🎤🎤 *MAUMIVU YA KWENYE NDOA SWALI NA MAJIBU*🎤🎤
Bwana Yesu asifiwe Dady,nina changamoto naomba unipelekee kwenye group,kwa sasa sina MB,mme wangu hanishirikishi kwenye ratiba zake,yaan kuna siku namsikia tu anasema ,nimepanga kuwasomesha watoto wa ndugu zangu wawili,mara unaona kasain mikopo ya milion sita ,nane .Mwisho yaan ndugu zangu anawachukuliaje
..........................................
_Anajibu Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa *Ev Elisha Kazimoto*(Psychologist & Counselor )_
WhatsApp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
.........
.........
*TUHITIMISHE MADA HII KWA KUANGALIA PANDE 2 YA MKE NA MME*
👉Kwanza kila changamoto,au tabia ina CHANZO chake au kichocheo chake aidha kutoka nje ya box au ndani ya box(maana kwamba kwa huyu aidha chanzo ni mwanamke - Nje ya box, au Mwanaume -Ndani ya box)
👉Shida kubwa ya kutatua migogoro ya ndoa au kushauri kwenye migogoro ya ndoa ni vigumu kupata Ushauri ulio suruhishi kwakuwa wana ndoa wengi wakileta mgogoro, analeta MATOKEO NA SI CHANZO,halafu Anazumgumzia kosa alilofanyiwa ila yeye alilo lifanya analificha au analihesabu kama si kosa.( hapo ndo huwa pagumu kushauri wana ndoa kama anayelalamika ni mmoja)
*TWENDE PAMOJA KWA TATIZO LA HUYU MAMA*
👉Mwana mama unahitaji kusoma NATURE na saikolojia ya mmeo vile vile mwanaume kusoma saikolojia ya mkeo ili mwende sambamba,ukishindwa hapo mtavurugana sana kwa vitu vidogo.
👉Hapa Tungejua kitu kimoja ingetusaidia sana, *Kwamba Tangu anamuoa huyu mama,mme amshirikishi kitu chochote?anaamua yeye mwenyewe au Imekuja hiyo tabia baada ya kuishi miaka 2,3,5....?*
👉Kama tangu anakuoa hakushirikishi kitu,anapanga tu mwenyewe.... Hapo tuta mtafsiri mwanaume katika nyanja zifuatazo.
1⃣Alikolelewa mfumo umemwathiri,katika makuzi yake hakuona mwanamke akithaminiwa na kupewa nafasi ya kupanga maisha so ni mwendelezo wa kifamilia damu ya utawala na ubabe
2⃣Ana makundi ya watu waliojengana fikra za kuwadharau wanawake kama viumbe visivyo na mchango wowote katika familia.
3⃣Ameoa mke asiye jishugulisha na chochote haingizi hata mia ni RECEIVER TU,halafu amekosa Ujanja wa kutumia nguvu ya mwanamke kumteka mme kimahaba mpaka akawa mtu wa kumshirikisha vitu vyote.
👉Kama tabia hii Imeanza baada ya wameisha ishi mwaka,1,2,3,5,.....Mwanamke ndo Amechangia, *Amezoea mazingira ameanza kupunguza huduma muhimu kwa mme.*
👉Niliongea vitu 2 juzi katika kutoa angalizo la mada hii.
👉Kosa kubwa wanawake wengi wanafanya ni Kutoa Adhabu isiyo sahihi kwa Kichwa cha familia., most of women Uona baada ya kukosewa eneo flani dawa pekee ya kumnyoosha mmewe ni KUMNYIMA SEX,bila kujua hapo ndo Unapandisha MASHETANI YA MWANAUME YEYOTE DUNIANI.(Kunyima kumegawanyika katika makundi 2)
1⃣Kunyima kwa kukataa kabisa
2⃣Kunyima kwa kutengeneza visababu sababu vyepesi, mara naumwa,mara sijisikii vzr,mara uende kutembea uchelewe,kuwa busy na watoto,kujipa kazi za ziada nakuzifanya hata kuchoka,kujipa usingizi fofofo wa uongo nk
👉Mwanaume anaakili sana ya kutambua hili unalofanya ni kwasababu umeambiwa sex sasa nikama hutaki.
👉Revenge ya mwanaume ni mbaya sana,akisha kuondoa kwenye Akili ataanza Kufanya mambo yake bila kukushirikisha na huyo awe ameokoka,ambaye hajaokoka vzr hapo anaenda na nje kupata sex.
👉Kinacho mpa nguvu ya kusikia moyo wa kukwambia kila kitu,kukushirikisha *NI MAHABA(SEX) NA HESHIMA UNAYO MPA* hilo ndo limewashinda wanawake waliokwenye ndoa ila WAKISHA ACHIKA NA KUWA MALAYA WANAYAWEZA(Hilo ndo malaya wote wanaoiba waume za watu wameweza)
👉Mpaka malaya aliyeiba mmeo anajua siri zote za mmeo,mipango yote nk kuliko wewe mwanandoa,SI DAWA,ni MAHABA NA HESHIMA ANAYOMPA MMEO vitu hivyo 2 vinafungua moyo wa mme Kusema yote *SI MJIFUNZE KWA DELILA NA SAMSONI* Umeona biblia imesema Delila alimpa Samson LIMBWATA ili aongee siri ya nguvu zake. NI PENZI TU(MME NI SEX,NARUDIA MME NI SEX NA HESHIMA KWISHA HABARI)
*_Sasa ninyi endeleeni kukaa rohoni sana msahau mahaba na heshima mtashangaa mmeo anaibiwa hivi hivi na anayemuiba unamzidi dashboard... Unashangaa kajamaa kanajua mipango yooote ya mmeo wewe hata 1 hujui na upo kwenye ndoa mwaka wa 10_*
Namaliza kwa kusema wamama wanaume hawa si wakorofi,wala jeuri,wala wajinga,Ujeuri,ujinga,na ukorofi mmeukuza ninyi, usipende kutawala hata kama wee unavheo na pesa mme hana,wee mfanye awe mtawala MPE MAHABA YA KUTOSHA,HESHIMA utaona kila kitu anakuuliza wewe kwanza ndo unampa mipango anaenda kutekeleza, UMEMTAWALA KIUTAALAMU.
*NARUDIA MAHABA(SEX)NA HESHIMA KWA MME NI DAWA YA MWANKE KUMTAWALA MME WAKE KIUJANJA NA AMANI NA FURAHA IKADUMU KWENYE NDOA NA UPENDO TELE.*
_Mchambuzi Ev Elisha Kazimoto(Psychologist & Counselor_
Whatsapp 0755444078
Facebook Elisha Kazimoto
Thursday, 19 December 2019
MAUMIVU YA NDOA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment