❓❓ *MAAJABU SITA (6) YA WANA NDOA*❓❓
_Haya ni maajabu ya kisaikolojia,waweza yaona ya kawaida ila ndo hivyo kama umekamatwa hapo huwezi kuwa na furaha,kwa namna yoyote unaishi kiugumu ugumu_
1⃣Huwezi mwamini mkeo au Mmeo, ila unakubali kulala naye kitanda kimoja na shuka moja❗
2⃣Huwezi mwambia nakupenda mke wangu au mme wangu, ila Unazaa naye watoto.❗
3⃣Huwezi muaga mkeo au mmeo popote unapo kwenda, ila Unamuomba Tendo la ndoa kwa sura ya upole.❗
4⃣Huwezi ongozana naye,wala kumtambulisha kwa watu kuwa huyu ni mpenzi wangu(wife/husband ),ila unaweza eneza ubaya wake kwa watu na bado mnakaa wote nyumba moja.❗
4⃣Huwezi kukaa na mmeo au mkeo mkazungumza kama marafiki,na kubadirishana mawazo, ila unapenda mkae muda wa kutosha kwenye tendo la ndoa.❗
6⃣Huwezi kumthamini mwenzako kama mtu mwenye umuhimu kwako,dhaifu sana hana uwezo wowote, ila Unamuita Baba/mama wa watoto wako.❗
_Haya yanashangaza sana, na Yajayo yanafurahisha_
*Raha ni kujipa mwenyewe na Stress ni Kujitengenezea*
#Mwanasaikolojiahazeeki.
Monday, 18 February 2019
MAAJABU 6 YA WANA NDOA
Sunday, 17 February 2019
WAWEZA KUKAA BILA SEX
*JE, KUNA UWEZEKANO WA MTU MWANAUME AU MWANAMKE KUKAA MUDA MREFU BILA KUSEX?*
_Suala hili hatuwezi lipa jibu ya mtazamo mmoja ili kulipa majibu ya uhakika lazima tuangalie Kisaikolojia linatafsiriwa vipi na kiroho linatafsiriwa kivipi_
✍Kwanza sex ni suala la Kihisia linalo ratibiwa na Hormones ( hisia zinaweza kutibuliwa na mazingira kwa kuona au kushikwa/contacts).
✍Shahuku/uhitaji wa sex kwa mwanaume na mwanamke unatofautiana, Kisaikolojia mwanaume anahitaji sana sex kuliko mwanamke japo( *Kuna wanawake wana kiwango kikubwa sana cha hamu ya sex kama au zaidi ya wanaume*) walio wachache....
✍Ila wanaume wanauwezo mdogo wa kuhimili kukaa bila sex kuliko wanawake kwasababu hawana njia mbadala ya regulation of body kama wana wake isipo kuwa kwenye ndoyo nyevu au wale wanaofanya Uharamu wa Masterbation.
✍Kwanini wanaume wanashindwa kustahimili kukaa bila sex kwa muda murefu? *Ni kwasababu Tamaa yao ipo kwenye Macho, kwa hiyo mara kwa mara wanatibuliwa Hisia zao kwa kutazama* tofauti na wanawake ambao hisia zao Utibuliwa kwa *Kushikwa shikwa na Kusifiwa saana na kwa sauti ya mahaba* jambo ambalo kwa halifanyiki mara kwa mara linatokea kwa nadra kwa muda maalumu. Kwa msingi huo kisaikolojia wanaume Sex kuikwepa ni nadra sana.
✍ *NB: Uwezo wa kijana kukaa bila sex muda mrefu bila shida ni mkubwa kuliko Mwanaume aliyeoa au Yule ambaye alisha onja sex* Aliyeonja sex uwezo wake wa kisaikolojia umeathiriwa kulinganisha na ambaye hajawahi kugusa.
✍ *Kiroho hapa ambapo penye msingi wa usalama kwa watu walio na Mungu* Udhibiti wa miili upo katika Nguvu za Roho Mtakatifu (Wafilipi 4:13....Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.) Kwa maana hiyo kuhimili kutofanya sex si kwamba kunashindikana ila Umeshikiliwa na nini....? Kama umeshikiliwa na Pepo,hisia tabia mazingira hutaikwepa zinaa ila kama Umeshikiliwa na Roho mtakatifu kuna nguvu ya KUSHINDA. Watu waliookoka kweli kweli wanajua Siri hii ya KUSHINDA kama, kiroho hauko vizuri HUWEZI JUA ninacho SEMA.
✍Ila kwa siri hii ya Nguvu ya KUSHINDA tunapewa na Roho mtakatifu ndo maana watu *wanaoa na kuolewa miaka 25,30,35,40 BILA KUGUSA SEX.* si kwamba hawana hisia,hawaoni SITES za kusex,wanaziona ila ndani yao wanapigiwa ALARM NA ROHO WA BWANA.
7 Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami.
Mwanzo 39:7
8 Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu.
Mwanzo 39:8
9 Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?
Mwanzo 39:9
👆👉 Kwa hiyo KUSHINDA kwetu kunatoka ndani.
✍ *NB* KUSHINDWA KWA MTU MMOJA SIYO KWAMBA WOTE WAMESHINDWA.
*_Kufanya sex ni maamuzi na kukaa bila kufanya sex ni maamuzi, na dhambi ngumu kuliko zote na yenye mazingira magumu ya kuitimiza ni sex_*
By Ev Elisha Kazimoto
©2019
Friday, 15 February 2019
KUSANYA YALOYO TAWANYWA
🔺🔺 *MKESHA WA MAOMBI YA KUKUSANYA YALIYO TAWANYWA NA ADUI*🔺🔺
Mnenaji: Ev Elisha Kazimoto
WhatsApp(Anointed)
*0755444078*
.......
.......
*8 Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya ao walio wake waliokusanywa.Isaya 56:8*
_Haleluya mwombaji na mtu unaye utafuta uso wa Mungu daima, ni haki kwetu kukutana na mahitaji yetu tuyaombayo mbele za Bwana_
✍Kila anayeingia katika maombi anapeleka haja za moyo wake kwa Bwana( HOJA ZENYE NGUVU) na Bwana ameahidi kutimiza,au kutupa matakwa yetu.
✍Tunapo zidi kumwomba Mungu juu ya *Safari yetu ya mwaka huu* kuna kazi moja na ya msingi tunahitaji kuifanya katika maombi yetu, nayo ni *Kuomba maombi ya Kukusanya Maishani mwetu*
✍ Yaliyo kusanywa ni maisha ya ushindi, maisha yenye kibali cha Bwana na utukufu,ni baraka zako ziko kapuni mwako lakini zikitawanywa shida inaingia katika mfumo wa maisha yako.
✍Angalia kwa nini tuombe maombi ya KUKUSANYA.
1⃣Ndoa ikitawanywa, amani inatoweka na migogoro inaingia(migogoro ya mahusiano,uchumba na ndoa ni matokeo ya Adui kutawanya Upendo kati yenu).
2⃣Uchumi ukitawanywa, maangaiko na madeni yasiyoisha na yasiyo na sababu yanaingia na Umaskini unajenga makao.
3⃣Elimu yako ikitawanywa,nguvu ya ujinga,kufeli inangia na matokeo yako ya kitaaluma yanadorola.
4⃣Kanisa likitawanywa, Migogoro,mafarakano,malumbano yanaanza, huduma za kiroho zinaanza kuwa KAVU,ibada zinasuasua,watu kurudi nyuma kiimani,watu kutookoka,lakini Mpenyo wa Kiroho na hali ya ulimwengu wa Roho wa kanisa kutokuwa swari.
✍Kumbuka, Adui ushugulika na ulimwengu wa roho kutawanya vitu *Vilivyo kusanywa na Maishani mwako* akifanikiwa kutawanya matokeo ndo yanaonekana huku katika ulimwengu wa kawaida hali kuwa Mbaya.
✍Sasa kama wana wa Mungu,wana maombi, *Wana wa Vita* Usiku wa Leo tusimama kwa Neno la Bwana kama alivyosema kwenye Neno lake, *_Anakusanya waliofukuzwa,na siyo hao tu atakusanya na wengine/mengine yaliyo zaidi ya hayo yaliyo kusanywa_* hiyo ndo kazi ya Bwana tukimwomba.
🤝Tunashimana,kama wana Kanisa,wana Ndoa, Wachumba,wana Familia, tunasema _Bwana Yesu wewe ni Bwana wa Utosherevu,adui ametawanya mambo yetu mengi,na mengine anawaza kuyatawanya,ila leo kwa Mamlaka ya Jina la Yesu Tunakusanya,tunaleta karibu,tunarudisha mahara pake,tunaita Kila kilicho tawanywa,rudi mahara pake kwa jina la Yesu,tunafunga njia zilizo tumika na zinapangwa kutumika kutawanya maisha yetu kwa damu ya Yesu,naifungua njia ya Bwana ya kukusanya mahitaji yangu(yetu), na Bwana Anikusanyie *Na zaidi ya hayo yaliyo tawanywa* ili maadui zangu waone kuwa nimejazwa,nimetosheka na msifu Bwana katika jina la Yesu,Leo na Kesho Bwana atakusanya na kutawanywa Kumekoma katika jina la Yesu AMEN_
✍👆Ikiwa umeomba maombi haya kwa Imani amini kuna vitu mbingu zinaanza kushugulika kwaajili yako Kukusanya na kukufunika kwa utukufu mkuu.
