🔑🔑🔑🔑🔑 *Ufunguo wa tano:5⃣(Mke/Mme) ANANIHITAJI MIMI NA SIYO VITU VINGINE*
_Uheri wewe uliye katika site ya kupata Maarifa yatakayo kufanya usiinfiliwe na mdudu alaye ndoa chini kwa chini,kwa kutumia sumu ya ujinga, sasa karbu tuendelee na ufunguo wa 5 kati ya 12 za ndoa ya furaha na kicheko_ by Psychologist Ev Elisha Kazimoto.
🔰Kuna Mistakes huwa inafanywa na wana ndoa kimzaa,kwa kudharau au kutojua, nini *_Mkeo/Mmeo anakuhitaji wewe kuliko vitu vyote, si suala la pesa zipo,hazipo, magari umenunua,matumizi unaachilia, na chakula unapika vizuri, hivyo vyote ni ziada ya ndoa_* Ila msingi mkubwa wa ndoa ni kwamba mwenzio ANAKUHITAJI WEWE, kama pesa zilikuwepo angekuwa anazihitaji angezitafuta na akapiga chini kuoa au kuolewa,ila anakuhitaji wewe, mtoto yupo au hayupo huyo ni waziada kwa utukufu wa Mungu ila yeye alikupenda wewe ndo alikuona kwa sura, *_Usipo kuwa makini kutumia nafasi yako ya kuhitajika, Usipo hitajika tena kwa huyo moyoni mwake,ndipo utakuwa umeizika ndoa yako_* wewe unahitajika sana kwa mwenzako.
🔰Kuhitajika kwako kuna sura pana sana, maneno yako matamu,ya faraja,yakusifia,yakupongeza yanahitajika sana kwa mwenzako, kujua mwenzako anahisi nini,anajisikiaje,anataka nini,nini kinamtatiza,nini ufanye ajisikie furaha huo ndo umuhimu wako kwa mwenzako.
🔰Ndoa nyingine zimepata shida sababu ya kuacha Ombwe(gap/vacuum )katika moyo wa mwenzake, lakini wao wanakuwa busy na mambo mengine,watoto,biashara,ofisi,huduma,simu nk,ilimradi pesa ipo,hauumwi,unakula,unavaa nk, hii siyo sawa. _wewe kama wewe unathamani zaidi ya pesa na magari na watoto_
🔰Je, mwenzako yuko huru kwako muda wowote,unapatikana kisaikolojia na kimwili anapokuhitaji?au upatikanaji wako niwa masharti, niwakuvizia,kubembeleza? Unahitajika kuwa *Available* Usije ukaweka kitu chochote kwenye nafasi yako kikuwakilishe kwa mwenzako pale anapokuhitaji.
*_Kuwa Availbale_* _Ni pamoja na kumfanya mwenzako asihisi upweke kihisia,kimwili na kiroho, bali ahisi kukamilika.
NB: _Maamuzi yako kwa mwenzako yakila siku katika kutimiza majukumu na wajibu wako katika familia na ndoa yanaweza mfanya mwenzako kuona/kujua Humuhitaji ata kama hujamwambia sikuhitaji, au hata kama hamjaachana. Fanya Mambo yatakayo mfanya mwenzako ahisi Wewe Unamwitaji sana, na yeye anakuhitaji sana katika naisha yake_
*Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto*
0755444078
Saturday, 20 May 2017
UFUNGUO WA 5
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment