Friday, 19 May 2017

UFUNGUO WA 4

🔑🔑🔑🔑4⃣ *Ufunguo wa Nne: IMENIPASA KUBEBA MADHAIFU YAKE ILI AWE NA FURAHA*
_Karibu kwenye mwendelezo wa kujifunza juu ya funguo 12 za ndoa yenye kicheko, na leo tunaangazia ufunguo wa 4, unajua nini? *Kwa Namna yoyote hatutaachia nafasi Kisaikolojia wala kiroho mpaka Adui aingize Sumu na mpasuko katika ndoa zetu* Fuatana na Msaikolojia Ev Elisha na Mungu akubariki_
♦Nianze kwa Kuzibua ufahamu wako, Wewe uliye binadamu unayeishi duniani Unayo mapungufu,unao udhaifu,pamoja na kuokoka,kutumika unao udhaifu *Kama mwanadamu* sizungumzii udhaifu wa Kutenda dhambi(Nielewe vizuri), Nasema hivi kama mwanadamu unao udhaifu, na Ndiyo maana ukaumbiwa Msaidizi mke/mme.
♦Miongoni mwa mapungufu uliyokuwa nayo, ni pamoja na kutojizalisha, kutoweza kujifariji,kujipa furaha,kutimiza mahitaji yako yote *Kikamilifu* kuna kutimiza mahitaji yako ila si kikamilifu, Ndo maana ukapewa Mwenza ili azibe mapungufu yako.
♦Yako mapungufu mengine unayaona kwa mwenzako,baada ya kuyapunguza umeyakuza kwa kuyatangaza kwa watu, kumsimanga kwayo,kumdharau kwa sababu ya mapungufu hayo na *_Huo huwa ndo mwanzo wa migogoro ya ndoa,mpasuko na kuachana_* kumbe ilibidi umsaidie,umtie moyo,umfanye aone mapungufu yake hayana nguvu katika ndoa yenu, bari faraja ndo imetawala *_Na huo huwa msingi wa ndoa imara na yenye furaha_*
♦Miongoni mwa vitu vinavyo mfanya mtu ajisikie vizuri na kuongeza upendo juu yako ni kuona unabeba udhaifu wake,unamtia moyo katika udhaifu wake,unajitahidi kuyabadirisha madhaifu yake yawe uwezo wa kufanikiwa. *_Ukifanya hivyo utaona mwenzako anakupenda sanaa,na kukuheshimu na kukuthamini_* Hii ndo ladha ya ndoa tunaitafuta katika maisha yetu.
NB: _Nahitimisha kwa Falsafa ya Mungu alosema *Nitakufanyia msaidizi wa kufanana nawe, unaielewa?* Maana ya kufanana si kwamba mtafanana kila kitu,tabia,kama we mchoyo basi unapewa mchoyo mwenzako,kama mdhaifu wa kusoma neno unapewa mdhaifu mwenzako, mfanano aloukusudia Mungu ni mfanano wa Kumkamilisha mwenzako,yaani atakufanyia msaidizi wa kukukamilisha(kujufunika katika upungufu wako) mfano wake ni huu, mfuniko wa soda na chupa ya soda ufanano wake ni mfuniko uzibe chupa siyo vikingane na mdono wa chupa hapo utaegesha tu mfuniko siyo kuifunga chupa iwe imara_ Basi Funika madhaifu ya mwenzako mfurahie ndoa.
   *_Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve)_*
         0755444078

No comments:

Post a Comment