*USIACHE KUOMBA,OMBA UKIKUSANYA WIKI HILI LOTE*
_Ulikuwa nami mnenaji wa SIRI za Bwana wa Majeshi EV Elisha Kazimoto(Anointed)_
*WhatsApp 0755444078*
©2⃣0⃣1⃣9⃣
OMBA BWANA AKUFICHE
🖥 *MKESHA WA MAOMBI YA KUOMBA KUFICHWA NA BWANA MBALI NA MIPANGO YA SIRI YA MAADUI ZETU*🖥
*_Mnenaji: Ev Elisha Kazimoto(Anointed)_*
WhatsApp 0755444078
.........
.........
_Shalom mwombaji,ni wiki lingine tunaendelea na vita,tunajipanga kwa safu mpya kila wiki Bwana anayo siri ya kutupa kuwaendea maadui zetu na kuwashinda na kuziteka baraka zetu. Leo twende *Mafichoni pa Bwana* huko kuna usalama mkuu.
1 Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.
Zaburi 64:1
2 Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;
Zaburi 64:2
3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,
Zaburi 64:3
4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.
Zaburi 64:4
5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?
Zaburi 64:5
6 Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa.
Zaburi 64:6
7 Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa.
Zaburi 64:7
👉👆Maombi ya Daudi,ilokuwa ni kumsihi Bwana asikie sauti yake. *_Ndugu yangu ni kwambie siri moja, hakuna mwanadamu wa kusikiliza sauti yako na malalamiko yako muda wote, ni Mungu tu wa kuomba asikie Sauti yako_*
👉Mara ngapi sauti yako imesikika mbele za watu uliowategemea lakini hukuona jibu? Mwambie Bwana leo naomba usikie sauti yangu.
👉Lakini mstari wa 2, Daudi anaomba kwa Bwana *Amfiche mbali na mashauri ya siri ya wabaya* Ndugu hujawahi kujua ya kuwa kuna wanaokupangia mipango Kinyume nawe unavyotamani kuwa?
👉Mipango ya siri ina lenga kukwamisha, kuua,kudhohofisha,kuteka,kuaibisha,kuangusha ndiyo maana inapangwa kwa siri,na inapangwa na watu wabaya na waovu.
👉Wakiwa katika mikakati na kupanga *_Kuua uchumba wako, uzao wako,ndoa yako,biashara yako,elimu yako na Huduma yako,kanisa kako_* sisi usiku huu nasi tunamwomba *Baba wa miujiza,mkausha bahari,mtuliza Dhoruba,tunamwambia TUNAOMBA UTUFICHE mbali na mipango yao miovu juu yetu mwaka huu* hapo ndipo tutakuwa tumewashinda ushindi wakishindo.
👉Kufichwa ni kuhifadhiwa,kutunzwa,kwa matumizi ya sasa na ya baadaye, kilicho *Fichwa* ni kazi kukipata mpaka aliye kificha akwambie nimekificha eneo hili.
👉Mungu anapo tuficha,anawafanya maadui zetu wapoteze muda wakitutafuta,wakati wanaangaika na Kujua tupo wapi,sisi tuko Safari ya mbali.
👉Unaonaje familia yako, kazi yako, huduma yako,mambo yako viwe mevikwa vazi la Maficho na Bwana, halafu maadui wanaangaika kuvipata wanakupita tu hawavioni,wanajikwa na kuanguka wee unasonga kwa ushindi,unatamani Yesu asirudi mapema..... *Ebu tuombe pamoja leo Nguvu ya maficho ya Bwana* Hatuhitaji kuwa wazi kwa adui zetu mwaka huu, tunamambo mengi ya kufanya watatuchelewesha.
" _Bwana Yesu weeni Bwana wa usalama,nakuja mbele zako,na vitu vyangu vyote,na maisha yangu yote na kuomba nifiche pamoja na wote walio nami, nisionekane mbeleya watesi,mashauri yao ya siri yashindwe kutekelezwa, mkono wako unitegemeze niwe salama,katika jina la Yesu AMEN_"
*Mnenaji alikuwa mimi mjumbe wa Bwana: Ev Elisha Kazimoto(Anointed) WhatsApp 0755444078*
©2019