Monday, 26 June 2017

MWANAMKE UNALETA MTIKISIKO GANI

🌈 *MJENZI LAZIMA AWE MTU ANAYETUMIA AKILI SANA*🌈
   *_Semina Ya Wamama_*
       ( *Ev Elisha Kazimoto*)
     WhatsApp      0755444078
*UTANGULIZI WA SOMO KATIKA SEMINA YA WAMAMA*
🏹 _Mwanamke Akiingia katika eneo lolote lazima yatokee mabadiriko makubwa yenye kutikisa maisha au mazingira._
1⃣ Hawa alipoingia kwa Adamu alisababisha kubarikiwa kwa baraka za kuongezeka( *Mwanzo 1:27-28*)
2⃣Hawa alipokosea alisababisha laana kubwa dunia nzima ( *Mwanzo 3:9-19*)
3⃣Delila alipoingia kwa Samsoni alifuta Utumishi wote na Unadhiri wa Samsoni kwa Mungu ( *Waamuzi 16:18-22*)
_Yako maeneo mengi yanayoonyesha uhusikaji wa mwanamke eneo lolote umeleta mtikisiko mkubwa ulio mzuri au mbaya_ *_wengine ni kama Mariamu kukubali kumzaa Yesu. Ikaleta wokovu duniani, Abigaili Kutuliza hasira ya mfalme Daudi juu ya mmewe Nabali na familia yote, Rahabu kuwaficha wapelelezi kafanikisha zoezi la upelelezi na kuokoa nyumba yake_* Hapa Swali la Msingi ni _WEWE MWANAMKE UNAPO HUSIKA KATIKA NDOA,FAMILIA NA KANISANI KWAKO UNALETA MTIKISIKO GANI? WA MAUTI AU UZIMA NA BARAKA?_
🏹 *Sasa tuanze kwa kuangalia Umuhimu na nafasi ulizopewa mwanamke kwa mujibu wa Biblia*
_Haleluya wamama Watumishi wa Kristo,mliopewa vyeo vingi na na Mungu katika Biblia kuonyesha uhalisia wenu. Mnaitwa Jeshi kubwa *Zaburi 68:11* Mnaitwa Wajenzi wa Nyumba/Ndoa *Mithali 14:1*, Mnaitwa Mke Mwema *Mithali 31:10*, Mnaitwa Msaidizi, *Mwanzo 2:18* Mnaitwa Walinzi, *Yeremia 31:22, Mnaitwa Waombolezaji *Yeremia 9:17-21* hizo zote na nyingine ni lugha za Kimungu zinazo tambulisha uhalisia,uwezo na sifa ya Mwanamke Aliye kusudiwa na Mungu katika *Familia, Ndoa na Kanisani* kama akikaa katika Nafasi yake Kwa Akili_
🌈🌈 *Andiko Kuu La Somo*🌈🌈
     *LUKA 14:25-32*
25 Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, 

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? 

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, 

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. 

31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? 

