Friday, 31 March 2017

WAKIMBIZE MAADUI ZAKO

🗡🗡🗡 *KIMBIZA MAJESHI YA ADUI WALOPANDA JUU YAKO* 🗡🗡🗡
    _0755444078_
  *Ev Elisha Kazimoto*
_Shalom mwana maombi,mtu wa vita,uliyenolewa na Bwana upigane na ushinde katika kila vita, leo ni Mkesha wa *Operation Kimbiza Adui zako hadi watokomee*_
*YEREMIA 50:41-44*
_41 Angalia, watu wanakuja watokao kaskazini; na taifa kubwa, na wafalme wengi wataamshwa toka pande za mwisho za dunia._

42 Wanashika upinde na mkuki; Ni wakatili, hawana huruma; Sauti yao inanguruma kama bahari, Nao wamepanda farasi; Kila mmoja amejipanga kama aendaye vitani, Juu yako, Ee binti Babeli. 
44  *_Angalia, atapanda kama simba toka kiburi cha Yordani juu ya malisho yasiyonyauka; lakini nitamkimbiza ghafula ayaache; na yeye aliye mteule nitamweka juu yake; maana ni nani aliye kama mimi? Tena ni nani atakayeniandikia muda? Tena ni mchungaji yupi atakayesimama mbele zangu?_*
👉Kila mara yanatumwa majeshi yaliyo elekezwa kuvuruga maisha yako, kuvuruga ndoa,uchumi,elimu na mfumo mzima wa maisha.
👉Majeshi hayo(mapepo na wachawi) yanatumia mazingira yako kukutia katika mazingira magumu.
👉Majeshi ya vita ya maadui mengine yanatoka kwenye familia,ntaani kwako,ofisini kwako na hata kanisani kwako yote kasi ni moja yazingire maisha yako na kuua yote uliyo nayo.
👉Tazama jeshi hilo linapanda na silaha za(magonjwa,chuki,mauti,dhoruba,umaskini,mikosi na nuksi) silaha zinalengo la kukuzimisha na kukupunguzia nguvu ya kushinda
✍ *_Lakini tunaye Bwana atushindiaye,simama kama mwombaji utoe upanga wako uwakimbize maadui na usiwaache kuzingira maisha yako,piga,ponda ruhusu silaha za Mungu ziwatawanye,kimbiza...Amuru wapigwe kwa mapigo,vunja miguu yao,wakimbize wasionekane tena katika mipaka yako_*
Maombi yetu huwa ni moto na kauli zetu zenye muunganiko wa Neno la Mungu huwa ni Upanga mkali hakuna adui wa kusimama mbele yako ukianza kuwasha moto.
*_Yoshua 1 : 5 - Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha._*
👉Anza kusema mchawi,huruhusiwi kusimama mbele yangu,magonjwa hurusiwi kusimama mbele yangu, nguvu ya kufeli darasani hurusiwi kusimama mbele yangu, umaskini,migogoro ya ndoa,utasa na kukataliwa hamrusiwi kusimama mbele yangu *Kimbia mtoweke mbele yangu* safisha mazingira yako,mipaka yako isisikike harufu ya maadui.
   *By Ev Elisha Kazimoto*
         _0755444078_

Tuesday, 14 March 2017

SAIKOLOJIA YA WAKAKA KATIKA MAHUSIANO

*SAIKOLOJIA YA VIJANA WA KIUME KATIKA MAHUSIANO*
       _Ev Elisha Kazimoto_
      *0755444078*
_Shalom mabinti,leo nahitaji kuongea na mabinti,ambao bado hawajaolewa,wanatafutwa,na wao wanatafutwa,wako tayari kupokea maombi ya kijana kulingana na vigezo ulivyo jiwekea_ Katika uchambuzi huu kuna vitu mtoto wa kike unahitaji kuvijua na kuviwekea umakini,maana wengi *Wamejikuta wanakaa bila kuolewa(wanachelewa kuolewa)si kwamba ndo malengo yao au mpango wa Mungu ila nikwasababu walishindwa kujua saikolojia ya vijana walio mpitia kumchumbia,wengine wakaishia kutopata mtu tena,wengine,wakaishia kuchumbiwa tu bila kuolewa,wengine wakaishia tumiwa tu kimwili,kuzalishwa na kuwa chombo cha starehe na kijana kujie dea* Nini kosa, *_Tambua Saikolojia ya vijana uweze kuingia kwenye ndoa kwa wakati na mtu sahihi_* tuwe pamoja katika uchambuzi huu,Ndoa sahii ipo si bahati ni mipango na maamuzi ( _Ev Elisha Mwanasaikolojia atakujuza maarifa hao_)
✍ *_Kosa kubwa wadada wanafanya ni kushindwa kutofautisha upendo halisi wa Ndoa na Upendo(Tamaa ya Ngono)_*wadada wengi wakiona kijana amemu approach basi wengi wao hujiachia,na pale wakiambiwa wewe ni mzuri,nimeona unafaa kuishi nawe,na hakika tutaoana,basi hapo ndipo saikolojia ya kike uingiliwa,na Wao uhamisha maisha yao yote,(nafsi,roho na mwili)na kuyaweka Rehani mikononi mwa kijana na *Hapo ndo saikolojia ya kiume uanza kukua na kutawala*
👉 Binti unapaswa kujua hakuna kijana yeyote duniani wa kuapproach binti kwa maneno mepesi yasiyo na ushawishi wa kitu kinaitwa NDOA( labda kama anajua wewe ni malaya wakuuza mwili anahitaji kununua) _Vijana wote wanasaikolojia moja wanaamini hivi, *Binti yeyote duniani anahitaji Ndoa,kuolewa na ndo Neno linawasumbua,hakuna binti anahitaji kuchezewa ila kuolewa,kwa hiyo lugha ya kwanza kumpata binti yeyote,uwe unamwitaji kingono kwa muda,au kumuoa ni mwambie Ntakuoa,atakupa moyo wake wote_
(kwa hiyo binti unahitaji kuwa makini baada ya kuambiwa ndoa,siyo mwisho wa usalama wa kujihakikishia ndoa,kuna safari nyingine ya pili ya kudhibitisha lugha ya ndoa,au ngono au ni partnership.
✍ *_Kosa kubwa la Pili wadada wanafanya ni Kujichumbia kabla ya Kuchumbiwa_* kuna kitu ni (Intrinsic force of love)msukumo wa ndani wa kupenda mtu hata kabla yeye hajakupenda, hapa wengi huchemka,unahitaji kuwa makini sana,ikitokea Unapata *_Intrinsic force of love kwa kijana_*kabla ya yeye kukutamkia kuwa anakupenda,usiju Ukajichumbia kabla ya kuchumbiwa unaweza ishia kuumizwa,au kupotezewa muda.
👉Kuna vitu wasichana wanashindwa kuelewa kwenye saikolojia ya vijana, *Kuna kupendwa, Kutamaniwa,na Kufurahiwa* Kijana Akikupenda Anatamka nia yake kwa uwazi,na anakuwa na anaanza kutamani kupata jibu,na akipata jibu kuna vitu ataanza navyo ntavibainisha mwisho wa uchambuzi.(Kwa kijana anaye kupenda usije ukajichumbia kumtengenezea mazingira ya wazi kuwa akuchumbie,kaa Nutral,mweshimu endelea na business zako,atakuja na utapendwa sanaa,ukijilengesha hata akija umepunguza asilimia za upendo na unaweza ukaachwa asije,au mkaishia katikati ya mahusiano.
👉Ukitamaniwa,utasumbuliwa sana kwa pressure bila uvumilivu na hakutakuwa na neno jipya la lengo kuu la maisha ya ndoa,kwa kijana huyu,ukijichumbia kabla ya kukujia maadam unaona anakufatilia,au unaona nikama ana mwelekeo wa kutosema utaishia kuumizwa au njiani.
