Monday, 22 May 2017

UFUNGUO WA 6

🔑🔑🔑🔑🔑🔑  *Ufunguo wa 6: NIKIYATAMBUA MAZURI YAKE(MKE/MME WANGU),NIKAYASIFIA NITAMFANYA AYATENDE ZAIDI*
_Kwa mara nyingine tunapanda ngazi ya Maarifa ili tufikie kilele cha Furaha,Amani na Upendo ulokusudiwa kuonekana katika ndoa za watu, leo tunaungalia ufunguo wa 6, *"the Issue of Acknowledging"* Tabia ya Kutambua jambo alilotenda mtu_ Karibu uoo nami mchambuzi  wako Psychologist Ev Elisha Kazimoto.
🏹Nianze kukupeleka katika Nature ya Binadamu na Saikolojia ya Binadamu ndo ujue wakati mwingine waweza fungua mlango kwa adui bila kujua au kwasababu ya maarifa kidogo na kupelekea msiba katika ndoa,leo upate maarifa usione gharama kuanza upya.
🏹Umewahi alikwa eneo kwenye sherehe au tukio flani muhimu, halafu wakasimamisha watu,au kuwatambulisha watu,wewe ukasahaulika unavyo jisikia? Umewahi ona umefanya kitu,kwenye jamii wanapo tambua michango ya watu halafu na wewe unechangia lakini waka mute,wasikutambue kwa mchango wako unavyo jisikia ?kuna namna ya kuumia na maswali ya kwa nini waniruke, wanipotezee, hawajaona kama nimefanya cha maana nk, *_Nature ya binadamu anatamani akifanya jambo atambuliwe,apongezwe, aambiwe Yes 👍 utaona kasi,furaha atakayo kuwa nayo_* Tabia hii tumeichota kwa Mungu, anahitaji asifiwe akutendeapo jambo.(Atambuliwe ndo maana huwa tunaoa ushuhuda, na bible inasema kila aliye na mwana anao ushuhuda.
🏹Kuna vitu vidigo sana ambavyo vinadharauliwa lakini kisaikolojia huwa ndo nguzo kubwa ya kichocheo cha hisia.
🏹Kama unapenda kuona mwenzako jinsi ambavyo hakuumbiwa kununa,au kuzira zira, na alivyo na sura nzuri,tabasamu zuri,lugha nzuri, nk, *_Anza kutambua matendo yake anayoyatenda_Mfano jizoeze kumwambia mwenzako, jambo hili umefanya vizuri, amevaa vizuri msifie mwambie umependeza sana, amepika chakula mwambie umepikia vizuri,kitamu, haba anefanya kitu katika familia kidogo au kikubwa mwambie umefanya vizuri sanaa.
🏹Neno Asantee,umefanya vizuri,umependeza, nashukuru, umejitahidi nk huonyesha jinsi mwenzako alivyo wathamani kwako, unavyo mkubali,alivyo wa pekee, na mpa mtu mzigo wa kuendelea kujitahidi kufanya bora zaidi kila siku. _Makosa mengine tuyaonayo yanafanywa na wenza wetu mpaka tunakereheka mpaka tuna hitirafiana, yaweza kuwa ni Matokeo *Yakuona makosa ya wenzetu na kuyazungumza mara kwa mara,kumlaumu kwa hayao, kisaikolojia umeendelea kumpa nguvu ya kukosea* kama vile ukiongea mazuri mara kwa mara kwa mwenza wako unampa nguvu ya kutenda hayo_ sasa ni wewe kuchagua kusifia moja,2,3....zuri alitendalo mwenza wako ili umpe nguvu ya kuyatenda hayo mengi? Au ulaumu madhaifu yake kila siku umpe nguvu ya kutenda hayo!
🏹 NB:  _Kuna vitu vina leta raha na kujisikia safe pale mwenzako anapokwambia nakupenda, polee kwa kazi, umefanya vizuri mpenzi wangu,umependeza, hivi kwani utata na kigugumizi kiko wapi?kama usipo mwambia mkeo au mmeo utamwambia nani? Mpaka unaingia kaburini hayupo mtu wa Karibu anayeweza chukua nafasi ya mwenza wako,auburudishe moyo wako wakati mwenza wako yupo hai,ukibana raha hiyo kuitengeneza pata pesa,utajiri but kisaikolojia utakuwa umevurugika na ndo hasara kubwa duniani utakuwa umepata._
    *Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve)*
        0755444078

No comments:

Post a Comment