*NGUZO ZA MAHUSIANO IMARA NA NDOA*
_Kuna mambo ya kuwa nayo makini unapo anzisha mahusiano,kisaikolojia ili yadumu,msichokane kuwa makini kufanya haya yafuatayo na usipo yafanya hata kama ulimuona mwenzako mzuri uramchoka_
1. *Hakikisha mnawasiliana mara kwa mara* _Mawasiliano yanavuta Attention ya mtu kukaa kwenye akili yako,na kitu kilicho kwenye akili mara kwa mara si kwa ubaya upendwa_
2. *Hakikisha mkihitirafiana,usifanye maamuzi magumu ya kumuumiza mwenzio,kumuadhibu,kumkomoa,kumsusia,au kukaa kimya kwa muda mrefu bila kutatua hitirafu ile* _Mkihitirafiana,jua ni ubinadamu,mrekebishe kama ni uchumba,au ndoa,kwa uchumba kama harekebishiki achana naye,kwenye ndoa,Ingia garama ya maombi,na kuendelea kumfundisha na kumwelekeza._
3. *Epuka kumlaumu mwenzako mara kwa mara kwa kila kosa* Lawama zina vunja moyo na kushusha nguvu ya hisia za upe do.
4. *Epuka kumwesabia makosa mwenzako* _kwamba hapa yamefika 2,3,6,.......samehe,likijirudia usirikumbushie kuwa umewahi kufanya,kukumbushia huonyesha na wewe huna roho ya msamaha,kwa hiyo na wewe ni mpuuzi_
5. *Kauli nzuri katika kuongea na kuwasiliana* _Usiwe na majibu ya mkato,kuongea ovyo mpaka unachosha_
6. *Weka tofauti ya Thamani kati ya mkeo/mmeo na watu wengine* _Hakikisha mwenzako anafahamu jinsi unavyo mchukulia wa tofauti na watu wengine katika kila eneo,onyesha kuheshimu na kumthamini,usi mfananishe na wengine. Kila unachoweza fanya kwa wengine yeye mzidishie_
7. *Sifa na zawadi*, _tambua uzuri,au kupendeza kwa mwenzako kila siku ( *Kila siku*) msifi kwa uziri,akivaa,akisuka au kunyoa,akipika nk, vina boost upendo_
8. *Neno Nakupenda lisiwe zito kwako* _Aliye naakili ya kulinda ndoa,na alichagua mwenza wake hakuchaguliwa na mtu hakikisha neno hili mwenzako analisikia kila siku,hutakuja kumchoka au kuchokwa_
9. *Usifanye maamuzi makubwa binafsi* _mfano kununua kiwanja,kujenga nyumba,kununua usafiri nk,mshirikishe mwenzako,inampa moyo wa kuona amethaminiwa_
10. *Kuwa makini na familia yalo na ya mwenzako* _Usiwe na upendeleo wa watu wa kwako,be fare,usiruhusu kilamoja atoe kauli kwa familia yenu,au kumsema ovyo mwenzako,mlinde atakupenda daima_
11. *_Msiache kuombea ndoa yenu au mahusiamo yenu shetani ni Adui wa furaha,amani na Upendo_*
*BY EV ELISHA*
Monday, 9 January 2017
NGUZO ZA MAHUSIANO IMARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment