_Swali: Kwa nini wadada ambao uwakataa watu waliowachumbia,wakikaa bila kuolewa uwarudia na kuomba au kutengeneza mazingira ya kurudiana?_
Anajibu: Msaikolojia Ev Elisha Kazimoto(0755444078)
*HAPA KUNA MAMBO MAKUBWA 2 YA KUANGALIA, KISAIKOLOJIA NA KIROHO*
👉Kuolewa na kuoa ni jambo la kiroho na kisaikolojia linaloenda na muda na kusudi.
👉Nianze na KISAIKOLOJIA.
👉Nikizungumza kisaikolojia najifanya kama kiroho sijatazama,ila mwisho nitayaunganisha nikisha chambua na kiroho.....
1⃣Kuoa na kuolewa kisaikolojia kunaenda na muda na mvuto wa hisia.....
1⃣Miaka 15-18, wadada wanakuwa wanapenda sanaa jinsia ya kiume(au mapenzi) hapa ni shida kwa wazazi yaani binti anafukuzia wakaka anaye hisi anampenda, hapa ndo unakuta mtu ana marafiki wa kiume hata 10,au wapenzi 10 na wore anawamudu.
2⃣miaka 19-25 anaanza kujiona mzuri sana anavyopendwa, hapa anakuwa na majibu ya dharau maana muda huu anamvuto mkubwa wa sura,kimaumbile (shape imekaa sawa) Anaanza kuchambua wanaume wapi wa kumuoa na hapa anapandisha vigezo vya mtu wa kumuoa,vigumu gumu na kujiona kama Malkia wa dunia, wanaume wote wanamtazama yeye tu.
Na hapa ni muda wa foleni ta wanaume kumchumbia, mambo yanageuka hapa Wanaume wanatiririka kumchumbia,kumtongoza wamchezee, siyo yeye kuwatafuta.( *Huu muda binti anahitaji kuwa makini sana, maana kwenye foleni inayokuja waweza poteza hata wa kwako) maana kipindi hiki ndo wadada ukataa kila mwanaume, anaye mkubali ni *Kwa kumtega kuona kama atakidhi vigezo vyote,siyo baadhi vyote*(Hapa wadada ujiona bado wadogo na wana take headlines za wavulana)
3⃣miaka 26- 30 wadada kama hana mchumba maalumu wanaanza kushtuka shutuka, kupunguza vigezo vyao, *Foleni ya wanaume inaanza kupungua* Muda huu uanza kujiona wamekuwa,uanza kuogopa kusema umri wao halisi, uanza kutafuta no au mwasiliano ya wanaume waliowahi mcuumbia kujua kama ameoa tayari, anaanza kutafuta urafiki kama kipindi cha miaka 15-18.
4⃣31-40 hiki ni kipindi kigumu sana kwa wadada, foleni za wanaume Ukata kabisa,mvuto aliokuwa nao mwanzo uanza kupotea, suraya kukomaa uanza kutokea,wamaume(vijana uanza kumpita mbali,anaanza kuheshimia kama mtu mzima., uanza kujilaumu, upunguza vigezo vyote ubakiza kigezo 1 tu cha awe ni MWANAUME aliyeokoka, wengine ubakiza mwaume tu.
👉Muda huu niwaupweke,wa kuomba sana mme,uanza kujutia makosa aloyafanya ya kukataa wanaume.
5⃣Miaka 40 kuendelea....muda huu niwakusuburia Neema za Mungu na Muujiza wa Bwana, saikolojia inakuwa imeisha koma kufanya kazi.
👉Kwa Upande wa Kiroho, ndoa inaenda na muda wa kusudi ka Mungu, kwa hiyo nimuhimu kukaa na Mungu vizuri,ili foleni ya wanaume inapokuwa nyingi,ujue nani kakusuduwa na Mungu au hayupo. Ukilitupilia mbali kusudi la Mungu akipita ndo imetoka hiyo,itakugharimu sana kumtafuta Mungu akutengenezee ubavu wako tena,au na mwanaume kule afungwe mje kukutana ukubwani huko.
*_Kwa hiyo kinacho sababisha kukaa wadada bila kuolewa kipo kiroho na kisaikolojia_*
By Ev Elisha Kazimoto(Anointed)
WhatsApp 0755444078
©2019
Wednesday, 30 January 2019
MIAKA YA KUCHANUA NA KUSINYAA
Friday, 25 January 2019
HUWEZI BADIRISHA NAFASI YANGU
🛤🛤 *MAOMBI YA KUZUIA MAADUI KUBADIRISHA BARAKA ZAKO MWAKA HUU*🛤🛤
_Mkesha Wa Maombi ya Nguvu ya Kuporomosha Nia Ovu ya Maadui dhidi yako katika Mwaka huu wa Baraka_
*Mnenaji: Ev Elisha Kazimoto(Anointed)*
WhatsApp 0755444078
.................
.................
8 Israeli
wana wa Yusufu, akasema, Ni nani hawa?
Mwanzo 48:8
9 Yusufu akamwambia babaye, Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa. Akasema, Tafadhali uwalete kwangu nami nitawabariki.
Mwanzo 48:9
13 Yusufu akawaweka wote wawili, Efraimu katika mkono wake wa kuume, kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli; na Manase katika mkono wake wa kushoto, kuelekea mkono wa kuume wa Israeli, akawasogeza karibu naye.
Mwanzo 48:13
14 Israeli akanyosha mkono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, huku akijua atiavyo mikono; maana Manase ndiye aliyezaliwa kwanza.
Mwanzo 48:14
15 Akambariki Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo,
Mwanzo 48:15
16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi.
Mwanzo 48:16
17 Yusufu alipoona kwamba babaye anaweka mkono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, ikawa vibaya machoni pake. Akauinua mkono wa babaye auondoe katika kichwa cha Efraimu, ili auweke juu ya kichwa cha Manase.
Mwanzo 48:17
18 Yusufu akamwambia babaye, Sivyo, babangu, maana huyu ni mzaliwa wa kwanza; weka mkono wako wa kuume kichwani pake.
Mwanzo 48:18
19 Babaye akakataa, akasema, Najua, mwanangu najua, yeye naye atakuwa taifa, yeye naye atakuwa mkuu; lakini ndugu yake mdogo atakuwa mkubwa kuliko yeye, na uzao wake watakuwa wingi wa mataifa.
Mwanzo 48:19
🛤Kuna wakati unahitaji kusimama katika nafasi yako kwenye Maombi kushugulikia Nguvu za maadui wanao Kusudia mabaya katika maisha yako, _Kuwazuia wasibadirishe mpango mzuri wa Mungu kwako_
🛤Siri moja ni hii, kila mmoja Mungu anao mpango mzuri kwake, ziko packages za baraka kila msimu,kila mwaka ambazo Mungu anaziachilia kwenye ulimwengu wa roho zikupate katika ulimwengu wa mwili.
🛤Ila kuna mchezo mchafu waweza fanyika katika ulimwengu wa roho na hata katika ulimwengu wa mwili Shetani kwa kutumia mawakala wake na watu, *Wenye Nafasi* iwe ofisini, iwe kwenye biashara, elimu,Kihuduma, kijamii *Watumike kubadirisha baraka zako* Lakini Habari njema kwa Watu wamtumainio Mungu ni kwamba, *_Harakati zote za siri na za Wazi Haziwezi fanikiwa kwakuwa Mkono wa Bwana uko juu yako hakuna wa Kuubadirisha_* Na leo tunasimama kwenye Maombi kuwa piga hao walioshikilia mpango Ovu juu yako ubatirishwe na Bwana wa Majeshi.
🛤Yusufu hakujua kuwa Efraimu *Tayari ana Alama ya Mungu ya kubarikiwa* akataka abadirishe mbaraka wake, Akamweka Mkono wa Kushoto kwa yeye abarikiye(Yakobo) na Manase akamweka mkono wa Kuume akijua huyu ndo anastahiri kubarikiwa.....Sikiliza mawazo ya wanadamu na kutazama kwa wanadamu Si kama Mungu aonavyo, Yakobo akiwa katika Roho *Alizuia Mission ya Yusufu ya kumbadirishia Efraimu baraka zake* Nami nataka nikwambie Kwa Maombi haya ya leo Tunaharibu Mission ya Maadui ya kujaribu kubadirisha baraka zako, Ndoa yako,uchumba wako, uchumi wako,elimu yako na Huduma yako, katika jina la Yesu watakomeshwa wao na mwisho itakuwaaibu yao.
🛤Sikiliza mtu wa Mungu,sijui kama *Efraimu alikuwa anatambua anachokifanya baba yake Yusufu* lakini alitulia( Tunahitaji Kutulia kwa Mungu acheze game na maadui zetu) Alisha sema Hakuna Hila ya ya mwanadamu itafanikiwa juu yako,ni kusudi la Mungu ndo litakalo fanikiwa.
*Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.Mithali 19:21*
🛤Kataa hila juu yako kufanikiwa kwa jina la Yesu, mwambie Bwana kusudi lako litimizwe kwangu mwaka huu.
🛤Ujasiri mkuu tulio nao ni kwamba, Mkono wa Mungu ukinyooshwa juu yetu hakuna mwanadamu wa kuurudisha nyuma, *Watatumia Mbinu zoote wazijuazo kukudhohofisha, hawatafanikiwa* Neno hili ni Hakika ni amina na kweli atatutetea kwa mkono wake wa nguvu.
24 Bwana wa majeshi ameapa, akisema, Hakika yangu kama vile vilivyoazimia, ndivyo itakavyokuwa; na kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyotokea;
Isaya 14:24
27 Maana Bwana wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma?
Isaya 14:27
🛤Tunapo funga mwezi huu kwa maombi,tunamwambia adui,na wanadamu wote waliokubali kutumika kama mawakala waadui,kuwambia *Pisha njia katika mwaka huu,Usiangaike kushikilia Kibali changu,Nafasi yangu,Uchumi wangu,Huduma yangu Uzao wangu....Mungu atakapo Ipinga Hila yako Utaumia* Huu ni Usiku wakutanga Maachilio katika ulimwengu wa Roho juu ya maisha yetu katika mwaka huu.
🛤Yakobo akamwambia Yusufu Mchezo unao ucheza juu ya Efraimu Naujua,unakusudia awe mdogo ila ndo Atakuwa mkubwa,na Manase unaye mwazia awe mkubwa ndiye atakaye kuwa mdogo..... *NAJUA NIWEKAVYO MIKONO JUU YAO KUWABARIKI*
🛤Unacho hitaji kama mwana maombi na mtu wa Mungu ni kuzingatia mambo makubwa 3 maishani mwako:
1⃣Jitambue na jihakikishe Uko sawa na Mungu,unaotaka nini maishani mwako,una nini maishani mwako kama Neema ya Mungu ndani yako.
2⃣Jitenge na Uovu(usimkose Mungu)lindi uchaji wako kwa Mungu hiyo ndo nguvu ya kuwasambaratisha wenye hila juu yako.
3⃣Kaa kimya(Zama kwenye maombi)usipambane na watu kimwili pambana nao katika maombi ushindi wetu unaanzia kwenye ulimwengu wa Roho. *Yuko Bwana wa Kumkemea adui yako* na Baraka zako zikakukalia daima, na lile uliloandikiwa na Bwana likatimia kwako.
*_Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu.Mwanzo 31:42_*
_Nimalize kwakukutia moyo wewe mtumishi wa Mungu ,ondoa Hofu na Mashaka kuhusu Kesho yako,anaiangaikia Bwana,haijalishi Vitawekwa Vigingi vingapi mbele yako,haijalishi ni kwa muda gani umepambana ila uoni mpenyo, saa yako ikaribu,na mwaka huu tunautangaza kuwa wa Bwana kutimiza,kulinda heshima yetu Kazi yetu ni Kukaa vizuri na Mungu,kumtafuta uso wake, Baraka,nafasi za wana wa Mungu wenye chapa ya Mungu malongo yao Hayafungwi na mtu yatakuwa wazi Daima,wanao angaika kukufungia Wanapoteza muda wao bure wewe ni Mzao wa Kifalme, Taifa takatifu la Mungu Ulinde Uraia wako wa Mbinguni Ushindi Nilazima, *Huu ni Mwaka wa Bwana Kutufanyia Nafasi na Kutuzidisha sana* Inuka acha kulia,acha kusononeka uwe kama Efraimu, uwe kama Yakobo, uwe kama Daudi na wengine waliotetewa na Bwana_
*_Nakutakia Mwaka wa Ushindi na mwezi mwingine wa kuuendea Muujiza na Nafasi yako katika jina la Yesu. Amen. By Ev Elisha Kazimoto(Anointed)_*
WhatsApp 0755444078
Monday, 21 January 2019
UFUNGUO WA 8
🔑🔑 *Ufunguo wa 8: Nahitaji Kujiona Sura yangu ndani ya moyo wa Mke au mme wangu*🔑🔑
_Huu ni mwendelezo wa Funguo 12 za ndoa yenye Furaha na Amani,ukiwa na mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa na Mwanasaikolojia *Ev Elisha Kazimoto(Anointed)* WhatsApp 0755444078_
🔑Kuna vitu vinasahaurika kwa watu kwakuwa wanaviona si vya muhimu,na kuna mambo yanajengeka mioyoni ambayo hayakutarajiwa, lakini yote ni kwa sababu kuna kitu kimoja cha Kisaikolojia kimepigwa teke na wahusika aidha kwa kutojua,au malezi au mazingira yamewafanya wajivue ufahamu wa kufanya yaliyo ya msingi na washikilie yasiyo ya msingi.
🔑Furaha ya ndoa Siyo Muujiza,ni *Mchakato wa Hiyari* wa kutumia akili na maombi(kwa wale wanaoamini katika Mungu).
🔑Umewahi kujiuliza kupindi *Mnachumbiana na huyo mwenzako* moyoni mwako na akilini mwako kulikuwaje? Kulikuwa *Kumejaa Sura yake* ndiyo maana mawasiliano ya barua,ya simu,ya kutafuta kuonana yalikuwa makubwa na ya mara kwa mara sana, angaiko la moyo Usipo muona au Kusikia sauti yake kwa muda lilikuwa linakutokea. Kilicho kuwa kina fanya hayo yote ni SURA YAKE ILIJAA MOYONI MWAKO, NA YAKO ILIJAA MOYONI MWAKE.
🔑Kilicho sababisha sura yake ijae kwako na yako ijae kwake ni nini? *Jibu rahisi sana, ni Kila mmoja alikuwa anatafuta kufanya kile anacho hisi mwenzake atapendezwa nacho, na kujizuia kufanya kileambacho anahisi kitamuumiza au muudhi mwenzake.* Ila kwa sasa Sura ya mwenzako Imefutika moyoni mwako au sura yako imefutika moyoni mwake, na kama ipo basi *Haionekani vizuri ina kivuli vuli* kwa nini? _Kwasababu, haujali tena Hisia za kufurahi au kuchukia kwa mwenzako_ bali unafanya unalo hisi una utashi wa kulifanya, unasema bila kujali kama lugha hiyo ni tamu kwa mwenzako au ni chungu,inajeruhi au inaganga moyo wake.
🔑Ila ujue sura yako ikifutika ndani ya mwenzako jua *Hamtokuja kutulia kwenye Ndoa, migogoro itapoa mwezi, ujao inaanza,mwaka, ujao inaanza....* Nini mwenzako HAJIONI SURA YAKE NDANI YAKO
🔑Kulinda Furaha na Amani ya ndoa yako hakikisha unatumia ufunguo huu, *Nataka nijione Sura yangu ndani yake* ukimwangalia unaona *_Huyu ndo chaguo sahii langu, huyu ananifaa, Nisinge mpata huyu nisinge fanikiwa,amenisahaurisha machungu yangu_* Usipo ona hayo utaona Neno kubwa jeusi kwenye Paji la Uso wake linalosomeka hivi... *"Laiti ningejua Nisinge Mchagua huyu"* Sura hiyo ikisha someka moyoni mwako mtaishi ndani kwa Maigizo bila Matumaini.
_Ndoa ni yako tu haina jirani wa kukubebea, ifanye uonavyo vyema waweza ifurahia_
*By Msaikolojia na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto (Anointed)*
WhatsApp 0755444078
©2019
Saturday, 19 January 2019
AINA ZA MAHUSIANO 5
💝💝 *UKIANZISHA MAHUSIANO HAKIKISHA UNAJUA HATIMA YAKE KWANZA*💝💝
_Uko Nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa na Mwanasaikolojia *Ev Elisha Kazimoto*_
WhatsApp 0755444078
.........
.........
Leo nipo kutibu majeraha ya Stress zisizo za Lazima zinazotengenezwana ukosefu wa Maarifa ya Saikolojia ya Mahusiano. *Special kwa Vijana wakike na wakiume* mlio katika Mahusiano na mtakao anzisha Mahusiano.
✍Unapo anzisha Mahusiano na mtu, jambo la kwanza *Hakikisha unajua haya mahusiano ni ya nini? Hatima yake niya nini?* Kujua ahatima ya Mahusiano yako itakusaidia kujipanga, kupalilia Mahusiano au Kuvunja Mahusiano yasije kukuletea Stress za bure na kuku haribia Sifa,muda na Malengo.
✍Zipo aina za Mahusiano yanayo anzishwa kwa lengo husika, ni muhimu kujua: *Kijana Sikia,Binti tulia kwa makini* usipo kuwa makini Utaishia kuumua na kulaani wakaka au wadada.
1⃣Mahusiano ya Kujioyesha.( *Show up*) _Haya haendi popote ni kwaajiliya yakujionyesha kwawatu kuwa nawe una mtu wa kukuweka busy kimahusiano_
👉Mahusiano ya mitoko zaidi, story nyingi, *I love you* nyingi ila HAKUNA NDOA.
2⃣Mahusiano ya Kutojiamini( *Partial Relationship*) _Mahusiano haya niya kupotezeana muda, mwanzilishi wa mahusiano,au aliye katika uhusiano Hana uhakika kama aliye naye ndo chaguo sahihi lake_ kuna wakati anaonyesha kuwa ndo yeye chaguo,kuna wakati anakuwa na wasiwasi anajivuta kama anataka asitishe ila anakosa namna ya kusitisha. *Mahusiano haya Uishia na ukaa kwenye lugha za I love you tu* hakuna Step yakuonyesha Kuna sehemu tunaekekea,umebaki muda flani tuoane, kila siku nikama ndo naanza Mahusiano.( WAWEZA ZEEKEA HUMUBIKA NDOA) lugha ni nzuri ila vitendo hewa.
3⃣ Mahusiano ya Ngono( *Sexual Relationship*) _Mahusiano haya yanadumu kwa kupena sex,lakini utumika lugha ya tutaoana kwakuwa nimejua uzuri wako,radha yako sitakuacha,lakini ukweli wake, pale mdada anapo onyesha kuhutaji Engagement kijana umzungusha,ndipo vituko uanza hata kukata mawasiliano,matusi ya uzembe wa sex uanza na hamu ya kijana kuingia katika ndoa uisha._ Hapa kama ni kijana atamtumia binti sana ila ndoa atakwepa kwepa.
4⃣Mahusiano ya Kitoto( *Childish Relationship*) _Mahusiano haya wahusika ni kama watoto wanaochezea tope na mikojo,wanatumia gharama,zawadi,muda,kuitana majina ya Mtarajiwa,kuambizana nakupenda lakini wanaweza maliza hata miaka 5 *Hakuna hatua,mipango maalumu inayoonyesha wanaingia kwenye ndoa lini* hawauishia kuachana huku wakipendana baada ya kuona muda unasonga ila hakuna dalili ya ndoa._
5⃣Mahusuano ya Ndoa ( *Marriage Relationship*) _Haya ni Mahusiano muhimu,yenye mipango,yenye malengo,yenye heshima,yenye kulinda hisia,yenye kulinda heshima,na yenye kumtanguliza Mungu_ Hapa muhusika Kijana *Utoa mwelekeo wa kuekekea ndoa* uonyesha harakati za michakato mahususi ya kuingia katika ndoa. Wakati huo huo mdada umtia moyo mwenzake,na kumwonyesha ushirikiano wa namna inavyowezekana kuifikia ndoa.
*_Kwenye Mahusiano haya wote wanakuwa wanataarifa wako wapi,wafanye nini na lini wanaingia kwenye ndoa_* wanakuwa na ujasiri wote wakuelezea Uhai wa mahusiano yao na Nia yao, mawasiliano yao yako juu.
NB: _Ukiona unapata ukakasi,utata wa kuelezea uhai,uimara wa mahusiano yako, jua mahusiano yako hayapo no 5,yatafute no 1 hadi 4._
*_Ulikuwa nami mchambuzi wa masuala ya Mahusiano na ndoa Mwanasaikolojia Ev Elisha Kazimoto(Anointed)_*
WhatsApp 0755444078
©2019
Wednesday, 16 January 2019
KUOANA NA MROMANI HAPANA
ππ *Swali: Me nilikuuliza kwamba ni sahihi mfano mtu kama mim nimkristo niliye okoka kuolewa na mroma au katoliki namaanisha*ππ
........
........
Anajibu Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto(Anointed)*
WhatsApp 0755444078
*SWALI LA WAZI LA KIIMANI NAMI NITALIJIBU KWA WAZI KIIMANI SIKISAIKOLOJIA*
_Wapendwa kuna wimbi kubwa na la kutisha katika kizazi cha sasa cha KUPANDIKIZA MACHOTARA wa Kiroho(Spiritual Mulattoes) Negro Christians who has double sides in faith, because of seeking Marriage_ sasa nitegee sikio nijibu kwa uwazi mkubwa sawa sawa na muuliza swali alivyo uliza.
π Note: Sipo kukwambia dhehebu lako ni mbaya au ni nzuri, ila ni uchambuzi wa swali kwa Kadri ya muuliza swali ila kupitia uchambuzi huu waweza PONA na ukasimama na Mungu.
*Fuatana nami Mchambuzi Ev Elisha Kazimoto(0755444078)* Utaweza kufunguka na kupata ufahamu juu ya maamuzi yako.
1⃣Kwanza tuelewe ( *Wale mliookoka, si kwa usanii na kivuli*) Ndoa ni Mpango wa Mungu na mwanzilishi ni wa ndoa Ni Mungu mwenyewe ndiye anayetoa KIBALI cha kuoa au kuolewa tukimwomba,tukikaa sawa naye... Siyo harakati zetu za kujitafutia mtu tunayeoana anaweza timiza ndoto zetu za maisha, Ila _Mungu anatupa mtu wa kutimiza kusudi lake kwenye maisha yetu._
18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanzo 2:18
ππ Mungu ndo wa kwanza kuoana Uhitaji wa ndoa kwa mwanadamu,si mwanadamu kuona uhitaji wa ndoa kabla ya Mungu ( *Hapo ndo tunaingiaga kwenye mfumo wa zoazoa yoyote*) ilimradi Anaweza kidhi Matarajio yako si Mapenzi ya Mungu ( *Ndo chimbuko la kuzoa Imani nyingine tofauti na yako, au kuiacha imani yako ili uoe au uolewe*)nayo hii ni Laana ya Kizazi cha sasa.
2⃣Pili,Mungu kusema atafanya msaidizi wa kufanana naye alikuwa anamaana kubwa ya kiroho na kiusalama, kuepusha mgongano wa Kiimani,Kufyonzwa nguvu za kiroho, Kuiandama miungu mingine badala ya Mungu aliye hai, Kuepusha kuzaa Machotara wa Kiroho wasio na upande wa kusimamia kiimani.
*_Kauli ya Mungu tangu zamani ni kutembea na kubariki watu watakao weza kuwafundisha watoto wao Imani ya Mungu wao Mungu wa Isaka na Yakobo_* sasa ninyi mlio imani Tofauti by NATURE mtawarithisha watoto wenu nini?
siku ile uliyosimama mbele za Bwana wako huko Horebu, Bwana aliponiambia, Nikusanyieni watu hawa, nami nitawasikizisha maneno yangu, ili wajifunze kunicha mimi siku zote watakazoishi duniani, wakapate na kuwafundisha watoto wao.
Kumbukumbu la Torati 4:10
ππ Si kwamba tunakataa Kuoana na Imani zingine kwasababu ya dhehebu,kwasababu ya uimbaji na kucheza ni *Kwa Maslahi ya Imani yako na watoto wako* Kama wazazi mna mashina mawili tofauti ya Imani,nani atawafundisha watoto niia ya Bwana? Wakati Malezi ni ya Pande mbili baba na mama walio mwili mmoja? Wakati kila mmoja wenu anaona imani yake ndo bora?
πBiblia imesema mlee mtoto katika njia ipasayo naye hata iacha hata atakapo kuwa mzee... Sasa mnalea mtoto kwa Imani ipi( kulingana na muuliza swali *Imani ya Kipentekoste/Kilokole au Kiromani?*) au unataka kusema mmoja ataamua kubadirika kumfuata mwingine... Kubadiri Imani kwaajili ya ndoa ni sawa na Kupata mtiani mark 10% wewe ukajiongezea 0 ikawa 100% halafu ukahisi umewin....kwenye karatasi watakaoona wataona umewin sana ila KIMANTIKI akilini mwako kuna 10% shida ni pale utakapo kuja mtiahani wa Taifa usio badorishwa, usiorudishiwa karatasi ndo 10 yako itaonekana,na utakuwa umefyonzwa akili na ujinga wa kujilewesha na kujidanganya haitakuwa 10 tena ila 05% na hapo ndo utahisi Maumivu makubwa na hasara kuliko maumivu na hasara ulizo kwepa darasani kupokea karatasi ya mark 10 na kutafuta kwa nini nimepata 10? Ukarekebisha ili upate 100 ya uhalali.
π *KIIMANI si sahihi wewe uliyeokoka,kuolewa/Kuoa Mromani wala Mromani Si sahihi wewe kuoa au kuolewa na Mlokole au mtu wa imani ya Kipentekoste unaichafua imqni yako na utazalisha NEGROES na utakutana na shida kubwa katika ndoa* kwa nini ni kwasababu ninyi wawili Misingi ya imani inayofautiana mbali sana, na Biblia imesema hivi, wasiopata wataendaje pamoja?
3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?
Amosi 3:3
ππ Hebu tujiulize na wewe uliye uliza swali..maswali haya machache:
1⃣Mromani anaamini na anaomba maombi kupitia kwa Mama wa Yesu Mariamu( Sala ya mama wa Mungu utuombee) *Ukitafuta kwenye Biblia hakuna mawasiliano kati ya aliye kufa na aliye hai* (Lakini Biblia imesema Wazi mwombezi wetu wanadamu Ni Roho Mtakatifu) (Imani ya Kipentekoste inaamini hivyo)
26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Warumi 8:26
ππHapa kuna shida kubwa, mtasimamaje pamoja kumwita Mungu juu ya ndoa yenu,watoto,mipango yenu na kupambana na nguvu za giza? Huyu anaombewa na Mariamu mama wa Yesu huyu anaombewa na Roho mtakatifu......(Jibu inabidi turudi kwenye Biblia mwongo wa Kikristo nani anastahili kuomba,na nani mwombezi).
2⃣Imani ya Romani *Haiamini kama kuna Kuokoka hapa Duniani* inaamini mtu akifa ndo anaokoka ndo anakuja kupewa Cheo cha Mtakatifu flani baada ya kupitia katika hatua kadha wa kadha...anatunukiwa cheti cha mtakatifu alisha kufa zamani.. Na Imani ya Kipentekoste kwa Mujibu wa Neno la Mungu Tunaamini wokovu ni hapahapa duniani wakati bado uko hai.
3 Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Zaburi 16:3
ππHilo ni miongoni mwa maandiko mengi sana yanayo zungumzia watakatifu wapo duniani siyo waliokufa, kama kuna waliokufa ni watakatifu sawa nao niwatakatifu ila si kwamba wanafanywa watakatifu baada ya kufa, Neno la Mungu linamuhusu Aliye hai ndo maana anasema *Kumcha Bwana ni kuchukia uovu Mithali 8:13* Marehemu hachukii uovu hivyo amchi Bwana,kama hakumcha akiwa duniani huyo No more time. *Msingi wa Kipentekoste ni kusisitizia utakatifu wa maisha yako ukiwa hapa duniani ndo Vasi lako la kujiandaa kumuona Bwana* Sasa hii si Imani ya Romani mtaishije watu mnaotofautiana mtazamo na Imani?
