Thursday, 24 May 2018

SEMINA SEHEMU YA 6

🛣 *SEMINA YA NENO LA MUNGU KUHUSU UTUMISHI WA MADHABAHUNI PA BWANA*🛣
  _By Ev Elisha Kazimoto(Whatsapp  0755444078)_
......................................
   *_Utumishi wa Kweli katika Yesu Kristo_*
      *SEHEMU YA 6*
*_Hatua 7 za Mtumishi wa Kweli wa Yesu Kristo_*
....
....
_Shalom kuhani wa Bwana na mtumishi wa Yesu Kristo,uliye madhabahuni na uliye na wito mkuu wa kuingia katika madhabahu ya Bwana kutumika,leo tuiangalie sehemu ya 6,katika hatua muhimu ambazo lazima uzipitie unapoelekea kutimiza ndoto zako,maono yako ya kutumika_
🍇5⃣ *Kuwa na shahuku ya kukutana na Yesu Kristo katika Huduma yako*, Mtumishi yeyote unayemuona yuko juu,na anendelea kupanda juu kihuduma,jua yakuwa ndani yake Alitengeneza *Shahuku kuu* ya namna huduma yake anatamani iwe,anatamani Yesu Kristo ajidhihirishe kwenye huduma kwa namna ya pekee,anatamani Mungu atukuzwe mno kupitia huduma yake, tofauti na watumishi waliopitia uchochoroni na kuibuka na nguvu kubwa za giza hao,shahuku yao ni *_Ajulikane,awe na heshima kuu,amiliki pesa na vitu vingi,aabudiwe nk_* hao ndo ambao hii hatua hawakuipitia walilipuka na uovu.
🍇Siri kuu ya huduma yoyote kuwa na nguvu na kibali kikubwa,ni *Shahuku ya ndani yako ikoje*,kiwango cha shahuku yako juu ya huduma yako,ndicho kiwango cha Harakati zako za kumtafuta Mungu na ndicho kiwango cha huduma yako itakavyo fanya kazi katikati ya watu.
*_"Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe."_*
(Methali 23:7 )Yohana 7:34-38,
🍇Hii ni dhahiri kuwa huduma yako haitakuwa kubwa kuliko nguvu iliyoko ndani yako. Watu wengi wanatamani huduma kubwa,yenye nguvu,ila shahuku yao ni ndogo ya kutamani Yesu atembee na wewe kwa viwango vikubwa,jitihada na mikakati ya kutembea na Mungu hana,ila anataka huduma kubwa.
NB: *_Tutaiona shahuku uliyo nayo ndani yako kwa kutazama,harakati unazofanya katika huduma yako kuifanya huduma yako itembee na uwepo wa Mungu_* lakini vitu unavyo fanya ili kujijingea uwezo na nguvu ya kutumika.
*_"Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu;"_*
(Waefeso 3:20 )
🍇 Bidii yako ndo kwa Mungu,ndo kiwango cha Mungu kujidhihirisha kwenye huduma yako.
(Methali 8 )
------------
17 *_Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona._*
18Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
*1Samweli 2:30, 1Mambo ya Nyakati 15:2, Zaburi 18:20*
🍇 6⃣ *Kuwa na Unyenyekevu*, Hii ni hatua muhinu sana mtumishi yeyote anayetaka kutumika chini ya uongozi wa Roho mtakatifu na na kuwa na huduma kubwa na yenye kibali. *_Kuinuliwa kwako kunategemea na kiwango chako cha Unyenyekevu mbele za Mungu na mbele za watu_*
🍇Watumishi wengi wanaoingia katika huduma na walio katika huduma hatua hii imewashinda,ndiyo maana wengi huduma zao zimekufa,wengine wamebaki wakawaida mno shida ni kutokuwa na unyenyekevu.
🍇Wewe unayetamani kumtumikia Mungu kwa viwango, *_Jiombee sana,na jitahidi kuwa mnyenyekevu_* hapo mdipo utaona huduma yako inaanza kushika kasi,ikipanda.
(1 Petro 5 )
------------
6 *_Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;_*
7huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
🍇Mungu anatukuza kwa wakati wake,wengi akiwa na *Kibali kidogo tu, Mwimbaji CD yake ikapigwa sana tu ikapendwa(single),muhubiri wagonjwa 10 wakapona,basi* kila mtu anamuona hana upakao,anaanza kuunda majina ya kuitwa na watu( *Senior,Mashuhuli,Wa kimataifa,......Mkuu nk*) ndugu yangu usipende kujitambulisha sanaa kwa maneno mengii,wacha Bwana akutambulishe kwa Kazi yake atakapoiwekea mkono.( *Mathayo 23:12,Waefeso 5:21*)
🍇7⃣ *Kuwa na Imani Timilifu* Hii ni hatua ya mwisho,katika yale,au katika zile hatua alizonipa Bwana kuhusu huduma. Huduma ya Kiroho inaendeshwa kwa Imani,kuamini juu ya Nguvu na uweza wa Mungu ( *_Yaani leo uoni kitu,ila unanena kitu kikubwa_*) watu wote waliokwisha kuwa na huduma kubwa ukiwauliza watakwambia jinsi walivyo mwamini Mungu katika uwezo wa kuwafikisha pale walipo.
🍇Imani haitoki hewani inatoka katika *kusikia*,unapoanza huduma yoyote kuwa makini na watu unaowasikiliza, *_Si kila mtu wa kumsikiliza,si kila mtumishi wa kumsikiliza_* wemgine ni watumishi mawakala wa adui ukiwasikiliza wanakuvunja moyo kabisa na huduma unaacha. Chagua watu wakusikiliza,wanaoamini katika *Positive*, hapa ni muhimu kuangalia watu wanaoendana na maono yako,na hapa si kila mtu *Umwambie maono yako* wengine wanaweza kukukatisha tamaa mpaka ukaona kana kwamba unacheza kuwaza hivyo unavyoiwazia huduma yako.
🍇Jikite kusikiliza Neno la Kristo na watumishi Hodari katika huduma wasio dhaifu wa imani.
*_"Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo."_*
(Waroma 10:17 )
🍇Uwezo wa kuifanya huduma yako iwe ya pekee ni kuamini katika kile unachokiona ndani yako,ambacho kwa akili ya kibinadamu si rahisi kukitarajia,hao ndiyo watumishi Mugu anapenda kufanya nao kazi na kuwajibu
(Waroma 4 )
------------
18Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
19 *Yeye asiyekuwa dhaifu wa imani*, alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa, (akiwa amekwisha kupata umri wa kama miaka mia), na hali ya kufa ya tumbo lake Sara.
🍇Mtu mwenye imani katika utumishi wake,utaona ni mtu aliye na imani(anamwamini)Mungu wake sana na hana mashaka naye kwa yale anayomwomba.
*_"Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao."_*
(Waebrania 11:6 )
Soma *Waebrania 10:35,Marko 9:17-22,* ondoa mashaka ndani yao kwa kuangalia mazingira magumu ya utunishi wako,angalia kusudi la wito wa Bwana ndiye awezaye kujenga sura mpya ya ushindi na utukufu.
🍇Unapojipanga katika kuingia kwenye utumishi huu wa Yesu Kristo,jiulize,hivi nimefikia viwango vya kumwangalia Mungu kama Mungu au bado na mwangalia Mungu kama Mungu mtu?
*_"Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa."_*
(2 Wakorintho 13: 5)
_Kufikia hapo niishie hapa katika sehemu ya 6 na katika hatua 7, sehemu inayofuta tutaangalia sifa 7 alizo nazo Mtumishi aliyekatika utumishi wa Kweli wa Yesu Kristo,ili uwe na maombi ya kujiombea umiliki sifa hizo ufae katika *Utumishi wa Madhabahuni pa Bwana aliye hai*_
By Ev Elisha Kazimoto(Whatsapp  0755444078)

No comments:

Post a Comment