Friday, 26 May 2017

KIPIGO KILEKILE

*_NAKUPIGA KWA KIPIGO KILEKILE ULICHO NIKUSUDIA_*
     *_Ev Elisha Kazimoto(0755444078)_*
( *Katika Mkesha wa Shusha Kipigo Kilekile Ulichokusudiwa na Maadui zako*)
Shalom Mwana Maombi _Kila mtu katika maisha ana mimba ya mafanikio, kuna mimba ya uchumi wako mkuu,kuna mimba ya ndoa ya kicheko,kuna mimba ya Elimu,mimba ya Ajira, mimba ya huduma na utumishi nyumbani mwa Bwana, hizo zote zimebebwa kwa uchungu,zinalelewa kwa uchungu,mpaka kuzaliwa ni kazi imetumika_
*KUTOKA 21:22-25*
22 Watu waume wakiteta pamoja, wakamwumiza mwanamke mwenye mimba hata akaharibu mimba, tena yasiwe madhara zaidi; sharti atatozwa mali kama atakavyomwandikia mumewe huyo mwanamke; atalipa kama hao waamuzi watakavyosema. 

23 Lakini kwamba pana madhara zaidi, ndipo utatoza uhai kwa uhai, 

24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu, 

25 kuteketeza kwa kuteketeza, jeraha kwa jeraha, chubuko kwa ajili ya chubuko. 
_Lakini wapo wanaume(maadui, wachawi,wanadamu wenye hila) uteta kwa pamoja, ufanya vikao vya siri ili kupambana na mwanamke mwenye mimba(mtu mwenye maono) na kuharibu._
🏹Sikiliza ewe mwanamke(mtu uliye beba ndoto za maisha yako) hao hawalengi kukuumiza tu ila na kuharibu mimba yako.
🏹Sasa ni vizuri kujua lengo la adui umshugulikie mapema kabla ya kuharibu kwa *Kipigo kilekile* alicho lenga juu yako.
🏹Kama mwana harakati wa kiroho,mwombaji katika mkesha wa leo, *_Tunawapiga maadui zetu katika ulimwengu wa roho kwa kipigo kilekile walicho kusudia juu yetu, Bwana awapige kwa Mauti ile ile walioikusudia juu yako iwe juu yao, Wapigwe kwa migogoro ya ndoa,ya kazini,umaskini ule ule walio ulenga juu yako_*
🏹Hatuwaachii, tafakari ni mamvo gani yanakusonga katika safari yako ya maisha,?(wanaume wameteta kuharibu minba yako)washushie kipigo kile kile,wapige kwa Ajali hiyo hiyo walokuandalia,kwa Aibu hiyo hiyo walioikusudia,magonjwa yale yale wanayo kurushia. ( *_Huu ni Usiku wa Kuvua Vazi bovu nakuwavika walio kuvalisha_*) Nikuwarudishia hayo hayooo!
*_Yeremia 30 : 16 - Basi, watu wote wakulao wataliwa; na adui zako wote watakwenda kufungwa; kila mmoja wao; na hao waliokuteka nyara watatekwa; na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo._*
Kataa kuliwa,kabla hawajala mimba yako Amuru watafunwe wao,Kabla hawajateka mambo yako Amuru watekwe wao kwa jina la Yesu.
*_Inuka,usiogope mimba yako itazaliwa ila kwenye maombi yako omba mimba yako isiharibiwe mpaka izaliwe,na mwambie Bwana Yesu ajuaye mwisho kabla ya mwanzo, mwambie Walio Teta gizani,makabulini,maofisini baharini na kwenye matambiko waharibu mimba yangu huko huko, Wageuziwe kwa kipigo kile kile walicho kilenga juu yangu kiwe juu yao wakati mimi na pita salama._*
🏹Nisikilize mtu wa Mungu, wabaya wako wataangukia mtegoni walioutega wenyewe,wakati wewe Unapita Salama waliko kutegea.
*ZABURI 141:9-10*
9 Unilinde na mtego walionitegea, Na matanzi yao watendao maovu. 

10 Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Pindi mimi ninapopita salama.
       *Ev Elisha Kazimoto*
       0755444078

No comments:

Post a Comment