Monday, 22 May 2017

UFUNGUO WA 7

🔑🔑🔑🔑🔑🔑🔑 *Ufunguo wa 7: MWENZANGU ANAHITAJI KUWA SALAMA(KULINDWA)*
_Salaam wana ndoa,kwa mara nyingine tunasogea katika meza ya Maarifa tupate ufunguo wa saba wa kufungulia chumba cha Amani na furaha cha ndoa zetu,na sasa tuangalie Nguvu ya kumlinda mwenzako inachochea vipi utulivu wa ndoa_ *Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto* katika uchambuzi wetu, karibu.
☔ Kuna vitu ukivitazama katika mwili wa mwanadamu waweza kuviona ni vidogo na havina maana saana kuvijali, kumbe ondoa uone balaa lake. ( _Umewahi kufikilia kope za macho yako ziki nyofolewa nini kitakutokea?ndani ya dk 1 unaweza usifumbue macho tena., au ulisha wahi kujiuliza kwa nini kope za macho yako zina cheza kila sekunde kama mshale wa saa? Zikitulia utakuwa kipofu kwa uchafu utakao vamia macho yako_) sasa kope za macho zina jua kitu kimoja *Jicho Lazima Lilindwe* muda wote ndo shuguli zingine ziende.
☔Mwana ndoa, mkeo/mmeo ni kama mboni ya jicho lako na wewe ni kope zake,unahitaji kuwa *Active Kumlinda* kumlinda kisaikolojia,kimwili na kiroho ndipo ndoa yenu itulie iwe ya furaha.
☔Kuna vitu mwana ndoa unahitaji kujua, moja kuna watu wakorofi, wapendao kujishugulisha na mambo ya wengine hata kujeruhi mioyo ya watu,iwe kazini au kanisani, hakikisha mwenzako anajua anaye mlinzi mtetezi katika maisha(Jenga mazingira ya kumwondolea mazingira ya Personal attacks za watu aidha kwa kupeana mbinu za kuishi,kufanya kazi,kuongea,ku interact na watu ili kupunguza mazingira ya mwenzako kujeruhiwa. *_Note. Mwenzako akijeruhiwa na watu nje,we ndo utaganga vidonda ndani  na wakati huo kuna vitu ndani vitavurugika_* Pili, Familia yako na ya mwenzako ziwekee mipaka ya kumnyoshea mkono,mdomo na macho mwenzako kufikia kumjeruhi(Wazazi, mawifi,mashemeji,ndugu zako)wajue mkeo/mmeo hawana *Mamlaka* yakumgeuza watakavyo, jua wewe *Ndo uliye na mkataba na mwenzako* hawa wengine ni wapita njia( Ukiruhusu mwenzako ashambuliwe, jua wao hawatakuwepo mchana wala usiku moto utakapo kuwa unawaka ndani mnaungua wawili.)
☔Tatu, Hakikisha katika maombi yako unamwombea mwenzako kila siku alindwe na maroho yavamiayo watu na kubadiri tabia zao. *_Si wote wenye migogoro ya ndoa zile tabia korifi ni nature yao, hapana walishambuliwa_* Ndo maana wenzao wanawashangaa na kuona hapana huyu mtu hafai kuishi naye wakati mwanzoni walioona wanafaa.
☔Kazi ya wachawi na mapepo ni kukupa tabia korofi itakayo mkera mwenzako mpaka muishi kinyume na matarajio na lengo lao la kuzalisha kizazi kibovu chenye malezi mabaya.
☔Uombapo mkinge mwenzako na maroho mabaya,kemea tabia mbaya zinazo kera, mauti, ulemavu,magonjwa sugu,mateso nk ili ndoa yenu ikae na furaha.
Nne, Mlinde mwenzako kisaikolojia hasa katika *_Utumiaji wa lugha nzuri katika mawasiliano,kumuhudumia huduma anazo stahili kama mme/mke asianze kuwaza huyu mtu vipi? Hakikisha tendo la ndoa kwako si mpaka ulazimishwe au ubembelezweee nk_* (huu ufunguo unajitegemea wa tendo la ndoa) tutauchambua peke yake.
NB: _Ndoa ni furaha ya wiwili,inayowafanya na wengine wavutiwe na ndoa na kumbariki Mungu,ila ndo ikiwa mbaya nijanga liumizalo kama mfiwa,na uzima furaha yakila kitu, kula vizuri,vaa vizuri lakini kisaikolojia unakuwa na maumivu makali zaidi ya utungu wa mwanamke mwenye mimba. Hayo yote tunayaepusha kwa Kulinda kona 4 hizo tulizoona, kumbuka maumivu ni yenu wawili ndani wengine wasababishaji life is going as usual. Usikubali kitu chochote,mtu yeyote awe kero,msumbufu kwa mkeo/mmeo_
    *Psychologist Ev Elisha Kazimoto*
          0755444078

No comments:

Post a Comment