Sunday, 10 November 2024

YATAINUKA MAWE KUCHUKUA NAFASI

🛜🛜 *UKIZEMBEA YATAINUKA MAWE KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKO* 🛜🛜
_Hili ni Neno la Kibiblia ila linanipeleka mbali mpaka kuyazumgumzia Mahusiano ya wana ndoa wa Kizazi cha Sasa_
*40 Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, mawe yatapiga kelele.Luka 19:40*
🛜We msomaji wangu anzia msitari wa 37, upate kisa kamili, sasa mimi mchambuzi kwakuwa sihubiri neno hapa, ila nachambua kisaikolojia ndoa kwa msingi wa Sentensi ya Kisaikolojia ya Luka 19:40, *_Hawa wakinyamaza Mawe yatapiga kelele_* Nisikilize vizuri nikusaidie kitu hapa.
🛜Katika Mahusiano (hasa ya ndoa) Kila mtu ana WAJIBU na Majukumu yake ya kutimiza ili kuimarisha Furaha na Upendo kwa wana ndoa hao.
🛜Kinachotesa na kusumbua ndoa nyingi pamoja na hila za shetani, ila ni Mwanandoa Mmoja wapo au wote *Kusahau, Kupuuzia, Kuacha Baadhi ya Majukumu muhimu yanayo muhusu kwaajili ya mwenza wake*
🛜Katika Msitari huo 37-40 unaona kuna Watu walitakiwa na ilikuwa ni wajibu kuna mtu inabidi wa Mwimbie, Wamtukuze, Wamsifu, Washangilie,wapige kelele kwaajili yake, Lakini kuna kundi la watu Wakawa wana mawazo ya Kuzuia kelele zile na sifa zile.
🛜Hawakujua umuhimu wa zile sifa na kelele anazopewa yule mtu(Yesu) au walijua ila WIVU TU, ndo uliwatuma.
🛜Sasa wao wakadhani kwakiamuru watoa sifa na kelele KUNYAMAZA watakuwa wamemkomoa Bwana Yesu.
🛜Yesu akataka kuwambia ukweli, kwamba *Sifa, Heshima, Kelele na Utukufu ni LAZIMA siyo muhimu tu* nilazima nipewe, ndo maana NINYI MKIKATAA NA MKAZUIA HAWA wasinipe NINACHO STAHILI, *Mawe Yatainuliwa Yafanye kazi ile ile iliyobidi ifanywe na hawa*
🛜Wana ndoa mnapo poa mnaanza kuruhusu MICHEPUKO?(Mawe hayo) yanainuka kufanya kazi ile ile, *_Ya Kutoa Matumizi, Kusifia, Kuongea naye kwa Mahaba, Kumpa Penzi kwa style zote na mbwembwe zote na furaha yote na muda wowote ANAPO LIHITAJI PENZI_*
🛜Kazi iliyokuwa ya wanadamu( mwanandoa) Inashikwa na Jiwe(Mchepuko).
🛜Unapaswa kujua jiwe halina mamsikio, wala alioni, na halina huruma likisha pewa kazi linafanya kazi mpaka litakapo pasuka au tupwa.( Ndo maana ndoa nyingi zinaugulia maumivu ya muda mrefu) jiwe haliachii karibuni.
🛜 Mwana ndoa, Unajua *_Mmeo/Mkeo Kipi kina mtesa kwako? Anachokihitaji sana, anachodai sana,kinachomfurahisha sana_* Aisee kuwa makini kifanye kwa gharama zozote Ukidharau ukahisi Unamkomoa, My friend Yakiinuka Mawe Kuanza Kupiga Kelele Uwezi Nyamazisha! Itakuwa imekula Kwako.

_Mwisho, kila mmoja kwenye mahusiano kuna kitu kina msumbua sana anakihitaji kwa mwenzake sana, wengine Heshima, wengine Pesa, wengine Kusikilizwa, Wengine kuhurumiwa, Wengine Kupendezeshwa, Wengine TENDO LA NDOA, wengine Kufanya Maendeleo, haya yote kila Mmoja anatakiwa Akae mkao wa Kuwajibika, Ukidharau na Kuona kawaida, Anayekihitaji Aoni kawaida, Atakacho Fanya Atatafuta Mawe ya Kupiga kelele maana tayari wanadamu Wamenyamazishwa, anatafuta kisicho nyamazishwa, na jiwe likianza kupiga kelele uwa linapiga kelele bila kuchoka likijua lenyewe halina sifa ya kupiga kelele limeokotwa tu kama mbadala, ndo maana halichoki, haliangalii changamoto lenyewe linajua likicheza Binadamu anarudi kwenye nafasi yake ya sifa. Tuzuie Mawe Kupata nafasi ya Kupiga Kelele kwa Kila mmoja kumtimizia Furaha Mwenza Wake_

*Ulikuwa nami Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI) 0755444078*

Sunday, 13 October 2024

WANA NDOA KULALA NA NGUO NI SAWA?

🫂🫂 *SWALI KWAKO MWANA SAIKOLOJIA NA MTUMISHI WA MUNGU EV: ELISHA KAZIMOTO* 🫂🫂
_"Kumekuwa na Malalamiko na Manunguniko kwa baadhi ya wanandoa Hawako Huru na Miili ya wenzi wao iwe mchana au usiku na hasa Utamaduni wa kulala na Nguo kwa Mwanandoa,iwe moja ya ndani au full hii imekaaje?_
..........................................
*_Nitajibu kamaulivyoniuliza, ila majibu yangu yatakuwa marefu kidogo Nitoe Elimu, Darasa la Kisaikolojia Katika Ndoa kwa wana ndoa,kuliko ya kujibu kwa ufupi kwamba si sawa au ni sawa, Nitoe ufafanuzi wa kina kama part 2 mpaka 3 au 4 Jitajidi usome zote, Kufikia Mwisho Usipo Pata Kuelewa na Kubadirika kama Mwana ndoa Jua Wewe Hukutakiwa Kuolewa au Kuoa ilibidi Ufe ukiwa Single_*
Uko Nami Mchambuzi wa Masuala ya Ndoa na Mahusiano Ev Elisha Kazimoto( 0755444078)
...........................................
💚💚💚💚💚💚💚💚💚💚💚
👉Wana ndoa tunahitaji kujua kitu kinaitwa *PSYCHOLOGICAL ETHICS OF MARRIAGE* (Tafsiri isiyo Rasimi.... Saikolijia ya Maadili ya Ndoa) 
Kwani unadhani ndoa ni ngumu? Nooo Tuna kwama kwenye Maadili ya Ndoa ya kisiakolojia yake.
👉Leo nitoe darasa kidogo kati ya maandiko yangu nimeandika juu ya ndoa(ukienda kwenye blog yangu au Google andika *Material Adimu University* )utakuta maarifa mengi yatakusaidia kwenye mahusiano na ndoa hata Huduma yako.
1️⃣Wana ndoa, Saikolojia inasema Ndoa ni *Uwanja Huru na wa Uchaguzi kwaajili ya Kujipa furaha ya Mwili, na Akili*
👉Hapa kuna vitu vingi tunavikosea sana wana ndoa, na Kwa hali hiyo *Usaliti, Uchepukaji, na Uzuri wa Mmwenzako Kupungua machoni pako na akili mwako havitaisha* mpaka pale wana ndoa tutaacha Ubabe na Ujuaji na Misimamo binafsi inayoua HISIA ZETU.
👉Wana saikolojia wanapokwambia ndoa ni Uwanja Huru...Wana maanisha, *Jitahidi sana Umfanye mwenzako Ajisikie Uhuru kwako kuanzia mwilini Mwako ajisikie yuko huru na mwili wako, Ajisikie huru kukupa mawazo, ajisikie huru kukukosoa, ajisikie huru kuku brand kwa marafiko zake au kwa watu, ajisikie huru kujieleza shida,changamoto na uhitaji wake*
👉Ukiona Una mnyima Mwenzako uhuru wa Baadhi ya vitu ambavyo Hakika anajua Ni Haki yake Kuwa huru navyo *Basi saikolojia inasema Atavipata tu kwa njia yoyote na popote bila kujalisha ni salama au si salama,ni wazi au siyo wazi* 
👉Kosa si lake, kosa ni la Aliye mnyima uhuru,. Japo kama ni kosa kiufundi ni la mtenda siyo msababishaji ila wanasaikolojia tunaamini Kosa limesukumwa na mtu.
NB: *Hapo Umejifunza nini kama mwana ndoa kwa point ya kwanza?*
👉Wanasaikolojia wanapo sema Ndoa ni Uwanja wa Uchaguzi,.... *Wanamaanisha Alipo kuchagua kuwa mme au mke wake alijua hakika Wewe Utampa Furaha*
👉Pili katika kile Kikubwa alichokichagua,  kila siku na kila saa ana machaguo yakeadogo madogo ya *Nini kitampa furaha kwa wakati mfupi mbali na wewe kuwa furaha yake ya kudumu maisha yote*
👉Anaweza CHAGUA SEX impe furaha muda huo( Je wewe upo tayari?),Anaweza akachagua Kupiga story nawe za Mahaba, je wewe huko tayari?, Anaweza akachagua Kukupa Zawadi au Anategemea Zawadi kwa kipindi flani,je wewe uko tayari? Anaweza kuchagua kutaka kusifiwa au kupongezwa,je wewe huko tayari? Anaweza kuchagua Mcheze michezo ya kimahaba,mapenzi,je wewe huko tayari!
👉Utafiti wa Kisaikolojia unaonyesha, Wanandoa wengi walio dumu kwenye ndoa miaka 10 kuendelea *Wamepoteza Utayari kwa wenzi wao pale wenzi wao wanapo Kuwa na Machaguo ya kuwapa furaha*
👉Ndiyo Maana wengi wameshangaa waume zao au wake zao waliokuwa Waaminifu kwao ila sasa Wameanza Kuwa Cheat! Si kwamba Udanganyifu kwenye ndoa umetokea kama TABIA YAKE NOOO NI MAZINGIRA yaliyo tengenezwa na mwenzi wake kwa Kukosa Utayari kwa Machaguo anayo yachagua mwenzi wake.
👉Saikolojia inasema, *Kila chaguo lililo chaguliwa na mtu, ila mwenza akakosa utayari Litatafutiwa Mbadala wa Utayari kwa mtu mwmingine ili Gap la kisaikolojia la furaha Lizibwe* 
NB: Gap likizibwa na mtu mwingine asiye sehemu ya ndoa linaweza kuwa chanzo cha kumpoteza mwenza jumla.
👉Saikolojia inapozungumzia *Furaha ya Mwili* aaah hapa aisee wana ndoa Turudi darasani na Tutulie kweli, Hapa kwa waliookoka msikemee mapepo kwenye ndoa ukiona mabadiriko kwa mwenza wako,Tulia ujihoji halafu kimya kimya anza mchakato wa mabadiriko mbali na hapo, Kuna maisha magumu unayaandaa mwenyewe bila kujua kumbe ungelijipa raha duniani na maisha yenyewe haya mafupi.
💚Kila mwana ndoa au niseme Binadamu anahitaji Furaha ya Mwili, sasa mimi hapa niko kwa wenye ndoa zao, wana saikolojia wanaposema, mtu anatafuta Furaha ya Mwili kwako elewa mambo haya:
🤝Kuna mtu anahisi raha kama akikukumbatia mkiwa mmelala(mwili wake anahisi raha)
🤝Kuna mtu anahisi raha iliyoje kama Aki Romance na wewe wakati na nje ya tendo la ndoa(mwili wake unatulia)
🤝Kuna mtu anajihisi raha akichezea Maziwa yako,kifua chako, hips zako, garden zako Ukiwa necked( anapata furaha sana)
🤝Kuna mtu anajihisi Raha akiwa kitandani nawe *Ukiwa Free mwilini mwako Hakuna Nguo Yoyote* ile ngozi kwa ngozi zikigusana (Ahaaa anahisi raha) yaani hapo ni nje ya tendo la ndoa.
🤝Kuna mtu anahisi raha ya mwili wake pale anapo shiriki tendo la ndoa nawe (Anahisi raha ya ajabu).
NB: *Sasa hatari ni nini? Ni pale mtu ametegemea furaha ya mwili wake aipate kwako na wewe Ukazuia, Jua moja kwa moja Furaha ya Mwili Itatafutwa tu Pengine.*
👉Sailolojia haijawahi kukaa na SHIMO WAZI (gap) mpaka lizibwe sasa hapo ndo kuna hatari ya ndoa na familia.
👉Wana saikolojia wanaposema..... *Furaha ya Akili* hapa napo pana tesa wengi, hapa kuna watu wana misongo ya mawazo, uchumi mgumu, taarifa mbaya, na masumbufu mengi ya maisha, sasa Eneo ambalo uwa lina ponya na kuwapa watu matumaini kama alivyokuwa ameumba Mungu ni Ndoa(Mwenza wako)
👉Kuna vitu ukifanyiwa vina leta furaha kwenye Akili yako na Unasahau changamoto kwa muda, siku na muda unakuwa unasogea.
1.Romantic Chatting ( mtumiane sms za kimahaba na za upendo na amani)
2.Sex play mcheze na kutaniana kama wachumba au kama wapenzi wapya.
3.Muitane majina ya kimahaba.
4.Mpongeze au msifie kwa kila kazi atakayo fanya au jambo atafanya.
5.Angalia Anatoa Ishara ya Kutaka sex,mwitikie positive bila vijisababu vya kuahirisha.
👉Haya mambo 5 yanaleta furaha ya Akili, Wewe Usipo mpa mambo haya 5, Atatafuta Eneo lolote la Kuyapata ili Akili Ituliepo, Aaipo Pata pa kutuliza akili ndo mtamuona mtu anadalili hizi.
1.Mahasira ya mara kwa mara.
2.Majibu ya mkato/ kukaa kimya
3.Anakaa mtandaoni sana kuliko na wewe.
4.Hafanyi jambo lolote kwako au kwenye familia yake mpaka mmemdai kitu flani.
NB: *Tuokoe familia zetu na ndoa zetu kwa Kurudi kwenye Maadili na Saikolojia ya Ndoa*

_Imeandaliwa na Mchambuzi wa Masuala ya Mahusiano na Ndoa, Mwana Saikolojia *Ev Elisha Kazimoto*(C.E.O- wa G.F.I)
Whatsapp 0755444078
E-mail : babaeve755@gmail.com

Monday, 23 September 2024

CCM UANACHAMA

Ndugu MWESIGA FEDERIK KAZIMOTO usajili wako umekamilika. Namba yako ya uwanachama ni C0001-8290-287-1. Lipia ada kupitia M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money au CRDB. Namba yako ya malipo ni C000182902871

Tuesday, 17 September 2024

TANESCO

Ndugu Mteja, Pokea Namba ya kumbukumbu ya malipo 991035199197, Kiasi 696,669.64 lipia ndani ya siku 90 kabla ya muda wake kuisha.TANESCO

Wednesday, 11 September 2024

ELISHA'S DOCUMENT 1.

APPLICATION NO. YA UMEME TANESCO
Mwesiga F.Kazimoto
App.No.160724-2949
Phone: 0755444078
NIDA:19870615-35521-00001-26
Urefu wa Mita. 120
Cost: Tsh.696,670/=

Tuesday, 13 February 2024

UHUSIANO KATI YA SAIKOLOJIA,MUNGU NA NDOA

⚠️⚠️ *Swali:1:kisaikolojia Kuna hasara ngani za kutokuwa kwenye mahusiano?*⚠️⚠️
 
ANAJIBU MCHAMBUZI WA MASUALA YA MAHUSIANO NA NDOA
*Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI) Mwana saikolojia*
Whatsapp 0755444078
Emaile;babaeve755@gmail.com
*HASARA ZA KISAIKOLOJIA KUTOKUWA KWENYE MAHUSIANO*
No.1.Hasara za kutokuwa kwenye mahusiano ni chache kuliko faida za kutokuwa kwenye mahusiano kisaikolojoa......
*Lakini kabla ya mambo yote niweke Angalizo la kisaikolojia*

✍️Hatuiingii kwa mahusiano kwa kutaka kwetu, bali NATURE & TIME force us to join relationship. ( _Yaani si kwamba tunajiamulia kwa kutaka kwetu kwamba niingie au niache niwe au nisiwe na mahusiano bali ASILI NA MUDA divyo vinatuingiza kwenye mahusiano_)
👉NATURE(ASILI....) Ubongo wa mwanadamu umegawanyika katika makundi 4( MAPENZI, IMANI-DINI, SIASA NA PESA) mapenzi yanabeba robo tatu ya asilimia zote za ubongo (75%) hapa ndo utajua uamui wewe ila NATURE ya maumbile yako ndo inakulazimisha kujoin relationship.
✍️Kama watu wangekuwa wanajiamulia kuingia kwenye mahusiano au kutoingia basi *Tusinge shuhudia watu kujiua kisa mapenzi au Kuumizwa mara ya kwanza, ya pili, ya tatu nk* ila tunavishuhudia hivyo vyote kwakuwa SI WATU WANAJIAMULIA kuingia katika mahusiano bali NATURE.
✍️TIME(muda) ni msukumo mkubwa kwa watu kuingia katika mahusiano, kuna muda ambao mtu HAONI UMUHIMU WALA HAJA YA MAHUSIANO, na kuna muda ambao mtu anaona Haja na Ulazima wa mahusiano. Kwahiyo hivi vitu viwili ( *Nature and Time haviruhusu mtu ajiamulie kuingia kwenye mahusiano au kutoingia*)KISAIKOLOJIA
✍️Tukirudi Kiroho ndo tutasema Mungu ndiye anayetuongoza na kutupa kibali au kutunyima kibali cha kuingia kwenye mahusiano.
*SASA TWENDE KWA SWALI*
👉Hasara za kutoingia kwenye mahusiano.
1️⃣Akili yako aikui inadumaa.
👉Mahusiano yanakuchemsha akili na kukukomaza,unajua namna ya kufanya maamuzi ya jumla na si ya kwako mwenyewe.
2️⃣Una kosa darasa bora la maisha na la hisia.
👉Mtu asiye kwenye mahusiano anauwezo mdogo wa kufikiri juu yake binafsi na juu ya hisia za watu.
👉Mahusiano yanakufanya *Akili yako ifikili kwaajili yako na kwaajili ya mpenzi wako*
👉Mtu anayefikiri kwaajili yake na mtu mwingine ni Imara zaidi kimaisha na kihisia kuliko anayejifikiria binafsi.
3️⃣Unakosa kipimo sahihi cha uwezo wako wa kihisia na kimaisha.
👉Kama hauna mahusiano, uwezi jua *nguvu yako ya kuvumilia, nguvu yako yakusamehe, kiwango chako cha kukosea watu, kiwango chako cha kuomba msamaha kama kinatosha* wewe ni Kipofu anayejiona na asiye ona vitu vingine.
4️⃣Kama hauna mahusiano uwezi jijua kiusahihi wewe ni mtu wa aina gani. *Unaweza kuwa na Mis interpretation* unavyojidhania sivyo ulivyo.
5️⃣Kama hauna mahusiano, unakosa nafasi ya kusahihisha makosa na mapungufu yako.
👉Mahusiano ni kioo cha mtu cha kujipima wema wake na ubaya wake, na kuurekebisha mapema kabla mabaya hayajamrekebisha na kumfungia milango ya kuonekana mtu muhimu.
*_Niseme naweza ishia hapa kwa leo, siku nyingine nitajibu faida za kuwa kwenye mahusiano, ila angalizo, Usilazimishe kuingia kwenye mahusiano kwa maana mahusiano yenyewe uwa ndo yanamwingiza mtu kwenye mfumo, tulia mpaka nature na time vikuvutea uingaie ndani ya mahusiano_*

Ulikuwa na mimi mchambuzi wa Masuala ya mahusiano, Mwana saikolojia *Ev Elisha Kazimoto(CEO-GFI)*
Phone; 0755444078
Emaile; banaeve755@gmail.com