🛣 *SEMINA YA NENO LA MUNGU KUHUSU UTUMISHI WA MADHABAHUNI PA BWANA*🛣
_By Ev Elisha Kazimoto._
Whatsapp 0755444078
.................................................
*SEHEMU YA 2*
_Haleluya mtumishi wa Mungu nakukaribisha tena katika Meza ya Maarifa ili upate hazina za kukuongoza katika utumishi ulio ndani yako_.
..
..
*_"Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako, Kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia; Watapanda juu ya madhabahu yangu kwa kibali, Nami nitaitukuza nyumba ya utukufu wangu."_*
(Isaya 60: 7)
...............................................
👉Unapojiandaa kwa utumishi,ni muhimu kujua kuwa, *Hatuipandi madhabahu ya Bwana kwa Mazoea,au tunapo jisikia,tunaipanda KWA KIBALI CHA BWANA* na wote walioipanda madhabahu ya Bwana kwa Kibali cha Bwana huduma zao zimekuwa na Impacts(Matokeo chanya).
👉Tuna huduma nyingi za watu wanafanya kama desturi,hazina mguso wa ndani,zina mguso wa hisia,hazina mlipuko wa nguvu za Mungu bali zina mlipuko kelele za ushabiki. Lakini Huduma yoyote ya Bwana Yesu ililenga ilete Mageuzi katika mioyo ya watu,mazingira na kumletea Kristo utukufu. Lakini huduma nyingi sasa zinepoteza *Harufu ya Uwepo wa Mungu* ndiyo maana tuna waigizaji,tuna watumia Nguvubza Giza ili kuwashawishi watu waone Matokeo ya Injili.
*_"Mungu naye akishuhudu pamoja nao kwa ishara na ajabu na nguvu za namna nyingi, na kwa magawanyo ya Roho Mtakatifu, kama alivyopenda mwenyewe."_*
(Waebrania 2: 4)
...................................................
👉Unaweza kuona,tangu mwanzo enzi za mitume Yesu Kristo aliambatana nao katika huduma walizofanya mitume kila walipo kanyaga.
👉Je, unajipanga kufanya huduma *_Kawaida au Huduma ya Tofauti yenye Impacts katika maisha ya watu na ufalme wa Kristo_*? Wewe ambaye ndani yako kuna mzigo wa kufanya huduma, *Tulia Magotimi pa Bwana* uamze huduma yenye Mguso wa Kimungu.
👉Tatizo kubwa la Injili *Feki,na mafundisho feki,uimbaji feki* tulio nao sasa ni watu Kukurupuka na kuingia kwenye huduma bila kutulia magotini mwa Bwana,wanajikuta wamepwaya katika tasnia hiyo,uwezo wa kuonyesha matokeo ya Kimungu hawana,ushindani ni mwingi kwenye mazingira, *_Ndo chanzo cha kutafuta njia mbadala za upako wa kishetani na kufanya ujanja ujanja tu wa kihuni_* tofauti na Misingi ya Neno la Mungu na Maadili ya wokovu.
👉Inawezekana kabisa kutembea na huduma yenye upako,kibali na mguso wa Kimungu bila ujanja wowote,uhuni wowote,wala nguvu mbadala yoyote ya kipepo, lakini lazima upate Maarifa ya Msingi ya kukuongoza katika kuifikia huduma yenye Ukweli na Usafi,maana zama hizi,unaingia kwenye huduma kama mwana kondoo katikati ya mbwa mwitu.
*_"Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua."_*
(Mathayo 10:16 )
...............................................................
👉 Mtumishi wa Mungu unayeingia kwenye huduma shika sana sentensi hiyo ya Yesu, *_"Nawatuma kama kondoo,kati ya mbwa mwitu"_* unayeanza huduma shika sentensi hii ili uwe salama katika huduma yako.
👉 Kuna mbwa mwitu kwenye huduma, *_Mbwa mwitu zinazotunia viambata na kuvitukuza(mafuta,chumvi,maji,sabuni,nk) kila maombezi bila jina la Yesu,mbwa mwitu wanaotunga nyimbo Zisizo mtaja Yesu mwanzo hadi mwisho(jiulize wana mtukuza nani,au biashara?),mbwa mwitu wanaoendesha deliverance kwa ngono,romance nk,mbwa mwitu wanao pachika maneno ya Kimungu kwenye biti ya msanii wa bongo fleva,mbwa mwitu wanao fanya futuring kuimba gospel(nyimbo za kumsifu na kumwabudu Mungu akiwa na mwana muziki wa bongo fleva,mbwa mwitu,anaye toa unabii feki,mbwa mwitu aneye jitukuza yeye katika kufanya miujiza bila kumtukuza Mungu,mbwa mwitu wanaofundisha mafundisho potofu ya kutukuza mtu,dini na kuudharau wokovu_* hao ndiyo unaoenda kufanya nao kazi. Swali: *Wewe umejipangaje*? Utafuata mkumbo wa hao mbwa mwitu au uanjipanga kumdhihirisha Yesu Kristo kama alivyo.
👉Huduma ya Yesu Kristo inaenda kwa kanuni,hatua kwa hatua,ila huduma feki zinaota kama uyoga,zina michanganyo nyingi na ushawishi mwingi usiotokana na Mungu.
👉 Huduma sahihi ya kweli ya Yesu Kristo,ndani yake haina ushawishi,imebeba nguvu(pumzi ya Mungu)ya kuponya,kubariki na kuinua,lakini injili (huduma)zilizovamiwa zina ushawishi mwingi ndani yake zinapofanyika wa kuvuna pesa,heshima na uovu(zinaa). *swali,ni je wewe unajipanga kuwa na huduma gani?*
_"Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,"_
(1 Wakorintho 2: 4)
................................................
👉Kumbuka Huduma ya Kimungu iliyo ya kweli, *Aihitaji nguvu sana za kimwili na kujipambania ili ujulikane,uwe na heshima au nguvu,inakuhitaji kutulia,kujifunza,kufufuata kanuni za kiroho utapanda,utaheshimika na utabarikiwa na Mungu mwenyewe* hii ndo huduma ya kweli unayoiendea kama wewe si mbwa mwitu.
*_"Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu."_*
(Yohane 12: 26)
_Basi kufikia hapo ni hitimishe sehemu ya pili ya Somo hili la Utumishi wa Kweli katika Kristo Yesu, Usikose sehemu ya 3 ya Namna ya Kukabiliana na Nguvu ya Wito katika hudum yako uanyoiendea_.
*By Ev Elisha Kazimoto(WhatsApp 0755444078)*
Wednesday, 16 May 2018
SEMINA-SEHEMU YA 2
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment