🔑🔑 *FUNGUO 12 ZA NDOA YENYE KICHEKO*🔑🔑
_Haleluyaa, ni haki yako kuifurahia ndoa na nimapenzi ya Mungu kila umwonapo mwenzako uhisi Mungu alikupendelea na kukuzawadia huyo. Njia nyepesi na muhimu ya kujenga dhana hizi mbili na zikawa katika uhalisia ni Kujifunza,kupata maarifa ili usikosee katika kutunza mwono wako wa kwanza_
*Leo naanza kukupakulia siri ya ufunguo mmoja mmoja npaka zitakapo isha 12*
1⃣ *NILIYE MCHAGUA(HUYU) NI MZURI NA NDIVYO ALIVYO*
🔑Ufunguo wa kwanza unajikita na saikolojia yako, mtazamo wa hisia zako na tafsiri za ndani za hisia zako, kabla ya kuangalia mazingira ya nje na madhaifu. _Kwa kawaida huwa hakuna mtu anachagua mtu mbaya kwake, huyo ulo mchagua ni sahii na ni mzuri, huwezi kumpenda kwa viwango,kabla saikolojia yako haimtazami kuwa ni mzuri(si suala uzuri wa sura tu,yaani ni mtu sahihii anaye tosha kukamilisha furaha yako) kwanza umfikirie na kumuona ni mzuri._
Sasa mapungufu mengine aliyo nayo yanaweza futwa,badirishwa,kwa mtazamo wako wa unamuonaje mwenzako?
Kuna kosa kubwa wana ndoa wanalifanya linaleteleza kupoteza ladha ya penzi lenu. *_Pindi ikitokea mwenzako akakosea kwako, mara moja,2,3 unafuta Uzuri wake kichwani mwako aliokuwa nao kwako hata ukamchagua_* hili ni kosa la kisaikolojia linaloweza kuifanya ndoa yako iyumbe.
Unajua wana ndoa,unapaswa kujua uwe mke au mme, kosa au kutofautiana, hakubadirishi utu na uzuri wa asili ulioona anao huyo mwenzako hata ukaamua kumfanya ni mtu wa pekee wa maisha yako. Hasa tuliookoka, unajua ndoa *Selection of a Single Best Pertner to Move with* si jambo linaloweza futwa na simple mistakes ndo maana Bible inasema alichounganisha Mungu mwanadamu hatenganishi mpaka kifo. _Jenga saikolojia ya makosa,itirafu ni sehemu ya kudhihirisha uhalisia wa binadamu yeyote,ila Uzuri wake ulio ndani yake ni bora zaidi ya makosa haya,sasa niweke mazingira ya kumsaidia kufuta makosa na kulinda uzuri wake kwangu_
NB: ya ufunguo wetu wa 1🔑leo, *_Usikubali Makosa ya kimazingira yafunike uzuri wako au wake kwa mwenza wako, pambana kuuona uzuri wake ndani yake na umsaidie auishi uzuri uliokufanya useme YES KWAKE_*
MWANASAIKOLOJI EV ELISHA KAZIMOTO.
*0755444078*
_PARADISE UNIVERSITY(MARRIAGE CORNER )_
Tuesday, 16 May 2017
FUNGUO WA 1 KATI YA 12
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment