ππ *Swali: Me nilikuuliza kwamba ni sahihi mfano mtu kama mim nimkristo niliye okoka kuolewa na mroma au katoliki namaanisha*ππ
........
........
Anajibu Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto(Anointed)*
WhatsApp 0755444078
*SWALI LA WAZI LA KIIMANI NAMI NITALIJIBU KWA WAZI KIIMANI SIKISAIKOLOJIA*
_Wapendwa kuna wimbi kubwa na la kutisha katika kizazi cha sasa cha KUPANDIKIZA MACHOTARA wa Kiroho(Spiritual Mulattoes) Negro Christians who has double sides in faith, because of seeking Marriage_ sasa nitegee sikio nijibu kwa uwazi mkubwa sawa sawa na muuliza swali alivyo uliza.
π Note: Sipo kukwambia dhehebu lako ni mbaya au ni nzuri, ila ni uchambuzi wa swali kwa Kadri ya muuliza swali ila kupitia uchambuzi huu waweza PONA na ukasimama na Mungu.
*Fuatana nami Mchambuzi Ev Elisha Kazimoto(0755444078)* Utaweza kufunguka na kupata ufahamu juu ya maamuzi yako.
1⃣Kwanza tuelewe ( *Wale mliookoka, si kwa usanii na kivuli*) Ndoa ni Mpango wa Mungu na mwanzilishi ni wa ndoa Ni Mungu mwenyewe ndiye anayetoa KIBALI cha kuoa au kuolewa tukimwomba,tukikaa sawa naye... Siyo harakati zetu za kujitafutia mtu tunayeoana anaweza timiza ndoto zetu za maisha, Ila _Mungu anatupa mtu wa kutimiza kusudi lake kwenye maisha yetu._
18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanzo 2:18
ππ Mungu ndo wa kwanza kuoana Uhitaji wa ndoa kwa mwanadamu,si mwanadamu kuona uhitaji wa ndoa kabla ya Mungu ( *Hapo ndo tunaingiaga kwenye mfumo wa zoazoa yoyote*) ilimradi Anaweza kidhi Matarajio yako si Mapenzi ya Mungu ( *Ndo chimbuko la kuzoa Imani nyingine tofauti na yako, au kuiacha imani yako ili uoe au uolewe*)nayo hii ni Laana ya Kizazi cha sasa.
2⃣Pili,Mungu kusema atafanya msaidizi wa kufanana naye alikuwa anamaana kubwa ya kiroho na kiusalama, kuepusha mgongano wa Kiimani,Kufyonzwa nguvu za kiroho, Kuiandama miungu mingine badala ya Mungu aliye hai, Kuepusha kuzaa Machotara wa Kiroho wasio na upande wa kusimamia kiimani.
*_Kauli ya Mungu tangu zamani ni kutembea na kubariki watu watakao weza kuwafundisha watoto wao Imani ya Mungu wao Mungu wa Isaka na Yakobo_* sasa ninyi mlio imani Tofauti by NATURE mtawarithisha watoto wenu nini?
siku ile uliyosimama mbele za Bwana wako huko Horebu, Bwana aliponiambia, Nikusanyieni watu hawa, nami nitawasikizisha maneno yangu, ili wajifunze kunicha mimi siku zote watakazoishi duniani, wakapate na kuwafundisha watoto wao.
Kumbukumbu la Torati 4:10
ππ Si kwamba tunakataa Kuoana na Imani zingine kwasababu ya dhehebu,kwasababu ya uimbaji na kucheza ni *Kwa Maslahi ya Imani yako na watoto wako* Kama wazazi mna mashina mawili tofauti ya Imani,nani atawafundisha watoto niia ya Bwana? Wakati Malezi ni ya Pande mbili baba na mama walio mwili mmoja? Wakati kila mmoja wenu anaona imani yake ndo bora?
πBiblia imesema mlee mtoto katika njia ipasayo naye hata iacha hata atakapo kuwa mzee... Sasa mnalea mtoto kwa Imani ipi( kulingana na muuliza swali *Imani ya Kipentekoste/Kilokole au Kiromani?*) au unataka kusema mmoja ataamua kubadirika kumfuata mwingine... Kubadiri Imani kwaajili ya ndoa ni sawa na Kupata mtiani mark 10% wewe ukajiongezea 0 ikawa 100% halafu ukahisi umewin....kwenye karatasi watakaoona wataona umewin sana ila KIMANTIKI akilini mwako kuna 10% shida ni pale utakapo kuja mtiahani wa Taifa usio badorishwa, usiorudishiwa karatasi ndo 10 yako itaonekana,na utakuwa umefyonzwa akili na ujinga wa kujilewesha na kujidanganya haitakuwa 10 tena ila 05% na hapo ndo utahisi Maumivu makubwa na hasara kuliko maumivu na hasara ulizo kwepa darasani kupokea karatasi ya mark 10 na kutafuta kwa nini nimepata 10? Ukarekebisha ili upate 100 ya uhalali.
π *KIIMANI si sahihi wewe uliyeokoka,kuolewa/Kuoa Mromani wala Mromani Si sahihi wewe kuoa au kuolewa na Mlokole au mtu wa imani ya Kipentekoste unaichafua imqni yako na utazalisha NEGROES na utakutana na shida kubwa katika ndoa* kwa nini ni kwasababu ninyi wawili Misingi ya imani inayofautiana mbali sana, na Biblia imesema hivi, wasiopata wataendaje pamoja?
3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?
Amosi 3:3
ππ Hebu tujiulize na wewe uliye uliza swali..maswali haya machache:
1⃣Mromani anaamini na anaomba maombi kupitia kwa Mama wa Yesu Mariamu( Sala ya mama wa Mungu utuombee) *Ukitafuta kwenye Biblia hakuna mawasiliano kati ya aliye kufa na aliye hai* (Lakini Biblia imesema Wazi mwombezi wetu wanadamu Ni Roho Mtakatifu) (Imani ya Kipentekoste inaamini hivyo)
26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Warumi 8:26
ππHapa kuna shida kubwa, mtasimamaje pamoja kumwita Mungu juu ya ndoa yenu,watoto,mipango yenu na kupambana na nguvu za giza? Huyu anaombewa na Mariamu mama wa Yesu huyu anaombewa na Roho mtakatifu......(Jibu inabidi turudi kwenye Biblia mwongo wa Kikristo nani anastahili kuomba,na nani mwombezi).
2⃣Imani ya Romani *Haiamini kama kuna Kuokoka hapa Duniani* inaamini mtu akifa ndo anaokoka ndo anakuja kupewa Cheo cha Mtakatifu flani baada ya kupitia katika hatua kadha wa kadha...anatunukiwa cheti cha mtakatifu alisha kufa zamani.. Na Imani ya Kipentekoste kwa Mujibu wa Neno la Mungu Tunaamini wokovu ni hapahapa duniani wakati bado uko hai.
3 Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Zaburi 16:3
ππHilo ni miongoni mwa maandiko mengi sana yanayo zungumzia watakatifu wapo duniani siyo waliokufa, kama kuna waliokufa ni watakatifu sawa nao niwatakatifu ila si kwamba wanafanywa watakatifu baada ya kufa, Neno la Mungu linamuhusu Aliye hai ndo maana anasema *Kumcha Bwana ni kuchukia uovu Mithali 8:13* Marehemu hachukii uovu hivyo amchi Bwana,kama hakumcha akiwa duniani huyo No more time. *Msingi wa Kipentekoste ni kusisitizia utakatifu wa maisha yako ukiwa hapa duniani ndo Vasi lako la kujiandaa kumuona Bwana* Sasa hii si Imani ya Romani mtaishije watu mnaotofautiana mtazamo na Imani?
14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
Waebrania 12:14
ππImani ya Kipentekoste inaamini andiko hilo na kulitendea kazi, lakini Imani ya Romani inasema ni Uongo, Huwezi kuwa Mtakatifu ukiwa Duniani hapa, wanasahu na *Wafilipi 4:13, inayosema Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu* lakini nenda ukasome mwenyewe *YOHANA 5:1-15* Uone nguvu ya utakatifu tunaitoa wapi.
3⃣Mromani anaamini *Sala kwa aliyekufa na kutolewa sadaka kuhamishwa kutoka kwenye mateso na kupokelewa na Mungu hata kama alikufa kwenye dhambi* Imani hii wapentekoste Haipo, Wapentekoste(Walokole wanaamini katika andiko la *Waebrania 9:27, linalosema baada ya kufa ni hukumu* hakuna sadaka wala sala za kubadiri nafasi ya marehemu kama ni mwenye dhambi motoni,mwenye haki mbinguni...Sasa mnaoana ili muandaaneje kwenda kwa Bwana mbinguni.?
4⃣Mromani anaamini Kumbatiza mtoto mdogo kwa kumwondolea dhambi ya asili, lakini Imani ya Kipentekoste inaamini ubatizo ni kwa mtu mzima, aliyekiri kwa kinywa chake na kumpokea Yesu moyoni mwake ndoa anabatizwa.(Kwa lugha nyingine inaanza Toba ndo unafuata ubatizo kwa mtu mzima mwenye akili timamu)
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Matendo ya Mitume 2:38
ππSasa watoto wenu watafuata ya nani,? *_Haya ni baadhi katika uchambuzi huu,ila Hatushauri na Hakuna kusudi la Mungu la Kuoana watu wa Imani tofauti. Huo ni Ukengeufu na Upagani wa yule anaye jihita Ameokoka maana yeye Anaijua Kweli yote,ika anajifanya hajui_*
πKuna Biashara ya UTAPELI ya kuokokeshana ili muoane kwa mwenye Maarifa ya Kimungu hatufanyi hiyo biashara isiyo zaa kununua Samaki aliye China ila unasema nitambanika na kumwekea vitunguu na nyanya nyingi nipoteze harufu, Haina shida Gharama zako,usumbu wako,harufu yako, hasara yako...muuzaji hana shida shida ni wee mlaji, Sisi tunanunua Samaki Fresh *Na tunamchunguza sana mpaka kwenye masikio, ili tusiingie hasara na gharama zisizo tarajiwa,huku tumetoa pesa yetu* Kama umeelewa mfano huu uheri. Ukitaka kufanya utapeli mwambie okoka tuoane sawa, yakiwabana,mkivurugana, yakikushinda kwani sisi Tuna hasara gani, kwani Mungu ana hasara gani, kwani utakapo kuwa unazunguka kwenye Maombezi na kuandika Vikaratasi vya kuombea ndoa yako, mmeo au mkeo au watoto wako, gharama tutakuwa tunatoa sisi Wahubiri, mkifukuzana kwenye ndoa ukarudi kwenu au mke akakuacha kwani Sisi tunaumia nini? Si ulichagua? Sometimes sisi wahubiri tunapambana sana kuvaa uhalisia wa wahuni tunaumia, Ukweli uko pale pale Ndoa ni yako, yakikushinda ni wewe ulichagua, Mungu niwademokrasia anasema CHAGUA, ila yeye anakushauri chagua Uzima ukichagua mauti Kufa umetaka mwenyewe. Ila hatutaacha kusema kweli.
*_NB: Kuchelewa kuolewa,au kuoa Siyo sababu ya Kuzoa Yeyote, Ghara ya kukwepa kuvumilia muda wa Mungu ulimgharimu Ibrahimu na Sara akazaa na Kijakazi, imetuletea shida mpaka sasa duniani kisa nimechelewa, umechelewa Unajua utaishi miaja mingapi? Unajua sababu ya kucheleweshwa? Vumilia pate mema ya Mungu_*
Nadhani nimejibu swali la muuliza swali mchambuzi alikuwa:
*Psychologist & Counselor Ev Elisha Kazimoto(Anointed)*
WhatsApp 0755444078
©2019
No comments:
Post a Comment