Saturday, 28 June 2025

VITOTO VYA 2000(PART IV)

👑 *VITOTO(VISICHANA)VYA 2000*  👑
........................................
               PART IV
_Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto( CEO-GFI)_
Phone :0755444078

5. *Wanaiba Pasipo na Ulinzi.* Ni makosa ya kiufundi kulalamikia mwizi wakati unajua KUFURI YAKO AU MLANGO WAKO NI MBOVU.
👉Suala la ulinzi ni changamoto kubwa kwa baadhi ya wanawake, Ogopa kitu Biblia imetamka wazi MWANAMKE ATAMLINDA MWANAUME.....
👉Anaye linda anajua *Mali zilizomo ndani, Thamani ya kilichomo ndani, na anajua Aina ya wezi watakao kuja kuiba wanapeleka wapi*
👉Hivi unadhani kuna siku mwislamu atakuja Kukuibia Nguruwe? Au Mlokole kukuibia kreti za bia na sigara? Wezi wa vitu husika wanajulikana wataiba nini na kuvipeleka wapi.
👉Sasa Mwanamke Ukiambiwa Kumlinda Mwanaume, *ULINZI WA KWANZA NI KULINDA HISIA ZAKE*  Siku ukidharau Hisia za mmeo ndo siku Umeanza kumpoteza kwa wezi.
👉Ukiambiwa Kumlinda mwanaume, *ULINZI WA PILI NI WA HESHIMA YAKE* Mwanaume akigundua kuna namna Haumpi heshima yake Ataitafuta kwa watu wengine wanaofanana na wewe(mwanamke/wanawake).
👉Ukiambiwa kumlinda mwanaume, *ULINZNI WA TATU HAKIKISHA UMEMPA UHURU WA KUSEMA CHOCHOTE KWAKO NA UMSIKILIZE* Ukiona mwanaume Ameacha Kukusema iwe kwa uzuri au ubaya kukurekebisha, akaona anaposema unamuona kero...Aisee Huna mme kashaenda kuwasema wengine waliotayari kusemwa na wakafuata.
👉Ukiambiwa Kumlinda mwanaume, *ULINZI WA NNE, MRUHUSU NAFURAHIA USUMBUFU WAKE KWENYE TENDO LA NDOA kama ni mzima wa eneo hilo siyo mgonjwa.
👉Miongoni mwa ALAMA ZA KUKWAMBIA BADO UJAIBIWA MME NI KUONA USUMBUFU WAKE KWENYE TENDO LA NDOA mara kwa mara kama dozi ya dawa.
👉Ukiona mme wako AMEACHA USUMBUFU kwako, kero juu ya tendo la ndoa kuna mambo 3 yametokea.
1.Amepata mbadala wako
2.Ni mgonjwa kwenye mifumo yake.
3.Ujiongezi kumfurahisha kitandani...Mpaka hapo Utaporwa.
👑Nini ufanye katika usumbufu wa mmeo katika tendo la ndoa, SOMA Majira, Tumia Kauli Tamu na Buni Mbinu za Ktuliza hisia kirafiki.
👉Tafauti na hapo wanasaikolojia wanasema unaweza Kaa na mtu aliyekuacha zamani kihisia ila uko naye kimwili, ila kuna mtu anamiliki Hisia zake, na Akimuona Anajisikia Raha na Amani kuliko wewe.
👑Kwa hiyo, Lugha ya *Vitoto vya 2000* ni vikali, Pisi kali, vinavunja ndoa za watu, Si za kweli, kama ni Sura uzuri walio nao ni wakawaida kama wako ndo maana na wewe Uliolewa ni kwasababu ya uzuri ulio mdatisha mmeo, kama ni Maumbile wana kama yako ndo maana mmeo alikuoa wewe, mnachotoafutia wewe mama wa 1980s, 1990s ni kwamba *Wewe Hauko Serious na Mali yako kuilinda, Wao wako serious na Kutafuta mtu aliyeumizwa kwake wampe furaha* Kazi yako kubwa OGOPA KUMUUMIZA mwenzako madaktari uchwara wengi mtaani watamvamia kumtibu hutampata, na akiponea mikononi mwao hao madaktari wa mtaani (vitoto vya 2000) unakazi ya kumrudisha kwako kihisia na kimwili.
NB: _Vitoto vya 2000 niwashauri na ninyi, si kwamba mtaa kwenye chati mpaka mfikishe miaka 30, 40 mtafutika, tulia mtafute ndoa zenu, jifunzeni kutokana na makosa ya dada zenu mjipange kutoyafanya pale mkipata ndoa zenu, mbali na hapo nanyi mtafanya makosa yale yale nanyi watakuja *Vitoto vya 2020* vitawatoa machozi kama mnavyota machozi ya wenzenu wa 19980s na 1990s_
Ulikuwa nami mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa
*Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)*
Phone no. 0755444078

VITOTO VYA 2000(PART III)

👑 *VITOTO (VISICHANA) VYA 2000* 👑
........................................
          PART III
Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa
*Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)*
Phone :0755444078

2. *Mme uliye naye ni chaguo lako la kwanza na la mwisho ndo maana mkaoana* unadhani mlivyoanza miaka ya kwanza mlikuwa mnakinzana hivo? Mliishi vizuri, mlielewana, mlikosana na mkasahishana na mkaendelea na amani yenu na upendo wenu, na akuna aliyekuwa na uwezo wa kumvuta mbali nawe, kwakuwa Hekima zako na maamuzi yako, na uchaguzi wako ulikusukuma kumlinda kwa Wivu mkubwa akae kwako.
👉Ila ulipoanza kumuona kama amwendani, kama ulitafutiwa, kama msumbufu kwako, mkorofi kwako, Ukasogeza moyo mbali wa kumkubali kama Chaguo lako la furaha ambalo unatakiwa kulilinda, ndipo *Wajanja vitoto vya 2000 vilikuja na mbinu za Kuonyesha Kujali na kuthamini Uanaume wake* Wamefanikiwa, watafanikiwa kumpora kwako.
👉Kama ulimpata mmeo huyo kiuhalali,Ulioana naye kwa kukubaliana, Basi Unawajibu wa Kukubaliana Tena naye namna ya kuishi kulingana na Anavyopenda yeye na wewe unavyopenda mbali na hapo.. Utaporwa.
3. *Miaka mlokaa pamoja Humjui Mmeo!* Utaibiwa mapema sana.
👉Wanasaikolojia wanasema, ukikaa na mme au mke kuanzia siku 1 mpaka miaka 9, mkigombana na kuitirafiana ni haki yenu maana bado hamjuani vizuri.
👉Ila kuanzia umri wa miaka 9 nakuendelea mkigombana, na kuitirafiana kiasi kwamba msielewane mpaka ndoa yenu ijulikane kwamba *Mgogoro wa ugomvi wenu ni huu* Basi ninyi ni Wapumbavu msiosaidika, na Mmoja kati yenu alitakiwa ASIOE MPAKA UZEE AU ASIOLEWE MPAKA ubibi kizee. Kwa nini?
👉Miaka 9, 10, 15, 20.... *Ujui Mme wangu Anatekwa hisia na mambo gani?*
👉Ujui mme wangu ni mdhaifu kwenye mambo gani kihisia? Na hapa panaweza tumiwa na wajanja kumchukua kwangu?
👉Ujui mme wangu anachukia nini ukifanya?
👉Ujui kumdanganya mmeo mpaka akaona ni kweli japo unajua si kweli ila lengo uweke amani ya ndoa yenu.
👉Ujui namna ya kumfurahisha mmeo,hata kama amechukia au ana stress ni mambo gani ukiyafanya anarudi kwenye mood?
👑Sasa wanawake wengi wa 1980s, 1990s wamefeli hapo, Anakosea, Anajihesabia haki, Hajui namna ya Kumrudisha mme haraka kwenye mood kutumia vitu anavyopendelea,  naye Anakaza Uso wa kununa mwanzo mwisho.
👑Kinachotokea ni nini, Vitoto vya *2000 viko makini na Neno Am Sorry Love, Am sorry baby, It will Never Happen Again, Sitakuumiza tena eeh?, Nambie unachotaka nifanye ntafanya ili uwe na Amani na furaha yetu irudi* Kwa maneno hayo machache MMEO ANAPORWA mbele yako asubuhi unaona.
4. Kuna Kosa la Kiufundi na la Kisaikolojia, wana ndoa wanafanya( mama) Kumuona mmeo wakawaidaaa, hana maajabu yoyote kama useless man(kwa kutumia Kosa au Makosa mlokosana). Ndo maana una Mtreat, unamchukulia kawaida, na haumpi heshima yake, uzito wake, na nafasi yake kwasababu ya mazoea na KUTOFUNDWA NA WAZAZI.
👉Changamoto kubwa ya Kizazi cha 1980s, na 1990s, na 2000s *Akija Fundwa na Mama Zao* wanafundana wao kwa wo mitandaoni na kwenye Saloon. Hapo hamuwezi kukaa na Waume, tutakuwa na Single Mother wengi na Wajane, na Walioachika wengi.
👉Hata wewe msomaji, moyoni mwako unajua, Mama Yako Alikufunda? Akakupa Miiko ya Ndoa na namnaya Kukaa na mme kwenye nyakati zote? Au Una Weza Kujivunia Ndoa ya Mama yako, aumaisha ya mama yako kwa baba yako ili na wewe Uwe na Adabu na heshima na utilivu kwa mmeo?
👉Haya mambo sisi tuliookoka Tueongezewa Jicho la tatu, Kuna Roho za kifamilia,kiukoo za Kupiga vita kwenye maombi na kwa kujilazimisha kwa vitendo kuzikimbia ili Ndoa yako idumu... Usipo kuwa makini unakuta Roho ya Bibi yako. mama yako, dada yako inakufuata wakati una Neema ya Wokovu ya kukuepusha na Nguvu hizo.
👉Huyo mmeo unayemuona wakawaida sana na hana jipya kwako,Ila pembeni yako, wamama,wadada, na hata wanaume wenzake wanamuona ni Mtu Special, mtu ambaye Atakuwa au anakuwa Karibu naye, kuitwa kwa jina lake *Anafaidi, Amependelewa* na wana WISH INGEWEZEKANA WAKAPATA HATA NAFASI YA SAA 1 waonyeshe unyenyekevu wao na heshima yao kwake wange fanya kwa bidii.
👉Hivi ndivyo Vitoto vya 2000 Uvizia hiyo nafasi, utakuta, *Vina nyenyekea, Vinaheshimu, vinatambua na kujali, maneno, hisia, sauti ya mmeo* sanaaaa ila wewe ujali hapo ndo Kuibiwa Uanzia hapo. Usipo badirika Mmeo anaibiwa kwa Heshima na Kusikilizwa.
👉Mama inabidi ujue kwamba mwanaume niliye naye Si wakawaida, afanani na wa wengine, huyu anaubora wake,sifa zake, na nguvu zake, lazima Nitambue hilo na nimpe heshima yake ili Aridhike na heshima yangu asirubuniwe na heshimaza  za nje.
_Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)_
Phone: 0755444078

VITOTO VYA 2000(PART II)

👑 *VITOTO VYA (VISICHANA ) VYA 2000* 👑
........................................
              PART II
_Na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa_
Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)
Phone: 0755444078
*26 Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;Waefeso 4:26*

*27 wala msimpe Ibilisi nafasi. Waefeso 4:27*
👑Ukiichunguza mistari hii nikama imeruhusu Kufanya Makosa, ila umepewa Taadhari Makosa kama binadamu, ila Uwe makini Makosa yakiendelea sana yatazaa Hatari ya Muharibu Kupata nafasi ya Kuharibu. ( *Nitarudi kuchambua*)
👑Wamama wenye Umri mzuri kwenye Ndoa Msiokuwa Vitoto vya 2000, miaka 30-45 mna kwama wapi kwenye Ndoa Mpaka Mnaibiwa Waume zenu na vitoto vya 2000?
👑Nina Maswali kadhaa naomba ujiulize vema halafu ntakwambia Ulipo kwama, Kama wa Kupona Upone kama unaendelea kulia na kulalamikia vitoto vya 2000 uendelee hivo hivo mpaka unazeeka ila Utabaki Sanamu la kwenye ndoa, una mme mwili, ila Roho na Hisia ziko kwingine, au Utaachika.
👑1️⃣ Hivi uliingia kwenye ndoa kwa hiari au kwa kulazimishwa?
👑2️⃣Hivi Mme uliye naye Ulitafutiwa au mlipendana na mkaona ndo mnaweza ishi pamoja?
👑3️⃣Hivi kwa miaka uliyokaa na mmeo Humjui mpaka anakuja mtu mgeni kumjua kuliko wewe na kufanikiwa kukupora?
👑4️⃣Hivi unajua Mmeo niwakawaida kwa watu wengine kama wewe unavyohisi niwakawaida kwako?
👑5️⃣Hivi Unajua kwamba Wezi, Mwizi Aibagi sehemu yenye ULINZI mkali,  wanaibaga sehemu iliyoachwa wazi au bila ulinzi?
👑Hayo maswali 5 ukielewa moja moja Utarudishiwa akili yako na Utakaa na mmeo kwa Utulivu sana na kufurahia na Autaibiwa kizembe tena.
👑Vitoto vya 2000 vimefanikiwa kuiba waume za watu kwa Kutumia Mapungufu ya wanawake wasiojali na hasa *Wanawake wa Kilokole* ambao wametumia MWAVULI WA WOKOVU kufanya Ubabe na kuishi kama wajane wasio na wanaume Wakidhani *Neema ya Wokovu waliyo nayo wao na waume zao Ni Mnyororo mkali usio mruhusu kujitikisa kwenye ndoa, atatulia hata angenyanyaswa kwenye ndoa* hili ndilo LANGO LA 1 LA UHARIBIFU WA NDOA ZA WANA WA MUNGU.
👑Nikinukuu maneno ya Askofu mkuu wa Kanisa la Kiroho la TAG, katika kongamano moja aliwahi kusema *Wanawake wa kilokole ni WAPUMBAVU walio wengi wameshindwa kuishi kama wanawake kwa waume zao*......... Mwisho wa kunukuu( nenda kaitafute YouTube).
👑Sasa vitoto vya 2000 vimeiba na vinaendelea kuiba na vitaendelea kuiba Wanaume wa wanawake wa miaka ya 1980s,1990s kwa sababu zifuatazo za maswali yale juu 5.
1. *Mwanamke uliingia kwenye ndoa kwa hiari Kutimiza Matakwa ya Ndoa* Kama ukufundwa na Wazazi wako(mama yako), basi ulipata hasara ya kwanza... Ilibidi ujue Matakwa ya Ndoa unayoiendea Uende Ukayatimize kwa bidii (HUWEZI KUIBIWA MME Ukiwa unatimiza Matakwa ya Ndoa)
👉 Kiroho(Kiimani/Kikanisa)Ulitakiwa ufundwe na mfungisha Ndoa akueleze matakwa ya ndoa uliyoichagua kwa hiari uende ukayatimize kwa moyo wote, (kama ukumsikiliza vizuri ulikuwa unawaza usiku wa Honeymoon) hiyo ndo Hasara ya 2 Usingeibiwa mmeo na vitoto vya 2000.
👉Nimezungumza *Kufundwa, na Kufundishwa* Ujue Matakwa ya Ndoa na uyatimize kwa bidii huwezi ibiwa mme.
👉Vitoto vya 2000 *Vinafundwa na Mitandao ya Kijamii Matakwa ya ndoa na Havijaingia kwenye ndoa Vinatumia Maarifa hayo Kuwapata Wanaume Waliokosa Furaha ya Ndoa kwasababu mwenye ndoa(mwenye mme wake) kashindwa kutimiza matakwa ya ndoa*
👉Baadhi ya Matakwa ya ndoa ni yapi?
A) utii kwa mme wako, hapa si suala la kumpigia magoti mme, ila mme yeyote anahitaji kuona,kukaa karibu na mke wake ambaye Kile anachomwambia kufanya, kutofanya, kufuata, Anakitii na hata kama hakubaliani nacho *Analugha,Matendo ya Staha na ushawishi* kwa mme wake kughairisha kile kitu.
👉Vitoto vya 2000 viko makini Kutii na kusikiliza, na kutekeleza MATAKWA ya mmeo kwa GHARAMA zozote, ila wewe Unarumbana na kuzozana, au Majibu ya mkato kwa  mmeo yasiyoonyesha unyenyekevu kwake hapo( Hutoboi) Wanamchukua mmeo mapema sana.
👑Ongeza Umakini na Adabu kwa Mmeo.
*Sehemu ya Pili imekamilika karibu sehemu ya tatu*
_Ulikuwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)_
Phone : 0755444078

VITOTO VYA 2000(PART I)

👑👑 *VITOTO(VISICHANA) VYA 2000* 👑👑
_Imeandaliwa na Mwalimu na Mtaalamu wa Saikolojia ya Mahusiano na Ndoa_
*Ev Elisha Kazimoto(C.E.O-GFI)*
Phone: 0755444078
........................................
             *PART I*
_Shalom shalom wale mnaojiita watoto wa 1980s,1990s na wale mnaoitwa watoto wa 2000 wote kwa pamoja Amani ya Bwana iwe nanyi_
👑Kuna lugha hii iliyo shika kasi hasa katika mitandao ya kijamii na kwenye vinywa vya Wanawake wengi walio kwenye Ndoa wakijaribu *Kubainisha Hatari, Ubovu na Ubaya wa Vitoto vya 2000(visichana)* kama Virusi hatari kwa Ndoa zao.
👑Baada ya Kusikia na kuendelea kufanya Utafiti wa Kisaikolojia kujua Chanzo cha Jina hili na sifa hizi kushika kasi kwa nyakati kama hizi, Kama *Mwanasaikolojia na Mshauri wa Ndoa nikapata Cha Kuzungumza* na Kusaidia Kizazi cha 2000 na cha miaka ya 1980s,1990s.
👑Nianze na Neno la Mungu chimbuko la Hekima zote za Saikolojia, kabla sijaenda kwenye Kweli za Wanasailolojia.
*Yeremia 31:22 Hata lini utatanga-tanga, Ee binti mwenye kuasi? Kwa maana Bwana ameumba jambo jipya duniani; mwanamke atamlinda mwanamume.*
👑Enyi wana ndoa, Enyi Wamama, Kabla ya Kutoa Majina yoyote na sifa zozote njema au mbaya kwa kizazi kinachoibukia, Lazima kwanza Turudi kwenye Neno la Mungu linasemaje Kuhusu Ndoa yako.
👑 *Ndoa Ni Taasisi Nyeti sana* Inayo hitaji Mtu mwenye akili Timamu ( _Nimewahi kuandika makala miaka ya 2017 inayosema *Ndoa inahitaji mtu Mwenye Akili Timamu* nenda kwenye blog yangu au Google andika hivyo ( Ndoa inahitaji mtu mwenye akili Timamu Material Adimu_) hii makala ina dawa nzuri ya uponyaji kwa wana ndoa.
👑Sasa Kumeibuka wimbi kubwa la Wadada wadogo kiumri (vitoto vya 2000 na Mashangazi ya miaka 1970s Kumiliki *Wanaume wa wamama wa miaka ya 1980s, 1990s* kiasi ambacho kimezaa Lugha mtandaoni, Vitoto vya 2000.
👑Hii Lugha ina maana gani kwa wana ndoa? Hizi lawama kwa kizazi cha watoto wadogo mabinti wa 2000 kuzoa Umaarufu usio na sababu wa *Kuiba, Kubeba, Kumiliki wanaume wa watu umetoka wapi?*
👑Kisaikolojia, Kuna *Makosa Makubwa* yanafanywa na Wanawake, wanaojiita *Wanawake wa 1990s, 1980s wenye ndoa zao* makosa ya Kiulinzi yaliyo toa Nafasi nzuri sana ya Bure kwa *Wajanja, Wasichana werevu wenye haja ya Mapenzi* Kuchukua waume zao.( Nitaelezea.....)
👑Kiroho, Wanawake hawa wenye ndoa wamefanya Makosa makubwa ya Kibiblia ambayo, *Wamempa Ibirisi Nafasi* ya Kushambulia Ndoa zao Vizuri bila kutumia nguvu kubwa.
👉Hapo unahitaji kutulia kujifunza vizuri usikosee.
*Hii ni Sehemu ya Kwanza, karibu kuendelea sehemu ya pili*

Sunday, 10 November 2024

YATAINUKA MAWE KUCHUKUA NAFASI

🛜🛜 *UKIZEMBEA YATAINUKA MAWE KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKO* 🛜🛜
_Hili ni Neno la Kibiblia ila linanipeleka mbali mpaka kuyazumgumzia Mahusiano ya wana ndoa wa Kizazi cha Sasa_
*40 Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, mawe yatapiga kelele.Luka 19:40*
🛜We msomaji wangu anzia msitari wa 37, upate kisa kamili, sasa mimi mchambuzi kwakuwa sihubiri neno hapa, ila nachambua kisaikolojia ndoa kwa msingi wa Sentensi ya Kisaikolojia ya Luka 19:40, *_Hawa wakinyamaza Mawe yatapiga kelele_* Nisikilize vizuri nikusaidie kitu hapa.
🛜Katika Mahusiano (hasa ya ndoa) Kila mtu ana WAJIBU na Majukumu yake ya kutimiza ili kuimarisha Furaha na Upendo kwa wana ndoa hao.
🛜Kinachotesa na kusumbua ndoa nyingi pamoja na hila za shetani, ila ni Mwanandoa Mmoja wapo au wote *Kusahau, Kupuuzia, Kuacha Baadhi ya Majukumu muhimu yanayo muhusu kwaajili ya mwenza wake*
🛜Katika Msitari huo 37-40 unaona kuna Watu walitakiwa na ilikuwa ni wajibu kuna mtu inabidi wa Mwimbie, Wamtukuze, Wamsifu, Washangilie,wapige kelele kwaajili yake, Lakini kuna kundi la watu Wakawa wana mawazo ya Kuzuia kelele zile na sifa zile.
🛜Hawakujua umuhimu wa zile sifa na kelele anazopewa yule mtu(Yesu) au walijua ila WIVU TU, ndo uliwatuma.
🛜Sasa wao wakadhani kwakiamuru watoa sifa na kelele KUNYAMAZA watakuwa wamemkomoa Bwana Yesu.
🛜Yesu akataka kuwambia ukweli, kwamba *Sifa, Heshima, Kelele na Utukufu ni LAZIMA siyo muhimu tu* nilazima nipewe, ndo maana NINYI MKIKATAA NA MKAZUIA HAWA wasinipe NINACHO STAHILI, *Mawe Yatainuliwa Yafanye kazi ile ile iliyobidi ifanywe na hawa*
🛜Wana ndoa mnapo poa mnaanza kuruhusu MICHEPUKO?(Mawe hayo) yanainuka kufanya kazi ile ile, *_Ya Kutoa Matumizi, Kusifia, Kuongea naye kwa Mahaba, Kumpa Penzi kwa style zote na mbwembwe zote na furaha yote na muda wowote ANAPO LIHITAJI PENZI_*
🛜Kazi iliyokuwa ya wanadamu( mwanandoa) Inashikwa na Jiwe(Mchepuko).
🛜Unapaswa kujua jiwe halina mamsikio, wala alioni, na halina huruma likisha pewa kazi linafanya kazi mpaka litakapo pasuka au tupwa.( Ndo maana ndoa nyingi zinaugulia maumivu ya muda mrefu) jiwe haliachii karibuni.
🛜 Mwana ndoa, Unajua *_Mmeo/Mkeo Kipi kina mtesa kwako? Anachokihitaji sana, anachodai sana,kinachomfurahisha sana_* Aisee kuwa makini kifanye kwa gharama zozote Ukidharau ukahisi Unamkomoa, My friend Yakiinuka Mawe Kuanza Kupiga Kelele Uwezi Nyamazisha! Itakuwa imekula Kwako.

_Mwisho, kila mmoja kwenye mahusiano kuna kitu kina msumbua sana anakihitaji kwa mwenzake sana, wengine Heshima, wengine Pesa, wengine Kusikilizwa, Wengine kuhurumiwa, Wengine Kupendezeshwa, Wengine TENDO LA NDOA, wengine Kufanya Maendeleo, haya yote kila Mmoja anatakiwa Akae mkao wa Kuwajibika, Ukidharau na Kuona kawaida, Anayekihitaji Aoni kawaida, Atakacho Fanya Atatafuta Mawe ya Kupiga kelele maana tayari wanadamu Wamenyamazishwa, anatafuta kisicho nyamazishwa, na jiwe likianza kupiga kelele uwa linapiga kelele bila kuchoka likijua lenyewe halina sifa ya kupiga kelele limeokotwa tu kama mbadala, ndo maana halichoki, haliangalii changamoto lenyewe linajua likicheza Binadamu anarudi kwenye nafasi yake ya sifa. Tuzuie Mawe Kupata nafasi ya Kupiga Kelele kwa Kila mmoja kumtimizia Furaha Mwenza Wake_

*Ulikuwa nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI) 0755444078*

Sunday, 13 October 2024

WANA NDOA KULALA NA NGUO NI SAWA?

🫂🫂 *SWALI KWAKO MWANA SAIKOLOJIA NA MTUMISHI WA MUNGU EV: ELISHA KAZIMOTO* 🫂🫂
_"Kumekuwa na Malalamiko na Manunguniko kwa baadhi ya wanandoa Hawako Huru na Miili ya wenzi wao iwe mchana au usiku na hasa Utamaduni wa kulala na Nguo kwa Mwanandoa,iwe moja ya ndani au full hii imekaaje?_
..........................................
*_Nitajibu kamaulivyoniuliza, ila majibu yangu yatakuwa marefu kidogo Nitoe Elimu, Darasa la Kisaikolojia Katika Ndoa kwa wana ndoa,kuliko ya kujibu kwa ufupi kwamba si sawa au ni sawa, Nitoe ufafanuzi wa kina kama part 2 mpaka 3 au 4 Jitajidi usome zote, Kufikia Mwisho Usipo Pata Kuelewa na Kubadirika kama Mwana ndoa Jua Wewe Hukutakiwa Kuolewa au Kuoa ilibidi Ufe ukiwa Single_*
Uko Nami Mchambuzi wa Masuala ya Ndoa na Mahusiano Ev Elisha Kazimoto( 0755444078)
...........................................
💚💚💚💚💚💚💚💚💚💚💚
👉Wana ndoa tunahitaji kujua kitu kinaitwa *PSYCHOLOGICAL ETHICS OF MARRIAGE* (Tafsiri isiyo Rasimi.... Saikolijia ya Maadili ya Ndoa) 
Kwani unadhani ndoa ni ngumu? Nooo Tuna kwama kwenye Maadili ya Ndoa ya kisiakolojia yake.
👉Leo nitoe darasa kidogo kati ya maandiko yangu nimeandika juu ya ndoa(ukienda kwenye blog yangu au Google andika *Material Adimu University* )utakuta maarifa mengi yatakusaidia kwenye mahusiano na ndoa hata Huduma yako.
1️⃣Wana ndoa, Saikolojia inasema Ndoa ni *Uwanja Huru na wa Uchaguzi kwaajili ya Kujipa furaha ya Mwili, na Akili*
👉Hapa kuna vitu vingi tunavikosea sana wana ndoa, na Kwa hali hiyo *Usaliti, Uchepukaji, na Uzuri wa Mmwenzako Kupungua machoni pako na akili mwako havitaisha* mpaka pale wana ndoa tutaacha Ubabe na Ujuaji na Misimamo binafsi inayoua HISIA ZETU.
👉Wana saikolojia wanapokwambia ndoa ni Uwanja Huru...Wana maanisha, *Jitahidi sana Umfanye mwenzako Ajisikie Uhuru kwako kuanzia mwilini Mwako ajisikie yuko huru na mwili wako, Ajisikie huru kukupa mawazo, ajisikie huru kukukosoa, ajisikie huru kuku brand kwa marafiko zake au kwa watu, ajisikie huru kujieleza shida,changamoto na uhitaji wake*
👉Ukiona Una mnyima Mwenzako uhuru wa Baadhi ya vitu ambavyo Hakika anajua Ni Haki yake Kuwa huru navyo *Basi saikolojia inasema Atavipata tu kwa njia yoyote na popote bila kujalisha ni salama au si salama,ni wazi au siyo wazi* 
👉Kosa si lake, kosa ni la Aliye mnyima uhuru,. Japo kama ni kosa kiufundi ni la mtenda siyo msababishaji ila wanasaikolojia tunaamini Kosa limesukumwa na mtu.
NB: *Hapo Umejifunza nini kama mwana ndoa kwa point ya kwanza?*
👉Wanasaikolojia wanapo sema Ndoa ni Uwanja wa Uchaguzi,.... *Wanamaanisha Alipo kuchagua kuwa mme au mke wake alijua hakika Wewe Utampa Furaha*
👉Pili katika kile Kikubwa alichokichagua,  kila siku na kila saa ana machaguo yakeadogo madogo ya *Nini kitampa furaha kwa wakati mfupi mbali na wewe kuwa furaha yake ya kudumu maisha yote*
👉Anaweza CHAGUA SEX impe furaha muda huo( Je wewe upo tayari?),Anaweza akachagua Kupiga story nawe za Mahaba, je wewe huko tayari?, Anaweza akachagua Kukupa Zawadi au Anategemea Zawadi kwa kipindi flani,je wewe uko tayari? Anaweza kuchagua kutaka kusifiwa au kupongezwa,je wewe huko tayari? Anaweza kuchagua Mcheze michezo ya kimahaba,mapenzi,je wewe huko tayari!
👉Utafiti wa Kisaikolojia unaonyesha, Wanandoa wengi walio dumu kwenye ndoa miaka 10 kuendelea *Wamepoteza Utayari kwa wenzi wao pale wenzi wao wanapo Kuwa na Machaguo ya kuwapa furaha*
