Friday, 15 February 2019

OMBA BWANA AKUFICHE

🖥 *MKESHA WA MAOMBI YA KUOMBA KUFICHWA NA BWANA MBALI NA MIPANGO YA SIRI YA MAADUI ZETU*🖥
*_Mnenaji: Ev Elisha Kazimoto(Anointed)_*
WhatsApp 0755444078
.........
.........
_Shalom mwombaji,ni wiki lingine tunaendelea na vita,tunajipanga kwa safu mpya kila wiki Bwana anayo siri ya kutupa kuwaendea maadui zetu na kuwashinda na kuziteka baraka zetu. Leo twende *Mafichoni pa Bwana* huko kuna usalama mkuu.
1 Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.
Zaburi 64:1

2 Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;
Zaburi 64:2

3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,
Zaburi 64:3

4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.
Zaburi 64:4

5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?
Zaburi 64:5

6 Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa.
Zaburi 64:6

7 Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa.
Zaburi 64:7
👉👆Maombi ya Daudi,ilokuwa ni kumsihi Bwana asikie sauti yake. *_Ndugu yangu ni kwambie siri moja, hakuna mwanadamu wa kusikiliza sauti yako na malalamiko yako muda wote, ni Mungu tu wa kuomba asikie Sauti yako_*
👉Mara ngapi sauti yako imesikika mbele za watu uliowategemea lakini hukuona jibu?   Mwambie Bwana leo naomba usikie sauti yangu.
👉Lakini mstari wa 2, Daudi anaomba kwa Bwana *Amfiche mbali na mashauri ya siri ya wabaya* Ndugu hujawahi kujua ya kuwa kuna wanaokupangia mipango Kinyume nawe unavyotamani kuwa?
👉Mipango ya siri ina lenga kukwamisha, kuua,kudhohofisha,kuteka,kuaibisha,kuangusha ndiyo maana inapangwa kwa siri,na inapangwa na watu wabaya na waovu.
👉Wakiwa katika mikakati na kupanga *_Kuua uchumba wako, uzao wako,ndoa yako,biashara yako,elimu yako na Huduma yako,kanisa kako_* sisi usiku huu nasi tunamwomba *Baba wa miujiza,mkausha bahari,mtuliza Dhoruba,tunamwambia TUNAOMBA UTUFICHE mbali na mipango yao miovu juu yetu mwaka huu* hapo ndipo tutakuwa tumewashinda ushindi wakishindo.
👉Kufichwa ni kuhifadhiwa,kutunzwa,kwa matumizi ya sasa na ya baadaye, kilicho *Fichwa* ni kazi kukipata mpaka aliye kificha akwambie nimekificha eneo hili.
👉Mungu anapo tuficha,anawafanya maadui zetu wapoteze muda wakitutafuta,wakati wanaangaika na Kujua tupo wapi,sisi tuko Safari ya mbali.
👉Unaonaje familia yako, kazi yako, huduma yako,mambo yako viwe mevikwa vazi la Maficho na Bwana, halafu maadui wanaangaika kuvipata wanakupita tu hawavioni,wanajikwa na kuanguka wee unasonga kwa ushindi,unatamani Yesu asirudi mapema..... *Ebu tuombe pamoja leo Nguvu ya maficho ya Bwana* Hatuhitaji kuwa wazi kwa adui zetu mwaka huu, tunamambo mengi ya kufanya watatuchelewesha.
" _Bwana Yesu weeni Bwana wa usalama,nakuja mbele zako,na vitu vyangu vyote,na maisha yangu yote na kuomba nifiche pamoja na wote walio nami, nisionekane mbeleya watesi,mashauri yao ya siri yashindwe kutekelezwa, mkono wako unitegemeze niwe salama,katika jina la Yesu AMEN_"
*Mnenaji alikuwa mimi mjumbe wa Bwana: Ev Elisha Kazimoto(Anointed) WhatsApp 0755444078*
              ©2019

No comments:

Post a Comment