiyo..
3.Binti anasema, *kadri siku zinavyoenda kila mtu anamsimamo wake,hapo ndo panamuacha hoi hajui afanyeje* kwa sentensi hii Binti ndani yake ni marehemu wa Kiroho,yaani hana hata Alarm ya mbali ya Roho mtakatifu wa kumshauri lipi ni mapenzi ya MUNGU (Ndo maana nikasema Hawa wote *Niwapagani,ila MPAGANI SENIOR ni dada, Huyu kaka ni Mpagani JUNIOR*)
(Waroma 8 )
------------
9Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
...
14Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.
...
16Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
Kwa lugha nyingine huyu dada ni msanii mwigizaji wa wokovu ila hana maisha ya UCHAJI MBELE ZA MUNGU. ( *SI MUHUKUMU ILA NASEMA NIKIONACHO KWA MUJIBU WA BIBLIA*) Maana wale wajifanyao wako Rohoni zaidi ya YESU hawachelewi kusema _USIHUKUMU_.
👉Hakuna mtu yeypte DUNIANI aliye okoka,ana Roho wa Mungu ndani yake,akafanya maamuzi ya kijinga na kishetani,bayo mpaka mtu aliyeokoka leo au mpagani anasema si sahihi.... Hayupo,ukimuona huyo jua ni BANDIA WA WOKOVU.
*MASWALI YA KUMUULIZA HUYO DADA*
1.Amempataje huyo kwa Mungu au kwa mtaani?
2.Miaka 6 anaombea uchumba au anaendesha uchumba kwa pesa na mapenzi?
3.Miaka 6 kwa mru asiyeokoka wawezaje kumzuia asifanye ngono( *je, ni kweli hajawahi kulala naye huyo kijana hata mara 1?) si jambo la hajabu ngono kwa mtu ambaye hajaokoka mwana dini ni BREAKFAST* si shida,si dhambi,hakuna hukumu,hakuna kujuta, ndiyo life style ya watu wa ufalme huo na wanajisifu kwa zinaa.
*NITARUDI KUHITIMISHA KWA LECTURE*
Kijana huyu hana kosa,wala shida,maana yeyote aweza oa atakaye jiingiza ndani ya 18 zake,hana limit ila tulio okoka tuna limit.
*"Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu cho chote."*
(1 Wakorintho 6: 12)
.
.
*_HIVI HIKI KIZAZI MBONA KINAPENDA KURAHISISHA SANA MAMBO HAYA YAHUSUYO IMANI KATIKA WOKOVU_*???!
Mtume Paulo akifufuka sasa ataliongoza kanisa la sasa,kama zamani zile alitaka kutia watu fimbo leo ingekuwaje watu wanavyo rahisisha mambo ya Mungu.
(1 Wakorintho 4 )
------------
20Maana ufalme wa Mungu hauwi katika neno, bali katika nguvu.
21Mnataka vipi? Nije kwenu na fimbo, au nije katika upendo na roho ya upole?
*_Inapofikia suala la kuizungumzia imani ya Wokovu,hatutamungunya maneno,japo wengi Wakristo feki wanaichukia kweli,wanahitaji utumie Hekima kuuubwa sana uovu uupe sura ya changamoto,Injili hiyo Mungu na aniepushie mbali katika utumishi wangu_*
WhatsApp 0755444078
No comments:
Post a Comment