*Ev Elisha Kazimoto anakuletea Sehemu ya Somo la Uchawi Haujawahi Kushinda Nguvu ya Mungu*
WhatsApp 0755444078
*Uchawi* ni Nguvu za giza, zinazotumiwa na watu walioamua kumtumikia shetani katika sekta hiyo ya uchawi ili *_Kuua, Kudhohofisha,Kuharibu,na kupoteza mwelekeo wa maisha ya watu wasio na hatia na walio na hatia katika ufalme wa giza_*
Fuatana nami:
*Mtu mwenye Akili ndiye Mwenyekushinda Uchawi*
*Zaburi 14:2,Mithali 15:24,Mika 6:9,Mathayo 7:24*
_Nizungumzie mtu mwenye akili ndipo utajua kuwa kushinda na kushindwa kwako na wachawi ni matokeo ya uwezo wa Akili ya Kimungu aliyo nayo mtu. Na baada ya somo hili umuombe Mungu akuongezee Akili ya Kimungu upate kushinda_
👉(Mithali 15:24.... Inaongelea mtu mwenye akili njia ya uhai uenda juu,sikiliza, mchawi hawezi pambana na wewe ukiwa juu,yeye ni mtu wa ufalme wa chini,ili akushinde lazima apige akili yako urudi chini,ndo akabiliane na wewe) ukiwa na uwezo wa kukaa kiroho juu utawashinda maadui wote.
👉Mtu mwenye Akili ni mwenye uwezo mbele ya adui yake, hata adui anajua hakuwezi kirahisi.
👉Mtu mwenye Akili anauwezo wa kupambanua mitego na njia za adui(wachawi) na njia sahihi ya Mungu.
👉Mtu mwenye Akili maamuzi yake,matendo yake ni kwa faida ya ufalme wa Mungu na nafsi yake.
*_Tukiwa na Akili yaani Uwezo ya Kimungu uchawi utamezwa mbele yetu_*( KUTOKA 7:12)
_Hivi umewahi kutafakari pale Haruni alipotupa fimbo chini ikawa nyoka ,na wachawi wa Farao wakatupa fimbo zao chini zikawa nyoka,ila fimbo ya Haruni ikazimeza,ulisha waza Haruni alipo ichukua fimbo yake ilo kuwa nyoka,ikageuka kuwa fimbo Wachawi Walibaki na nini?_ Jibu jepesi; *Fimbo zao zilishamezwa,walibaki mikono mitupu,ila Haruni tu na fimbo yake*
👉Hapo ndo ujue uchawi mbele ya mwenye Akili(uwezo wa Kimungu )unamezwa halafu adui anabaki bila bila,mpaka anakuogopa.
*_Uwezo wa Kutambua,kupambanua unakufanya kuwa mtu hatari kwa Wachawi na adui yako anaye tumia mitego ya siri_*
( *1Samweli 18:20-28, Luka 12:54-57, 19:41-44*)
👉Ukiwa na uwezo wa kutambua mambo wewe si rahisi kutekwa na wachawi na kukuharibia mwelekeo wa maisha yako.
👉Njia anayoitumia adui kukunasa kwa hila,ukiwa mtu mwenye akili na mwepesi wa kutambua,hiyo hiyo njia ndo itatumika kukuletea ushindi na adui yako (mchawi kuaibika).
👉 _Lakini fahamu hili, Maamuzi yako na matendo yako,huwafanya watu,(Maadui na wenye haki)Kutambua kuwa ni Nguvu ipi,ya ufalme upi inatumiliki(1Smweli 18:28, Marko 8:31-33)_
*ANINA ZA WACHAWI NA UCHAWI WAO*
1⃣ Wachawi walogao kwa kutumia madawa *Mambo ya Walawi 19:26*
2⃣ Wachawi walogao kwa maneno(watu watumiao maneno kwa lengo la kuua,kudhohofisha,kuharibu na kupoteza mwelekeo wa maisha ya mtu) *Isaya 32:7-8*
3⃣ Wachawi(watu wenye roho ya kichawi,matendo ya kichawi)wakiwa na dawa au bila dawa. *1Samweli 18:10-11, Yoshua 9:4-17, Zaburi 10:7, 31:13, 36:3, Mithali 12:20*
4⃣ Wachawi walio tafuta uchawi kwa sababu zao za kulipa kisasi,au maangaiko kwa waganga wa kienyeji kutafuta majibu ya matatizo yao. *Kutoka 7:22, 2Mambo ya Nyakati 16:12,Isaya 19:3*
5⃣ Wachawi walio rithishwa na wazazi wao. Kila mzazi humrithisha mwanae vitu vyema au vibaya ili kuendeleza sifa ya mzazi, kwa faida ya mzazi au mtoto mwenyewe. *Kumbukumbu la Torati 21:15-17, Ayubu 13:26*
6⃣ Wachawi wanao tumikishwa na nguvu ya kichawi bila kujua(matokeo ya kutokaa katika nafasi ya kiroho sawa sawa, au kwakuwa rafiki na wachawi) *Isaya 14:3,1Wafalme 12:4,Wagalatia 4:3,Isaya 19:3*
_Hizo zote ni aina za wachawi wanao tumika kuharibu,kuua na kupoteza mweleo wa watu,kanisa,ndoa,kazi na elimu nk,ila ukiwa mtu mwenye akili na awezaye kutambua hao wote watamezwa mbele yako_
*SOMO KAMILI LINA KUJA*
Friday, 11 August 2017
UCHAWI UNAMEZWA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment