Thursday, 18 May 2017

UFUNGUO WA 3

🔑🔑🔑3⃣ *Ufunguo wa tatu: MFANYE MWENZAKO WA PEKEE*
_Karibu tena katika ngazi ya tatu,tunapo tumia 🔑 kufungua chumba cha tatu kati ya 12 vya ndoa ya kicheko na furaha_
✍Ladha ya ndoa kwa mwanandoa yeyote ipo katika Kutofautisha kati ya watu wengine,vitu vingine na Mpenzi wako( Huu ndo ufauru wa kukinda penzi lenye furaha)
✍Nikupe siri moja ambayo wanandoa wengi wanaitupa njiani mara baada ya kuoana na kusogea mbele miaka 2,3,6..... Unajua tendo ulilolifanya (baba kumchagua huyo mkeo) au wewe mama tendo la kusema YES kwa huyo uliye naye sasa *_Ulifanya tendo la kuonyesha Upekee kati yake na wengine wote,ndo maana mkapendana sanaaa sababu ya kuonyeshana utofauti kwa uchaguzi_* Nini sasa kinawafanya watu wawe chini ya migogoro? Inaweza kuwa nguvu ya kumtofautisha mwenzako na wengine,vitu vingine impotea au imepungua.
✍ *Kwa nini nimfanye mwenzangu wa pekee?* Ukilielewa swali hiki vizuri hutokuja kuruhusu vitu vidogo vizime vicheko vya ndoa yenu. *Swali ni Kwa nini*
🔑 Anavyo nifaa,hayupo mwingine wakunifaa vile( kumbuka watu wote wanamipaka mikubwa katika kukuhudumia,kukufurahisha na kukutunza, *Ila mmeo/mkeo hana mipaka* hivyo Una sababu yakumfanya mwenzako aonekane wa pekee.
🔑Sababu nyingine, Niliwaacha wengine,kwaakili yangu timamu na kuona huyu anafaa kuliko wengine, Tendo la kufanya maamuzi ya kuoana na huyo ni kumfanya pekee, basi fanya tendo lingine la kuteleleza mambo ya matendo yabkila siku ya kumuonyesha mwenzako ni wapekee.
✍Je, unahitaji usimchoke mwenzako?  Jitahidi kumfanyia mambo atakayoona kweli ni mimi ni watofauti. *_Ili uonyeshe upekee kwa mwenzako, chunguza vitamanio vyake,anapenda nini, anahitaji nini, vitu gani vina kamata hisia zake, vifanye hivyo utaifanya ndoa yako iwe na burudani_*
✍Mama, ndani onyesha upekee wa mmeo,kwa mapishi,vyakula,kumuhudumia kwa kipaumbele, hayo mambo yanaonyesha upekee kwake,na nguvu ya upendo inaongezeka.
✍Baba, mfanye mkeo aone kati ya wanawake wengi na yeye anapendwa,anafanyiwa vitu vya kipekee, surprise, outing ndogo ndogo,simple gift nk, upendo unakua, ujue si wote wanayafanya,sasa ukiyafanya ndo unamfanya wa pekee.
🔑🔑🔑 NB: _Jambo moja unahitaji kulihifadhi Akilini,Ndoa ni Gharama ukikwepa gharama hata kama mlianza kwa vicheko, mtaendelea kwa kununiana, ingia gharama ya Kumfanya mwenzako wa pekee tofauti na wanawake wengine na Wanaume wengine, Pili ujue, kumuona wakawaida na kumshusha thamani haikusaidii ila inakugharimu,maana hutatafuta mwingine,hatatoka wa mwingine aje kukuzibia pungu lake, pambana mwenyewe kumfanya Ang'are kuliko wote_
   *Mwanasaikoloji Ev Elisha Kazimoto*
       0755444078

No comments:

Post a Comment