32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali. 
_Katika Andiko kuu kuna vipengele kama 7 tutakavyo simamia katika Uchambuzi wa Somo letu la *Mjenzi (Mwanamke)Anahitaji kutumia Akili sana* ili tuweze kunusurisha Kanisa la Mungu, Familia zetu, Ndoa zetu,Uhai wetu na Maisha yetu ya kiroho_
1⃣ *Maamuzi yako kwa yale unayo yafuata kuyatimiza* ( mstr 26)
2⃣ *Mzigo ni wa maisha niwa kwako tu*(mstr 27)
3⃣ *Muda wa Kutafakari Hatima yako kama kuna faida katika maamuzi yako* (mstr 28)
4⃣ *Wanaokuzunguka wanakutafsiri vipi kwa maisha hayo ulochagua*( mstr 29)
5⃣ *Udhaifu wako utakapo julikana na watu, utakuwa na nguvu za kuendelea mbele?*(mstr 30)
6⃣ *Una ufahamu juu ya Adui yako unayepambana naye asiharibu hatima yako?*(mstr 31)
7⃣ *Jipime uwezo wako kabla ya maamuzi*(mstr 32)
🎸 Kuna mambo unahitaji ufunuliwe au ufundishwe na watu waliofunuliwa siri hiyo ndo ufanikiwe katika hayo, zaidi ya hapo utajiona ni mtu usiye na faida duniani( *Zaburi 32:8*)
🎸 Wanawake adui amewaondoa kwenye Msingi wa uhalisia wao, baada ya kugundua ni Wadhaifu wa Kutumia Akili Ipasavyo katika kujenga maisha yao ya kiroho,ndoa na familia
*_1 Wakorintho 15 : 34 - Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe._*
🎸Maadui(wachawi na shetani na mapepo yake) ili waharibu kiroho chako,familia yako au ndoa yako (kwako wewe mwanamke)ni kuchezea akili zako(kukudanganya)
*_2 Wakorintho 11 : 3 - Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo._*
🎸 *Sifa kubwa* ya mwanamke mwenye Akili(Maarifa)Kibiblia Ni mwanamke mwenye _uwezo wa Kujenga Nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe_( Akili +Juhudi binafsi)kusababisa raha katika Nyumba( yaani Mkusanyiko wa watu, tangu *Ndoa yake, familia-watoto na Kanisa*)
*_Mithali 14 : 1 - Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe._*
🎸AKILI; Ni uwezo wa kufanya Maamuzi Sahihi yenye faida kwako(kukunufaisha) kwa lugha nyingine *_Mwanamke yeyote anaye fanya maamuzi yenye kumletea Hasara kiroho, kihuduma na katika ndoa, huyo Hana Akili Kabisa_* ni sawa na mtu Aziniye (mwanaume aziniye na mwanamke)
*_Mithali 6 : 32 - Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake._*
🎸🎸 *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* Ni Yule anaye jua kuwa Maisha Safi,au ya Shida, Dhiki, Raha ni yake na familia yake tu, wala haya muhusu rafiki yake au adui yake.
🎸🎸🎸 *Mwanamke mwenye Akili yakujenga hatima yake* Ni yule anaye jiuliza maswali ya kiroho,kimwili na kisaikolojia,kuwa kama mambo yakiniharibikia anayeumia ni nani, au ya kinyooka anaye faidika ni nani.(Ndipo anachukua maamuzi yakutenda au kuacha)
🎸4⃣ *Mwanamke mwenye akili ya kujenga hatima yake* Ni yule anaye tafsiri nguvu ya maamuzi yake itakavyo athiri nyumba yake,kanisa la Mungu na kupitia hiyo Mungu atainuliwa au atashushwa.
🎸5⃣ *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* anauwezo wa kuzuia madhaifu yake,ya familia yake na ndoa yake yasijulikane na mtu wa nje mpaka ayamalize mwenyewe.
🎸6⃣ *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* Ni yule mwenye Uwezo wa Kubainisha Maadui zake kutoka katika marafiki zake na kuwadhibiti.
🎸7⃣ *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* Ni yule anaye tambua udhaifu wake na uwezo wake, na akadhibiti udhaifu wake usiathiri maisha yake
❌❌ *ALAMA ZA WANAWAKE WACHAWI WACHANGIAO KUBOMOA NDOA YAKO NA TABIA YAKO NA KIROHO CHAKO*❌❌
1⃣ _Wanapenda kukuaminisha kuwa wao ni marafiki wazuri kuliko waleulokuwa unawaona ni rafiki zako_
2⃣ _Wanapenda Kusimulia udhaifu wa mchungaji na mama mchungaji na viongoziwa kanisa_
3⃣ _Wanahitaji mambo ya siri siri, hawatendi mambo yao uhuru, mpaka wajifichefiche_
5⃣ _Wanapenda Kusimulia madhaifu tu ya waume zao na kuyahusianisha na ya mme wako_
6⃣ _Ni washauri na wahimizaji wa kumfanyia mmeo vitendo vya ukomoaji kama kumnyima tendo la ndoa_
7⃣ _Wanapenda kutengeneza vikosi makanisani kwa lengo la kuwaumiza wengine wanao wachukia_
8⃣ _Wanapenda kujadiri kila ujumbe na matangazo kanisani kwa lugha ya Leo alikuwa anamuongelea mtu flani_
9⃣ _Wanapenda kumteka mtu kwa zawadi tata(za ovyo)_
🔟 _Wakitafuta kukuingiza katika kundi la kichawi kanisani ukagoma wanatengeneza genge la kukuchukia milele.
*_Ukiwa mwanamke mwenye ndoto za kwenda mbinguni,kumtumikia Mungu,kuwa na ndoa nzuri, jipange kuamua kutumia Akili vizuri katika maisha yako. Ulikuwa nami mchambuzi wa masuala ya Kisaikolojia,Mahusiano na Ndoa, Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve) WhatsApp 0755444078_*

