*KUISHI KWANGU NI HASARA KWA ADUI*
*_Ev Elisha Kazimoto_*
*0755444078*
_Shalom leo usiku wa maombi ya mkesha,nikuletee message fupi ya kusimamia katika vita yako ya kiroho na kimwili_
👉Mara nyingi tunawindwa,hatujui au tunajua ila ujue unawindwa na wachawi,watu wenye wivu na maisha yako,lakini sikiliza neno moja kabla ya mambo yote( Kuokoka ni kupakwa mafuta ya ushindi,mafuta hayo huwezi kuyafuta juu ya mtu kabla hajatimiza kusudi la kupakwa mafuta yale)
1 Samweli 20 : 31 - Maana wakati mwana wa Yese akiwa hai juu ya nchi, wewe hutafanikiwa, wala ufalme wako. Basi, sasa peleka, ukamlete kwangu, maana hakika yake atakufa huyu.
*_Kumbe kuendelea kuishi kwangu kama mpakwa mafuta,kunawafanya maadui kutofanikisha madili yao. Nasema Sitakufaaa kwa jina la Yesu madili ya maadui yaendelee kukwama_*
👉Ni sikilize,kinaposemwa kifo na kutofanikiwa panua akili yako na ufahamu wako wa kiroho( maadui wanajua kuendelea kwako kusimama kiroho,kuwa moto kiroho hawatafanikisha kukunasa wewe na familia yako, mpaka kwanza waue kiroho chako) *Sema hafi mtu*
👉Wachawi wanajua,kanisa likiendelea kuwa na maombi,umoja,mikesha ya nguvu,naombi ya kufunga hawataweza kuliua,kulivuruga,kuteka watu,kwa hiyo wanahitaji waue kwanza hizo program zinazoleta mchemko wa kiroho ndo waweze fanikisha biashara yao( *Sema Halipozwi kanisa hili*)
👉Wanadamu,maadui wanajua kama ndoa yako itaendelea kuwa ya furaha na amani,hawatafanikisha kuvuruga uzao wenu na uchumi wenu na maendeleo yenu, kwa hiyo mpaka wawagonganishe vichwa kwanza( *Sema hatugongani katika ndoa hii*)
_Hivi sentensi ambayo iko pale kwenye msitari umeielewa,Sauli(adui wa Daudi) anamwambia Yonathani, "Mwana wa Yese awapo hai katika nchi wewe hautafanikiwa,mlete kwanza auwawe" umeitafakari?_ Adui hawezi kufanikiwa mbele ya mwenye haki,aliyepakwa mafuta ya ushindi,mpaka kwanza akuue,akuondoe mbele yake. *_Sasa hasara kwa maadui,bahati mbaya,mafuta ya wokovu na utumishi tukiyo pakwa hayaruhusu mtu kuuwawa kabla ya kukamilisha kusudi alilopewa_*
👉Sasa nizamu ya kuomba,kupangua mauti zote zilizoandaliwa juu yako, *Mauti za ndoa, za uchumi ,za kazi,za afya za kiroho,nazibatilisha kwa jina la Yesu,naita upako wa maguta ya Kristo ya wokovu tuliyo pakwa ya uhishe kila kitu ili maadui wasifanikiwe mikakati yao*
_Isaya 61 : 10 - Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu._
*_Huu ni mwaka @2017 wa Kwenda mbali hazimishwi mtu,hakwamishwi mtu,harudishi nyuma mtu,hafi mtu mpaka tumefika tuendapo kwa utukufu wa Mungu baba_*
Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve)
@Anointedman
*0755444078*
Friday, 12 May 2017
SABABISHA HASARA KWA ADUI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment