🔺🔺 *MKESHA WA MAOMBI YA KUKUSANYA YALIYO TAWANYWA NA ADUI*🔺🔺
Mnenaji: Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp(Anointed)
*0755444078*
.......
.......
*8 Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya ao walio wake waliokusanywa.Isaya 56:8*
_Haleluya mwombaji na mtu unaye utafuta uso wa Mungu daima, ni haki kwetu kukutana na mahitaji yetu tuyaombayo mbele za Bwana_
✍Kila anayeingia katika maombi anapeleka haja za moyo wake kwa Bwana( HOJA ZENYE NGUVU) na Bwana ameahidi kutimiza,au kutupa matakwa yetu.
✍Tunapo zidi kumwomba Mungu juu ya *Safari yetu ya mwaka huu* kuna kazi moja na ya msingi tunahitaji kuifanya katika maombi yetu, nayo ni *Kuomba maombi ya Kukusanya Maishani mwetu*
✍ Yaliyo kusanywa ni maisha ya ushindi, maisha yenye kibali cha Bwana na utukufu,ni baraka zako ziko kapuni mwako lakini zikitawanywa shida inaingia katika mfumo wa maisha yako.
✍Angalia kwa nini tuombe maombi ya KUKUSANYA.
1⃣Ndoa ikitawanywa, amani inatoweka na migogoro inaingia(migogoro ya mahusiano,uchumba na ndoa ni matokeo ya Adui kutawanya Upendo kati yenu).
2⃣Uchumi ukitawanywa, maangaiko na madeni yasiyoisha na yasiyo na sababu yanaingia na Umaskini unajenga makao.
3⃣Elimu yako ikitawanywa,nguvu ya ujinga,kufeli inangia na matokeo yako ya kitaaluma yanadorola.
4⃣Kanisa likitawanywa, Migogoro,mafarakano,malumbano yanaanza, huduma za kiroho zinaanza kuwa KAVU,ibada zinasuasua,watu kurudi nyuma kiimani,watu kutookoka,lakini Mpenyo wa Kiroho na hali ya ulimwengu wa Roho wa kanisa kutokuwa swari.
✍Kumbuka, Adui ushugulika na ulimwengu wa roho kutawanya vitu *Vilivyo kusanywa na Maishani mwako* akifanikiwa kutawanya matokeo ndo yanaonekana huku katika ulimwengu wa kawaida hali kuwa Mbaya.
✍Sasa kama wana wa Mungu,wana maombi, *Wana wa Vita* Usiku wa Leo tusimama kwa Neno la Bwana kama alivyosema kwenye Neno lake, *_Anakusanya waliofukuzwa,na siyo hao tu atakusanya na wengine/mengine yaliyo zaidi ya hayo yaliyo kusanywa_* hiyo ndo kazi ya Bwana tukimwomba.
🤝Tunashimana,kama wana Kanisa,wana Ndoa, Wachumba,wana Familia, tunasema _Bwana Yesu wewe ni Bwana wa Utosherevu,adui ametawanya mambo yetu mengi,na mengine anawaza kuyatawanya,ila leo kwa Mamlaka ya Jina la Yesu Tunakusanya,tunaleta karibu,tunarudisha mahara pake,tunaita Kila kilicho tawanywa,rudi mahara pake kwa jina la Yesu,tunafunga njia zilizo tumika na zinapangwa kutumika kutawanya maisha yetu kwa damu ya Yesu,naifungua njia ya Bwana ya kukusanya mahitaji yangu(yetu), na Bwana Anikusanyie *Na zaidi ya hayo yaliyo tawanywa* ili maadui zangu waone kuwa nimejazwa,nimetosheka na msifu Bwana katika jina la Yesu,Leo na Kesho Bwana atakusanya na kutawanywa Kumekoma katika jina la Yesu AMEN_
✍👆Ikiwa umeomba maombi haya kwa Imani amini kuna vitu mbingu zinaanza kushugulika kwaajili yako Kukusanya na kukufunika kwa utukufu mkuu.
*USIACHE KUOMBA,OMBA UKIKUSANYA WIKI HILI LOTE*
_Ulikuwa nami mnenaji wa SIRI za Bwana wa Majeshi EV Elisha Kazimoto(Anointed)_
*WhatsApp 0755444078*
©2⃣0⃣1⃣9⃣
Friday, 15 February 2019
KUSANYA YALOYO TAWANYWA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment