Friday, 25 January 2019

HUWEZI BADIRISHA NAFASI YANGU

🛤🛤 *MAOMBI YA KUZUIA MAADUI KUBADIRISHA BARAKA ZAKO MWAKA HUU*🛤🛤
_Mkesha Wa Maombi ya Nguvu ya Kuporomosha Nia Ovu ya Maadui dhidi yako katika Mwaka huu wa Baraka_
*Mnenaji: Ev Elisha Kazimoto(Anointed)*
WhatsApp 0755444078
.................
.................
8 Israeli
wana wa Yusufu, akasema, Ni nani hawa?
Mwanzo 48:8

9 Yusufu akamwambia babaye, Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa. Akasema, Tafadhali uwalete kwangu nami nitawabariki.
Mwanzo 48:9

13 Yusufu akawaweka wote wawili, Efraimu katika mkono wake wa kuume, kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli; na Manase katika mkono wake wa kushoto, kuelekea mkono wa kuume wa Israeli, akawasogeza karibu naye.
Mwanzo 48:13

14 Israeli akanyosha mkono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, huku akijua atiavyo mikono; maana Manase ndiye aliyezaliwa kwanza.
Mwanzo 48:14

15 Akambariki Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo,
Mwanzo 48:15

16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi.
Mwanzo 48:16

17 Yusufu alipoona kwamba babaye anaweka mkono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, ikawa vibaya machoni pake. Akauinua mkono wa babaye auondoe katika kichwa cha Efraimu, ili auweke juu ya kichwa cha Manase.
Mwanzo 48:17

18 Yusufu akamwambia babaye, Sivyo, babangu, maana huyu ni mzaliwa wa kwanza; weka mkono wako wa kuume kichwani pake.
Mwanzo 48:18

19 Babaye akakataa, akasema, Najua, mwanangu najua, yeye naye atakuwa taifa, yeye naye atakuwa mkuu; lakini ndugu yake mdogo atakuwa mkubwa kuliko yeye, na uzao wake watakuwa wingi wa mataifa.
Mwanzo 48:19
🛤Kuna wakati unahitaji kusimama katika nafasi yako kwenye Maombi kushugulikia Nguvu za maadui wanao Kusudia mabaya katika maisha yako, _Kuwazuia wasibadirishe mpango mzuri wa Mungu kwako_
🛤Siri moja ni hii, kila mmoja Mungu anao mpango mzuri kwake, ziko packages za baraka kila msimu,kila mwaka ambazo Mungu anaziachilia kwenye ulimwengu wa roho zikupate katika ulimwengu wa mwili.
🛤Ila kuna mchezo mchafu waweza fanyika katika ulimwengu wa roho na hata katika ulimwengu wa mwili Shetani kwa  kutumia mawakala wake na watu, *Wenye Nafasi* iwe ofisini, iwe kwenye biashara, elimu,Kihuduma, kijamii *Watumike kubadirisha baraka zako* Lakini Habari njema kwa Watu wamtumainio Mungu ni kwamba, *_Harakati zote za siri na za Wazi Haziwezi fanikiwa kwakuwa Mkono wa Bwana uko juu yako hakuna wa Kuubadirisha_* Na leo tunasimama kwenye Maombi kuwa piga hao walioshikilia mpango Ovu juu yako ubatirishwe na Bwana wa Majeshi.
🛤Yusufu hakujua kuwa Efraimu *Tayari ana Alama ya Mungu ya kubarikiwa* akataka abadirishe mbaraka wake, Akamweka Mkono wa Kushoto kwa yeye abarikiye(Yakobo) na Manase akamweka mkono wa Kuume akijua huyu ndo anastahiri kubarikiwa.....Sikiliza mawazo ya wanadamu na kutazama kwa wanadamu Si kama Mungu aonavyo, Yakobo akiwa katika Roho *Alizuia Mission ya Yusufu ya kumbadirishia Efraimu baraka zake* Nami nataka nikwambie Kwa Maombi haya ya leo Tunaharibu Mission ya Maadui ya kujaribu kubadirisha baraka zako, Ndoa yako,uchumba wako, uchumi wako,elimu yako na Huduma yako, katika jina la Yesu watakomeshwa wao na mwisho itakuwaaibu yao.
🛤Sikiliza mtu wa Mungu,sijui kama *Efraimu alikuwa anatambua anachokifanya baba yake Yusufu* lakini alitulia( Tunahitaji Kutulia kwa Mungu acheze game na maadui zetu) Alisha sema Hakuna Hila ya ya mwanadamu itafanikiwa juu yako,ni kusudi la Mungu ndo litakalo fanikiwa.
*Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.Mithali 19:21*
🛤Kataa hila juu yako kufanikiwa kwa jina la Yesu, mwambie Bwana kusudi lako litimizwe kwangu mwaka huu.
🛤Ujasiri mkuu tulio nao ni kwamba, Mkono wa Mungu ukinyooshwa juu yetu hakuna mwanadamu wa kuurudisha nyuma, *Watatumia Mbinu zoote wazijuazo kukudhohofisha, hawatafanikiwa* Neno hili ni Hakika ni amina na kweli atatutetea kwa mkono wake wa nguvu.

24 Bwana wa majeshi ameapa, akisema, Hakika yangu kama vile vilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa; na kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyotokea;
Isaya 14:24

27 Maana Bwana wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma?
Isaya 14:27
🛤Tunapo funga mwezi huu kwa maombi,tunamwambia adui,na wanadamu wote waliokubali kutumika kama mawakala waadui,kuwambia *Pisha njia katika mwaka huu,Usiangaike kushikilia Kibali changu,Nafasi yangu,Uchumi wangu,Huduma yangu Uzao wangu....Mungu atakapo Ipinga Hila yako Utaumia* Huu ni Usiku wakutanga Maachilio katika ulimwengu wa Roho juu ya maisha yetu katika mwaka huu.
🛤Yakobo akamwambia Yusufu Mchezo unao ucheza juu ya Efraimu Naujua,unakusudia awe mdogo ila ndo Atakuwa mkubwa,na Manase unaye mwazia awe mkubwa ndiye atakaye kuwa mdogo..... *NAJUA NIWEKAVYO MIKONO JUU YAO KUWABARIKI*
🛤Unacho hitaji kama mwana maombi na mtu wa Mungu ni kuzingatia mambo makubwa 3 maishani mwako:
1⃣Jitambue na jihakikishe Uko sawa na Mungu,unaotaka nini maishani mwako,una nini maishani mwako kama Neema ya Mungu ndani yako.
2⃣Jitenge na Uovu(usimkose Mungu)lindi uchaji wako kwa Mungu hiyo ndo nguvu ya kuwasambaratisha wenye hila juu yako.
3⃣Kaa kimya(Zama kwenye maombi)usipambane na watu kimwili pambana nao katika maombi ushindi wetu unaanzia kwenye ulimwengu wa Roho. *Yuko Bwana wa Kumkemea adui yako* na Baraka zako zikakukalia daima, na lile uliloandikiwa na Bwana likatimia kwako.
*_Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu.Mwanzo 31:42_*
_Nimalize kwakukutia moyo wewe mtumishi wa Mungu ,ondoa Hofu na Mashaka kuhusu Kesho yako,anaiangaikia Bwana,haijalishi Vitawekwa Vigingi vingapi mbele yako,haijalishi ni kwa muda gani umepambana ila uoni mpenyo, saa yako ikaribu,na mwaka huu tunautangaza kuwa wa Bwana kutimiza,kulinda heshima yetu Kazi yetu ni Kukaa vizuri na Mungu,kumtafuta uso wake, Baraka,nafasi za wana wa Mungu wenye chapa ya Mungu malongo yao Hayafungwi na mtu yatakuwa wazi Daima,wanao angaika kukufungia Wanapoteza muda wao bure wewe ni Mzao wa Kifalme, Taifa takatifu la Mungu Ulinde Uraia wako wa Mbinguni Ushindi Nilazima, *Huu ni Mwaka wa Bwana Kutufanyia Nafasi na Kutuzidisha sana* Inuka acha kulia,acha kusononeka uwe kama Efraimu, uwe kama Yakobo, uwe kama Daudi na wengine waliotetewa na Bwana_
*_Nakutakia Mwaka wa Ushindi na mwezi mwingine wa kuuendea Muujiza na Nafasi yako katika jina la Yesu. Amen. By Ev Elisha Kazimoto(Anointed)_*
WhatsApp 0755444078

No comments:

Post a Comment