Saturday, 24 June 2017

MJENZI UTUMIA AKILI SANA

🌈 *MJENZI LAZIMA AWE MTU ANAYETUMIA AKILI SANA*🌈
   *_Semina Ya Wamama_*
       ( *Ev Elisha Kazimoto*)
     WhatsApp      0755444078
_Shalom wamama Watumishi wa Kristo,mliopewa vyeo vingi na na Mungu katika Biblia kuonyesha uhakisia wenu. Mnaitwa Jeshi kubwa *Zaburi 68:11* Mnaitwa Wajenzi wa Nyumba/Ndoa *Mithali 14:1*, Mnaitwa Mke Mwema *Mithali 31:10*, Mnaitwa Msaidizi, *Mwanzo 2:18* Mnaitwa Walinzi, *Yeremia 32:21*, Mnaitwa Waombolezaji *Yeremia 9:17-21* hizo zote na nyingine ni lugha za Kimungu zinazo tambulisha uhalisia,uwezo na sifa ya Mwanamke Aliye kusudiwa na Mungu katika *Familia, Ndoa na Kanisani* kama akikaa katika Nafasi yake Kwa Akili_
🌈🌈 *Andiko Kuu La Somo*🌈🌈
     *LUKA 14:25-32*
25 Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, 

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? 

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, 

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. 

31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? 

32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali. 
_Katika Andiko kuu kuna vipengele kama 7 tutakavyo simamia katika Uchambuzi wa Somo letu la *Mjenzi (Mwanamke)Anahitaji kutumia Akili sana* ili tuweze kunusurisha Kanisa la Mungu, Familia zetu, Ndoa zetu,Uhai wetu na Maisha yetu ya kiroho_
1⃣ *Maamuzi yako kwa yale unayo yafuata kuyatimiza* ( mstr 26)
2⃣ *Mzigo ni wa maisha niwa kwako tu*(mstr 27)
3⃣ *Muda wa Kutafakari Hatima yako kama kuna faida katika maamuzi yako* (mstr 28)
4⃣ *Wanaokuzunguka wanakutafsiri vipi kwa maisha hayo ulochagua*( mstr 29)
5⃣ *Udhaifu wako utakapo julikana na watu, utakuwa na nguvu za kuendelea mbele?*(mstr 30)
6⃣ *Una ufahamu juu ya Adui yako unayepambana naye asiharibu hatima yako?*(mstr 31)
7⃣ *Jipime uwezo wako kabla ya maamuzi*(mstr 32)
🎸 Kuna mambo unahitaji ufunuliwe au ufundishwe na watu waliofunuliwa siri hiyo ndo ufanikiwe katila hayo, zaidi ya hapo utajiona ni mtu usiye na faida duniani( *Zaburi 32:8*)
🎸 Wanawake adui amewaondoa kwenye Msingi wa uhalisia wao, baada ya kugundua ni Wadhaifu wa Kutumia Akili Ipasavyo katika kujenga maisha yao ya kiroho,ndoa na familia
*_1 Wakorintho 15 : 34 - Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe._*
🎸Maadui(wachawi na shetani na mapepo yake) ili waharibu kiroho chako,familia yako au ndoa yako (kwako wewe mwanamke)ni kuchezea akili zako(kukudanganya)
*_2 Wakorintho 11 : 3 - Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo._*
🎸 *Sifa kubwa* ya mwanamke mwenye Akili(Maarifa)Kibiblia Ni mwanamke mwenye _uwezo wa Kujenga Nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe_( Akili +Juhudi binafsi)kusababisa raha katika Nyumba( yaani Mkusanyiko wa watu, tangu *Ndoa yake, familia-watoto na Kanisa*)
*_Mithali 14 : 1 - Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe._*
🎸AKILI; Ni uwezo wa kufanya Maamuzi Sahihi yenye faida kwako(kukunufaisha) kwa lugha nyingine *_Mwanamke yeyote anaye fanya maamuzi yenye kumletea Hasara kiroho, kihuduma na katika ndoa, huyo Hana Akili Kabisa_* ni sawa na mtu Aziniye (mwanaume aziniye na mwanamke)
*_Mithali 6 : 32 - Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake._*
🎸🎸 *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatia yake* Ni Yule anaye jua kuwa Maisha Safi,au ya Shida, Dhiki, Raha ni yake na familia yake tu, wala haya muhusu rafiki yakeau adui yake.
🎸🎸🎸 *Mwanamke mwenye Akiliyakujenga hatina yake* Ni yule anaye jiuliza maswali ya kiroho,kimwili na kisaikolojia,kuwa kama mambo yakiniharibikia anayeumia ni nani, au ya kinyooka anaye faidika ni nani.(Ndipo anachukua maamuzi yakutenda au kuacha)
🎸4⃣ *Mwanamke mwenye akili ya kujenga hatima yake* Ni yule anaye tafsiri nguvu ya maamuzi yake itakavyo athiri nyumba yake,kanisa la Mungu na kupitia hiyo Mungu atainuliwa au atashushwa.
🎸5⃣ *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* anauwezo wa kuzuia madhaifu yake,ya familia yake na ndoa yake yasijulikane na mtu wa nje mpaka ayamalize mwenyewe.
🎸6⃣ *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* Ni yule mwenye Uwezo wa Kubainisha Maadui zake kutoka katika marafiki zake na kuwadhibiti.
🎸7⃣ *Mwanamke mwenye Akili ya kujenga hatima yake* Ni yule anaye tambua udhaifu wake na uwezo wake, na akadhibiti udhaifu wake usiathiri maisha yake
❌❌ *ALAMA ZA WANAWAKE WACHAWI WACHANGIAO KUBOMOA NDOA YAKO NA TABIA YAKO NA KIROHO CHAKO*❌❌
1⃣ _Wanapenda kukuaminisha kuwa wao ni marafiki wazuri kuliko waleulokuwa unawaona ni rafiki zako_
2⃣ _Wanapenda Kusimulia udhaifu wa mchungaji na mama mchungaji na viongoziwa kanisa_
3⃣ _Wanahitaji mambo ya siri siri, hawatendi mambo yao uhuru, mpaka wajifichefiche_
5⃣ _Wanapenda Kusimulia madhaifu tu ya waume zao na kuyahusianisha na ya mme wako_
6⃣ _Ni washauri na wahimizaji wa kumfanyia mmeo vitendo vya ukomoaji kama kumnyima tendo la ndoa_
7⃣ _Wanapenda kutengeneza vikosi makanisani kwa lengo la kuwaumiza wengine wanao wachukia_
8⃣ _Wanapenda kujadiri kila ujumbe na matangazo kanisani kwa lugha ya Leo alikuwa anamuongelea mtu flani_
9⃣ _Wanapenda kumteka mtu kwa zawadi tata(za ovyo)_
🔟 _Wakitafuta kukuingiza katika kundi la kichawi kanisani ukagoma wanatengeneza genge la kukuchukia milele.
*_Ukiwa mwanamke mwenye ndoto za kwenda mbinguni,kumtumikia Mungu,kuwa na ndoa nzuri, jipange kuamua kutumia Akili vizuri katika maisha yako. Ulikuwa nami mchambuzi wa masuala ya Kisaikolojia,Mahusiano na Ndoa, Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve) WhatsApp 0755444078_*

Sunday, 18 June 2017

UNAJIITA MADAM KUMBE UMEACHIKA!

🏹🏹  *ACHA UTAPELI WA KUJIFICHA KANISANI KUMBE ULISHA ANGUKA KIROHO*🏹🏹

( *_Kujiita Madam/Kaka kumbe Ulishaachika kwenye Ndoa_*)

      Ev Elisha Kazimoto

        *0755444078*

⛱ _Shalom watu wa Mungu mnaoitazamia Mbingu takatifu zilizo wekwa tayari kwa *walio jikana na watakatifu*_ leo napenda nizungumze na wana ndoa na wana ndoa watarajiwa kuhusu kamchezo kakitapeli kanako anza kuchomoza kutoka juu kwa *_Watu Maarufu_* kanisani mpaka watu wakawaida sana ndani ya kanisa( *_Kamchezo  hako kakitapeli kanisani ni Watu kuwaacha Wenzi wao(Mke wake/mme wake)na kujipachika Jina Feki la MADAM/KAKA....._* Kutengeneza Dili la kukwapua kiurahisi kijana wa watu,au binti wawatu kiurahisi. (Acha UTAPELI wewe ni Nyoka hatari ambaye watu wote imewapasa wakukimbie na sumu yako kali yakufisha).

*_Mathayo 19 : 9 - Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini._* 

⛱ Wewe mwanamke au mwanaume unayeachana na mwenzako unatumia Biblia gani?Ukristo wa wapi huo wa kiongozi gani huyo(mmeligeuza kanisa Taasisi ya siasa ya kuoa na kuacha, kama vyama vya siasa,leo chama hiki kesho kile)acheni utapeli wewe ni *Mzinifu Mkubwa* mwana wa Jehanamu wewe.

⛱Umeachana na mmeo na kujiita *Madam* madam wa wapi, mbona hutulii bado unawavulia nguo vijana,wanaume? Unahisi umaarufu wako au unyonge wako unakupa tiketi ya *Kutuchafulia Sura na Vazi la Wokovu wetu?* Jehanamu ya moto inakungoja(mbinguni hakuna umaarufu wa pesa,uimbaji na ma CD yako au uinjilisti wako au Utume na Unabii wako)

⛱Unaacha mkeo eti Mungu amekuongoza umuoe mwingine, hivi wewe unajua Ndoa mbele za Mungu, wewe ni *Mzinifu tu kama wengine* unatumia biblia gani? Acha KUJIFICHA Nyuma ya mwavuli ⛱⛱⛱⛱wa huduma eti mimi nabii mtume,mwimbaji *wee jambazi hatari katika mwili wa Kristo* na leo nakupiga kwa mawe mpaka uache utapeli huo kwa jina la Yesu.

*_1 Wakorintho 7 : 10 - Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe;_*

⛱Wokovu wetu una kanuni siyo kirabuni. Kwa nini unaachana na mwenzako? Mnaachana kwa misingi ya kimaandiko au mnaachana kwa misingi ya uhuni wako,kiburi chako ,tabia zako na uzembe wako mbele za Mungu mpaka shetani amewalipua?

⛱Haya umeaua kuachana na mwenzako unaouwezo wa *Kuilinda imani na uaminifu wako kwa Mungu usioe tena au kuolewa tena au kuwaka tamaa?* mbona baada ya kuachana na mwenzako _Unaanza kuruka fensi? Unalala na vijana vidogo vidogo kama watoto wako au wadogo zako?mbona unaangaika kuchumbia na kujirahisisha kwa wanaume? Umri wako wewe ndo wa kujirahisisha kwa vijana vidogo?wee ulishaanguka zamani, nisawa na gari bovu limesimama kumbe haliwezi kuwaka_

*_1 Wakorintho 7 : 11 - lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe._*

⛱Na ninyi *Wachungaji vipofu,mitume wenye njaa,manabii wahuni* unamfungishaje ndoa huyo Jambazi wa kike/kiume madhabahuni patakatifu Kwa Biblia ipi,andiko lipi huku ukijua huyu amevurunda kwa mme wake /mke wake?au njaa?umefungisha ndoa maskini wangapi wa aina hiyo?au unahisi Biblia inapendelea? *_Na wewe ni mtumishi Hewa tu, njaa tu, rudi msalabani_* lakini hii inatuonyesha jinsi gani Madhabau yako ni Feki, Chafu, na Ovu. Simamia kweli ya Kristo ulilinde kundi.

⛱ *_Hivi nawewe unayeoa aliyeachwa na mwenzake kwa vijitabia vyake na wewe ni mbovu, utaachwa vilevile_* jiulize kilicho mtoa kule siyo umalaika wake ila ni ushetani wake(kama ameachana na mwenzake na kuoa au kuolewa bila kuzingatia kanuni za Biblia)jua *_umeoa au olewa na jambazi lililo jeruhiwa_* ni pole sasa ila majeraha yakipona hata kama ni miaka 5, 10 baadaye litakunyonga na wewe.

*_Mithali 17 : 11 - Mtu mwovu hataki neno ila kuasi tu; Kwa hiyo mjumbe mkali atatumwa kwake._*

⛱Makanisani kumekuwa kimya, leo Mimi kama Mjumbe mkali nimetumwa kwako, wala sina haja ya unipende au unichukie,ila ujumbe umefika, *Wewe Ni mzinifu,Tapeli na Jambazi kubwa la Kiroho kanisani* unajifichia kwenye unaarufu wako wa Kuimba, Utume,Unabii,uchungaji mbinguni na jehanamu hakuna umaarufu huo, wala hutukomoi sisi, humkomoi mmeo au mkeo,unajikomoa, kufa utakufa na jehanamu utaingia na ma CD yako ya nyimbo mpya unatunga kila siku na kuhubiri redioni utaviacha uende uchomeke peke yako.( *Wala sikuhukumu ila wewe na matendo yako ndo yanakuhukumu*) hauna la kujitetea.....

⛱ Ooho mimi huyu kwanza hatukufunga ndoa Kanisani tulioana hivi hivi(kwanza viapo ni vya wanadamu), Acha uhuni umemzalisha/mzalia watoto wa ngapi. Ulipo kuwa unafunua utupu wake ulikuwa hujui kuwa unamfunua lakini hamjafunga ndoa? *Acha uhuni wako* 

⛱Eti huyu mwenzangu simuelewi,yaani mkorofiii mi namuacha, kwani kuna aliye kutongozea huyo,si ulioana naye kwa mbwembwe? Kaa naye huyo rudi kwa Mungu umwombee akae sawa, *Acha kuharibia wenzako* walio safi wanamtaka huyo,wenye haki za kumuoa au kuolewa naye kwa kanuni za kibiblia.

⛱Oooho tangu tuoane ni vurugu tupu, naona siyo mapenzi ya Mungu, *Wee tapeli tu na muhuni* mapenzi ya Mungu unayaona leo baada ya mapenzi kugeuka shubili kaa kwenye jehanamu hiyo uloingia kwa kupenda na tamaa zako.

⛱⛱ *_Ninyi wana ndoa Majambazi mnao oana na kuachana msituharibie vijana wetu, mnabadirisha taratibu na kuondoa mipaka ya Wokovu taratibu, angalia neno hili( Mithali 22 : 28 - Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani, Uliowekwa na baba zako._*) sasa vijana wanaoana na yeyote kwa kisingizio akileta za kuleta na piga chini, miaka 2 najiita *_MADAM..../KAKA..... Halafu nazoa mwingine_* mshindwe, acheni wokovu mrudi duniani kwenye ukahaba na uhuni ijulikane moja kuliko kutuchafulia upepo na sura ya wokovu tuloupokea kwa gharama kubwa msalabani. Huu ndo msimamo wa Biblia 

*_Kutoka 19 : 12 - Nawe utawawekea mipaka watu hawa pande zote, ukisema, Jihadharini, msipande mlima huu, wala msiuguse, hata mapambizo yake; kila mtu atakayeugusa mlima huu, bila shaka atauawa._*

_Ukiyajua hayo ni Heri ukiyatenda, Ulikuwa na mimi Mjumbe Mkali kwa Wahuni( *Mithali 17:11*) 

            *_Ev Elisha Kazimoto (Baba Eve)_*

      *0755444078*

                 ©2⃣0⃣1⃣9⃣

Saturday, 10 June 2017

BUDGET KATIKA FAMILIA

🏹🏹 *BUDGET KATIKA FAMILIA NA UTATA WAKE*🏹🏹
    _Swali linasema hivi,:wew ni mwanamke mna familia wew na mumeo wote ni wafanyakaz,unajitoa sana na pesa za mshahara kufanya maendeleo makubwa ila unapotumia pesa ya mumeo kwa ajili ya matumiz ya nyumban anagomba sana hata kama ni elfu mbili na unakuta umemueleza kabisa?!!!je mke afanyej kuinusuru ndoa yake?_
🏹Hapa kuna vitu vya msingi vya kuvitazama sana katika ndoa ya watu wa aina hii. *_Kwanza kuna shida ambayo hawakuiweka sawa kipindi cha Uchumba_* maana kipindi cha uchumba ndipo tunaweka sawa mambo ya kifamilia( *Mfumo wa kupata watoto interval, mfumo wa kiuchumi mtakao tumia kuimarisha uchumi wa familia yenu, kama wote niwafanyakazi, mnatumiaje pesa zetu maana hiyo ndo Income yenu* kwa hiyo mkikosea kuzungumza kipindi cha Uchumba mifumo ya maisha yenu mtakavyo iendesha jua huwezi kukwepa migogoro na changamoto nyingi latika ndoa kaa sababu mnaingia kwenye mkataba wa ndoa mkiwa na mawazo tofauti sasa kuyafanya yawe mawazo sawa maana yake(Mnahitaji kipindi cha Uchumba kingine lakini ndani ya ndoa)jambo ambalo ni gumu pia kulifanya kwa ubora ila lazima mlifanye kwa mstakabari wa ndoa yenu(muda wa mazungumzo)
Ndo maana kipindi cha ucumba kikawekwa na kikashauriwa kisiwe chini ya miezi 6 na kisizidi miaka 3, kwa malengo kwamba wachumba wapate muda wa kuwekana sawa katika tofauti, na kama hakuna makubaliano ndo maamuzi ya Break up uchukuliwa(Maana ndoa ni mkataba wa kudumu)kama utaingia bila maridhiano jua ndo mwanzo wa migogoro isiyo isha.
🏹 Pili,  *Aina ya ndoa*  katika suala la Budget ndani ya familia ubora na mtafuruko katika familia unaweza tokana na Aina ya Ndoa, Ndoa nyingi zilizo pitia *Process 4 zza ndoa*ara nyingi shida hii huwa ni ndogo,au hakuna( Process ya 1.Kupenda, 2.Kuchumbia 3.Kulipa maali na 4.Kufunga ndoa,) 90% wamaume wapo radhi, cooperative na wake zao na huipa ndoa *Thamani* kuliko pesa au kitu chochote, kwa hiyo hufanya matumizi kwa madhauriano na Malengo.
🏹 Ila kwa ndoa zilizo ruka hatua 4, zenye mazinhira haya 👉(1.Imeanza ngono ndo ikazaa ndoa, 2.binti kupata mimba ndo ikalazimisha ndoa, 3.Kutumia pesa kushawishi binti akupende, au kijana akupende ikapelekea kuoana, 4.Binti kujichumbia, na kujioza) haya mazingira huondoa Thamani na nguvu ya Ndoa na kwa saikolojia ya wanaume huwa mioyo yao inakuwa na mambo 2. *Moja, Kuonyesha ubabe kwa mke wake maana siyo ndoa ya gharama, Pili .. Jeuri ya huwezi kutoka na ukitoka hana hasara.*
🏹Lakini Shida na Chimbuko la mzozo huu wa budget ya familia mwanaume kuwaka pale mke akigusa pesa ya mme wake, shida ipo hapa( *_Uelewa mdogo kuhusu ndoa na maana ya ndoa_*) katika ndoa vitu vyote ni vya pamoja, kinacho hitajika ni mipango, mazungumzo na mpangilio wa matumizi kulingana na kipato chenu.
🏹 *SULUHISHO* nini mama afanye, lazima kwanza atafakari ameingiaje katika ndoa hiyo? pili hakikisha unatumia lugha nzuri kuwasiliana na mmeo katika kila kitu, tatu Jitahidi kuongea na mwenzako kwa kila maamuzi ya kifedha unataka kuyafanya, nne jaribu kumshawishi mmeo mpange budget ya mwezi na mmeo na mpeane pesa ya ziada kila mtu kwa matumizi binafsi. tano kama mmeakoka wote ingia kwa maombi kuombea ndoa yenu. sita Onana na mwanasaikolojia kiofisi upate Counseling & Guidance.
   *Ev Elisha Kazimoto*
         0755444078

Friday, 2 June 2017

HILI VAZI BASI NATUPA

*HILI VAZI BASI,   NALIVUA*
     _Ev Elisha Kazimoto_
          *0755444078*
_Shalom mwana maombi,mkeshaji,mwana maombi,mtakatifu wa Mungu uitwaye mtu wa vita,nakukaribisha sasa katika ujumbe huu wa *Operation Tupa Vazi Chakavu, Vaa Vazi Jipya* katika mkesha wa maombi_
🏹Kila vazi katika ulimwengu wa mwili lina tafsiri zake na maali pake pale linapo valiwa na mtu, kuna vazi ukivaa utasikia, _Bibi harusi, mwanasheria, mchungaji, kafiwa, huyu mjane,kahaba na mtanashati nk, vazi lina nguvu ya kukutambulisha kwa watu,eneo lolote hata kabla hujaongea *Vazi lina Nguvu ya Kukushusha au Kukupandisha* kuwa makini sasa tunapo uangalia ulimwengu wa roho_
*_Yona 3 : 6 - Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu._*
🏹Katika ulimwengu wa roho tunatambulikana pia kwa vazi,maisha yako unayoishi katika mwili yaweza kuwa ni aina ya Vazi ulilovikwa katika ulimwengu wa roho aidha *umevikwa na Mungu au Shetani na Mawakala wake* vazi hilo ndilo linakufanya uwe na nguvu katika mwili au uwe dhaifu.
*_Isaya 61 : 10 - Nitafurahi sana katika Bwana, nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu._*
🏹 Kuna watu wana maisha ya kukataliwa, mikosi, Kila mahusiano ya uchumba yanavunjika,hata yule uliyesema huyu basi tutafunga ndoa naye anapotea,kila biashara inaharibika,ndoa migogoro aiishi, *_Shida ipo kwenye vazi Ulilo vikwa, vazi la migogoro,vazi la kukataliwa,vazi la nuksi_* unahitaji kupigana katika maombi kuchana na kuvua vazi hilo.
*_Marko 10 : 50 - Akatupa vazi lake, akaruka, akamwendea Yesu._*
Vazi leo lazima litupwe, vazi walilokuvisha wachawi,katika ukoo lazima litupwe kuleee.
🏹Kuna mavazi ya laana walikuvika, Katika maombi ya leo tumia mstari huu, kwamba Yesu alijika vazi la Laana ili mimi nivikwe vazi la Baraka
*_Zaburi 109 : 18 - Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake. Ikamwingilia moyoni kama maji, Na kama mafuta mifupani mwake._*
🏹Omba vazi ambalo hata wanadamu wataligombania, kazini wataligombania,kanisani wataligombania, vijana wakiume ma wakike wataligombania.
*_Zaburi 22 : 18 - Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura._*
_Saa ya kuvua vazi baya na kuvaa vazi jipya_
       *_Ev Elisha Kazimoto_*
        0755444078

Thursday, 1 June 2017

HATUA MUHIMU ZA MAHUSIANO

*SWALI LA KISASA NA ATHARI ZAKE*
*Shalom nna swali wapendwa....*

*Hivi kwann sasa kumeshika kasi sana watu wakishakuwa na mahusiano tu wanapost wapenzi wao ktk mitandao ya kijamii.?????*
  _Katika Kujibu Swali hili, Mwanasaikolojia *Ev Elisha Kazimoto* anachambua hivi;_

🏹Mahusiano ni photocopy ya uchumba, ambapo original ya mahusiano anayo mwenzako  moyoni mwake, ambayo akijiridhisha ndo atakupa hiyo origina na utaichana photocopy,sasa akiigomea asikupe ndo utaumbuka,..... Kuna vitu ambavyo vijana wanapaswa kujifunza katika mahusiano (Kuna Kipindi cha Mlipuko, Kuna kipindi Cha Wasi wasi, Kuna kipindi Cha Utulivu, Kuna kipindi cha Uhakika, kuna Kipindi cha Agano) hivi vipindi vyote vina maana yake na kazi zake,usipo jua vipindi hivi utakuwa mtu wa kuumizwa na kujishangaa na kubadirisha profile picture kila muda.Kabla ya kujiachia na Sura ya mtu jua vipindi hivi vya kisaikolojia ili usijiharibu kisakolojia baada ya Malengo yako kutokamilika.
🏹Kipindi cha Mlipuko ni kipindi cha Mahusiano ya mwanzo ambapo kila mtu anakuwa na mvuto wa nje tu kwa mwenzake, hapa ndipo watu huwa na upendo wa upofu,hasikii aambaliki,hajali mvuto na hisia za mwonekano, sauti, pesa na umbo utawala hapa. (kipindi hiki hakuna aliye na details za mwenzake) ukijifanya kipindi hiki huyo wako kaa sawa unawezaachwa mkiingia kipindi cha  details
🏹Kipindi cha Pili katika mahusiano nikipindi cha wasiwasi,hapa mtu uanza kujifikiria,je ni kweli huyu ndo awe wa milele?kweli atatosha kwenye maisha yangu, hivi nikiamua kabisa nioane naye kama atabadirika itakuwaje? Hapa watu uanza kuona utofauti wa siku za kwanza wameanza mahusiano, na muda waliopo kuna tofauti ya mawasiliano,zawadi,usiriazi(seriousness )unapungua au unaongezeka. Hapa ndo kipindi watu utengenezewa mazingira ya kumwacha mtu(kumpiga kibuti)au kuamua kuwa niridhike naye tu..(hapa kuwa makini pia)usijiaminishe sanaaaa, unapoona mtu anavitabia vya Siri,vinavyokuoa mashaka PIGA CHINI KABLA YA KUMUWRKA MOYONI KAMA MTARAJIWA,ukivifumbia macho vitabia hivyo....Usidhani utambadirisha ndani,asiyebadirika kipindi cha urafiki na Uchumba huyo ni JIWE LA MTONI,linapigwa maji haliyeyuki ila LINA TEREZA TU mile na milele. PIGA CHINI HUYO.
🏹Kipindi cha Utulivu ni kipindi ambacho watu sasa uamua kuingia katika uchumba(muda huu mtu uanza kuona vitu muhiu sana kwa mwenzake anaye muhitaji,uona huyu anaweza kukamilisha ndoto zangu)kipindi hiki taarifa zinazoaminisha uzuri na ubora wa mtu uongezeka(ila hubaki maswali machache ya hivi huyu hatanisaliti kuuniumiza? Hivi tania hii mbona kama itanisumbua, nighairi au niache tu atakaa sawa)ila utulivu uongezeka.
🏹Kipindi cha Uhakika,nikipindi ambacho hata Maali imeisha lipwa,na pete imewekwa kidoleni, hapa ni muda ambao mtu amekubaliana na mapungufu yaliyopo,ameridhika na viwango alivyo navyo mwenzake, kiroho,kimwili na kiuchumi. Wengi wenye akili ya mahusiano ndo wakitaka huweka profile picture za wenzi wao, katika level hii kuvunji mahusiano ni NADRA SANA aidha pepo,au madhaifu makubwa yamejitokeza kukiwepo kupoteza uaminifu(zinaa).
🏹Kipindi cha Agano, ni hatua ya mwisho ambayo ni maamuzi yasiyo na mashaka,ya wazi ya kuridhia kuungana na mwenzake kwa kufunga ndoa. Huu ni muda Amazing, wa furaha ya kuvua ujana na kuanza ndoa.
*_Hatua hii ndo maana wakaweka Honeymoon muda kutuliza mwili,saikolojia,shukrani kwa Mungu na kwa mwenzako, kuenjoy Mahaba ulo yasotea kwa muda mrefu, My Take ukiwa na uwezo Piga Siku 7-10 Hotelini aisee_*
_Uchambuzi huu umeandaliwa na Mwanasaikolojia ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto*_
          0755444078