👉Kuna kijana anakufurahia,yaani unampendeza,ulivyo tu ,mambo yako anakufurahia,anatamani kuwa karibu na wewe tu, (Ila hana mpango wa kukuoa)hawa ni aina ya vijana ambao hupenda Companion ship ya jinsia ya kike( *_anaweza kuwa rafiki yako wakaribu sana kama mchumba,mpenzi wako hata miaka 5,na ukala pesa zake za kutosha ila hautakuja kuolewa naye,mtaongea mambo ya ndoa,ya watoto ila hafanyi maamuzi ya kuku engage 💍.
👉(Kwa vijana wa aina hii 2,kutamaniwa na kufurahiwa binti ukijichumbia kabla ya kuchumbiwa utaumizwa),
👉(Kwa kijana anaye kupenda,atafunguka,usione anavyokuonyeshea kukuhitaji wewe ukamu overtake kujichumbiauta poteza nafasi yako na upendo mwingi aliokuwa nao kwako utashuka)
✍ *_Kosa kubwa lingine wadada wanafanya pasipo kujua au kwa kujua,ila nje ya saikolojia ya vijana ni Kutoa majibu mepesi katika maswali magumu,na kutoa majibu magumu katika maswali mepesi_* hii ni kama imekukoroga ila ndo ilivyo,unampoteza mtu kwa kutojua nyakati na saikolojia yake. Mabinti wengi akiwa hayupo katika nafasi ya Uhitaji mkubwa,aidha kuna kijana anamtarajia kichwani,au wakati alio nao yuoo kwenye chati ya mvuto mkubwaaa wa foleni za vijana,ndo muda mabinti hutoa majibu Magumu kwa 6a kukatisha tamaa,kudharau kwa vijana wenye maswali mepesi ya nimekupenda tuoane.
👉 Hapo majibu magumu yanatolewa yanayofanya vijana saikolojia zao ziinuke za kukudharau na kupeana taarifa kuhusu tabia zako,katika wale watakao pata taarifa zako za majibu yako magumu kuna watakao jitoa kuja kujusumbua wakuze upuuzi wako,kuna watakao kukwepa nakuonyana kutokuendea.(mpaka hapo upo hatarini kupata mtu asiye sahii au kuumizwa tu ,maana hawaji kukuoa ila kukukomoa)
👉Kuna muda wakati(miaka ya mdada inaanza kusogea,mvuto wa kubabaisha watu unaanza kupungua na walio kufahamu,kusumbua enzi hizo kuisha na kuwa tayari na watu wao au ndoa zao,saikolojia ya kike uanza kuyumba ndipo *Majibu mepesi hutolewa na wadada* muda huo kwa maswali magumu ya kufanya ngono ili muoane hupewa majibu ya Yes,maswali ya kuchumbiwa na mpagani,mtu wa imani dhaifu hupewa majibu ya Yes. (Hapa ndipo mabinti huzoa mimba,hupoteza ubikra,uchezewa na kuachwa,huacha wokovu ili uolewe,ndipo huanza kuwatafuta aliowapa majibu magunu kipindi kile,ili awape majibu mepesi kwa sasa)sasa ukikutana na kijana katili ulompa majibu magumu,saizi unampa mepesi hakuoi mpaka amekuchezea kimwili mpaka akuchoke,then akuache,au akuoe kwa kukuhurumia.
*Saikolojia ya Kijana Muoaji iko hivi*
👉Akikupenda anakufungukia kwa namna ya utilivu,adabu na kwa utaratibu.(hakai kimya baada ya kukusoma)
👉Ataeleza nia yake ya kukuoa itakayo ambatana na vitendo vya kauli yake.nia ya kuoa siyo ngono
👉Ataanza kukuleta katika mikakati ya ndoa,siyo simu na outing za I miss u,mwaaah,nakupenda tu,ila ni mikakati ya maisha ya baadaye.
👉Atakuheshimu kama mtarajiwa wale na atauheshimu mwili wako,atataka iwe heshima ya ndoa,hata hisia zikimzidia,aweza eleza hisia zake(matter of love)lakini atasimamia heshima yako na yake na ya Mungu.
👉Ataanza kukuingiza katika program za Kimungu ili kuandaa harusi na ndoa ya utukufu wa Mungu.
👉Ngono na uchafu wote,hutausikia kinywani mwake,bali kusisitiza usafi na uaminifu kati yenu.
_Mbali na hayo saikolojia ya kijana kama haina hiya,basi ndo saikolojia za wanao tamani,furahia uwepo wako_
Ulikuwa na mimi Mchambuzi mtaalamu wa mahusiano na ndoa, *Ev Elisha Kazimoto* (Baba Eve)
        *0755444078*

Friday, 10 March 2017

PIGA UPOFU ADUI APOTEE NJIA

*ADHABU INAYO MFAA ADUI YAKO NI APIGWE UPOFU*
     _Na Ev Elisha Kazimoto_
       *0755444078*
_Shalom mwana wa Mungu,mpiganaji wa vita ya kiroho,katika mkesha wa leo wa maombi ya operation *PIGA UPOFU ADUI APOTEE NJIA* ninakuletea ujumbe wa neno la Mungu utakao kuongoza katika vita hivi na utwae Ushindi wako kwa jina la Yesu_
Kabla ya kuanza mapambano lazima ujue *Sumu,Hila,Uuaji na Ubaya wa Adui* katika maisha yako.
*Mithali 19 : 21 - Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama*
*_Maadui wote hawa uwaonao kwenye ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili(Mapepo na Wachawi,wanadamu) ndani yao wamejaa Hila na sumubyakuua mafanikio yako,maisha yako ya kiroho,huduma yako,ndoa yako,uchumi wako,kazi yako na ofisi yako hata uzao wako na Afya yako,waweza kuonekana kwa macho wanacheka,lakini ndani yao na mikakati yao na vijao vyao vya siri ni Kuua_* sasa hii ni Saa ya Kuwapiga Upofu Wapotee Njia.
*MWANZO 19:9-11*
9   _Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango._ 

10 Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango. 

11  _Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango._
✍Kuna ufunuo mkubwa katika mistari hii na tukio la ujio wa Malaika kwa Lutu na Ghasia za watu waovu kuwatafuta malaika wawatende mabaya.
✍Katika maisha kuna Vitu vya baraka vinaletwa au vimeletwa na Mungu katika maisha yako vikufanikishe,vikuinue vikusaidie, lakini kuna maadui wamevivizia na wanavisonga wakidai vitoke kwenye maisha yako,wanahitaji kuviharibu.
✍Wachawi wameizonga familia yako,ndoa yako uchumi wako mpaka hauna amani(kama watu wa sodoma walivyo izonga nyumba ya Lutu wakiwataka malaika wawatende uovu,hata Lutu akakosa amani)Suluhisho lilikuwa nikuwapiga Upofu watu hawa,wakapotea njia biashara ikawa imeisha.
✍Usiwatolee maadui vitu vyako vya thamani kwasababu ya hofu kwao(kama Lutu alitamani awape Mabinti zake mabikira ili wasiwasumbue wageni wake) *Usiwape, Mwambie Bwana Wapige Upofu wapotee njia nisonge mbele*.
✍Je,kuna watu wanakutelemkia katika maisha yako?wamekuzingira kona zote huoni pa kutokea,unahisi maisha magumu? Usiogope,yupo *Bwana Mpiga Upofu kwa Maadui* mwite sasa awapige Upofu hao nao watajikuta mikononi mwa adui zao.👇👇👇👇
2  _Wafalme 6 : 18 - Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha._
✍Adui yako hawezi acha kukufatilia katika maisha yalo,ndoa yako,ofisi yako au elimu yako kama *Bado Anaona* macho ni taa,yanasaidia kufatilia,yanaonyesha njia yakupitia,ili *Adui Aache Kukufatilia* Mpige Upofu,Ziba macho yake,atapotea NJIA.👇👇👇👇
_Luka 11 : 34 - Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote unao mwanga; lakini likiwa bovu, mwili wako nao una giza._
✍Sasa twende kutoa adhabu kwa kila adui aonekanaye kuwa msumbufu katika maisha yetu,juu ya kanisa la Bwana,kazini,ofisini,katika ndoa,darasani,kwenye Afya,kwenye uchumi nk👇👇👇👇👇
_Kumbukumbu la Torati 28 : 28 - Bwana atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;_
*Mpige Adui kwa Wazimu,na Upofu apotelee mbali kwa jina la Yesu,kinywa chako ni Upanga,anza kushulikia wachawi hao*.
    *By Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve)*
         0755444078

PIGA UPOFU ADUI APOTEE NJIA

*ADHABU INAYO MFAA ADUI YAKO NI APIGWE UPOFU*
     _Na Ev Elisha Kazimoto_
       *0755444078*
_Shalom mwana wa Mungu,mpiganaji wa vita ya kiroho,katika mkesha wa leo wa maombi ya operation *PIGA UPOFU ADUI APOTEE NJIA* ninakuletea ujumbe wa neno la Mungu utakao kuongoza katika vita hivi na utwae Ushindi wako kwa jina la Yesu_
Kabla ya kuanza mapambano lazima ujue *Sumu,Hila,Uuaji na Ubaya wa Adui* katika maisha yako.
*Mithali 19 : 21 - Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama*
*_Maadui wote hawa uwaonao kwenye ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili(Mapepo na Wachawi,wanadamu) ndani yao wamejaa Hila na sumubyakuua mafanikio yako,maisha yako ya kiroho,hyduna yako,ndoa yako,uchumi wako,kazi yako na ofisi yako hata uzao wako na Afya yako,waweza kuonekana kwa macho wanacheka,lakini ndani yao na mikakati yao na vijao vyao vya siri ni Kuua_* sasa hii ni Saa ya Kuwapiga Upofu Wapotee Njia.
*MWANZO 19:9-11*
9   _Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango._ 

10 Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango. 

11  _Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango._
✍Kuna ufunuo mkubwa katika mistari hii na tukio la ujio wa Malaika kwa Lutu na Ghasia za watu waovu kuwatafuta malaika wawatende mabaya.
✍Katika maisha kuna Vitu vya baraka vinaletwa au vimeletwa na Mungu katika maisha yako vikufanikishe,vikuinue vikusaidie, lakini kuna maadui wamevivizia na wanavisonga wakidai vitoke kwenye maisha yako,wanahitaji kuviharibu.
✍Wachawi wameizonga familia yako,ndoa yako uchumi wako mpaka hauna amani(kama watu wa sodoma walivyo izonga nyumba ya Lutu wakiwataka malaika wawatende uovu,hata Lutu akakosa amani)Suluhisho lilikuwa nikuwapiga Upofu watu hawa,wakapotea njia biashara ikawa imeisha.
✍Usiwatolee maadui vitu vyako vya thamani kwasababu ya hofu kwao(kama Lutu alitamani awape Mabinti zake mabikira ili wasiwasumbue wageni wake) *Usiwape, Mwambie Bwana Wapige Upofu wapotee njia nisonge mbele*.
✍Je,kuna watu wanakutelemkia katika maisha yako?wamekuzingira kona zote huoni pa kutokea,unahisi maisha magumu? Usiogope,yupo *Bwana Mpiga Upofu kwa Maadui* mwite sasa awapige Upofu hao nao watajikuta mikononi mwa adui zao.👇👇👇👇
2  _Wafalme 6 : 18 - Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha._
✍Adui yako hawezi acha kukufatilia katika maisha yalo,ndoa yako,ofisi yako au elimu yako kama *Bado Anaona* macho ni taa,yanasaidia kufatilia,yanaonyesha njia yakupitia,ili *Adui Aache Kukufatilia* Mpige Upofu,Ziba macho yake,atapotea NJIA.👇👇👇👇
_Luka 11 : 34 - Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote unao mwanga; lakini likiwa bovu, mwili wako nao una giza._
✍Sasa twende kutoa adhabu kwa kila adui aonekanaye kuwa msumbufu katika maisha yetu,juu ya kanisa la Bwana,kazini,ofisini,katika ndoa,darasani,kwenye Afya,kwenye uchumi nk👇👇👇👇👇
_Kumbukumbu la Torati 28 : 28 - Bwana atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;_
*Mpige Adui kwa Wazimu,na Upofu apotelee mbali kwa jina la Yesu,kinywa chako ni Upanga,anza kushulikia wachawi hao*.
    *By Ev Elisha Kazimoto(Baba Eve)*
         0755444078