👉Ndiyo Maana wengi wameshangaa waume zao au wake zao waliokuwa Waaminifu kwao ila sasa Wameanza Kuwa Cheat! Si kwamba Udanganyifu kwenye ndoa umetokea kama TABIA YAKE NOOO NI MAZINGIRA yaliyo tengenezwa na mwenzi wake kwa Kukosa Utayari kwa Machaguo anayo yachagua mwenzi wake.
👉Saikolojia inasema, *Kila chaguo lililo chaguliwa na mtu, ila mwenza akakosa utayari Litatafutiwa Mbadala wa Utayari kwa mtu mwmingine ili Gap la kisaikolojia la furaha Lizibwe* 
NB: Gap likizibwa na mtu mwingine asiye sehemu ya ndoa linaweza kuwa chanzo cha kumpoteza mwenza jumla.
👉Saikolojia inapozungumzia *Furaha ya Mwili* aaah hapa aisee wana ndoa Turudi darasani na Tutulie kweli, Hapa kwa waliookoka msikemee mapepo kwenye ndoa ukiona mabadiriko kwa mwenza wako,Tulia ujihoji halafu kimya kimya anza mchakato wa mabadiriko mbali na hapo, Kuna maisha magumu unayaandaa mwenyewe bila kujua kumbe ungelijipa raha duniani na maisha yenyewe haya mafupi.
💚Kila mwana ndoa au niseme Binadamu anahitaji Furaha ya Mwili, sasa mimi hapa niko kwa wenye ndoa zao, wana saikolojia wanaposema, mtu anatafuta Furaha ya Mwili kwako elewa mambo haya:
🤝Kuna mtu anahisi raha kama akikukumbatia mkiwa mmelala(mwili wake anahisi raha)
🤝Kuna mtu anahisi raha iliyoje kama Aki Romance na wewe wakati na nje ya tendo la ndoa(mwili wake unatulia)
🤝Kuna mtu anajihisi raha akichezea Maziwa yako,kifua chako, hips zako, garden zako Ukiwa necked( anapata furaha sana)
🤝Kuna mtu anajihisi Raha akiwa kitandani nawe *Ukiwa Free mwilini mwako Hakuna Nguo Yoyote* ile ngozi kwa ngozi zikigusana (Ahaaa anahisi raha) yaani hapo ni nje ya tendo la ndoa.
🤝Kuna mtu anahisi raha ya mwili wake pale anapo shiriki tendo la ndoa nawe (Anahisi raha ya ajabu).
NB: *Sasa hatari ni nini? Ni pale mtu ametegemea furaha ya mwili wake aipate kwako na wewe Ukazuia, Jua moja kwa moja Furaha ya Mwili Itatafutwa tu Pengine.*
👉Sailolojia haijawahi kukaa na SHIMO WAZI (gap) mpaka lizibwe sasa hapo ndo kuna hatari ya ndoa na familia.
👉Wana saikolojia wanaposema..... *Furaha ya Akili* hapa napo pana tesa wengi, hapa kuna watu wana misongo ya mawazo, uchumi mgumu, taarifa mbaya, na masumbufu mengi ya maisha, sasa Eneo ambalo uwa lina ponya na kuwapa watu matumaini kama alivyokuwa ameumba Mungu ni Ndoa(Mwenza wako)
👉Kuna vitu ukifanyiwa vina leta furaha kwenye Akili yako na Unasahau changamoto kwa muda, siku na muda unakuwa unasogea.
1.Romantic Chatting ( mtumiane sms za kimahaba na za upendo na amani)
2.Sex play mcheze na kutaniana kama wachumba au kama wapenzi wapya.
3.Muitane majina ya kimahaba.
4.Mpongeze au msifie kwa kila kazi atakayo fanya au jambo atafanya.
5.Angalia Anatoa Ishara ya Kutaka sex,mwitikie positive bila vijisababu vya kuahirisha.
👉Haya mambo 5 yanaleta furaha ya Akili, Wewe Usipo mpa mambo haya 5, Atatafuta Eneo lolote la Kuyapata ili Akili Ituliepo, Aaipo Pata pa kutuliza akili ndo mtamuona mtu anadalili hizi.
1.Mahasira ya mara kwa mara.
2.Majibu ya mkato/ kukaa kimya
3.Anakaa mtandaoni sana kuliko na wewe.
4.Hafanyi jambo lolote kwako au kwenye familia yake mpaka mmemdai kitu flani.
NB: *Tuokoe familia zetu na ndoa zetu kwa Kurudi kwenye Maadili na Saikolojia ya Ndoa*

_Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, Mwana Saikolojia *Ev Elisha Kazimoto*(C.E.O- wa G.F.I)
Whatsapp 0755444078
E-mail : babaeve755@gmail.com