🛣 *SEMINA YA NENO LA MUNGU KUHUSU UTUMISHI WA MADHABAHUNI PA BWANA*🛣
_By Ev Elisha Kazimoto(Whatsapp 0755444078)_
.......................................
*_Utumishi wa Kweli Katika Kristo Yesu_*
*SEHEMU YA 4:*
*"Hatua 7 za Utumishi wa Kweli Katika Yesu Kristo"*
....
....
....
_Shalom mtumishi wa Mungu uliye shambani mwa Bwana,leo nikusogeze hatua nyingine muhimu sana katika utumishi wa kweli katika Yesu Kristo. Hapa tutaziona *Hatua Muhimu 7 ambazo kila mtumishi unaye muona anatumika katika ofisi yoyote ya Kimungu(Mungu aliye hai) amezipitia. Lakini kwanza kabla ya kuiangalia hatua mojamoja nikurejeshe katika Sehemu ya mwisho ya Nguvu ya wito inavyo unganika na hatua za utumishi_
🌲 *Wito wa Mungu* uambatana na nguvu za Mungu ili kuuandaa moyo wa mtu kuweza kumtafuta Mungu na kutembea na Mungu ili afanye kazi alopewa.
*"Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi."*
(Matendo 1: 8)
🌲Na nguvu ya Mungu katika wito huleta shahuku ndani ya mtu ya kutaka kufanya kazi. Na hapa ndipo mtu ua za harakati kubwa za Kumtafuta BWANA kwa maombi ya kufunga kwa kasi.( *_Hapa katika kumtafuta Mungu kwa kasi inabidi uwe makini sana_*) wengine wameishia kuzungumza na Shetani na wala siyo Mungu( Nina shuhuda na mifano ya watu wengi).
🌲 Jambo la kujua hapa katika kumtafuta Mungu kwa kasi,ndipo *_Unausogelea ulimwengu wa Roho wenye wafalme wawili Mungu na Shetani_* wote wanafanya kazi katika ulimwengu wa roho,na ukisha fika kule *kila mmoja atataka kusema nawe* changamoto ya wengi hapa ni *Kupambanua sauti* nani anasema naye,kati ya Mungu na shetani.
(1 Yohane 4 )
------------
1Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
2Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.
3Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
.........................................
🌲Kwenye eneo hili la kupambanua roho(sauti)unapoanza huduma,ukiwa katika mchakato wa wito unapo mtafuta Mugu kwa kasi, LAZIMA UWE NA MENTOR( Mzazi wa Kiroho aliye makini katika huduma), wengi waliokosea katika Eneo la Kumtafuta Mungu kwa kasi, wameishia *Kuja na Mafunuo feki,machafu,ya uongo,ya ngono,ya utapeli,ya kiuganga,maigizo* lakini ni kweli alifunuliwa,aliongea na Mungu,malaika,akamwelekeza la kufanya katika huduma yake,hiyo siyo shida kufunuliwa, *_Shida ni nani kakufunulia?_*
(2 Wakorintho 11 )
------------
12Lakini nifanyalo nitalifanya, ili niwapinge hao watafutao nafasi wasipate nafasi; ili kwamba katika neno hilo wajisifialo waonekane kuwa kama sisi.
13Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.
14Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
...........................................
🌲 Ndiyo maana utasikia watu wanasema, *_(Hapana,mtumishi huyu hapana,huyu siye Mungu,haya ni mafunuo ya kuzimu)_* shida imetoka kule hakupata mtu wakumsaidia kutafsiri sauti ile.
(1 Samueli 3 )
------------
4basi, wakati huo Bwana akamwita Samweli; naye akasema, Mimi hapa.
5Akamwendea Eli kwa haraka, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akasema, Sikukuita; kalale tena. Naye akaenda, akalala tena.
6Bwana akaita mara ya pili, Samweli! Samweli! Akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Akajibu, Sikukuita, mwanangu; kalale tena.
7Basi Samweli alikuwa hamjui Bwana bado, na neno la Bwana lilikuwa bado halijafunuliwa kwake.
8Bwana akamwita Samweli mara ya tatu. Naye akaondoka akamwendea Eli, akasema, Mimi hapa; kwa maana uliniita. Ndipo Eli akatambua ya kuwa Bwana ndiye aliyemwita yule mtoto.
...........
...........
*HATUA 7 MUHIMU ZA KIROHO KUZIPITIA*
......................................
1⃣ *Utakatifu* Hii ni sifa ya kwanza kabisa kwa mtu yeyote anayetaka kumtumikia Mungu wa kweli aliye hai, lazima awe *Mtakatifu*,maana hapa unaenda kufanya kazi na Mungu mtakatifu na Roho wake mtakatifu. Sasa huwezi enda kufanya kazi ofisi usiyo kuwa na sifa zake.( *Zaburi 14:2,16:3*)
👉Mungu akipo taka kusema na mtumishi wake au kumtumia kwanza ni kumuagiza *Kuvua viatu/uchafu,tabia zisizo faa ndo amsogelee* Mungu hawasiliani na *mtu mchafu* (Yohana 9:31),ila anaweza toa maelekezo kwa mtu mchafu atafute kutakasika.
(Kutoka 3 )
------------
4Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
5Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
👉Hautaweza mumtumikia Mungu kama huja vua tabia zako za asili na matendo yako yasiyo faa,hata yale unayo yachukulia poa,vua kwanza ndo utumiwe na Mungu.
"Huyo amiri wa jeshi la Bwana akamwambia Yoshua, Vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo."
(Yoshua 5: 15)
👉Kumbuka kwenye huduma,au utumishi madhabahuni pa Bwana,hatupokei tu Maagizo ya Mungu bali tunaongea na Mungu,sasa usipokuwa mtakatifu sawa na Mungu alivyo mtakatifu,hutapata *kuzungumza na Mungu,* ila utapokea maagizo ya Mugu ya kukuonya.
(1 Petro 1 )
------------
15bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
16kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
👉Unahitaji kumuona Bwana katika huduma yako? Pigania *Kuvaa vazi la Utakatifu* viwango vyako vya utakatifu,ndo viwango vyako vya kumsogelea Mungu,na unapomsogelea Mungu zaidi ndo unapata *wepesi wa kusikia* haraka pale tu anapo nong'ona nawe,na ndo madhihirisho ya nguvu zake yanatokea.
"Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;"
(Waebrania 12: 14)
...............................................
*_Nihitimishe sehemu ya nne,tukutane sehemu ya 5,mafundisho haya na mengine mengi katika nyanja mbali mbali yanapatikana kwenye magroup yangu ya Whatsapp na facebook kwa no.0755444078_*
No comments:
Post a Comment