Thursday, 18 May 2017

UFUNGUO WA 2

🔑🔑2⃣ *Ufunguo wa Pili: MIMI NDIYE FURAHA YA MWENZANGU(MKE/MME WANGU*)
_Karibu katika mwendelezo wa uchambuzi wa funguo 12 za Ndoa ya Furaha na Amani,na leo ni ufunguo wa pili *Mimi ndiye Furaha yake* Karibu_
✍Katika maisha hakuna jambo zuri kama kumfanya mwenzako(hasa kwetu wana ndoa)Afurahi,ajisikie utulivu wa wewe kuwepo, na wewe kuwa sehemu ya maisha yake.
✍Kosa kubwa la Kisaikolojia kwa wana ndoa,ni kususia hisia za mwenzako, kutojali hisia za mwenzako. Jambo unalopaswa kujua ni Hakuna mtu aliye Katika Agano la ndoa anayeweza kujifurahisha mwenyewe,au kufurahishwa na mtu mwingine, isipo kuwa yule aliyeungwa naye. Ndiyo maana maumivu yakuumizwa na mwenzako katika ndoa ni makali kuliko yale unayoweza kuumizwa na mtu yeyote, na ndiyo maana mtu akiumizwa na watu,kazini,ofisini nk,akija ndani akakuta furaha saikolojia yake ya maumivu inapoa haraka kuliko aloumizwa kwenye ndoa aende nje,hata angepata exposure ngapi maumivu hayakomi, mpaka mwenzake atakapo Amua kumfurahisha.
✍Usidharau Furaha katija maisha ya ndoa, furaha *_Inafungua mioyo ya wana ndoa,inatoa mwanga mpya wa mawazo mapya kwa mtu_* hakuna aliyefanikiwa kifamilia kiroho au kimaendeleo kama hamja fikia hatua kupeana,kutunziana furaha.
✍Miongoni mwa vitu wana ndoa ni vya kujali sana ni kutengeneza mazingira ya mwenzako kufurahi, *_Usitegemee katika maisha yako kufurahi, kama mwenzako hajafurahi_* Furaha ya mwenzako ndo inayo zalisha furaha yako.
✍Nini kinafanya mwenzako awe na furaha? Ni swali muhimu, lakini ni swali lililo wazi na lakisaikolojia, (hakuna aliyeoa auvolewa bila kufurahishwa na mwenzake) mambo yaliyo kufurahisha tangu unampata huyo mpaka ukasema YES,vitu hivyo nivyakulinda. _Ndoa zimeingia katika migogoro hata kuvunjika baada ya wanandoa kuruhusu mmoja kuumia,kuzalisha uchungu,na kudharau hisia za mwenzako hata kupelea uchungu wake kukuambukiza na ndipo Amani upotea._
✍Vitu gani vinamfurahisha mmeo/mkeo( *Caring yako,Lugha yako, huduma yako,kumpenda Mungu kwako, Uaminifu wako etc*)?
Ukihitaji ndoa yenye kudumu katika Amani, na Vicheko, hakikisha unalinda furaha ya mwenzako,buni vitu vinavyo mfanya afurahi , *_Ni nature, Furaha kuzalisha vitu vizuri, umewahi kusoma andiko linalosema Furaha ya Bwana ni Nguvu zetu?_* hiyo ndo nafasi ya furaha. Hakikisha mke/mme wako anafurahi kwa uwepo wako.
✍ Usichanganye, pesa,mali nk (Vitu )siyo chemichemi ya furaha ya mwenzako, ni maisha yako mwenyewe ya kila siku mbele ya mwenzako.
NB: Kumfanya mwenzako afurahi ni kutengeneza network ya maisha yasiyo na stress na kujuta.
     *_Ev Elisha Kazimoto_*
       0755444078

No comments:

Post a Comment