14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
Waebrania 12:14
ππImani ya Kipentekoste inaamini andiko hilo na kulitendea kazi, lakini Imani ya Romani inasema ni Uongo, Huwezi kuwa Mtakatifu ukiwa Duniani hapa, wanasahu na *Wafilipi 4:13, inayosema Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu* lakini nenda ukasome mwenyewe *YOHANA 5:1-15* Uone nguvu ya utakatifu tunaitoa wapi.
3⃣Mromani anaamini *Sala kwa aliyekufa na kutolewa sadaka kuhamishwa kutoka kwenye mateso na kupokelewa na Mungu hata kama alikufa kwenye dhambi* Imani hii wapentekoste Haipo, Wapentekoste(Walokole wanaamini katika andiko la *Waebrania 9:27, linalosema baada ya kufa ni hukumu* hakuna sadaka wala sala za kubadiri nafasi ya marehemu kama ni mwenye dhambi motoni,mwenye haki mbinguni...Sasa mnaoana ili muandaaneje kwenda kwa Bwana mbinguni.?
4⃣Mromani anaamini Kumbatiza mtoto mdogo kwa kumwondolea dhambi ya asili, lakini Imani ya Kipentekoste inaamini ubatizo ni kwa mtu mzima, aliyekiri kwa kinywa chake na kumpokea Yesu moyoni mwake ndoa anabatizwa.(Kwa lugha nyingine inaanza Toba ndo unafuata ubatizo kwa mtu mzima mwenye akili timamu)
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Matendo ya Mitume 2:38
ππSasa watoto wenu watafuata ya nani,? *_Haya ni baadhi katika uchambuzi huu,ila Hatushauri na Hakuna kusudi la Mungu la Kuoana watu wa Imani tofauti. Huo ni Ukengeufu na Upagani wa yule anaye jihita Ameokoka maana yeye Anaijua Kweli yote,ika anajifanya hajui_*
πKuna Biashara ya UTAPELI ya kuokokeshana ili muoane kwa mwenye Maarifa ya Kimungu hatufanyi hiyo biashara isiyo zaa kununua Samaki aliye China ila unasema nitambanika na kumwekea vitunguu na nyanya nyingi nipoteze harufu, Haina shida Gharama zako,usumbu wako,harufu yako, hasara yako...muuzaji hana shida shida ni wee mlaji, Sisi tunanunua Samaki Fresh *Na tunamchunguza sana mpaka kwenye masikio, ili tusiingie hasara na gharama zisizo tarajiwa,huku tumetoa pesa yetu* Kama umeelewa mfano huu uheri. Ukitaka kufanya utapeli mwambie okoka tuoane sawa, yakiwabana,mkivurugana, yakikushinda kwani sisi Tuna hasara gani, kwani Mungu ana hasara gani, kwani utakapo kuwa unazunguka kwenye Maombezi na kuandika Vikaratasi vya kuombea ndoa yako, mmeo au mkeo au watoto wako, gharama tutakuwa tunatoa sisi Wahubiri, mkifukuzana kwenye ndoa ukarudi kwenu au mke akakuacha kwani Sisi tunaumia nini? Si ulichagua? Sometimes sisi wahubiri tunapambana sana kuvaa uhalisia wa wahuni tunaumia, Ukweli uko pale pale Ndoa ni yako, yakikushinda ni wewe ulichagua, Mungu niwademokrasia anasema CHAGUA, ila yeye anakushauri chagua Uzima ukichagua mauti Kufa umetaka mwenyewe. Ila hatutaacha kusema kweli.
*_NB: Kuchelewa kuolewa,au kuoa Siyo sababu ya Kuzoa Yeyote, Ghara ya kukwepa kuvumilia muda wa Mungu ulimgharimu Ibrahimu na Sara akazaa na Kijakazi, imetuletea shida mpaka sasa duniani kisa nimechelewa, umechelewa Unajua utaishi miaja mingapi? Unajua sababu ya kucheleweshwa? Vumilia pate mema ya Mungu_*
Nadhani nimejibu swali la muuliza swali mchambuzi alikuwa:
*Psychologist & Counselor Ev Elisha Kazimoto(Anointed)*
WhatsApp 0755444078
©2019