🛣 *SEMINA YA NENO LA MUNGU KUHUSU UTUMISHI WA MADHABAHUNI PA BWANA*🛣
_By Ev Elisha Kazimoto_
Whatsapp 0755444078
......................................
*UTANGULIZI*
_UJUE UTUMISHI WA MADHABAHU YA BWANA ALIYE HAI_
...
...
_Shalom watu wa Mungu alie hai,nikuombe sasa ukae mkao wa kupokea kitu kutoka kwa Bwan wewe uliye katika hema hii ya Bwana,uliye na mzigo na kazi ya Mungu,kuna vitu Mungu atasema nawe,na utajengwa na kuwa mtumishi wa viwango vinavyo takikana mbele za Mungu na Mbele za watu( *Mithali 3:4-5*).Fuatilia mfululizo wa masomo haya soku kwa siku ujipange kumtumikia Mungu aliye hai. Somo langu kuu ni :UTUMISHI WA KWELI KATIKA KRISTO YESU,hilo ndo somo tutalichambua kwa kina,ila kwa sasa mwanzo wa semina hii kuna vitu nataka nikuwekee kama msingi,hasa wewe ambaye *Bado unachipuki katika utumishi na unatamani kwenda mbali* kuna misingi Roho mtakatifu anahitaji akuwekee_.
✍Kwanza utumishi huu unaouendea, na ulio nao siyo *_Deal la mwanadamu,eneo la kutokea kimaisha,au kujiegesha baada ya kustaafu,au kupotezeapo muda baada ya kukosa ajira au la kufanya,siyo eneo la kujichomeka,ni eneo Takatifu,Ni Kipawa unapewa na Mungu aliye juu kwaajili ya Kuujenga mwili wa Kristo,na siyo kujenga maisha yako_* (Waefeso 4:11-12). Yaani Mungu anapokupa Hudum,Kipawa(Karama yoyote)analenga isaidie kuujenga mwili wake yaani Kanisa ili kukamilisha Kusudi la Ukombozi wa mwanadamu pale msalabani.
*_"Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa." (Methali 17: 8)_*
✍Mungu anapoweka mzigo wowote ndani yako,anakuwa ameuwekea vipimo vya kutosha kukuhakikishia kila eneo,kona,mahali utakapo Simama kuhudumia watu wa Mungu kwa huduma yoyote ile watu wanabarikiwa,Matokeo yanaonekana ya Kipawa chako(Gift)alichokupa Mungu) *_Kazi yako ni kutambua kipawa ukichopewa na Mungu na kukikuza kwa kanuni za Kimungu,utaona kinavyo fanya kazi kwa viwango vikubwa popote pale_* kipawa cha Mungu kina cover dunia yote( _Kila kigeukapo ufanikiwa_).
✍Changamoto kubwa ya huduma nyingi hasa katika zama hizi,ni *_Huduma za kujipa,kujipachika,kutafuta sifa,kupata eneo la kutokea kimaisha,mahali pa kujipatia mahitaji ya tamaa zako,mahali pa kushindana na mwenzako,ni za kuangalizia(kuiga ili mrafi upate watu wa kukuunga mko)_* tumeacha Huduma za KUITWA NA MUNGU,kusikia Mzigo mkubwa wa kufanya kazi ya Mungu na unapozembea au kutoifanya unakosa AMANI kabisa na unataabika moyoni. Huma hizo zimekuwa Adimu.
✍Changamoto nyinginw tumekuwa na wimbi la Wahuni tu wa kidunia wapagani ambao hana neno la Mungu lolote ndani,wamekimbilia kanisani siyo kuokoka na kumtumikia Mungu,ila kupiga madili na kujinufaisha wao na familia zao, ndiyo maana tuna watu wanao *Tumika chini ya nguvu za giza,ushirikina,madawa,kafara na waabudu shetani huku wakitumia kivuli cha Wokovu* ndani yao hawana mzigo na kondoo wa Bwana na utukufu wa Mungu,wao wana mzigo na kupata mahitaji yao waliyoyakusudia na heshima yao.
✍ Sasa ndugu mtumishi wa Mungu unaye jiandaa kuingia katika utumishi huu wa Kristo ni vizuri ukajipima kuwa *Shahuku yako,Mzigo wako upo wapi:*
1.Kupata fedha
2.Heshima
3.Kushindana
4.Uonekane na watu
5.Na wewe upo na kazi ya kukuweka busy
6. _Kuujenga mwili wa Kristo na kumzalia Yesu Matunda,na kuiandaa taji yako ya uzima._
Tafakari na uendelee kufuatana nami katika semina hii upate kitu cha kukusaidia kutimiza shahuku yako.
✍ Huduma ni kama mbegu,inapandwa,inaota,inakuwa mpaka kutoa matunda mengi,huwenda huduma yako ilo kama mbegu moyoni mwako,mwingine imeanza kuota,mwingine imeisha weka majani na matawi,mwingine maua yamechanua,mwingine matunda yaeweka hayajaiva,mwingine tayari watu wanachuma kwa kasi matunda, hivo usiwe na haraka au wivu,au kutafuta njia za mkato za kuivisha matunda wakaati bado ndo mche unaota majani,tulia fuata kanuni za kiutumishi, *Uivishe kwa wakati* hapo ndo utafurahia utumishi wako wenye faida.
........................................................
*_Hii ni sehemu ya kwanza ya semina,katika somo letu la utumishi wa wa Kweli katika Kristo,usiache kufatilia somo hili mpaka mwisho. Ni mimi Ev Elisha Kazimoto_*
Whatsapp 0755444078
Tuesday, 15 May 2018
SEMINA-SHEHEMU YA 1.UTANGULIZI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment